Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio ya taasisi na mashirika ya umma nchini unategemea kwa kiwango kikubwa uimara wa mifumo ya utawala bora, uwajibikaji na uongozi wenye maono yanayolenga matokeo.



Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Chacha Marigiri, alipowasilisha mada kuhusu ‘Utawala bora katika mashirika ya Umma na Majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Hazina’  katika Mkutano wa Jukwaa la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma Zanzibar uliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip Airport.



Katika wasilisho lake Jumapili, Mei 24, 2026, Marigiri alisema kuwa kasi ya kufikia maendeleo endelevu haiwezi kupatikana kwa uwekezaji pekee, bali kupitia mifumo imara ya usimamizi inayohakikisha rasilimali za umma zinalindwa na kuzalisha kwa maendeleo ya Taifa.


Alisema thamani ya uwekezaji wa Serikali katika taasisi za umma na kampuni ambazo Serikali ina hisa chache kwa sasa imefikia Sh92.3 trilioni, hali inayodhihirisha umuhimu wa kuendelea kuimarisha mifumo ya utawala bora na usimamizi wa uwekezaji wa umma.





Kwa sasa Ofisi ya Msajili wa Hazina inasimamia uwekezaji wa umma wenye jumla ya taasisi 308, zikijumuisha taasisi za kibiashara, zisizo za kibiashara pamoja na uwekezaji wa ndani na nje ya nchi.


Hali hiyo inaifanya OMH kuwa mhimili muhimu katika kulinda na kuongeza thamani ya mali za Serikali.


Bw. Marigiri alisema jukumu la OMH linaenda zaidi ya usimamizi wa kawaida mpaka kuhakikisha taasisi za umma zinaendeshwa kwa nidhamu ya kifedha, zinakuwa na ufanisi wa kiutendaji na zinaendana na vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.


Alitaja maeneo muhimu ya mamlaka na majukumu ya OMH kuwa ni pamoja na kusimamia utendaji wa taasisi za umma, kufuatilia faida na marejesho ya Serikali kupitia gawio, kushauri kuhusu uteuzi na tathmini ya bodi, kufanya tathmini ya utendaji pamoja na kushauri Serikali kuhusu maamuzi ya uwekezaji.


Katika hatua nyingine, aliwataka wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu kuendelea kuimarisha mifumo ya utawala kwenye taasisi zao kwa kuzingatia matumizi ya teknolojia, usimamizi wa vihatarishi, usimamizi wa maadili pamoja na maamuzi inayozingatia takwimu.


Alisema uzoefu wa mataifa yaliyofanikiwa kiuchumi kama Singapore, Norway, China na Malaysia unaonesha kuwa mafanikio ya uwekezaji wa umma yanategemea zaidi ubora wa usimamizi kuliko ukubwa wa uwekezaji wenyewe.


“Taifa lolote halifanikiwi kwa kumiliki taasisi za umma pekee; mafanikio yanatokana na namna taasisi hizo zinavyosimamiwa kwa weledi, uwajibikaji na malengo muda mrefu,” alisema.


Aidha, alibainisha kuwa OMH imeandaa Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu (2025/26–2049/50) unaolenga kuifanya ofisi hiyo kuwa kichocheo cha upanuzi wa uchumi kupitia uwekezaji wa Serikali na hasa katika sekta za kimkakati ikiwemo usafirishaji, nishati, fedha, kilimo, viwanda, utalii na madini.


Alisema mafanikio ya uwekezaji wa umma yataendelea kutegemea ushirikiano wa karibu kati ya bodi za taasisi, watendaji wakuu, Serikali na taasisi za usimamizi ili kujenga taasisi imara, zenye ushindani na zinazotoa matokeo yanayopimika kwa maendeleo ya Taifa.




Happy  Lazaro,Arusha .

Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude,amezindua rasmi chapa yake  mpya ya gesi safi ya kupikia, LOTI GAS,huku akisisitiza umuhimu wa matumizi ya nishati safi kwa maendeleo ya afya, mazingira na uchumi wa wananchi.



