Happy Lazaro,Arusha .



MBALI na ubunifu wa teknolojia za kilimo na mifugo unaoendelea kuonyeshwa katika Maonesho ya Nanenane, wageni wanaotembelea viwanja hivyo wamepata pia nafasi ya kufanya safari ya kipekee ya ladha kupitia vyakula vinavyobeba utamaduni wa mataifa mbalimbali katika banda la Cheesy Bite lililopo Nanenane Njiro .


Katika kona moja ya maonesho hayo, harufu ya vyakula vinavyoandaliwa kwa ustadi huwavutia wageni kusimama, kuonja na kujionea namna sekta ya utalii wa chakula (food tourism) inavyozidi kukua nchini. Wengi huchukua muda kupumzika na kufurahia milo yenye mchanganyiko wa mapishi ya kisasa yanayokidhi ladha tofauti za wateja.



Akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonesho hayo ,Mmoja wa wafanyakazi katika katika hoteli hiyo, Maryam Mlau , amesema wameamua kuandaa menu inayowapa wageni uzoefu wa kuonja vyakula vya asili tofauti bila kulazimika kusafiri nje ya Tanzania.


 Maryam ameeleza kuwa wageni hupata fursa ya kufurahia vyakula kama Chicken Loaded Fries, Beef Loaded Fries, Halloumi Loaded Fries pamoja na burger za nyama ya ng'ombe na kuku ambazo zimekuwa zikivutia wengi.



Ameongeza kuwa, si Watanzania pekee wanaovutiwa na vyakula hivyo, bali pia wageni kutoka mataifa mbalimbali wanaotembelea maonesho hayo, jambo linaloonyesha kuwa chakula kimeendelea kuwa sehemu muhimu ya utalii na uzoefu wa msafiri anapotembelea eneo jipya.



Amesema kuwa,mazingira mazuri, huduma zenye ukarimu na kuzingatia viwango vya usafi vimechangia kuwafanya wageni wengi kurejea tena, huku baadhi yao wakichagua kutumia huduma ya kusafirishiwa chakula pale wanaposhindwa kufika moja kwa moja.



"Wadau wa utalii wanaeleza kuwa utalii wa chakula unaendelea kushika kasi duniani, ambapo wageni hutafuta sio tu vivutio vya asili na utamaduni, bali pia ladha zinazotofautisha eneo moja na jingine"amesema Maryam.

 


"Hali hiyo imeifanya sekta ya huduma za chakula kuwa sehemu muhimu ya kuongeza thamani ya maonesho makubwa kama Nanenane."amesema Maryam .



"Kadri maonesho hayo yanavyoendelea, wageni wanaondoka wakiwa si tu na maarifa mapya kuhusu kilimo na mifugo, bali pia na kumbukumbu za ladha mbalimbali walizozionja, jambo linaloifanya Nanenane kuwa zaidi ya maonesho ya uzalishaji—bali pia jukwaa la kukutanisha tamaduni kupitia chakula."amesema 



 


By Happy Lazaro, Arusha.



Farmers have been encouraged to visit the Corteva Agriscience pavilion at the ongoing Nanenane Agricultural Exhibition at Themi Grounds in Arusha to acquire knowledge on the use of improved maize seed varieties, receive professional agronomic advice, and explore modern agricultural technologies aimed at increasing maize productivity and yields across Tanzania.



The call was made by Corteva Agriscience Agronomist Fikiri Kalobelo while speaking to journalists about the technologies and innovations the company is showcasing during this year's exhibition.



 He said Corteva is participating in the event to demonstrate its advanced Pioneer maize seed technologies, which are specifically developed to suit different agro-ecological zones across the country.



Kalobelo explained that the company is committed to ensuring that every farmer visiting the Corteva pavilion receives quality services, technical support, and comprehensive knowledge on modern maize production.


 Farmers are being trained on every stage of maize cultivation, from selecting the right seed varieties and applying proper agronomic practices to adopting technologies that enhance productivity and maximize yields.



"Our objective is to empower farmers with technologies and farming practices that enable them to achieve higher yields and better-quality harvests," he said.



For Tanzania's lowland production zones, Corteva recommends the Pioneer P2848W hybrid, which matures within 80 to 90 days and can produce an average yield of 25 to 30 bags per acre when recommended agronomic practices are followed.



For the medium rainfall zones, the company is promoting Pioneer P3531W and PHB 30G19 hybrids, which have the potential to produce between 35 and 40 bags per acre.


 According to Kalobelo, these hybrids produce hard and heavy kernels, giving farmers greater economic value under the current grain marketing system, where maize is traded based on weight rather than volume. He added that these varieties are also ideal for roasting and have become highly preferred by both fresh maize traders and consumers.



