SHIRIKA la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limeingia kwenye hatua kubwa ya kuimarisha ulinzi na doria angani baada ya Kamishna wa Uhifadhi, Massana G. Mwishawa, kukagua ndege ndogo mbili (2) mpya aina ya Savannah zilizonunuliwa hivi karibuni.



Ndege hizo zimenunuliwa kupitia mradi unaofadhiliwa na BMZ, uliotekelezwa chini ya Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani. Lengo kuu la ununuzi huo ni kuongeza nguvu katika doria na uhifadhi wa wanyamapori kwenye Hifadhi za Taifa za Serengeti na Nyerere.


Ukaguzi huo umefanyika leo katika Karakana iliyopo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar, ambapo ndege hizo zinaendelea kuunganishwa tayari kwa kazi.


Akiwa uwanjani hapo, Kamishna Mwishawa amewapongeza mafundi wanaoendelea na kazi ya uunganishwaji wa ndege hizo kwa umakini mkubwa.


Pia, ametoa pongezi za kipekee kwa marubani wawili (2) ambao ni Askari Uhifadhi wa TANAPA. Marubani hao kwa sasa wapo kwenye hatua za mwisho za mafunzo yao maalum ya kurusha ndege hizo ili kuhakikisha usalama na ufanisi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.


Ndege hizo za kisasa aina ya Savannah zinatarajiwa kuanza doria rasmi angani mwanzoni mwa mwezi Oktoba, 2026, hatua itakayosaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti ujangili na kulinda rasilimali za taifa.

 



Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro Abdul-Razaq Badru ameuambia mkutano wa 48 wa kamati ya Urithi wa Dunia kuwa Ngorongoro ni sehemu pekee ambayo binadamu duniani kote wanaweza kupata ushahidi sahihi wa chimbuko la asili ya binadamu.



Akizungumza mjini Busan,Jamhuri ya Korea wakati akiongoza Mkutano wa pembeni (Side event) ulioandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kupata uelewa wa pamoja kuhusu hali ya uhifadhi wa eneo la  Hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni eneo la Urithi wa Dunia, Badru amesema Ngorongoro ina ushahidi uliohifadhiwa wa nyayo za binadamu na masalia ya kale katika eneo la Laetoli na Olduvai zinazothibitisha suala hilo.


“Ngorongoro si tu eneo la utalii bali pia ni mahali ambapo historia ya binadamu wote kisayansi ilianzia”, alisema kamishna Badru.


Katika kikao hicho ameeleza kuwa kila nyayo iliyohifadhiwa ndani ya hifadhi ya Ngorongoro inawakumbusha kurudi nyumbani kuona historia hiyo.


Badru amefafanua  kuwa Ngorongoro ni sehemu ambayo binadamu alianzia kutumia zana mbalimbali za mawe kama teknolojia ya awali ya shughuli za kibinadamu na ndipo alipoanza kufanya harakati za kimaisha.


Mkutano wa kamati ya Urithi wa Dunia una lengo la kufanya maamuzi kuhusu maeneo mapya yanayopendekezwa kuingizwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia na kuimarisha juhudi za pamoja za kulinda, kuhifadhi, na kusimamia kwa uendelevu maeneo yenye thamani kubwa ya kiutamaduni na asili duniani.

 


WANANCHI wa Kijiji cha Manyire, Kata ya Mlangarini mkoani Arusha, wameanza rasmi ujenzi wa shule yao ya sekondari. Hatua hii inaleta ukombozi mkubwa wa kielimu na kumaliza changamoto ya muda mrefu ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.


Utekelezaji wa mradi huo umeanza kushika kasi kufuatia Serikali kutoa fedha za awamu ya kwanza. Tayari mradi umekabidhiwa rasmi, ambapo wananchi kwa kushirikiana na mkandarasi wapo kazini kuchimba msingi wa majengo ya shule hiyo.

Diwani wa Kata ya Mlangarini, Emanuel Mrema, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka mradi huo unaogusa maisha ya wananchi.

"Ujenzi wa shule hii ni faraja kubwa kwa wananchi wa Manyire ambao kwa miaka mingi walikosa shule ya sekondari karibu. Watoto wetu walilazimika kutembea hadi kilomita 24 kila siku kufuata masomo, jambo lililoathiri mahudhurio na maendeleo yao kitaaluma," alisema Mrema.