Aidha Mkuu wa wilaya  huyo ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wananchi hao kutumia nishati hiyo kwa wingi ili kutunza mazingira .




Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkude ameipongeza kampuni ya LOTI GAS kwa uwekezaji wake ambao amesema unaenda sambamba na dira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa lengo la kupunguza matumizi ya kuni na mkaa ili kulinda mazingira pamoja na afya za wananchi.


Mkude amesema mwitikio wa matumizi ya nishati safi nchini umefikia asilimia 28.6, huku juhudi mbalimbali zikiendelea kuhakikisha taifa linafikia malengo yaliyojiwekea katika sekta hiyo muhimu.


"Uwekezaji wa kampuni ya LOTI GAS umefungua fursa za ajira kwa vijana na kuchangia kukuza uchumi wa Mkoa wa Arusha pamoja na taifa kwa ujumla."amesema Mkude .


Aidha ameihimiza menejimenti na watumishi wote wa LOTI GAS kuhakikisha wanazingatia viwango vya usalama, ubora wa bidhaa pamoja na kutoa huduma bora kwa wateja ili kujenga imani kwa wananchi.


"Nawasihi wananchi wa Arusha na Watanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa ya matumizi ya nishati safi, akibainisha kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wenye nia njema ili kuweka mazingira bora ya biashara na maendeleo nchini."amesema Mkude .



Akizungumza kwenye uzinduzi huo ,Mkurugenzi wa Loti Energies, Collins Kimaro amesema kuwa , dira ya kampuni hiyo ni  kuona Tanzania ambayo kila nyumba—kuanzia  Arusha hadi maeneo ya vijijini—inaweza kutumia nishati safi ya kupikia kwa usalama, kwa upatikanaji rahisi na kwa gharama  rafiki.


Aidha amefafanua kuwa ,  tofauti ya Loti Gas ni kwamba inakuletea amani kwani  afya inalindwa kwa sababu hamna moshi,mitungi misafi na mipya na amani kutokana na usalama, imepimwa na ina vigezo vyote na ni bei rafiki.



Aidha ameongeza kuwa,gas hiyo inapatikana kwa urahisi, madukani au kwa delivery .ambapo mteja anapelekewa sehemu yoyote .



"Uzinduzi huu umefanyika chini ya kampeni ya “Tupo Jikoni na Loti – Gesi ya 

Kuaminika Kwako”, ambapo uzinduzi huo  umeambatana na shindano la kupika supu lililoonyesha  matokeo mazuri na ladha ya kuvutia, kuthibitisha ubora wa Loti Gas katika matumizi ya kila siku."amesema  Mkurugenzi Kimaro.




Uzinduzi huo ambao umefanyika katika ukumbi wa  Aim Mall Arusha ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali ambao kwa pamoja  wamepongeza kampuni ya Loti Energies kwa uwekezaji huu inayounga mkono malengo ya serikali ya kuendeleza nishati safi ya kupikia kwa Watanzania wote.



"Uzinduzi ulionyesha pia uwepo wa wakala wengi wa Loti Gas, jambo linalothibitisha 

kuwa tayari Loti Gas imeanza kupatikana sokoni Arusha, ikiwa na mitungi ya kilo 6 na 

kilo 15, na mpango wa kupanua zaidi kadri mahitaji yanavyoongezeka."amesema Kimaro.




 


Na Mwandishi wa OMH


Dar es Salaam. Tanzania imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China katika mageuzi ya mashirika ya umma, ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa serikali wa kuongeza ufanisi, faida na uwajibikaji katika uwekezaji wa umma.



Nia hiyo ilibainishwa Jumatatu, Mei 18, 2026, wakati Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian, pamoja na ujumbe wake, walipotembelea Ofisi ya Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na menejimenti ikiongozwa na Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, kuhusu uwekezaji, maendeleo ya miundombinu na uhamishaji wa teknolojia.



