Happy Lazaro,Arusha .



KAMPUNI ya  EFTA Tanzania imewazawadia  wakulima waliokopa zana za kilimo na kurejesha mikopo yao kwa uaminifu, kwa kuwarejeshea nusu ya riba waliyoilipa wakati wa marejesho ya mikopo hiyo.



Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa EFTA Tanzania, Nicomed Bohay wakati akizungumza katika hafla ya kukabithi hundi za rejesho la asilimia 50 ya riba kwa wateja waliorejesha mikopo yao kwa nidhamu hafla iliyofanyika katika maonesho ya nanenane Njiro.



Bohay amesema Taasisi hiyo imeamua kurejesha takribani shilingi milioni 100 kwa wateja wake nchini kama motisha ya ulipaji mzuri wa mikopo.



"jumla ya wateja 37 nchini tayari wamenufaika na mpango huo mwaka huu, huku kila mmoja akipokea kiasi tofauti cha fedha kulingana na kiwango cha riba alicholipa."amesema  Bohay .



 Amesema kuwa, mpango huo unawahusu wakulima waliokopa matrekta, matrela na zana nyingine za kilimo na kutekeleza masharti ya mikopo bila kuchelewa.


Bohay  amesema EFTA, ambayo hutoa mikopo ya zana mbalimbali bila kuhitaji dhamana na inaofisi nane nchini, inashiriki Maonesho ya Nanenane katika kanda tano za Arusha, Dodoma, Morogoro, Mbeya na Mwanza. 


Amesema  kuwa,mwaka huu taasisi hiyo imeamua kutumia maonesho hayo kuwatambua wateja wake bora na kuonyesha kuwa uaminifu katika ulipaji wa mikopo una manufaa ya moja kwa moja.


Amefafanua  kuwa mafanikio ya wateja katika ulipaji yameifanya EFTA kupunguza kwa kiwango kikubwa mikopo chechefu (NPL), ambayo kwa sasa ipo asilimia moja pekee.


Bohay ameongeza kuwa,kiwango hicho ni cha kuvutia katika sekta ya fedha na kimeiwezesha taasisi hiyo kuelekeza sehemu ya fedha ambazo zingetengwa kwa ajili ya mikopo chechefu kurudi kwa wateja wake kama zawadi.


Aidha, amewahimiza wakopaji wote nchini kujenga utamaduni wa kulipa mikopo kwa wakati, akisema rekodi nzuri ya mkopaji huwekwa kupitia mfumo wa Credit Reference Bureau wa Benki Kuu ya Tanzania na humrahisishia kupata mikopo kutoka taasisi mbalimbali za fedha siku zijazo.



 Amesema hatua hiyo inalenga kujenga uhusiano wa kudumu kati ya taasisi za fedha na wakulima, pamoja na kuhamasisha matumizi ya mikopo yenye nidhamu kwa maendeleo ya sekta ya kilimo.


Wakizungumza mara baada ya kukabithiwa mfano wa hundi hizo wakulima hao walishukuru kwa namna taasisi hiyo inavyowajali na kuwapa motisha wa kuendelea kukopa zaidi.


"Kitendo kilichofanywa na Taasisi hii ni mfano wa kuigwa na taasisi zingine kwani kinatupa moyo wa kuendelea kukopa zaidi zana za kilimo ambapo taasisi hii imekuwa mkombozi mkubwa sana kwa wakulima."amesema .



Kwa upande wao wateja walionufaika na mkopo huo , Sebastian Gwalku kutoka  Mkoa wa Manyara amesema kuwa ,amekuwa  mteja wa EFTA kwa kupata mkopo uliomwezesha kukuza shughuli  za biashara ambapo kupitia mkopo huo ameweza  kuendeleza biashara na kuongeza kipato.


"Leo ninafurahi sana kuwa miongoni mwa wanufaika wanaokabidhiwa hundi kama ishara ya kutambua uaminifu wetu katika kurejesha mikopo kwa wakati na nawashukuru sana EFTA kwa fursa hii na kwa kuendelea kuwawezesha wafanyabiashara na wajasiriamali kufikia malengo yao."amesema .