Mrema alimpongeza Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Dkt. Johannes Lukumayi, kwa juhudi zake za kupigania mradi huo bungeni. Pia aliishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Arusha chini ya Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Selemani Msumwi, kwa ushirikiano uliowezesha mradi kuanza.


Alibainisha kuwa vijana wa eneo hilo wamejitokeza kwa wingi kushiriki hatua za awali za ujenzi. Diwani huyo aliwasisitiza wananchi kuendelea kushirikiana na kulinda miradi ya maendeleo kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

"Watoto wetu hawapaswi kurithi migogoro au visasi. Wanapaswa kurithi miradi ya maendeleo itakayoboresha maisha yao na kuwasaidia kufikia ndoto zao," alihitimisha Mrema.

 


Mwambata wa ubalozi wa Oman nchini Tanzania, Abdulrahman Salim Algaad akiwa na familia yake, ametembelea Hifadhi ya Ngorongoro na kushuhudia maajabu ya utalii yaliyopo katika kivutio namba moja cha utalii barani afrika

 


Akimpokea mwambata huyo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za Utalii na Masoko Mariam Kobelo ameeleza kuwa jitihada za mamlaka hiyo kuwafikia wadau mbalimbali zimeendelea kuzaa matunda ambapo watumishi kutoka balozi mbalimbali ndani na nje ya nchi wamendelea kutembelea hifadhi hiyo.

 


Akiwa ndani ya hifadhi hiyo, Abdulrahman Algaad na familia yake walipata fursa ya kushuhudia wanyamapori adimu wakiwa katika mazingira yao ya asili, wanyamapori wakubwa watano, misitu, maporomoko ya maji, urithi wa utamaduni na mambo kale, makumbusho ya urithi geopark na kueleza kuwa ndoto na hisia alizokuwa nazo zimekutana na uhalisia.

 

Mwambata huyo ameonyesha kuvutiwa na uzuri wa Hifadhi ya Ngorongoro na vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania na kupongeza hatua za uhifadhi zinazofanyika na kuifanya Ngorongoro kuendelea kuheshimika kimataifa na kuwa eneo la urithi wa dunia lenye hadhi tatu za kimataifa.

 


Kwa upande wake, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia huduma za utalii na masoko, Mariam Kobelo amebainisha kuwa ziara za viongozi na maafisa wa kidiplomasia wanaotembelea Ngorongoro zinachangia kuitangaza Tanzania kimataifa, kuimarisha ushirikiano katika sekta ya utalii, kuongeza ushirikiano kupitia diplomasia ya uchumi.

 

Happy Lazaro, Arusha.

Serikali imeweka bayana kuwa mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yatategemea kwa kiwango kikubwa mchango wa Mawakili wa Serikali, hususan katika kusimamia masuala ya kisheria yanayohusu miradi mikubwa ya maendeleo na uwekezaji.



Akifunga mafunzo maalumu ya siku tatu kwa Mawakili wa Serikali yaliyofanyika jijini Arusha, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Zainab Katimba, amesema wakati umefika kwa mawakili hao kuwa zaidi ya washauri wa sheria na kuwa wadau muhimu wa maendeleo ya Taifa kupitia utaalamu wao.



Ameeleza kuwa mafunzo hayo yamekusudiwa kuwajengea uwezo wa kukabiliana na changamoto mpya zinazojitokeza katika mazingira ya utawala na uchumi, huku akiwataka kutumia maarifa waliyoyapata kuboresha usimamizi wa mikataba, utoaji wa ushauri wa kisheria na utatuzi wa migogoro kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi.



Kwa mujibu wa Katimba, Serikali inahitaji wataalamu wa sheria wanaoweza kufanya uchambuzi wa kina, kufikiri kimkakati na kuhakikisha kila mkataba au uamuzi wa kisheria unalinda rasilimali za Taifa na kuchangia ukuaji wa uchumi.



Amesema anaamini washiriki wa mafunzo hayo watakuwa chachu ya mabadiliko katika taasisi wanazotoka na wataongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao, hatua itakayosaidia kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.



Naye Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Samwel M. Maneno, amesema programu hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ya taaluma ya sheria, ikijumuisha mada kuhusu mikataba ya kimkakati, ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), usimamizi wa vihatarishi vya kisheria, usuluhishi wa migogoro pamoja na matumizi ya Akili Unde (AI) katika utoaji wa huduma za kisheria.