Akizungumza katika kikao hicho, Mchechu alisema Tanzania inalenga kujifunza kutoka China katika kusimamia na kuleta mageuzi ya mashirika ya umma kupitia mfumo wa Tume ya Usimamizi na Uendeshaji wa Mali za Serikali ya China (SASAC), akibainisha kuwa Ofisi ya Msajili wa Hazina ni taasisi ya kimkakati yenye dhamana ya kusimamia uwekezaji wa Serikali.



Alisema kutokana na jukumu hilo, Ofisi ya Msajili wa Hazina inaona umuhimu wa kuwa na ushirikiano wa karibu na taasisi za China, hususan katika maeneo ya uwekezaji, usimamizi wa mashirika ya umma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


“Tunapofanya mageuzi ya taasisi zetu, tunataka kujifunza kutoka kwa nchi ambazo zimefanikiwa kupitia njia hii. China ni mojawapo ya mifano bora duniani katika kufanya mageuzi kwenye mashirika ya umma,” alisema.



Mchechu alisema baadhi ya mashirika yanayosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina tayari yana ushirikiano mzuri na taasisi mbalimbali za China, hali ambayo imeongeza umuhimu wa kuimarisha zaidi ushirikiano kati ya pande hizo mbili.


Pande hizo mbili pia zilijadili umuhimu wa kubadilishana uzoefu katika usimamizi wa mashirika ya umma, utekelezaji wa mageuzi ya taasisi pamoja na maendeleo ya miundombinu na uhamishaji wa teknolojia.



Mchechu alisema Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa sasa inasimamia taasisi na kampuni 308 ambazo serikali ina uwekezaji, zikiwemo 252 ambazo Serikali ina hisa nyingi.


Alieleza kuwa uwekezaji huo umefanywa katika sekta mbalimbali muhimu ikiwemo usafiri wa anga, nishati, mafuta na gesi pamoja na madini.


Aidha, alisema serikali inaendelea na mageuzi ya kupunguza utegemezi wa ruzuku, kuongeza mchango wa gawio serikalini, kuimarisha uwajibikaji wa taasisi na kutoa uhuru zaidi wa kiutendaji kwa mashirika ya umma.


“Hata kama tunataka uchumi uongozwe na sekta binafsi, sekta ya umma isiyo na ufanisi itaendelea kuwa kikwazo kwa sekta binafsi kustawi,” alisisitiza.

Katika mazungumzo hayo, Bw. Mchechu pia aligusia ushirikiano unaoendelea kati ya Tanzania na China katika miradi ya kimkakati ikiwemo usafiri wa majini, madini na uendeshaji wa bandari.


Pia aliishukuru China kwa kuendelea kutoa fursa za mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, akieleza kuwa watumishi sita walinufaika na mafunzo mwaka jana huku wengine watatu wakitarajiwa kupata mafunzo mwaka huu.


“Mafunzo haya yamekuja wakati muafaka na yana mchango mkubwa katika kujenga uwezo wa watumishi wetu,” alisema.


Akizungumza katika kikao hicho, Balozi Mingjian alisema China iko tayari kushirikiana na Tanzania katika kubadilishana uzoefu wa mageuzi ya kiuchumi na mabadiliko ya taasisi.


Alisema sera ya Mageuzi na Ufunguaji Uchumi ya China iliyoanza mwaka 1978 ilisaidia kuibadilisha nchi hiyo kiuchumi licha ya changamoto kubwa katika miaka ya awali ya utekelezaji.


“Tuko tayari kabisa kushirikiana na ndugu zetu wa Tanzania katika uzoefu huu wa kitaasisi,” alisema.


Aliongeza kuwa China itaendelea kuunga mkono ajenda ya Tanzania ya viwanda kupitia biashara, miundombinu, teknolojia na mafunzo ya watumishi.


Pia alibainisha kuwa serikali ya China itaendelea kutoa nafasi za mafunzo kwa watumishi wa umma wa Tanzania katika maeneo ya mabadiliko ya kidijitali, utawala na usimamizi wa uchumi.



