![]() |
| Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Salum Hamduni |
JESHI la polisi mkoani Arusha linamshikilia Mbise Lukumo, (30) kwa tuhuma za mauaji ya wanawake mbalimbali jijini hapa likiwemo la Anna Edward,(44) aliyeuawa januari 25, mwaka huu na kupelekea maandamano makubwa ya wanawake.
MAHAKAMA Kuu kanda ya Arusha imemuru kuuzwa kwa awamu mali za hoteli ya kitalii ya Impala ili kulipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya wafanyakazi wa hoteli hiyo na Naura yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 500.

Wafanyakazi wa hoteli za Impala na Naura Sping wakimsikiliza Kaimu Afisa kazi mkoani Arusha, Emmanuel Mweta aliyekuwa akiwaeza uamuzi uliotolewa na mahakama
Aidha imeamuru fedha zitakazobaki mara baada ya wafanyakazi hao kulipwa zikabidhiwe benki ya NBC ambayo inaidai hoteli hiyo zaidi ya shilingi bilioni 1.5
Jaji, Mohamed Gwae ametoa amri hizo, Januari 8, mwaka huu wakati akitoa uamuzi kwenye maombi ya pingamizi yaliyowasilishwa na kampuni ya Impala na benki ya NBC wakipinga kutekelezwa kwa amri ya ukamataji na uuzwaji wa mali za Impala ili kulipa madeni ya mishahara.
Amri hiyo ilitolewa na Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha , Masijala ndogo ya kazi.
"Kwa kuwa hakuna 'secured creditor' mwingine zaidi ya benki ya NBC ambaye hana pingamizi ila anataka alipwe kile kutakachobaki baada ya mali kuuzwa na wafanyakazi kulipwa madai yao," alisema jaji Gwae akitoa uamuzi wake na kuongeza.
...unaposema kiuzwe ila kisiuzwe chini ya kiwango ambacho kimethaminiwa. Msiuze kwa mradi tu unauza.
Nilikuwa najiuliza kwenye hiyo kesi nyingine ambapo kuna Kiwanja namba 16, 17, 18 na 19 vile ni tofauti na vile 20, 21, 22 na 23 sasa kwa nini kwani vile havitoshi mpaka muuze vyote? ...
...Naomba majibu hawa waliofanyia tathmini manake mimi sivijui sisi tunaongelea kwenye makaratasi hatujaviona najua Impala manake nimelala najua Naura na Ngurdoto,".
Mkurugenzi Pelagia alimfafanualia Jaji Gwea kuwa viwanja hivyo ni tofauti ingawa hivyo ambavyo namba zake zimefuatana vimeungana viwanja viwili vina hati moja.
"Kwa nini msiuze hivi 20, 21, 22 na 23 kwanza hivi kama isipopatikana ndipo muuze hivyo vingine. Wanasema usishangilie kifo cha mwenzako manake na wewe utakuja kufa tu hakuna yeyote atakayeenda mbinguni bila kufa," alisema Jaji Gwea wakati akitoa uamuzi wake huo na kuongeza.
...Mimi natoa amri hii viuzwe kwanza viwanja namba 20 mpaka 23 kama hakuna utimilifu wa hiyo tuzo ndiyo mnaenda kwenye mambo mengine,".
Baada ya uamuzi huo Pelagia alisema kwa kuwa mmliki wa Naura na Impala ni mmoja hivyo fedha zitakazopatikana zitalipa madeni ya yote jambo ambalo jaji aliweleza kuwa hayo hayaihusu mahakama kama wanaweza kufanya hivyo wafanye kinachotakiwa wafanyakazi walipwe kabla mali hazijauzwa.
HOJA ZA BENKI YA NBC
Awali akipitia hoja za waleta maombi, Jaji Gwae alisema kuwa Benki ya NBC iliwasilisha hoja tano za pigamizi kupitia wakili, Wilbard Massawe kutoka kampuni ya Mawalla.
Alisema wakili Massawe aliieleza mahakama kuwa hana shida na kuuzwa kwa mali zilizokamatwa ila izingatiwe tu kwamba benki ina maslahi na benki itakuwa tayari kupata kile kitakachokuwa kimebaki baada ya wafanyakazi kulipwa madeni yao.
"Hata hivyo kwenye hoja zao walisisitiza kutambuliwa kuwa wanaidai Impala hivyo walipwe fedha zitakazobaki mara baada ya wafanyakazi kulipwa madeni yao?" alisema Jaji Gwae akisoma hukumu hiyo.
Alisema kuwa Kaimu afisa kazi mkoani Arusha, Emanuel Mweta, alikubaliana na hilo kwa kile alichoeleza kuwa kwa kuwa NBC haipingi wafanyakazi kulipwa malimbikizo ya mishahara yao.