Aidha, amewataka  Mawakili wa Serikali kuendelea kuyafanyia kazi maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu kuongeza ubora wa utendaji wa taaluma ya sheria, ikiwa ni pamoja na kusoma na kuyatumia mafunzo yaliyomo katika kitabu Mama Samia Doctrine of Law ili kuimarisha uchambuzi wa masuala ya kisheria na usimamizi wa mikataba ya Serikali.



Mafunzo hayo ya Bespoke 2026, yaliyobeba kaulimbiu "Repositioning State Attorneys for Strategic Legal Leadership in Realizing Tanzania Development Vision 2050," yaliwakutanisha Mawakili wa Serikali kutoka wizara, taasisi, wakala na mamlaka za serikali za mitaa kwa lengo la kuongeza ufanisi wa uongozi wa kisheria katika kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya Taifa.



 


Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro ikiongozwa na makamu Mwenyekiti Dkt. Harriet Mtae jana tarehe 11 julai, 2026 imekagua uboreshaji wa miundombinu ya utalii eneo la Nyayo za Laetoli lililopo hifadhi ya Ngorongoro 



Wakiwa Laetoli Wakurugenzi hao wamekagua uhifadhi wa Nyayo zilizogundulika katika eneo hilo miaka zaidi ya milioni 3.6 iliyopita na kuangalia hatua za utekelezaji wa mradi wa Geopark unaohusisha ujenzi wa jengo la kupokelea wageni, jengo la kupumzika wageni, jengo lililojengwa kwa ajili ya kuhifadhi Nyayo sambamba na miundombinu mingine.


Naibu Kamishna wa Uhifadhi Joas Makwati anayesimamia uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii ameeleza kuwa ziara hiyo imelenga kutathmini utekelezaji wa miradi inayofanywa na mamlaka kwa lengo la kuimarisha shughuli za uhifadhi, kuboresha huduma za utalii na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Hifadhi ya Ngorongoro.



Pamoja na kukagua miundombinu ya utalii wakurugenzi hao wamepokea taarifa ya hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na mipango ya kuendelea kuboresha mazingira ya utalii na shughuli za uhifadhi.


Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NCAA, Dkt. Harieth Mtae, alisema miradi hiyo inaakisi dhamira ya mamlaka ya kuendelea kuwekeza katika uboreshaji wa vivutio vya utalii na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wageni.





Ameongeza kuwa maboresho hayo yanatarajiwa kuongeza thamani ya vivutio vya utalii, kuvutia watalii zaidi na kuendelea kuitangaza Hifadhi ya Ngorongoro kama moja ya vivutio vinavyoongoza duniani.



 



Waziri wa maliasili na utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) leo tarehe 10 julai, 2026 amekutana na bodi ya wakurugenzi mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro katika ofisi za mamlaka hiyo zilizopo Karatu mkoani Arusha na kusisitiza umuhimu wa bodi hiyo kufuatilia kwa karibu shughuli zote za utendaji ili kuanza mwaka mpya wa fedha 2026/2027 kwa kasi na ufanisi.


Mhe. Kijaji amesema  kuwa bajeti ya mwaka mpya wa fedha inaanza na utekelezaji wa dira ya taifa ya maendeleo ya mwaka 2050 hivyo vikao vyake na bodi za taasisi zilizopo chini ya wizara vina lengo la kuanza utekelezaji wa dira, bajeti na ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa pamoja.


Ameitaka bodi hiyo kuongeza nguvu katika kuimarisha uhifadhi, kutangaza utalii  na kusimamia maendeleo ya jamii na kusisitiza kuwa jitihada hizo ziendane na kasi ya kukamilisha miundombinu wezeshi ikiwemo barabara kuu ya Loduare hadi Golini, kuimarisha mawasiliano ndani ya eneo lote la hifadhi, kukamilisha mradi wa fensi ya umeme ili kupunguza migongano kati ya wanyamapori na wananchi, kudhibiti ujangili na kuendelea kuimarisha mahusiano ya hifadhi na wananchi wanaoizunguka.


“Tulinde uhifadhi wa Ikolojia ya Ngorongoro kwa wivu mkubwa, tuendelee kubuni mazao mapya ya utalii na kuyatangaza, tujipange kikamilifu kuhakikisha Ngorongoro kama premium destination inawafikia na kuwashawishi wageni watakaohudhuria matukio ya AFCON, mkutano wa umoja wa Mabunge duniani, tuzo za  dunia za utalii na shindano la Miss world ambapo matukio yote yatafanyika Tanzania kati ya mwezi oktoba 2026 na Julai mwaka 2027”  amesisitiza Dkt. Kijaji.