"Ninawahamasisha wafanyabiashara wengine kutumia fursa zinazotolewa na EFTA na kuhakikisha wanarejesha mikopo yao kwa wakati ili nao waweze kunufaika na fursa kama hii."amesema .



 




Happy Lazaro,Arusha .



MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imewahamasisha wananchi na wawekezaji kutumia fursa ya kuanzisha vituo vya mafuta vijijini ili kuboresha upatikanaji wa huduma hiyo, kuongeza usalama wa wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika maeneo ya pembezoni.



Akizungumza leo  katika Maonesho ya Nanenane Njiro ,Meneja wa EWURA kanda ya kaskazini , George  Mhina amesema mamlaka hiyo imepunguza masharti ya uwekezaji wa vituo vya mafuta vijijini ili kuvutia wawekezaji wengi zaidi. 


Amesema hatua hiyo inalenga kumaliza tatizo la uuzaji wa mafuta kwenye vidumu na chupa, jambo ambalo linaweka maisha na mali za wananchi katika hatari kutokana na mafuta kuwa kemikali zinazoweza kusababisha majanga endapo zitahifadhiwa au kuuzwa isivyo salama.



Mhina ameongeza   kuwa tofauti na vituo vikubwa vya mijini vinavyohitaji mtaji wa zaidi ya Sh milioni 200 hadi 300, uwekezaji wa kituo cha mafuta kijijini unaweza kuanza kwa mtaji wa takribani Sh milioni 40 hadi 50.


 

"Wananchi wengi zaidi wanaweza kuingia kwenye biashara hiyo huku wakihakikisha mafuta yanayouzwa yanakidhi viwango vya ubora na bei zilizopangwa na EWURA."amesema Mhina .



Amefafanua zaidi kuwa, uwekezaji huo utasaidia pia kukuza shughuli za kilimo, mifugo na biashara nyingine za vijijini kwa kuhakikisha upatikanaji wa mafuta kwa uhakika, jambo litakalorahisisha usafirishaji na uzalishaji katika sekta mbalimbali za uchumi.



"Mbali na sekta ya mafuta, banda letu  katika maonesho ya Nanenane linatoa elimu kuhusu sekta za maji, umeme na usafi wa mazingira."amesema Mhina .


" Wananchi wanapata fursa ya kufahamu miradi mikubwa ya maji inayotekelezwa na Serikali katika maeneo ya Arusha, Same, Mwanga, Handeni, Korogwe, Tanga na Pangani, inayolenga kuboresha huduma za maji kwa maelfu ya wananchi."amesema Mhina .



Aidha amewataka  wananchi kutumia mafundi wa umeme wenye leseni zinazotolewa na EWURA wakati wa kufunga miundombinu ya umeme majumbani au kwenye biashara zao na kuonya  kutumia mafundi wasio na sifa kwani  kunaweza kusababisha hitilafu za umeme, ajali na hasara kubwa za mali na maisha.



"Nawakaribisha wananchi kutembelea banda lake ili kupata elimu kuhusu haki na wajibu wao katika sekta zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo pamoja na fursa mbalimbali za uwekezaji zinazochochea maendeleo ya uchumi na ustawi wa jamii."amesema Mhina .



"Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kutumia Maonesho ya Nanenane kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi, haki za watumiaji wa huduma za nishati na maji, pamoja na namna ya kuwasilisha malalamiko wanapokumbana na changamoto za huduma."amesema Mhina .


Amesema  kuwa ,Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan gesi ya LPG, ili kulinda afya za wananchi na mazingira. Alisema EWURA ina jukumu la kusimamia sekta hiyo na kuhakikisha huduma zinatolewa kwa kuzingatia viwango na usalama.