HOJA ZA IMPALA
Jaji Gwae alisema kuwa, Wakili wa Impala, Richard Massawe aliwasilisha maombi ya pingamizi chini ya hati ya kiapo akidai kuwa mali zilizoamriwa kukamatwa zina thamani kubwa kuliko madeni ya mshahara wanayodaiwa.
Alidai mali zilizoamriwa kukamatwa na kuuzwa zina thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tano wakati madeni ya malimbikizo ya mishahara ni zaidi ya shilingi milioni 500.
Jaji alitupilia mbali pingamizi la Impala walilokuwa wanadai Kaimu Afisa kazi wa mkoa, Mweta hakuwa sahihi kufungua maombi hayo mahakamani kwani sheria inataka kamishina wa kazi ndiyo ayafungue.
"Nimepitia sheria nimeona afisa kazi anaweza kufungua mashauri hayo kwani anamwakilisha kamishina wa kazi.Ukizingatia mleta maombi namba moja (Impala) na utayari wake wa kuwalipa wafanyakazi nimeona maombi haya hayana msingi," alisema Jaji Gwae na kuongeza.
...Kwa kuwa yule anayedaiwa kuwa kuna suala la 'guarantee' ambapo mkopo ulichukuliwa (NBC Bank) anasema yeye hana pingamizi. Kama wangekuwa wale ndo wanapinga ingetakiwa waangaliwe manake wale ndiyo wana 'secured creditor',".
Jaji Gwae alisema kuwa kwa kuwa NBC anayetaka atambuliwe baada ya kuuzwa hivyo vitu hivyo kwa msingi huo kuna hivyo viwanja ambavyo vimeshafanyiwa tathmini ya juu bilioni 1.8 lakini wao (Impala) wanasema ni bilioni 8 ingawa hakuna tathmini nyingine iliyofanyika.
"Kwa kuzingatia kwamba kutoka Novemba mwaka jana kesi hii iko hapa mahakamani lakini kwa kuzingatia pia wale wanaowakilishwa na mjibu maombi, Afisa kazi, (wafanyakazi) hawajalipwa mshahara mpaka leo, na kwa kuzingatia kwamba mleta maombi habishi kwamba anadaiwa na wafanyakazi naamuru uuzwaji wa mali iliyokamatwa kwa amri ya msajili iuzwe haraka baada ya kutangaza," alisema jaji Gwea akimaliza kutoa uamuzi kwa upande wa hoteli ya Impala.
HOTELI YA NAURA SPRING
Jaji Gwae pia alisoma uamuzi kwenye maombi ya pingamizi ya hoteli ya Naura Spring dhidi ya utekelezwaji wa amri ya Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha , Masijala ndogo ya kazi ya kuuzwa kwa magari matano na viwanja vinne.
"Sitarudia hoja zote za mawakili na afisa kazi manake ni zilezile ila mali zilizokamatwa ni magari matano na yamefanyiwa utathmini Kesi hii inahusu utekelezaji na 83/2020 ndiyo walifungua kwa msajili," alisema Jaji Gwae.
Alisema "hoja ya mawakili wa Impala kuwa wakurugenzi, Kama Rando (Mrema) hakuwa mkurugenzi lakini Pelagia Mrema yupo lakini pia wasimamizi wa mali za marehemu wapo tulitegemea wafanye kiapo kwamba huyu hakuwa mkurugenzi kubatilisha kikao cha Machi 14, 2019 kilichowateua Rando na Janet,".
....Kama wale kina Herode waliokuwa wanaiwakilisha kampuni kwenye kesi kama wasingekuwa wanatambuliwa na mkurugenzi, Pelagia lakini pia kwa wasimamizi wa mirathi wa marehemu, Mrema, Micheli Mrema wangefanya kiapo cha kuwakana vinginevyo wakili utabaki unasema tu ila wao hawajasema chochote," alisema Jaji Gwae.
WAFANYAKAZI WA IMPALA WANENA
![]() |
| Baadhi ya wafanyakazi wa hoteli za Impala na Naura wakiwa kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Masijala ndogo ya Kazi Arusha |
Kiongozi wa wafanyakazi wa Impala na Naura Jacob Joel alisema wanaishukuru mahakama na serikali kupitia ofisi ya idara ya kazi ambayo ndiyo waliowawakilusha kwenye shauri hilo.
"Tunaishukuru sana mahakama kwa kutupatia haki yetu maana kwa sasa hivi ni takribani miezi 16 tumekuwa tukisota bila kupata mishahara," alisema Jacob.
Alisema wafanyakazi wa Impala wanadai zaidi ya milioni 397 na wafanyakazi wa Naura wanadai zaidi ya shilingi milioni 107 ikiwa ni malimbikizo ya mishahara.