Katibu wa Bodi, ambae ni kamishna wa Uhifadhi Ngorongoro Abdul-Razaq Badru amemueleza Mhe. waziri kuwa, Ngorongoro imepiga hatua ya kimageuzi kwenye mifumo ya kidijitali (ICT Transformation), uhifadhi endelevu kwa kuimarisha doria za kisasa, kuboresha miundombinu hasa barabara ya tabaka gumu kutoka geti la loduare hadi Seneto (km 29.5) kwa gharama ya TZS 80.3 bilioni  


Badru ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2025/26 eneo la Ngorongoro idadi ya watalii ilifikia 1,061,620 na fedha shilingi 269.5 Bilioni zilikusanywa. Ngorongoro imeendelea na jitihada za kulinda hadhi tatu za kimataifa kutoka UNESCO ambazo ni Urithi wa Dunia (World Heritage Site), Hifadhi ya Biosphere (Man and Biosphere Reserve), na Geopark ya Dunia (Ngorongoro-Lengai Global Geopark) ili ziendelee kuinufaisha nchi yetu.


Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi Ngorongoro Dkt. Harriet Mtae amemueleza Mhe waziri kuwa, katika kipindi cha miezi sita (06) iliyopita bodi ya Ngorongoro imetekeleza majukumu  kwa kuzingatia sheria, kanuni pamoja na maelekezo ya Serikali ili kuhakikisha Mamlaka inatekeleza kikamilifu dhamana yake ya kuhifadhi maliasili za Wanyamapori, malikale na urithi wa dunia, kuendeleza utalii endelevu na kuboresha shughuli za maendeleo ya jamii.

 


Tukio la Ngorongoro kuonesha vivutio vya utalii mubashara kupitia runings kubwa iliyofungwa katika banda la Wizara ya Maliasili na Utalii

limevutia wananchi wengi wanaotembelea  maonesho ya 50 ya biashara ya kimataifa jijini  Dar es Salaam kwa kuoneshwa maajabu yaliyopo Ngorongoro hususan Kreta ya Ngorongoro, makundi ya wanyama mbalimbali ikijumuisha pundamilia, nyumbu, swala, nyati na wanyama adimu kama  faru, simba, tembo na  na  chui na kujihisi kama wapo nyumbani Ngorongoro.



Afisa Uhusiano Mkuu wa Ngorongoro  Walter Mairo ameeleza kuwa  kupitia runinga iliyofungwa viwanja vya maonesho wageni wanaotembelea wanaona wanyama aina mbalimbali ndani ya Kreta, tambarare za Ndutu ambapo maisha ya Nyumbu kuzaliwa, kukua, kusafiri na kurejea na kuanza kizazi kipya kila mwaka


Mairo ameongeza kuwa, matukio mubashara yanaonesha wananchi jinsi teknolojia ya kidigitali na utalii wa asili vinavyoweza kushirikiana kuelimisha, kuburudisha na kuonyesha ushahidi kuwa Ngorongoro si tu hifadhi, bali ni jukwaa la kidunia linalounganisha urithi, biashara na teknolojia sehemu moja.


Karibu Sabasaba timu yetu yenye wabobezi na watopezi imejipanga kukupa  hadhithi za Ngorongoro zitakazokuduwaza kuwa Ngorongoro sio mahali pa kuangalia tu, bali mahali pa kuelewa, kujifunza na kuishi uzoefu usiosahaulika.

 



Na Mwandishi wa OTR


Kibaha, Pwani. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2 trilioni kama mapato yasiyo ya kodi katika mwaka huu wa fedha 2026/27, ikiwa ni zaidi ya lengo la Sh1.79 trilioni ambalo Serikali imeipa taasisi hiyo.



Akifungua Mkutano wa Pili wa Baraza la Wafanyakazi wa OTR uliofanyika Alhamisi, Julai 9, 2026, wilayani Kibaha, mkoani Pwani, Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, alisema kufikiwa kwa lengo hilo kutategemea kuongeza kasi ya utendaji, ubunifu, ushirikiano na uwajibikaji ndani ya OTR na katika taasisi na kampuni 308 zinazosimamiwa na ofisi hiyo.



"Ili tuweze kufikia lengo letu la kukusanya Sh2 trilioni katika mwaka wa fedha 2026/27, itatubidi tutanue mbavu na kutoa jasho zaidi," alisema Bw. Mchechu.