"These varieties remain fresh for longer after harvest without losing quality, giving both farmers and traders greater market confidence and better returns," Kalobelo noted.



For areas receiving moderate to high rainfall, Corteva recommends the Pioneer P3812W hybrid, which has been developed to perform well under such conditions.


 The variety can produce between 35 and 40 bags per acre while offering strong tolerance to leaf diseases and ear rot commonly associated with excessive rainfall.



Kalobelo explained that Pioneer P3812W matures within 115 to 125 days and consistently produces high-quality grain, helping farmers minimize losses caused by prolonged rains. He added that Corteva remains committed to supplying improved seed varieties and professional agronomic support to enhance agricultural productivity nationwide.


Besides Pioneer maize hybrids, Corteva also supplies Pannar maize seed varieties suitable for all production zones in Tanzania. 


For lowland and low-rainfall areas, the company recommends PAN 3M-05, which matures within 75 to 80 days and yields between 25 and 30 bags per acre. The variety is characterized by strong stalks and performs well in both low and moderate rainfall conditions.



For the medium production zones, Corteva recommends PAN 53, a variety well known for producing sweet maize suitable for roasting. The hybrid yields between 35 and 40 bags per acre and has strong stalks that withstand different growing conditions.


 Kalobelo said PAN 53 was specifically developed to withstand the effects of climate change and performs well in areas receiving moderate to high rainfall while still producing good harvests even when rainfall is below normal.



For the highland production zones, Kalobelo highlighted PAN 9M-91, popularly known as "The Real Answer" because of its outstanding performance and high yield potential. He described it as a new hybrid that produces abundant harvests with hard and heavy kernels.



In addition, Corteva has prepared trial seed packs (Funpacks) for selected farmers while collecting their contact information to enable continuous technical support even after the exhibition concludes. Kalobelo emphasized that the company's commitment to farmers extends beyond selling seed, focusing instead on continuous follow-up and professional guidance to help farmers achieve their production goals.



"That is why we say Corteva enriches lives. Our mission is not simply to sell seed but to transform farmers' livelihoods through improved seed varieties and the right agricultural technologies," he said.



He added that Corteva's culture is built on maintaining close relationships with farmers by providing continuous training and technical assistance, making the company a trusted partner in improving agricultural productivity and enhancing farmers' livelihoods.



 


Happy Lazaro,Arusha.


Wananchi wametakiwa kutumia bidhaa za umeme jua kutoka kampuni ya teknolojia ya  ZOLA ELETRIC kwa ajili ya matumizi mbalimbali kwani  bidhaa hizo  zina ubora wa hali ya juu .



Hayo yamesemwa  jijini Arusha na Afisa masoko wa kampuni hiyo Moses Vikael wakati akizungumza katika mbio za Redcross Marathon Arusha zilizofanyika katika uwanja wa Stadium jijini Arusha .



 "Tunafanya kazi ya uuzaji na usambazaji wa sola katika maeneo mbalimbali nchini kupitia mtandao wa mawakala wetu, kuanzia mijini hadi vijijini, na katika sekta zote za biashara, taasisi na makazi ya wananchi."amesema Moses.



"Lengo letu ni kuhakikisha kila eneo lenye uhitaji wa nishati linapata suluhisho bora la umeme wa jua kutoka kampuni yetu "amesema Moses.



Moses ameongeza  kuwa,kitendo hicho kilichofanywa na Redcross ni mfano wa kuigwa kwani kwa mara ya kwanza wameweza kufanya mbio hizo kwa mkoa wa Arusha jambo ambalo limeweza kuleta hamasa kubwa kwa wananchi wa Arusha .


"Tunashukuru sana kwa namna ambavyo.Redcross mmeweza kutupa mwaliko wa kuwa wafadhili katika jambo hili na tunawaahidi kuendelea kushirikiana na nyie katika kila hatua "amesema  Moses.



Aidha ametoa wito kwa wananchi mbalimbali kiwa na tamaduni za kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zao kwani michezo ni afya na inasaidia kuondokana na maradhi mbalimbali ambayo yangeweza kutokea .




 



Happy Lazaro,Arusha .


WAKULIMA  kanda ya kaskazini wametakiwa kutembelea banda la kampuni ya Kibo Seed katika maonesho ya nanenane ili kuweza kupata elimu  kuhusu matumizi ya  mbegu bora za mahindi na mbogamboga ili kuongeza uzalishaji.