" Tunadai zaidi zaidi ya milioni 500 maana mpaka sasa bado hawajatusimamisha kazi, bado tunatambuliwa kama wafanyakazi kwa sababu bado hawajatupa barua za kutusimamisha kazi," alisisitiza Jacob.
Kamanda wa polisi mkoani Arusha, (RPC), Salumu Hamduni
MKAZI wa Elerai jijini Arusha, Badru Abdallah, (38) anadaiwa kumchoma kwa pasi mtoto wake mwenye umri wa miaka 12.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Salumu Hamduni ameeleleza kupitia taarifa yake aliyoitoa jana kwa vyombo vya habari kuwa tukio hilo lilitokea januari 16, mwaka huu majira ya saa mbili usiku.
Mtoto mdogo jina limehifadhiwa miaka 12, alijeruhiwa kwa kuchomwa na pasi ya umeme mgongoni na Baba yake mzazi aitwaye Badru Abdallah, (38), )mrangi na mkazi wa Elerai," alisema kamanda Hamduni.
Alisema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi na mara baada ya upelelezi kukamilika jalada litapelekwa ofisi ya Taifa ya mashtaka kwa ajili ya hatua zaidi.
Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Salum Hamduni
Mkazi wa Sakina, Olaiis Wavii (46) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake mwenye umri wa miaka mitatu.
Serikali imetoa miezi mitatu kwa wenye shehena ya vifungashio visivyokidhi viwango vya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) vinaondolewa sokoni.
Agizo hilo limetolewa Januari 8, 2020 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Ofisi hiyo jijini Dodoma kuhusu matumizi ya vifungashio vya plastiki kutumika kama vibebeo vya bidhaa.
Ummy alisema hatua hiyo ya Serikali imechukuliwa baada ya kuwepo kwa vifungashio vinavyotumika kama vibebeo vilivyozagaa madukani, sokoni na maeneo mbalimbali.
Alisema kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana kutokana na katazo la mifuko ya plastiki siku za hivi karibuni kumejitokeza changamoto ya matumizi ya vifungashio vya plastiki aina ya tubings visivyokuwa na sifa na hivyo kutokukidhi matakwa yaliyowekwa na TBS.
Aidha, Waziri Ummy aliongeza kuwa vifungashio hivi kwa sasa vinazalishwa kwa wingi na kwa ukubwa mbalimbali na vimekuwa vikitumika kama mifuko ya kubebea bidhaa sokoni na kuleta dhana kuwa mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku imerudi kivingine kama “vifungashio”.
Alisema mifuko hii imeanza kuzagaa kwenye mazingira ya mitaa yetu na vijiji vyetu kwa kasi kubwa, na hivyo kurudisha nyuma mafanikio makubwa tuliyoyapata katika kipindi chote cha kupambana na changamoto ya mifuko ya plastiki.
Kwa mantiki hiyo Waziri Ummy aliwataka wasambazaji, wazalishaji wa vifungashio hivi na waagizaji kuacha mara moja kuzalisha, kusambaza, kuuza na kutumia vifungashio hivyo na kusisitiza kuwa baada ya kipindi hicho Serikali haitatoa tangazo lingine lolote kuhusiana na katazo la matumizi ya vifungashio visivyokuwa na ubora.
Waziri huyo alisema Serikali itachukua hatua kali kwa mujibu kisheria na katika kipindi hiki tunaendelea na operesheni maalumu kuwabaini wanaokwamisha mafanikio haya kwa kuzalisha na kusambaza vifungashio hivyo na hatutawavumilia watu hawa.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Joseph Malongo alisema Ofisi hiyo itashirikiana na TBS kuanza kampeni ya kupitia tena mifuko ya ‘non woven’ kwani kuna uwezekano wa kuwepo kwa mifuko isiyo na viwango.
Malongo alisema Serikali ilipoweka katazo la mifuko ya plastiki iliweka pia viwango vya mifuko ya aina hiyo akitaja kuwa ni lazima iwe na uzito wa gramu 70 kwa mita ya mraba moja ili itumike kwa zaidi ya mara moja.
Aliongeza kuwa pia lazima mifuko hiyo iwe na nembo ya TBS ili kuonesha kuwa imekidhi vigezo vinavyotakiwa pamoja na kutambulisha jina la mzalishaji.
Kigezo Kingine ni viwe na lakiri (Seal), ikimaanishwa kuwa kifungashio kinatakiwa kifungashwe na anayefungasha bidhaa yake ili kuuza kabla ya kwenda sokoni.
Pia, Waziri Mkuu alikagua nyumba 7 za Wakuu wa Idara za Halmashauri ya Mji wa Mbinga zilizojengwa na Serikali kwa gharama ya sh. Milioni 321.771.