Alisisitiza kuwa mafanikio hayo yatawezekana ikiwa OTR itaendelea kujenga mazingira bora ya kazi, kuimarisha utamaduni wa taasisi unaovutia na kuhifadhi watumishi wenye uwezo, sambamba na kuhakikisha uwekezaji wa Serikali wenye thamani ya Sh92.3 trilioni unazalisha matokeo yanayoonekana kwa wananchi.



Katika mwaka wa fedha 2025/26, OTR ilikusanya Sh1.327 trilioni kama mapato yasiyo ya kodi, ikiwa ni ongezeko la asilimia 30 kutoka Sh1.028 trilioni zilizokusanywa mwaka 2024/25.



Kati ya kiasi hicho, gawio lilichangia Sh800.5 bilioni, sawa na asilimia 60 ya makusanyo yote; michango ya asilimia 15 ya mapato ghafi kutoka taasisi za umma zisizo za kibiashara ilifikia Sh406 bilioni, sawa na asilimia 30 ya makusanyo; huku mapato mengineyo, yakiwemo faida za uwekezaji na michango mingine inayotokana na umiliki wa Serikali, yakifikia Sh121.5 bilioni, sawa na asilimia 10 ya makusanyo yote.


"Wajibu wetu sasa ni kulinda mafanikio haya na kutoridhika na tulipofika. Tunapaswa kuhakikisha OTR inakuwa taasisi yenye uwezo na utayari wa kutekeleza wajibu wake mkubwa zaidi katika kusimamia uwekezaji wa umma na kuchangia utekelezaji wa Dira 2050," alisema.


Alisema tangu kuanza kwa mwaka mpya wa fedha Julai 1, 2026, matarajio ya Serikali, wananchi na wadau kuhusu mchango wa OTR katika uchumi yameongezeka.


"Ofisi ya Msajili wa Hazina ina ahadi na wajibu mkubwa kwa Serikali wa kuvuka viwango vya sasa vya gawio na michango, kuendelea kuongeza thamani ya uwekezaji wa Serikali na kuhakikisha mapato yasiyo ya kodi yanaendelea kukua," alisema.


Bw. Mchechu alisema azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni kuongeza mchango wa mapato yasiyo ya kodi hadi kufikia asilimia 10 ya mapato yote ya Serikali ifikapo mwaka 2030, kutoka wastani wa sasa wa takribani asilimia tatu.


Alisema kufikia lengo hilo kutahitaji taasisi zinazosimamiwa na OTR kuongeza tija, ufanisi na mapato, kuimarisha nidhamu ya kifedha, kupunguza utegemezi usio wa lazima kwa Serikali, pamoja na OTR yenyewe kuongeza ubora, kasi na ufanisi wa usimamizi wake.


"Hii ni ahadi kubwa, na utekelezaji wake unategemea mchango wa kila mmoja wetu," alisisitiza.

Aliwataka watumishi kuongeza ubunifu katika utekelezaji wa majukumu yao, kufanya kazi kwa kasi, ubora na ufanisi, kutumia teknolojia na takwimu kufanya maamuzi bora, kuimarisha utamaduni wa uwajibikaji na ushirikiano, kuendelea kujifunza na kujenga uwezo, pamoja na kusimamia kwa uadilifu matumizi ya rasilimali za umma.


"Kila mtumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina anapaswa kuona uhusiano wa moja kwa moja kati ya kazi anayofanya na matokeo yanayotarajiwa na Taifa," alisema.


Akizungumza Juni 30, 2026, wakati wa kupokea gawio na michango ya Sh1.327 trilioni kutoka OTR, Rais Dkt. Samia aliitaka taasisi hiyo kuhakikisha mashirika na taasisi za umma zinaongeza tija, ufanisi na ushindani, huku zikipunguza utegemezi wa ruzuku za Serikali na kuimarisha uwezo wa kujitegemea kifedha.


"Mafanikio haya yasitufanye turidhike. Uwekezaji wa umma ni mkubwa na matarajio ya wananchi ni makubwa zaidi," alisema Rais Samia.


Alionya kuwa taasisi zinazofanya vizuri zisifiche udhaifu wa zile zinazosuasua.