Balozi mingjian alisema Tanzania na China zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu wenye kuaminiana, akitaja ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini China mwaka 2022 kuwa sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya mataifa hayo mawili.


Kikao hicho pia kilijadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika uongezaji thamani wa madini, ambapo Tanzania inalenga kuanzisha viwanda vya ndani vya kusafisha na kuchakata madini ya kimkakati.


Vilevile, pande hizo mbili zilijadili mustakabali wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), ambayo mwaka huu inatimiza miaka 50 ya uendeshaji wa kibiashara.

 


The Tanzanian government has continued to invest heavily in tourism infrastructure development as part of broader efforts to strengthen the sector’s competitiveness and increase its contribution to the national economy.

Speaking in Parliament in Dodoma on May 15, 2026, the Minister for Natural Resources and Tourism, Ashatu Kijaji said the government has made major progress in improving access and services within key tourist destinations across the country.

While presenting the ministry’s revenue and expenditure estimates for the 2026/27 financial year, Dr Kijaji revealed that the government completed the construction of three airstrips in Nyerere National Park and Ruaha National Park. She added that construction of the Mikumi Airstrip is expected to be completed by October 2026.

The minister further explained that eight additional airstrips located in Mikumi, Ruaha, Nyerere and Serengeti National Park have been rehabilitated to improve transportation services for tourists visiting the parks.

According to Dr Kijaji, the government has also constructed and rehabilitated 3,757.92 kilometers of roads and 523.14 kilometers of walking trails in protected areas, making it easier for visitors to access tourist attractions.

Tourism infrastructure has also been strengthened through the construction of six visitor rest areas and nine entry gates in Nyerere, Mikumi and Ruaha national parks.

In addition, tourism centers have been established in the forests of Mount Meru Forest Reserve, Vikindu, Mwambesi, Pindiro, Mount Rungwe and Lake Duluti. One tourist camp has also been constructed in the Kilombero Nature Forest Reserve.

Dr Kijaji said the investments are already delivering positive results, including improved accessibility to tourist attractions, enhanced visitor experiences, and increased employment and business opportunities for communities living near conservation areas.

She noted that the improvements have also contributed to higher government revenue and continued growth of the tourism industry.

Highlighting the impact of the improvements in Tanzania’s Southern Circuit, the minister said the number of tourists increased from 197,402 to 205,520 between July 2025 and April 2026. During the same period, revenue rose from 24.6bn/- to 27.7bn/-.

The minister said the achievements demonstrate the government’s commitment to continue improving tourism infrastructure in order to strengthen Tanzania’s position in the global tourism market, stimulate economic growth and improve the livelihoods of citizens.



"The 14th East African Community (EAC) Armed Forces Command Post Exercise has officially opened in Nairobi, Kenya, to strengthen regional security collaboration. 

Running from May 6 to May 28, 2026, the multinational event trains military, police, and civilian personnel to handle modern security threats together."

 Strengthening Regional Defense



The multinational exercise, dubbed Ushirikiano Imara, has officially commenced at the Ulinzi Sports Complex. The training brings together personnel from EAC Partner States to improve interoperability and collective security. Participants focus on joint capabilities in Peace Support Operations, Counter-Terrorism, Counter-Piracy, and Disaster Management.

Addressing Complex Threats



EAC Deputy Secretary General Andrea Aguer Ariik Malueth emphasized that the region faces complex, interconnected threats like transnational organized crime. He noted that these challenges require stronger coordination, practical cooperation, and timely information sharing among defense institutions.

 A Shared Vision for Peace


Kenya’s Vice Chief of the Defence Forces, Lieutenant General John Omenda, highlighted that no nation can stand alone against criminal groups like Al-Shabaab and Boko Haram. Under the theme “Enhancing Regional Readiness for Peace, Security and Resilience,” Exercise Director Major General John Nkoimo stated that the command post drills will significantly improve multinational operational effectiveness.