Ameongeza kuwa , maandalizi ya michuano ya AFCON inayotarajiwa kufanyika Tanzania yameongeza umuhimu wa matumizi ya nishati safi, ikiwemo kwenye magari na mabasi, ili kuchangia utunzaji wa mazingira na kuendana na viwango vya kimataifa vya usafiri wa kisasa.



"Mbali na kutoa elimu kuhusu nishati safi, EWURA pia inawafundisha wananchi namna ya kutambua na kutetea haki zao wanapopata huduma za maji, umeme na mafuta. Alieleza kuwa wananchi wengi hukumbana na changamoto kama kucheleweshwa kuunganishiwa maji au umeme, bili zisizo sahihi, au kupata mafuta yasiyo na ubora yanayoweza kuharibu vyombo vya usafiri."amesema Mhina .



Mhina amesisitiza  kuwa badala ya kuvumilia changamoto hizo, wananchi wanapaswa kufahamu njia sahihi za kuwasilisha malalamiko kwa EWURA ili yapatiwe ufumbuzi kwa wakati. Kwa mujibu wake, mamlaka hiyo imeweka mifumo ya kupokea na kushughulikia malalamiko ya watumiaji wa huduma zote inazosimamia.



"EWURA imewahimiza wananchi wanaotembelea Maonesho ya Nanenane kutembelea banda lake ili kupata elimu kuhusu matumizi salama ya nishati, haki za watumiaji wa huduma za maji na nishati, pamoja na fursa mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma na maendeleo ya wananchi"amesema .



 


Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) kwa kushirikiana na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu  (HESLB) imetoa elimu kwa jamii ya Ngorongoro kuhusu  mfuko wa  Ngorongoro Scholarship Fund  unaolenga kuwezesha wanafunzi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kupata fursa ya masomo ya elimu ya juu kupitia ufadhili Ngorongoro Fund.  




Elimu hiyo iliyotolewa katika ofisi za Ngorongoro ilijumuisha wadau muhimu wanaoguswa na mpango huo ambao ni viongozi wa jamii, wanafunzi pamoja na wadau mbalimbali ambao wamepewa uelewa kuhusu vigezo vya mkopo, sifa za waombaji pamoja na kupitia na kujadili mwongozo wa programu ya Ngorongoro Scholarship Fund.



Katika kikao hicho, viongozi wa jamii wamepongeza hatua ya Mamlaka ya kushirikiana na HESLB katika kuandaa na kuboresha mwongozo wa mfuko huo, wakieleza kuwa utasaidia kuweka utaratibu unaozingatia usawa, uwazi na mahitaji ya wakati katika kuwawezesha wanafunzi wenyeji kupata fursa za elimu ya juu.



Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji Ngorongoro,  Edward Maura, aliipongeza Mamlaka ya Ngorongoro na HESLB kwa kutoa elimu kuhusu Ngorongoro Scholarship Fund hasa jinsi wanufaika wanavyoweza kutambua fursa, kujaza fomu na kufuata taratibu za kuomba ufadhili.



“Tunawapongeza Ngorongoro na Bodi ya Mikopo kwa kutoa elimu hii kwa jamii na wanafunzi na kusaidia kuwaondolea wanafunzi changamoto na uelewa mdogo wa namna ya kuomba na kupata mikopo huu, tunaamini maamuzi haya ya Serikali yanalenga  kuimarisha mahusiano kati ya jamii na Ngorongoro na tunaamini wanafunzi na jamii  watatumia  fursa zinazotolewa kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa” alisema Mh. Maura.



Utekelezaji wa program hii unalenga kuimarisha ushirikiano na kuboresha huduma za jamii kwa wananchi wa Ngorongoro ambapo elimu wanayopata itasaidia ushiriki wao katika program za uhifadhi endelevu na kuvutia wageni kupitia vivutio vya utalii vilivyopo.



 


Waswahili husema nyumba njema haikosi wageni na hii imedhihirika leo tarehe 4 Agosti, 2026 baada ya Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar mhe Zubeir Ali Maulid kutembelea eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.