"Kila taasisi iliyokabidhiwa mali za umma inapaswa kujieleza kwa lugha ya matokeo: imezalisha nini, imeongeza thamani kiasi gani, imechangia mapato kiasi gani, na imepunguza kwa kiwango gani utegemezi wake kwa Serikali," alisema.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mipango, Utafiti na Maendeleo wa OTR, Bw. Emanuel Luvanda, alisema utekelezaji wa Mpango Mkakati wa OTR wa mwaka 2026/27–2030/31 utaweka mkazo katika kuimarisha utawala bora, uongozi na usimamizi wa rasilimali watu, usimamizi wa utendaji, uhamasishaji wa rasilimali, kuboresha uwekezaji, ushirikishwaji wa wadau na kuijengea taasisi uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Aliyasema hayo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na vipaumbele vya Mpango Mkakati wa OTR mbele ya Baraza la Wafanyakazi.


Naye Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Chacha Marigiri, alisema OTR itaendelea kuwawezesha watumishi kuongeza elimu na ujuzi kupitia mafunzo na kujiendeleza kimasomo ili kuboresha utendaji na kuongeza tija.


"Tutaendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa watumishi wetu," alisema, huku akisisitiza kuwa hakutakuwa na nafasi kwa watumishi wavivu na wazembe.


 



mwandishi wetu,Arusha.


Shirika la Kimataifa la watetezi wa haki za binaadamu, Defend Defenders  limeipa Shirika la wanahabari ya kusaidia jamii za asili(MAIPAC) vifaa vya Ofisi ili kurahisisha utendaji kazi kwa kidigitari.



Vifaa hivyo, vipya vya kisasa vimekabidhiwa leo Julai 9,2026 MAIPAC na  Kampuni ya uuzaji wa vifaa vya kidigitari ya Soud& Vision Ltd ya jijini Arusha,baada ya kulipiwa na shirika hilo la kimataifa.


Defend Defenders kabla ya kutoa msaada huo kwa MAIPAC ,lilifanya ukaguzi wa usalama wa TEHAMA kwa mashirika mbalimbali katika ukanda wa Afrika ya Mashariki na hivyo, kubaini MAIPAC kuwa na uhitaji wa vifaa vya kisasa vya ofisi na MAIPAC kuomba msaada huo.



Akizungumza baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa MAIPAC, Mussa Juma amesema, vifaa hivyo vitasaidia sana utendaji kazi wa MAIPAC na utunzwaji wa kanzi data kwa muda mrefu.


"Tunawashukuru sana Defend Defenders kwa msaada huu mkubwa, ambao sasa utawezesha MAIPAC kuboresha utendaji kazi na mfumo wa usalama kidigitari ili kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi na wanachama wake"amesema


Amesema Defend Defenders ni shirika ambalo limekuwa na mahusiano kwa muda sasa na MAIPAC kwani tayari liliwahi kutoa mafunzo kwa wanahabari kuhusiana na masuala ya Kisaikolojia  na ustawi kwa wanahabari na pia masuala ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii na masuala ya utafutaji rasilimali kwa Asasi za kiraia.


"Defend Defenders wamekuwa wadau wetu wakubwa na tumekuwa na ushirikiano mzuri tangu, tulipounganishwa na Mtandao wa watetezi wa haki za binaadamu nchini(THRDC),kupitia mafunzo mbali mbali ya uboreshwaji utendaji kazi kwa watetezi wa haki za binaadamu"amesema


Juma alieleza kumshukuru sana Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo, Hassan Shire kwa misaada mbali mbali kwa MAIPAC na mashirika mengine  na kuomba ushirikiano huo kuendelea kuimarishwa zaidi ili kukabiliana na changamoto wanazokabiliana nazo watetezi wa haki za binaadamu.


Kwa upande wake, Meneja Utawala wa MAIPAC, Andrea Ngobole alisema,msaada huo pia utasaidia utunzwaji mzuri wakumbukumbu za wanachama wake ambao ni wanahabari na hivyo, kuwezesha kupatiwa mafunzo mara kwa mara kulingana na mahitaji.


Awali,Msimamizi wa mifumo ya TEHAMA wa Defend Defenders Hillary Kahoza alipotembelea MAIPAC alishauri uboreshwaji wa mifumo wa TEHAMA ili kuhifadhi vyema taarifa na kujilinda na wadukuzi mitandaoni.


Hata hivyo, Kahoza alipongeza shirika la MAIPAC kwa kazi nzuri linazofanya hasa katika kutoa elimu kwa wanahabari na wananchi ya jamii za asili kuhusiana na matumizi sahihi ya mitandao na masuala ya usalama katika mitandao na uzingatiaji wa sheria katika matumizi ya mitandao ya kijamii.