 Hayo yamesemwa leo jijini Arusha na Afisa Uzalishaji wa Mbegu wa  kampuni ya Kibo Seed Co.Ltd ,Marko Msheishiwa wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonesho ya  nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Taso Njiro.


 Amesema  kampuni hiyo inashiriki Maonyesho ya Nanenane 2026 ikiwa na lengo la kuwaelimisha wakulima kuhusu matumizi ya mbegu bora za mahindi na mbogamboga ili kuongeza uzalishaji.



Ameongeza kuwa ,kampuni hiyo  inazalisha na kusambaza mbegu za mahindi kwa kanda mbalimbali za kilimo nchini, zikiwemo kanda ya chini, ya kati na ya juu, ili kuhakikisha kila mkulima anapata mbegu zinazolingana na mazingira yake.



Akizungumzia maandalizi ya maonesho ya mwaka huu, Msheishiwa amesema yameboreshwa zaidi kuliko miaka iliyopita, ambapo mazao ya maonesho yalipandwa kwa wakati, yakatunzwa vizuri na sasa yanaonyesha matokeo halisi ambayo yatawawezesha wakulima kujifunza kwa vitendo.


Ameongeza  kuwa, moja ya sifa zinazotofautisha mbegu za Kibo Seed na kampuni nyingine ni ubora wake, hususan kwa mahindi yanayofaa kuchomwa na kukobolewa, ambayo ni matamu na yanakubalika na watumiaji wengi.


Kwa upande wa uzalishaji, amesema mavuno hutegemea ukanda na aina ya mbegu inayotumika. Mbegu za ukanda wa chini zinaweza kutoa tani 2 hadi 2.5 kwa ekari, ukanda wa kati tani 3 hadi 3.5, huku ukanda wa juu ukifikia tani 4 hadi 5 endapo mkulima atafuata kanuni bora za kilimo.


Aidha, amesema changamoto kubwa inayowakabili baadhi ya wakulima ni kutokuchagua mbegu sahihi kulingana na ukanda wao wa kilimo pamoja na kutofuata kanuni za uzalishaji, ikiwemo kupanda kwa wakati, kutumia mbolea stahiki na kutunza shamba ipasavyo.


Aidha Msheishiwa ametoa wito kwa wakulima na wananchi kutembelea banda la Kibo Seed katika maonyesho ya Nanenane jijini Arusha ili kupata elimu kuhusu mbegu bora, kuona mashamba ya mfano na kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa kampuni hiyo.

 



Unaweza kusema dili limetiki kufuatia klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam kuchagua kivutio namba moja cha utalii barani Africa kufanya uzinduzi wa wiki ya simba na jezi mpya ya mnyama kwa mwaka 2026.



Uzinduzi uliofanyika leo tarehe 1 Agosti, 2026 eneo la Ngoitoktok katika kasoko ya Ngorongoro ulipambwa na upepo mwanana unaotokana na mawimbi kutoka bwawa la Ngoitoktok likipambwa na Viboko wanaogelea huku ulinzi ukiimarishwa na familia za Simba waliosheheni kreta ya Ngorongoro.



Akizungumzia tukio hilo la kihistoria lililojumuisha uzinduzi wa logo ya miaka 90 ya Simba ulihudhuriwa na menejimenti ya Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro iliyoongozwa na Naibu Kamishna huduma za Shirika Aidan Makala na mashabiki zaidi ya 300 kutoka ndani na nje ya Nchi.



“Tukio hili ni matokeo chanya kati ya ushirikiano wa Klabu ya Simba na hifadhi ya Ngorongoro, tumetangaza utalii wa ndani, wanasimba wamerudi nyumbani lakini kubwa zaidi ni kuchagiza utalii wa michezo kuelekea mashindano ya AFCON ya mwaka 2027 yatakayofanyika hapa Nchini” Naibu Kamishna Aidan Makala.



Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba Ahmed Ally amebainisha kuwa Ngorongoro ni zaidi ya hifadhi, ina vivutio vingi vya utalii ambapo asili, urithi wa utamaduni na malikale vinaishi pamoja, hivyo Simba kufanya uzinduzi huo ndani ya hifadhi ni kurudisha mashabiki nyumbani na kuwadhihirishia kuwa ndoto, maono na hisia zao zinakutana na uhalisia uliopo Ngorongoro.





















 


Na Queen Lema, Arusha

 

MKOA wa Arusha unatarajiwa kusimama miguu yote miwili kesho Agosti Mosi, wakati Princess Lounge, moja ya kumbi maarufu na zenye mvuto mkubwa wa kipekee barani Afrika Mashariki, itakapofanya maadhimisho makubwa ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.