Akiwa katika geti la Loduare Spika Maulid alipata taarifa ya vivutio vya eneo hilo iliiyotolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Mariam Kobelo ambapo alielezwa kuendelea kuimarika kwa shughuli za uhifadhi,utalii na maendeleo ya jamii.


Aidha, haitoshi Spika Zubeir alielezwa kuhusiana na maajabu ya mchanga unaohama uliopo eneo la Olduvai ambapo mamia ya watu ambao mapenzi yao yamelega lega humiminika katika eneo hilo kuimarisha mapenzi.



Kwa mujibu wa simulizi za kihistoria kutokana na mchanga huo kuwa na asili ya sumaku wapendao wakifika mahali hapo penzi huwa motomoto na kuimarika.


Akizungumza baada ya ziara hiyo Spika Zubeir ametoa wito kwa watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii ili kujifunza na kupata utulivu.



Spika Zubeir ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kufanya kazi usiku na mchana katika kulinda uhifadhi, kusimamia utalii na maendeleo ya jamii.

  


Happy Lazaro,Arusha .



MBALI na ubunifu wa teknolojia za kilimo na mifugo unaoendelea kuonyeshwa katika Maonesho ya Nanenane, wageni wanaotembelea viwanja hivyo wamepata pia nafasi ya kufanya safari ya kipekee ya ladha kupitia vyakula vinavyobeba utamaduni wa mataifa mbalimbali katika banda la Cheesy Bite lililopo Nanenane Njiro .


Katika kona moja ya maonesho hayo, harufu ya vyakula vinavyoandaliwa kwa ustadi huwavutia wageni kusimama, kuonja na kujionea namna sekta ya utalii wa chakula (food tourism) inavyozidi kukua nchini. Wengi huchukua muda kupumzika na kufurahia milo yenye mchanganyiko wa mapishi ya kisasa yanayokidhi ladha tofauti za wateja.



Akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonesho hayo ,Mmoja wa wafanyakazi katika katika hoteli hiyo, Maryam Mlau , amesema wameamua kuandaa menu inayowapa wageni uzoefu wa kuonja vyakula vya asili tofauti bila kulazimika kusafiri nje ya Tanzania.


 Maryam ameeleza kuwa wageni hupata fursa ya kufurahia vyakula kama Chicken Loaded Fries, Beef Loaded Fries, Halloumi Loaded Fries pamoja na burger za nyama ya ng'ombe na kuku ambazo zimekuwa zikivutia wengi.



Ameongeza kuwa, si Watanzania pekee wanaovutiwa na vyakula hivyo, bali pia wageni kutoka mataifa mbalimbali wanaotembelea maonesho hayo, jambo linaloonyesha kuwa chakula kimeendelea kuwa sehemu muhimu ya utalii na uzoefu wa msafiri anapotembelea eneo jipya.



Amesema kuwa,mazingira mazuri, huduma zenye ukarimu na kuzingatia viwango vya usafi vimechangia kuwafanya wageni wengi kurejea tena, huku baadhi yao wakichagua kutumia huduma ya kusafirishiwa chakula pale wanaposhindwa kufika moja kwa moja.



"Wadau wa utalii wanaeleza kuwa utalii wa chakula unaendelea kushika kasi duniani, ambapo wageni hutafuta sio tu vivutio vya asili na utamaduni, bali pia ladha zinazotofautisha eneo moja na jingine"amesema Maryam.

 


"Hali hiyo imeifanya sekta ya huduma za chakula kuwa sehemu muhimu ya kuongeza thamani ya maonesho makubwa kama Nanenane."amesema Maryam .



"Kadri maonesho hayo yanavyoendelea, wageni wanaondoka wakiwa si tu na maarifa mapya kuhusu kilimo na mifugo, bali pia na kumbukumbu za ladha mbalimbali walizozionja, jambo linaloifanya Nanenane kuwa zaidi ya maonesho ya uzalishaji—bali pia jukwaa la kukutanisha tamaduni kupitia chakula."amesema 



 


By Happy Lazaro, Arusha.