Shirika MAIPAC limekuwa na miradi kadhaa ikiwepo mradi wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa maarifa ya asili mradi uliofadhiliwa na shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP) kupitia programu ya miradi midogo ya mfuko wa mazingira duniani(GEF) na Ofisi ya makamu wa Rais(mazingira), Mradi wa kupinga ukeketaji wilayani Longido,Mradi wa utunzaji vyuanzo vya maji kijiji cha Selela wilaya ya Monduli mradi wa ujuzi wa kidigitari kwa wanafunzi wa kike.


Kwa wanahabari MAIPAC imekuwa na mradi wa kufundisha wanahabari uandishi wa habari za amani,mradi kukabiliana na magonjwa ya mlipuko, ,mradi wa kuwafundisha wanahabari 140 nchi nzima uandishi wa mazingira na sheria zake, unofadhiliwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni(UNESCO)


MAIPAC pia limekuwa shirika la kwanza nchini, kuandaa Kitabu juu ya umuhimu wa maarifa ya asili katika utunzwaji wa mazingira,kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi  na utunzwaji wa vyanzo vya maji,kitabu ambacho kimesambazwa bure kwa lengo ya kushawishi maarifa ya asili ambayo kila jamii inayo yaunganishwe na maarifa ya kisasa  na kutumiwa na watungaji ya sera kwa manufaa ya taifa.





ARUSHA, TANZANIA – Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), ametoa maagizo sita makuu kwa Kamishna mpya wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Massana Gibril Mwishawa, akimtaka kuimarisha utendaji na kuhakikisha sekta ya utalii inaongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi wa taifa.


Waziri Kijaji alitoa maagizo hayo leo Julai 9, 2026, jijini Arusha wakati akiongoza hafla ya uapisho wa Kamishna Mwishawa. Kabla ya uteuzi wake uliofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mnamo Julai 2, 2026, Mwishawa alikuwa akihudumu kama Naibu Kamishna wa Uhifadhi wa shirika hilo. Anachukua nafasi ya Kamishna Mstaafu, CPA Musa Nassoro Kuji, ambaye amemaliza muda wake wa utumishi.

Maagizo Sita ya Waziri Kijaji



Katika hotuba yake, Waziri Kijaji alimtaka kiongozi huyo mpya kuelekeza nguvu na weledi katika maeneo yafuatayo:
  1. Kusimamia na kuboresha miundombinu ndani ya hifadhi zote nchini.
  2. Kuvutia na kuongeza fursa za uwekezaji wa kimkakati.
  3. Kubuni na kuanzisha bidhaa mpya za utalii ili kuongeza mnyororo wa thamani.
  4. Kusimamia mapato kwa ufanisi mkubwa ili kuzuia upotevu.
  5. Kuimarisha uhusiano mwema na jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi.
  6. Kusimamia nidhamu, uadilifu, weledi na ustawi wa watumishi, ikiwemo kulipa maslahi yao kwa wakati.
"Ushirikiano na wananchi wanaozunguka hifadhi ni nguzo muhimu sana katika kulinda rasilimali hizi za taifa," alisisitiza Waziri Kijaji.

Kauli ya Bodi ya Wadhamini



Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA, Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali George Waitara, aliahidi kuwa bodi yake itaendelea kutoa ushirikiano na miongozo thabiti kwa menejimenti ili kufikia malengo yaliyowekwa. Jenerali Waitara aligusia pia umuhimu wa uwazi, akitaka utoaji wa mrejesho wa utendaji kazi uhusishe maafisa na askari wa ngazi zote ili kuongeza ufanisi.

Shukrani na Ahadi ya Kamishna Mpya



Akizungumza baada ya kula kiapo, Kamishna wa Uhifadhi, Massana Gibril Mwishawa, alieleza kuwa hifadhi za taifa ni hazina kubwa ya kiikolojia, kiuchumi na kijamii ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kwenye mapato ya serikali na miradi ya kimkakati kama ufuaji wa umeme.
Alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumpa dhamana hiyo kubwa, huku akiahidi kuiongoza TANAPA kwa misingi ya uzalendo, uwajibikaji na uadilifu.


"Nitaingiza nguvu mpya kwa kushirikiana kwa karibu na watumishi wote wa TANAPA ili kuendeleza na kuimarisha mafanikio ya taasisi yetu," alisema Kamishna Mwishawa.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, viongozi wa dini, wadau wa utalii, pamoja na wakuu wa taasisi nyingine za uhifadhi nchini.



