JAMHURI- SABAYA AFUNGWE NA ACHAPWE VIBOKO KWA KUINAJISI TAASISI YA URAIS

 



ALIYEKUWA Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya akiingia mahakamani kusikiliza hukumu kwenye kesi inayomkabili ya unyag'anyi wa kutumia silaha

JAMHURI yaomba mahakama impe adhabu kali,aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili kwani kwa matendo ya unyang’anyi wa kutumia nguvu na kutumia silaha aliyoyafanya akiwa kazini ameinajisi taasisi ya Rais iliyomteua.

 

Ombi hilo limetolewa na Wakili wa serikali, Felix Kwetukia mbele ya  Hakimu Mkazi Mwandamizi, Odira Amworo kwenye Makahama ya Hakimu Mkazi Arusha baada ya mahakama hiyo kuwatia hatiani Lengai Ole Sabaya, na wenzake Silvester Nyegu na Daniel Bura kwa makosa mawili ya unyang’anyi wa kutumia nguvu na kosa moja la unyang’anyi wa kutumia silaha.

 

Wakili wa serikali, Felix Kwetukia, mheshimiwa hakimu hatuna kumbukumbu ya makosa ya  jinai waliyowahi kutiwa hatiani ila ni rai yetu kwamba kwa kosa la pili la unyang’anyi wa kutumia silaha wahukumiwe kama sheria ya adhabu kifungu namba 287 A kinavyoelekeza.

 

“Kinasema ni adhabu kwa kufungwa jela miaka isiyopungua 30 na ni rai yetu kwamba kwa kuwa kifungu hiki kimeeleza kuwa wanaweza kupewa pamoja na adhabu ya kuchapwa viboko au wasipwe sisi upande wetu tunaomba wapate adhabu ya viboko.

 

Kwa kosa la kwanza na la tatu la unyanganyi wa makundi ambao adhabu yao ni kifungo kisochopungua miaka 30 na adhabu ya viboko au bila viboko ni rai yetu wachapwe hata kwa kosa la kwanza na la tatu ni rai yetu adhabu ya viboko iambatane nao,” 

 

Mheshimiwa  tumeomba adhabu hiyo kali kwa sababu mhukumiwa wa kwanza kwa kuwa mteule wa Rais kwa kipindi hicho na kujihusisha na vitendo vya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujiingiza katika unyang’anyi wa nguvu

 

Alifanya vitendo ambavyo si vizuri kwa mamlaka yake ya uteuzi na jamii ya Watanzania kwa kadiri ya makuzi na haiba ya vijana waliolelewa katika malezi mazuri.

 

Hivyo ni rai yetu adhabu kali itolewe ili iwe fundisho kwake pamoja na grupu lake

 

Kwa kuwa alikuwa mteule wa Rais alikuwa anaidhalilisha mamlaka yake ya uteuzi kwa kutenda mambo kinyume na hati yake ya uteuzi ilivyokuwa inamwelekeza.

 

Umri wa washitakiwa wote ambao wametiwa hatiani ni umri wa vijana ambao wana nguvu ya kufanya kazi walipaswa kujipatia kipato kwa njia halali na si kujiingiza katika matendo ya uhalifu hususani unyanganyi wa kutumia silaha kwa msingi huo mheshimiwa hakimu ni rai yetu ingawa ni mara yao ya kwanza kutiwa hatiani basi kama vifungu vya 287 A vya adhabu na 217 vinavyoelekeza basi adhabu kali dhidi ya watiwa hatiani wote iweze kutolewa.

 

MAOMBI YA UNGAMO 

 

Wakili, Moses Mahuna kwa niaba ya Lengai Ole Sabaya aliiomba mahahakama impunguzie mteja wake adhabu kwani hiyo ni mara yake ya kwanza  kutiwa hatiani.

 

“Tunaleta maombolezo kwa niaba ya mshitakiwa 

wa kwanza, baada ya mahakama kumtia hatiani kwenye makosa hayo mawili ni kweli sheria inatoa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka 30 ambacho kinaweza kuambatana au kisiambatane na adhabu ya viboko,” ameeleza wakili Mahuna na kuongeza.

 

…Tunaomba mahakama immtazame mtuhumiwa wa kwanza kwa jicho la huruma kwa kuwa ni mtenda kosa kwa mara ya kwanza na hakuna rekodi za nyuma zozote za kutiwa hatiani

 

Hata hivyo mheshimiwa, mtuhumiwa huyu wa kwanza amekuwa mtumishi wa umma kwa kipindi kirefu licha haya yaliyopo hapa mahakamani ni mamnbo mengi amelitendea Taifa katika utumishi wake.