Farmers have been encouraged to visit the Corteva Agriscience pavilion at the ongoing Nanenane Agricultural Exhibition at Themi Grounds in Arusha to acquire knowledge on the use of improved maize seed varieties, receive professional agronomic advice, and explore modern agricultural technologies aimed at increasing maize productivity and yields across Tanzania.



The call was made by Corteva Agriscience Agronomist Fikiri Kalobelo while speaking to journalists about the technologies and innovations the company is showcasing during this year's exhibition.



 He said Corteva is participating in the event to demonstrate its advanced Pioneer maize seed technologies, which are specifically developed to suit different agro-ecological zones across the country.



Kalobelo explained that the company is committed to ensuring that every farmer visiting the Corteva pavilion receives quality services, technical support, and comprehensive knowledge on modern maize production.


 Farmers are being trained on every stage of maize cultivation, from selecting the right seed varieties and applying proper agronomic practices to adopting technologies that enhance productivity and maximize yields.



"Our objective is to empower farmers with technologies and farming practices that enable them to achieve higher yields and better-quality harvests," he said.



For Tanzania's lowland production zones, Corteva recommends the Pioneer P2848W hybrid, which matures within 80 to 90 days and can produce an average yield of 25 to 30 bags per acre when recommended agronomic practices are followed.



For the medium rainfall zones, the company is promoting Pioneer P3531W and PHB 30G19 hybrids, which have the potential to produce between 35 and 40 bags per acre.


 According to Kalobelo, these hybrids produce hard and heavy kernels, giving farmers greater economic value under the current grain marketing system, where maize is traded based on weight rather than volume. He added that these varieties are also ideal for roasting and have become highly preferred by both fresh maize traders and consumers.



"These varieties remain fresh for longer after harvest without losing quality, giving both farmers and traders greater market confidence and better returns," Kalobelo noted.



For areas receiving moderate to high rainfall, Corteva recommends the Pioneer P3812W hybrid, which has been developed to perform well under such conditions.


 The variety can produce between 35 and 40 bags per acre while offering strong tolerance to leaf diseases and ear rot commonly associated with excessive rainfall.



Kalobelo explained that Pioneer P3812W matures within 115 to 125 days and consistently produces high-quality grain, helping farmers minimize losses caused by prolonged rains. He added that Corteva remains committed to supplying improved seed varieties and professional agronomic support to enhance agricultural productivity nationwide.


Besides Pioneer maize hybrids, Corteva also supplies Pannar maize seed varieties suitable for all production zones in Tanzania. 


For lowland and low-rainfall areas, the company recommends PAN 3M-05, which matures within 75 to 80 days and yields between 25 and 30 bags per acre. The variety is characterized by strong stalks and performs well in both low and moderate rainfall conditions.



For the medium production zones, Corteva recommends PAN 53, a variety well known for producing sweet maize suitable for roasting. The hybrid yields between 35 and 40 bags per acre and has strong stalks that withstand different growing conditions.


 Kalobelo said PAN 53 was specifically developed to withstand the effects of climate change and performs well in areas receiving moderate to high rainfall while still producing good harvests even when rainfall is below normal.



For the highland production zones, Kalobelo highlighted PAN 9M-91, popularly known as "The Real Answer" because of its outstanding performance and high yield potential. He described it as a new hybrid that produces abundant harvests with hard and heavy kernels.



In addition, Corteva has prepared trial seed packs (Funpacks) for selected farmers while collecting their contact information to enable continuous technical support even after the exhibition concludes. Kalobelo emphasized that the company's commitment to farmers extends beyond selling seed, focusing instead on continuous follow-up and professional guidance to help farmers achieve their production goals.



"That is why we say Corteva enriches lives. Our mission is not simply to sell seed but to transform farmers' livelihoods through improved seed varieties and the right agricultural technologies," he said.