 



Katika Viwanja vya Sabasaba, timu ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ikiongozwa na Kamishna wa Uhifadhi Abdul-Razaq Badru tarehe 6 June, 2026 ilivifunika viwanja hivyo huku macho na masikio ya wananchi waliotembelea yakijielekeza kwenye Kampeni ya Ngorongoro inayojulikana kama Karibu Nyumbani.



Akizungumza na Waandishi wa Habari katika siku maalum ya Ngorongoro, Kamishna Badru amewaeleza kuwa umuhimu wa kampeni hiyo inatokana na historia kwa kuainisha wazi kuwa binadamu wa kale kutembea kwa miguu miwili historia yake alipatikana ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.


Ameeleza kuwa ushahidi uliopo wa zaidi ya miaka milioni 3.6 unaonesha binadamu huyo aliweza kutembea na kufanya shughuli zake kwa kutumia zana za miaka hiyo, kuyatawala mazingira na kuishi bila shida yoyote.


Mhifadhi Mambokale wa Ngorongoro Ladislaus Kashaija akitoa maelezo kuhusu kwanini Ngorongoro inajivunia historia hiyo ameeleza kuwa inatokana na ushahidi wa wanazuoni duniani kote kuitaja Ngorongoro kama sehemu yenye ushahidi wa kutosha kuhusu historia ya binadamu.


Mchezaji wa timu ya soka ya Simba Shomari Kapombe amesema kuwa atakuwa chachu ya luwashawishi wanasoka wenzie kuitangaza Ngorongoro kuwa chanzo cha mpira wa miguu kwa kuwa historia ya binadamu kutembea kwa miguu miwili imeanzia hapo.


Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro imeshiriki tukio la siku ya Ngorongoro (Ngorongoro Day) katika viwanja vya sabasaba kwa kuhamasisha washiriki warudi Nyumbani Ngorongoro kwani mwenda kwao si mtumwa.

 


The tourism and art sectors in Tanzania are poised for a significant economic boost this October following the announcement of the upcoming Arts and Crafts Festival. This major event is specifically designed to stimulate the creative economy and showcase the country’s unique cultural heritage. Through this strategic platform, local artisans will gain exclusive opportunities to access new commercial markets both domestically and internationally.



Preparations for the festival are being spearheaded by the Tanzania International Tourism Festival (TITF) in collaboration with the Tanzania Federation of Crafts and Arts (TASFA). This strategic partnership aims to bring together sculptors, painters, fashion designers, jewelers, and potters from various regions across the country. This collective gathering of artisans will create a unified force to showcase the rich tapestry of Tanzania’s cultural legacy.



The Director of TITF, Ibrahim Jamal, officially announced the event during a press briefing held at the Grand Melia Hotel in Arusha. In his remarks, Jamal emphasized that the festival is built on a vision to integrate the art and tourism sectors. The primary goal of this strategy is to add tangible value to local creative works and provide sustainable economic opportunities for artists.

Beyond conventional product exhibitions, the festival will feature specialized capacity-building sessions driven by professional training. Attending artists will receive expert guidance on how to enhance the value and quality of their products to compete effectively in the global marketplace. Additionally, they will be trained on intellectual property rights protection and modern marketing strategies to penetrate foreign markets via the tourism sector.

Jamal added that the festival will serve as a dynamic, live platform where artisans can display and sell their products on the spot. This will provide an excellent opportunity for them to exchange experiences, learn innovative production techniques, and strengthen the creative economy value chain. The event is highly anticipated to inspire a renewed commitment to high-quality, productive manufacturing among local creators.

The festival itinerary is set to be highly engaging, featuring live art production demonstrations. Visitors will have the opportunity to experience professional workshops, business training, strategic networking sessions, and traditional music and dance performances. These business-to-business (B2B) meetings will connect artists directly with high-profile buyers and investors from diverse corporate sectors.



Furthermore, Joseph Rumanyika from TITF noted that the platform is expected to attract key stakeholders in art, tourism, and culture from both within Tanzania and abroad. 


The presence of international participants will position this festival as a vital bridge for promoting Tanzania globally through its unique handicrafts. Rumanyika believes that artistic heritage plays a pivotal role in boosting the country's cultural tourism brand.

Representing the artist community, Simon Venance commended the initiative, stating that the festival continues to build essential business and entrepreneurial skills among local creators. 


He concluded by highlighting that art is a reliable source of employment and income, and this festival will help them secure new markets to elevate their livelihoods. Venance firmly believes that creative works will carry the true identity and economic progress of Tanzanian artisans.