 

Hivyo ni rai yetu kwamba mahakama inapotoa adhabu imtazame kwa jicho la huruma hata hivyo mshitakiwa amekuwa akitoa ushirikiano wa kutosha tokea alipokamatwa.

 

Alishirikiana na vyombo vya dola vyotetokea alipokamatwa mpaka akaletwa hapa mahakamani.

Hata hivyo kama ilivyotanguliwa kusemwa na wakili msomi Felix Kwetukia ni dhahiri kwamba ni kweli kuwa mtuhumiwa ana umri wa miaka 34 ambaye bado ni nguvu kazi ya Taifa.

 

Ni rai yetu mahakama izingatie umri wake huo kwa kuwa adhabu hizi za makosa yake yote haya ni miaka 30 kwa 30 ni ombi mahakama inapoenda kutoa adhabu izingatie mchango wake kwa Taifa hasa na umri wake na kumpatia adhabu ambayo itamwezesha kutumikia hiyo adhabu ndani ya kipindi ambacho kitatosha kumrekebisha na hatimaye kumruhusu kurudi kuendelea kutoa mchango wake katka Taifa hili.

 

Na ni ombi letu ikikupendeza adhabu hizo ziende kwa pamoja, hiyo miaka 30, 30 iende kwa pamoja  

manake sipoenda kwa pamoja ni miaka 90 hivyo ni ombi letu mheshimiwa hukumu hiyo isitafsiriwe kama kifungo cha maisha kwa kifungo cha miaka 90 kumfanya atoke akiwa na  miaka 120 (mahakama kicheko).

 

Jambo linguine ana familia pia inamtegemea, ana mke na watoto, na ana wazazi pia wanamtegemea kwa hiyo tunaiomba mahakama izingatie hayo yote.

 

Wakili, Silvester Kahunduka kwa niaba ya mshitakiwa wa pili, Silvester Nyegu alieeleza mahakama kuwa ni kweli kuwa mshitakuwa wa pili  ametiwa hatiani na mahakama yako kwa makosa matatu ambayo yote adhabu yake ni miaka 30.

 

“ Mheshimwa tunakuja mbele ya mahakama yako kwa maombolezo kuwa bado ni kijana mdogo ana miaka 26 tu,  hii ni nguvu ya uchumi katika Taifa hili  lakini vilevile ana familia inayomtegemea kwa maana ya wazazi wake na ndugu zake kwa maana hiyo tunaiomba mahakama katika kutoa adhabu ione hilo,” ameomba wakili Kahunduka na kuongeza.

 

…Jamhuri imeomba wapewe dhabu na viboko lakini adhabu ya viboko ni maamuzi ya mahakama na adhabu za viboko mara nyingi zinalalamikiwa mara nyingi kama adhabu ambazo zinautweza utu wa watu…

 

..Tunaiomba mahakama hii kwa kutumia mamlaka iliyo nayo katkka kuamua izingatie kwamba hiyo ni adhabu ambayo inakuwa inalalamikiwa sana  na ikiwezekana mahakama isitoe adhabu hiyo.…

 

Hakimu akasema kulalamikiwa    siandiki kwa sababu adhabu hiyo iko kisheria wakili akakubalina naye

 

Wakili, Freedolin Gwemelo kwa niaba ya mshitakiwa wa tatu, Daniel Bura aliieleza mahakama kuwa hili ni kosa lake la kwanza hana rekodi yoyote ya kosa la jinai, mshitakiwa bado ni kijana ni nguvu ya Taifa anayetakiwa kwenye jamii na kutimiza sera ya nchi hii ya ‘kazi iendelee’.

 

Hakimu akauliza ni sera au kauli mbiu wakili Gwemelo akajibu kauli mbiu.

 

Wakili Gwemelo akaendelea kuomba kuwa, “mtuhumiwa namba tatu anategemewa na familia yake akiwemo mama yake ambaye umri umeenda na ni tegemeo kwa wadogo zake kwa hiyo ndiyo jicho la familia yake kwa sasa… 

 

…Ni rai yetu makosa yanayomkabili adhabu yake iende kwa pamoja na iwe ndogo ili aweze kuja kuihudumia familia, na adhabu ya viboko mheshimiwa naomba isiwepo kwa sababu ni adhabu ambayo hailindi utu na kwa kuwa ipo chini ya uwezo wa mahakama hii basi adhabu hii isiwepo ni hayo tu mheshimiwa,”.

 

 

 

 

0 Comments:

Post a Comment