He added that Corteva's culture is built on maintaining close relationships with farmers by providing continuous training and technical assistance, making the company a trusted partner in improving agricultural productivity and enhancing farmers' livelihoods.



 


Happy Lazaro,Arusha.


Wananchi wametakiwa kutumia bidhaa za umeme jua kutoka kampuni ya teknolojia ya  ZOLA ELETRIC kwa ajili ya matumizi mbalimbali kwani  bidhaa hizo  zina ubora wa hali ya juu .



Hayo yamesemwa  jijini Arusha na Afisa masoko wa kampuni hiyo Moses Vikael wakati akizungumza katika mbio za Redcross Marathon Arusha zilizofanyika katika uwanja wa Stadium jijini Arusha .



 "Tunafanya kazi ya uuzaji na usambazaji wa sola katika maeneo mbalimbali nchini kupitia mtandao wa mawakala wetu, kuanzia mijini hadi vijijini, na katika sekta zote za biashara, taasisi na makazi ya wananchi."amesema Moses.



"Lengo letu ni kuhakikisha kila eneo lenye uhitaji wa nishati linapata suluhisho bora la umeme wa jua kutoka kampuni yetu "amesema Moses.



Moses ameongeza  kuwa,kitendo hicho kilichofanywa na Redcross ni mfano wa kuigwa kwani kwa mara ya kwanza wameweza kufanya mbio hizo kwa mkoa wa Arusha jambo ambalo limeweza kuleta hamasa kubwa kwa wananchi wa Arusha .


"Tunashukuru sana kwa namna ambavyo.Redcross mmeweza kutupa mwaliko wa kuwa wafadhili katika jambo hili na tunawaahidi kuendelea kushirikiana na nyie katika kila hatua "amesema  Moses.



Aidha ametoa wito kwa wananchi mbalimbali kiwa na tamaduni za kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zao kwani michezo ni afya na inasaidia kuondokana na maradhi mbalimbali ambayo yangeweza kutokea .




 



Happy Lazaro,Arusha .


WAKULIMA  kanda ya kaskazini wametakiwa kutembelea banda la kampuni ya Kibo Seed katika maonesho ya nanenane ili kuweza kupata elimu  kuhusu matumizi ya  mbegu bora za mahindi na mbogamboga ili kuongeza uzalishaji.




 Hayo yamesemwa leo jijini Arusha na Afisa Uzalishaji wa Mbegu wa  kampuni ya Kibo Seed Co.Ltd ,Marko Msheishiwa wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonesho ya  nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Taso Njiro.


 Amesema  kampuni hiyo inashiriki Maonyesho ya Nanenane 2026 ikiwa na lengo la kuwaelimisha wakulima kuhusu matumizi ya mbegu bora za mahindi na mbogamboga ili kuongeza uzalishaji.



Ameongeza kuwa ,kampuni hiyo  inazalisha na kusambaza mbegu za mahindi kwa kanda mbalimbali za kilimo nchini, zikiwemo kanda ya chini, ya kati na ya juu, ili kuhakikisha kila mkulima anapata mbegu zinazolingana na mazingira yake.



Akizungumzia maandalizi ya maonesho ya mwaka huu, Msheishiwa amesema yameboreshwa zaidi kuliko miaka iliyopita, ambapo mazao ya maonesho yalipandwa kwa wakati, yakatunzwa vizuri na sasa yanaonyesha matokeo halisi ambayo yatawawezesha wakulima kujifunza kwa vitendo.


Ameongeza  kuwa, moja ya sifa zinazotofautisha mbegu za Kibo Seed na kampuni nyingine ni ubora wake, hususan kwa mahindi yanayofaa kuchomwa na kukobolewa, ambayo ni matamu na yanakubalika na watumiaji wengi.


Kwa upande wa uzalishaji, amesema mavuno hutegemea ukanda na aina ya mbegu inayotumika. Mbegu za ukanda wa chini zinaweza kutoa tani 2 hadi 2.5 kwa ekari, ukanda wa kati tani 3 hadi 3.5, huku ukanda wa juu ukifikia tani 4 hadi 5 endapo mkulima atafuata kanuni bora za kilimo.