  

๐ŸšจBilioni 38 Kuanzisha Mapinduzi ya Nishati Kikuletwa: 


๐Ÿ“Mtambo wa ATC Kuziba Pengo la Umeme Kaskazini na Kuokoa Fedha za Kigeni Ifikapo Novemba 2026


๐Ÿ“ŒKuondoa Uhaba wa Wataalamu



Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza shilingi bilioni 38 katika Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) Kampasi ya Kikuletwa ili kuondoa kabisa uhaba wa wataalamu wa nishati jadidifu nchini. 


Mradi huu mkubwa wa ujenzi wa mtambo wa kufua umeme kwa nguvu ya maji (Hydropower) unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo Novemba 2026, huku ukilenga kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Kanda ya Kaskazini.



Mratibu wa Mradi wa EASTRIP kutoka ATC na Kaimu Meneja wa Kampasi ya Kikuletwa, Mhandisi Sithole Mwakatage, amebainisha kuwa uwekezaji huo unajenga Kituo cha Umahiri cha Nishati Jadidifu kitakachotumia mfumo wa kisasa wa ujifunzaji kwa vitendo.


Aliyasema hayo wakati wajumbe wa Kamati Tendaji ya Usimamizi na Uongozi wa Mradi wa Kuendeleza Ujuzi (EASTRIP) walipotembelea kituo hicho kilichopo Hai mkoani Kilimanjaro leo Mei 14, 2025.


"Tumejenga kituo cha kufua umeme wa maji chenye uwezo wa kuzalisha megawati 1.65, ambacho kina dhana ya 'Factory for Teaching' (Kiwanda cha Kufundishia). Wanafunzi wanajifunza kwa vitendo kuanzia siku ya kwanza wanapoingia chuoni," alisema Mhandisi Mwakatage.


Teknolojia ya Kipekee Kusafisha Gridi ya Taifa



Mhandisi Mwakatage alieleza kuwa mtambo huo una upekee mkubwa wa kiteknolojia ukilinganisha na mitambo mingine nchini, kwani una uwezo wa kujiwasha wenyewe bila kutegemea nguvu ya gridi ya taifa wakati wa dharura (Black Start capability).

"Ni mtambo wa kisasa unaotegemea betri, na mfumo wake wa msisimko (excitation system) unatumia umeme kutoka vyanzo vya betri na kuanza kufua umeme. Mtambo huu uko kimkakati kuisaidia gridi pale inapokuwa imefeli," alifafanua Mwakatage.



Mradi huu unaenda kutatua changamoto ya muda mrefu ya mdororo wa voltage katika Kanda ya Kaskazini, hatua itakayookoa fedha za nchi zilizokuwa zikitumika kununua umeme nje ya nchi.

"Hapo awali, serikali ilikuwa imelazimika kununua umeme kutoka nchini Kenya kwa ajili ya kuimarisha voltage (Voltage Stabilization), lakini sasa uwepo wa mtambo huu unaenda kupunguza au kuondoa kabisa tatizo hilo."

Malengo Makuu na Hatua za Utekelezaji





Naye Mhandisi wa ATC anayesimamia mradi huo eneo la Kikuletwa, Mhandisi Adam Mfangavo, alieleza kuwa mradi una malengo makuu mawili: kutumika kama kituo cha umahiri cha mafunzo, uzalishaji, na ukarabati wa mifumo ya hydropower, pamoja na kuzalisha umeme utakaoingizwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia shirika la TANESCO.

Mhandisi Mfangavo alifafanua kuwa mradi unatekelezwa katika awamu mbili:



Awamu ya Kwanza: Ujenzi wa majengo mawili na ufungaji wa mitambo ulikamilika rasmi Machi 2026.



Awamu ya Pili: Imeanza mwezi huu wa Mei 2026 na itachukua miezi sita hadi kukamilika kwake Novemba 2026.