 Akizungumza kuelekea tukio hilo la kihistoria, Mkurugenzi wa Princess Lounge, Catherine Urasa, amesema wameandaa sherehe kubwa na ya kukata na shoka itakayoweka historia mpya ya burudani mkoani Arusha.

Catherine amebainisha kuwa tangu kuanzishwa kwake, Princess imekuwa nguzo kuu na kichocheo kikubwa cha sekta ya burudani, huku ikisifika kwa kulisha vyema hisia za wapenda bata na starehe mkoani hapa.

Alieleza kuwa kwa kuzingatia Arusha ni kitovu cha utalii nchini, Princess Lounge imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwenda sambamba na hadhi hiyo kwa kutoa burudani na huduma za kiwango cha kimataifa zinazovutia wageni wa ndani na nje ya nchi.


"Tunatimiza mwaka mmoja sasa wenye mafanikio makubwa sana. Tunafurahi kwa upendo na mapokezi tuliyopata, na tunapenda kuwaahidi wateja wetu kuwa tumejipanga vyema zaidi kuendeleza na kuiboresha sekta hii ya burudani kwa viwango vya juu zaidi," alisema kwa kujiamini Catherine.


Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo amejivunia namna biashara hiyo ilivyoweza kuwa mkombozi kwa vijana kwa kutengeneza fursa za ajira kwa wale ambao hapo awali hawakuwa na kazi kabisa.


"Kama mnavyojionea wenyewe, hapa tuna mabinti warembo na wachapakazi ambao ni sehemu ya nembo yetu. Pia tuna vijana mahiri wa muziki (DJs) na wataalamu wa kuchoma nyama tamu na zenye ladha ya kipekee, ambao wote kwa pamoja ndio siri na nguzo ya mafanikio ya Princess," aliongeza.


Kufuatia hatua hiyo, Catherine ametoa wito na mwaliko rasmi kwa Watanzania wote na wakazi wa jiji la Arusha kujitokeza kwa wingi kesho kusherehekea kwa pamoja mafanikio hayo, ambapo kutakuwa na mfululizo wa burudani za kusisimua, vinywaji vya kila aina, na vyakula vya kutosha.



Maafisa na askari  wa jeshi la Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro waliopoteza maisha, kujeruhiwa na kufanya kazi kwa uhodari wametunukiwa vyeti na fedha kutokana na kujitoa kwao kwa hali na mali kulinda rasilimali za wanyamapori na misitu.



Tuzo hizo zimetolewa tarehe 31 Julai 2026 kwenye maadhimisho ya  siku ya  askari wanyamapori duniani ambayo huadhimishwa kwa lengo la kuutambua mchango wa  askari hao katika kulinda rasilimali za nchi na kuenzi mchango wa Askari 10 waliopoteza maisha yao na kujeruhiwa wakiwa kazini katika hifadhi ya Ngorongoro.



Naibu kamishna wa Uhifadhi huduma za shirika Aidan Makala  amewapongeza askari wote wa jeshi la uhifadhi kutokana na  kujitoa kwa hali na mali katika kazi hiyo huku akiwasisitiza kufanya kazi kwa kushirikiana na wananchi ili kulinda matakwa ya haki jinai.



Naibu Kamishna Makala ameleza kuwa,  askari  wa  uhifadhi ni nguzo ya ulinzi wa rasilimali za wanyamapori  na misitu ambapo  kazi hiyo haiishii kukabiliana na ujangili pekee  bali inakwenda sambamba na kudhibiti uharibifu wa mazingira hususan vyanzo vya maji, ulinzi wa maisha na mali za watu dhidi ya wanyamapori wakali na waharibifu na kuelimisha jamii kutunza rasilimali hizo.

 


Akielezea kuhusu maadhimisho ya siku ya  askari wanyamapori duniani, Afisa Uhifadhi mkuu anayesimamia idara ya huduma za Ulinzi Bw. Emmaanuel Kaaya amesema kuwa Siku hiyo ilianza kuadhimishwa mwaka 2007, kwa ushirikiano baina ya Shirikisho la Kimataifa la Askari wa Wanyamapori (International Rangers Federation - IRF) na mashirika mengine ya kimataifa. 


Lengo la kuanzishwa kwa maadhimisho haya ni kuutambua mchango wa Askari wa Wanyamapori na kuuenzi mchango wa Askari waliopoteza maisha wakiwa kazini. Ni siku ya kuwatambua na kuenzi mchango wa mashujaa wanaojitolea kila siku kuhakikisha hifadhi zetu zinaendelea kuwa salama kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.