Awali ,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Grace Quintine alimweleza Waziro mkuu kuwa lengo la miradi hiyo ni kuboresha mazingira ya makazi ya watumishi wa halmashauri ikiwa ni pamoja na kupunguza kilipa posho za nyumba kwa kila mwezi

(HABARI KWA HISANI YA BBC)
Wanatumia baadhi ya viungo kwa pamoja


Maria aliwahi kula kwa ajili ya mwenzake kwa miaka mitano.
![]() |
| Moja ya nyumba iliyoathirika na Mvua |
Katika Mkoa wa Arusha Habari Tanzania tunaripoti Tukio la January 2 katika wilaya ya Meru ambapo kaya nne ziliathirika na mvua hizo kwa kuvunjiwa nyumba zao na uharibifu Mkubwa wa vyakula.
Kaya zilizoathirika na mvua hizo zipo kwenye kitongoji cha Nkoamangashi katika Kata ya Kikatiti. Familia hizo ni kama ifuatavyo Famila Charles Litoi mbise, Familia ya Bw. Frank Charles, familia ya Emanuel Wariaeli, na Familia ya Ndugu Afraeli Emanuel.
Kufauatia athari hizo Viongozi wa maeneo hayo Kitongoji hadi kata wakawa karibu zaidi kuzinusuru familia hizo kutokana na janga hilo.
Diwani wa kata ya Kikatiti Mh. Elias Mungure akawataka wasamaria wema kuungana na wanakitongoji hao ili kufidhia hasara zilizotokea na kuzinusuru kaya hizo dhidi ya njaa baada ya vyakula kuharibiwa.
![]() |
| Diwani wa Kata ya Kikatiti Mh Elias Mungure akitoa maelekezo wakati akiwapa pole wahanga wa Tukio hilo. |
![]() |
| Mifuko 8 ya Saruji na Chakula kwa familia zilizoathirika na mvua iliyonyesha hapo Jana. |
Awali Mwenyemiti wa kitongoji hicho Jacob Emanuel alieleza tukio hilo lilivyotokea na kuwa wa kwanza kutoa msaada wa haraka pamoja na kutoa taarifa kwa viongozi wengine kwa ajili ya msaada zaidi.
Wakati mvua hizo zikinyesha na tukio hilo kutokea majira saa tisa za alasiri mmoja wa mwana kaya alieleza ilivyokuwa huku kwa bahati nzuri Hakukua na mtu aliyejeruhiwa.
Mashuhuda wanasema mvua kubwa iliyoambatana na Upepo mkali , mawe ya barafu iliezua mabati ya nyumba na pelekea kuta za nyumba kuvunjika bibaya , Ripoti hii pia ilishuhudia hali ya nyumba hizo pamoja na Miti mikubwa ya maeneo hayo ilivyovunjwa vunjwa ovyo.
Bw. Moris amewaambia Waandishi wa Habari kuwa pamoja na Sera ya Elimu bure kuwa msaada Mkubwa katika Wilaya hiyo kumekuwa na changamoto kadhaa inayoikabili sekta ya Elimu ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanafunzi wa jamii ya kifugaji kuwa na tabia ya kutoroka masomo Mara kwa Mara kitendo kinachodhoofisha Maendeleo ya Elimu katika Wilaya hiyo.
Licha ya Miundombinu ya majengo kuwa changamoto katika baadhi ya Halmashauri mbalimbali nchini kwa mujibu wa Mkurugenzi Moris Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Haina tatizo la uhaba wa Miundombinu ya Madarasa.
Aidha Mkurugenzi Moris ameleza kuwa Karatu ina makabila ambayo haipatikani maeneo mengine ya Mkoa wa Arusha ikiwemo jamii ya Wahazabe jamii na Jamii za kifugaji jamii ambayo ina mifumo ya kuhama hama hivyo kupelekea watoto wao kushindwa kuhudhuria masomo.
Kufuatia adha hiyo Halmashauri imekuwa ikilazimika kufanya misako ya Mara kwa Mara ili kuwarudisha wanafunzi wanotoroka shule ili kuendelea na masomo hivyo kukwamisha shule hizo kufanya vizuri.
Mkurugenzi Moris amesema Halmashauri yake imedhamiria kujenga Bweni katika baadhi ya maeneo ambayo imezungukwa na Jamii nyingi za kifugaji na jamii ya wahazabe jamii inayoishi kwa Uwindaji na kula matunda.
Katika Hatua nyingine Moris ameongeza kuwa Ujenzi wa Bweni hizo ukikamilika itasaidia kuhakikisha kuwa wanafunzi hao kutoroka masomo yao hivyo itachangia kuongeza ufaulu katika shule zao.
Katika matokeo ya Darasa la Saba mwaka 2017 Halmashauri ya Karatu imeshika nafasi ya 6 kati ya Halmashauri saba za Mkoa wa Arusha.



