"Novemba mwaka huu, mradi utaanza kuzalisha umeme kiasi cha Megawati 1.65, unaoweza kutosha kulisha umeme magorofa 100. Mtambo ukitengeneza umeme utaanza kusambaza kwenye gridi ya taifa na pia kutumika kwa ajili ya ufundishaji," alisema Mhandisi Mfangavo.

Mradi huu tayari unanufaisha jamii inayozunguka kituo kwa kupata fursa za ajira, huku wanafunzi wa fani za Hydropower, Nishati Jua (Solar), Mitambo (Mechanical), na Umeme wakipata mafunzo ya vitendo (Industrial Practical Training).

Kupaa kwa Idadi ya Wanafunzi na Miundombinu Mpya



Kutokana na maboresho haya, Kampasi ya Kikuletwa inajipanga kupokea ongezeko kubwa la wanafunzi kutoka 70 wa awali hadi kufikia 600 mara mradi utakapoanza kazi. Chuo kimejenga kampasi mpya yenye madarasa, karakana (workshops), na mabweni ya kutosha.



Katika hatua ya kipekee, chuo kimejenga hosteli maalum kwa ajili ya wanafunzi watu wazima wenye watoto ili kuwawezesha kusoma bila vikwazo. Mbali na nishati ya maji, kuna mipango ya kupanua kituo hicho ili kuwa na mashamba ya nishati ya jua (Solar Farm), nishati ya upepo (Wind Power), na nishati ya biogas ili kukifanya kuwa kituo kamili cha umahiri katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.


Wanafunzi wanaosoma chuoni hapo wameonyesha kuridhishwa na uwekezaji huo mkubwa unaowapa fursa ya kujifunza kwa vitendo na mazingira bora ya chuo.



"Ninaridhishwa sana na mafunzo yanayotolewa hapa chuoni pamoja na mandhari nzuri sana ya chuo hiki," alisema Christina Mushi, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza anayesomea fani ya Mabomba (Plumbing).



Naye mwanafunzi mwenzake, Paulo Ngoyaine, aliongeza kuwa: "Chuo kiko vizuri sana na mafunzo yake yanatolewa kwa vitendo zaidi, jambo linalotujengea uwezo mkubwa."



Kukamilika kwa mradi huu kunatajwa kuwa mkombozi wa soko la ajira nchini, kwani utazalisha nguvu kazi maalum (workforce) itakayosaidia kuendesha miradi mingine mikubwa ya kimkakati kama ule wa Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP), ambalo linahitaji wafanyakazi wataalam zaidi ya 2,000 kwa wakati mmoja.


Mradi wa EASTRIP ni wa kikanda unaotekelezwa katika nchi za Afrika Mashariki ambapo kwa upande wa Tanzania, mradi huo unahusisha ujenzi na uimarishaji wa vituo vya umahiri katika vyuo vitatu vikuu: Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Dar es Salaam (DIT), na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).

Vituo hivyo vinatarajiwa kutoa mafunzo ya kitaalamu na ya vitendo katika sekta za nishati jadidifu, teknolojia ya habari na mawasiliano, uchakataji ngozi, pamoja na usafirishaji wa anga. 


Hatua hii inalenga kuongeza ujuzi wa vijana na kuimarisha ushindani wa kikanda katika soko la ajira. 

 


Maadhimisho ya siku ya Urithi wa Dunia Afrika yaliyofanyika katika Makumbusho ya Urithi Jiopaki mjini Karatu tarehe 5 Mei, 2026 yameyakutanisha makabila makuu manne yanayounda Jiopaki ya Ngorongoro Lengai ambayo ni wamasai, wahadzabe, wairaqw na wadatoga na hivyo kuunganisha kutaniko kubwa la urithi wa dunia katika ukanda wa Afrika Mashariki. 