Kwa upande wake kamishna msaidizi mwandamizi wa Uhifadhi Gloria Bideberi amebainisha kuwa katika maadhimisho haya, Mamlaka imetoa vyeti na fedha taslimu  kwa zaidi ya watumishi 30 ikiwa ni sehemu ya kuutambua mchango wao katika kazi kwa kipindi cha mwaka 2025/26.


Maadhimisho hayo yalipambwa na michezo mbalimbali iliyojumuisha  mpira wa miguu, kukimbiza kuku, mazoezi ya viungo na maonesho ya kwata mbalimbali.

 



Mkuu wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Gabriel Makalla, ametoa agizo zito kwa wananchi wote waliolipwa fidia kupisha ujenzi wa miundombinu ya barabara za kujiandaa na Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON 2027). 

Agizo hilo linalenga kumpa nafasi mkandarasi kuendelea na kazi hiyo bila vikwazo.


Makalla alitoa agizo hilo kufuatia ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi na upanuzi wa miundombinu hiyo yenye urefu wa kilometa 9.1. Mradi huu mkubwa unatekelezwa kwa njia nne na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilioni 87.9.

Maeneo Yanayohusika na Upanuzi wa Barabara
Mradi huo unajumuisha maeneo muhimu yafuatayo jijini Arusha:

  • Makutano ya Ngarenaro – Mzunguko wa Kisongo
  • Makutano ya Ngarenaro – Kona ya Nairobi

  • Makutano ya Ngarenaro – Soko la Kilombero
  • Kauli ya RC CPA Amos Makalla
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Makalla alimshukuru Rais kwa kutoa fedha hizo na kuwasihi wadau wote kushirikiana ili kukamilisha mradi huo kwa wakati.

"Nimshukuru  Rais kwa kuwezesha ujenzi wa barabara hizi, niwaombe watalamu wa sekta zote kutoa ushirikiano kuhakikisha hakuna kizuizi kwa Mkandarasi kufanya kazi. Serikali ishawalipa fidia wananchi wote kwa barabara zote za AFCON. Zaidi ninawashukuru ambao wameshaondoka, wameonesha uzalendo, na ambao hawajaondoka niwaombe waondoke ili kupisha ujenzi."

Manufaa Makubwa ya Mradi Huu Jijini Arusha
Kukamilika kwa miundombinu hii kutaleta mapinduzi makubwa kiuchumi na kijamii katika Jiji la Arusha:
Kuchochea Utalii na AFCON 2027: Barabara hizi zitakuwa kiungo muhimu wakati wa michuano na zitaboresha sekta ya utalii.
  1. Kupunguza Msongamano: Zitasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto ya foleni za magari jijini Arusha.
  2. Kutokomeza Mafuriko: Meneja wa TANROADS Mkoa wa Arusha, Mhandisi Reginald Massawe, amebainisha kuwa mradi huu utajenga mitaro mikubwa ya kupeleka maji Mto TANAPA. Hii itaondoa kabisa kero ya mafuriko katika maeneo ya Majengo, Shamsi, na Ngarenaro.
Ujenzi huu ni hatua kubwa kuelekea maandalizi ya AFCON 2027 na maboresho ya kudumu ya Jiji la Arusha.


SHIRIKA la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limeingia kwenye hatua kubwa ya kuimarisha ulinzi na doria angani baada ya Kamishna wa Uhifadhi, Massana G. Mwishawa, kukagua ndege ndogo mbili (2) mpya aina ya Savannah zilizonunuliwa hivi karibuni.



Ndege hizo zimenunuliwa kupitia mradi unaofadhiliwa na BMZ, uliotekelezwa chini ya Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani. Lengo kuu la ununuzi huo ni kuongeza nguvu katika doria na uhifadhi wa wanyamapori kwenye Hifadhi za Taifa za Serengeti na Nyerere.


Ukaguzi huo umefanyika leo katika Karakana iliyopo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar, ambapo ndege hizo zinaendelea kuunganishwa tayari kwa kazi.


Akiwa uwanjani hapo, Kamishna Mwishawa amewapongeza mafundi wanaoendelea na kazi ya uunganishwaji wa ndege hizo kwa umakini mkubwa.


Pia, ametoa pongezi za kipekee kwa marubani wawili (2) ambao ni Askari Uhifadhi wa TANAPA. Marubani hao kwa sasa wapo kwenye hatua za mwisho za mafunzo yao maalum ya kurusha ndege hizo ili kuhakikisha usalama na ufanisi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.


Ndege hizo za kisasa aina ya Savannah zinatarajiwa kuanza doria rasmi angani mwanzoni mwa mwezi Oktoba, 2026, hatua itakayosaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti ujangili na kulinda rasilimali za taifa.