Mkuu wa wilaya ya Karatu, Dkt Lameck Karanga amesema uwepo wa makabila hayo, historia yao pamoja na kuenzi tamaduni zao ni utajiri mkubwa kwa Tanzania na kutoa wito kwa wadau na jamii kwa ujumla kuendelea kulinda maeneo ya urithi wa dunia na kuibua maeneo mapya yatakayoingizwa katika orodha ya Urithi wa Dunia ili kuongeza thamani ya ubora wa kipekee ulimwenguni (Outstanding Universal Value) na kuvutia wageni wengi zaidi.



Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Utalii na Maendeleo ya Jamii Ngorongoro Joas Makwati ameeleza kuwa mamlaka itaendelea kuongeza juhudi za kulihifadhi eneo la Ngorongoro ambalo ni urithi wa dunia na kultangazia zaidi kama eneo pekee lenye Ushahidi wa kisayansi kuhusu historia ya binadamu unaoeleza kuwa binadamu kwa kuthibitishwa na ugunduzi wa masalia ya binadamu wa kale na zana za mawe zilizopatikana katika bonde la Olduvai. 



Kwa upande wake Naibu Katibu wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania Dkt. Khamis Said ameeleza kuwa tangu Tanzania ijiunge na UNESCO imepata mafanikio mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuridhia mikataba kumi (10) ya UNESCO,Kuwepo kwa Hifadhi Hai za Mwanadamu na Mazingira sita (6) na Kuwepo kwa maeneo saba (7) ya urithi wa Dunia.


Kauli mbiu ya siku ya urithi wa dunia kwa mwaka huu ni “Kusherekea siku ya Urithi wa Dunia na kukuza Viongozi wa baadaye”. (Celebrating Africa’s Heritage, Mentoring the Leaders of Tomorrow).



Kutoka Pemba, Unguja, Mji mkongwe, Bagamoyo, Kondoa, Magofu ya kilwa, paa la mlima kilimanjaro na maeneo mengine ya Tanzania, wadau wa urithi wa dunia wamekutana katika Makumbusho ya Urithi Geopark Karatu Mkoani Arusha yanayosimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro  kwa lengo la kuadhimisha   Urithi wa Dunia Afrika yaliyoanza leo tarehe 04/05/2026 hadi tarehe 05/05/2026.




Wakiwa katika jengo la makumbusho ya Urithi Geopark Wadau hao wameelezwa jinsi Ngorongoro ilivyo ni utajiri wa urithi wa dunia kutokana na uumbwaji wake uliotokana na mlipuko wa volcano zaidi ya miaka milioni mbili iliyopita na kutengeneza kasoko iliyokusanya asili, uhai wa binadamu, mifumo ya ikolojia, na ustawi wa viumbe mbalimbali.



Katika  taarifa yake kwa vyombo vya habari Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Abdul-Razaq Badru amewashukuru wadau wote hasa Shirika la Umoja wa Mataifa la  Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)   kwa kuipa fursa Ngorongoro kuandaa na kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo kwa mwaka huu.



Wadau wa urithi wa duania wakiwa katika Makumbusho ya Urithi Geopark walipata fursa ya kuelezewa kuhusu uthibitisho wa wasomi unaoeleza wazi historia ya chimbuko la binadamu wa kale aliyepatikana katika bonde la olduvai  takribani milioni  2 iliyopita na ushahidi wa Nyanyo za binadamu wa kale  katika eneo la Laetoli takribani miaka  3.6 iliyopiTa ambapo binadamu hao walitembea kwa miguu miwili.





Taasisi zinazoshiriki maadhimisho hayo ambazo zinasimamia maeneo ya urithi wa dunia ni pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Mamlaka ya Uzimamizi wa Wanyamapori (TAWA), Wakala wa Huduma za misitu Tanzania (TFS), pamoja na wawakilishi wa maeneo ya urithi wa dunia kutoka Zanzibar.

 


ARUSHA, TANZANIA – Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema kuwa uhuru wa vyombo vya habari nchini hauwezi kudumu wala kuwa wa kweli ikiwa wanahabari wenyewe hawana uhakika wa kipato na ustawi wa kiuchumi.



Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani jijini Arusha, Makonda ameeleza kuwa hali duni ya kiuchumi inawaweka wanahabari katika mazingira magumu yanayowafanya washawishiwe kwa urahisi na maslahi ya wanasiasa au wafanyabiashara.



Amesema hali hiyo ni hatari kwa uadilifu wa taaluma kwani inafungua milango kwa watu wenye maslahi binafsi kufadhili wanahabari ili kulinda taswira zao badala ya kuripoti ukweli.



Makonda amesisitiza kuwa mwelekeo wa sasa wa vyombo vya habari lazima ubadilike. Amewataka wanahabari kuacha kujikita zaidi kwenye siasa na "kubrand" watu, na badala yake waelekeze nguvu zao katika kuibua na kutangaza fursa za kiuchumi zilizopo nchini, hususan katika sekta za utalii, kilimo na biashara.

"Tanzania ina utajiri mkubwa wa vivutio vya utalii na bidhaa zenye ushindani kama kakao, parachichi na tangawizi. Ikiwa vyombo vya habari vitatoa kipaumbele kwa sekta hizi, vitasaidia kuvutia uwekezaji, kutafuta masoko ya kimataifa, na hatimaye kujijengea msingi imara wa mapato," alisema Makonda.

Aidha, amebainisha kuwa vyombo vya habari ni nguzo muhimu katika kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa viwanda. Amesema kuna umuhimu wa wanahabari kubobea katika uchambuzi wa sekta za uzalishaji ili kusaidia Taifa kunufaika na rasilimali zake kwa kuongeza thamani ya bidhaa (value addition), badala ya kuishia kuuza malighafi nje ya nchi.

Makonda amehitimisha kwa kukemea tabia ya baadhi ya wanahabari kutumika kama vyombo vya kulinda maslahi ya watu fulani, akisisitiza kuwa mwelekeo huo unadhoofisha uaminifu wa umma kwa tasnia ya habari na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.




Arusha

The United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO), in collaboration with the Media Aid for Indigenous and Marginalized Communities (MAIPAC) and the Tanzania Information Services (Maelezo), is developing a specialized guidebook for journalists and digital content creators operating in areas inhabited by marginalized groups.



The guidelines aim to help media professionals and content creators navigate the ethical landscape, cultural values, and traditions of indigenous communities—specifically the Hadzabe, Maasai, Datoga, and Akie—before producing or disseminating any content related to them.



MAIPAC Executive Director, Mussa Juma, announced the initiative yesterday during a panel discussion held in Arusha to commemorate World Press Freedom Day (WPFD). The session focused on the impact of digital content creation and the role of Artificial Intelligence (AI) in enhancing professional journalistic standards.

Juma noted a rising trend of both local and international content creators visiting these communities, particularly the Hadzabe, and publishing material without proper consent or in ways that violate cultural ethics and dignity.



“In response to these challenges, MAIPAC, UNESCO, and the Information Department are drafting a specific manual for working with these communities. This will ensure that media activities are conducted ethically and with full respect for the dignity of these people,” Juma stated.



In addition to the guidebook, MAIPAC is partnering with UNESCO, Maelezo, and SAVVY Media to provide digital literacy training for these communities. The project aims to empower them to use social media effectively, understand their digital rights, and benefit economically from the information and advertisements generated about their way of life.

“We will build their capacity to use digital platforms for their own benefit and help them recognize their digital rights, which will ultimately uplift their local economies,” Juma added.

During the discussion, digital creators and officials from the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) emphasized that AI and digital tools should be embraced as transformative aids for youth and community development rather than being viewed as a threat.


Mdindi Samboga, Chairman of the Hadzabe community in the Eyasi Valley, Karatu District, expressed gratitude for the initiative. He remarked that while his community has gained significant fame on social media recently, they rarely see any tangible benefits from the exposure.

“People come to take our pictures and interview us. We hear that we are very popular in the cities, but we don't benefit from it at all—sometimes we are only given alcohol. We are now asking for assistance so that we can benefit fairly from our own image and culture,” Samboga said.