Aidha, amesema changamoto kubwa inayowakabili baadhi ya wakulima ni kutokuchagua mbegu sahihi kulingana na ukanda wao wa kilimo pamoja na kutofuata kanuni za uzalishaji, ikiwemo kupanda kwa wakati, kutumia mbolea stahiki na kutunza shamba ipasavyo.


Aidha Msheishiwa ametoa wito kwa wakulima na wananchi kutembelea banda la Kibo Seed katika maonyesho ya Nanenane jijini Arusha ili kupata elimu kuhusu mbegu bora, kuona mashamba ya mfano na kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa kampuni hiyo.

 



Unaweza kusema dili limetiki kufuatia klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam kuchagua kivutio namba moja cha utalii barani Africa kufanya uzinduzi wa wiki ya simba na jezi mpya ya mnyama kwa mwaka 2026.



Uzinduzi uliofanyika leo tarehe 1 Agosti, 2026 eneo la Ngoitoktok katika kasoko ya Ngorongoro ulipambwa na upepo mwanana unaotokana na mawimbi kutoka bwawa la Ngoitoktok likipambwa na Viboko wanaogelea huku ulinzi ukiimarishwa na familia za Simba waliosheheni kreta ya Ngorongoro.



Akizungumzia tukio hilo la kihistoria lililojumuisha uzinduzi wa logo ya miaka 90 ya Simba ulihudhuriwa na menejimenti ya Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro iliyoongozwa na Naibu Kamishna huduma za Shirika Aidan Makala na mashabiki zaidi ya 300 kutoka ndani na nje ya Nchi.



“Tukio hili ni matokeo chanya kati ya ushirikiano wa Klabu ya Simba na hifadhi ya Ngorongoro, tumetangaza utalii wa ndani, wanasimba wamerudi nyumbani lakini kubwa zaidi ni kuchagiza utalii wa michezo kuelekea mashindano ya AFCON ya mwaka 2027 yatakayofanyika hapa Nchini” Naibu Kamishna Aidan Makala.



Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba Ahmed Ally amebainisha kuwa Ngorongoro ni zaidi ya hifadhi, ina vivutio vingi vya utalii ambapo asili, urithi wa utamaduni na malikale vinaishi pamoja, hivyo Simba kufanya uzinduzi huo ndani ya hifadhi ni kurudisha mashabiki nyumbani na kuwadhihirishia kuwa ndoto, maono na hisia zao zinakutana na uhalisia uliopo Ngorongoro.





















 


Na Queen Lema, Arusha

 

MKOA wa Arusha unatarajiwa kusimama miguu yote miwili kesho Agosti Mosi, wakati Princess Lounge, moja ya kumbi maarufu na zenye mvuto mkubwa wa kipekee barani Afrika Mashariki, itakapofanya maadhimisho makubwa ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.


 Akizungumza kuelekea tukio hilo la kihistoria, Mkurugenzi wa Princess Lounge, Catherine Urasa, amesema wameandaa sherehe kubwa na ya kukata na shoka itakayoweka historia mpya ya burudani mkoani Arusha.

Catherine amebainisha kuwa tangu kuanzishwa kwake, Princess imekuwa nguzo kuu na kichocheo kikubwa cha sekta ya burudani, huku ikisifika kwa kulisha vyema hisia za wapenda bata na starehe mkoani hapa.

Alieleza kuwa kwa kuzingatia Arusha ni kitovu cha utalii nchini, Princess Lounge imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwenda sambamba na hadhi hiyo kwa kutoa burudani na huduma za kiwango cha kimataifa zinazovutia wageni wa ndani na nje ya nchi.


"Tunatimiza mwaka mmoja sasa wenye mafanikio makubwa sana. Tunafurahi kwa upendo na mapokezi tuliyopata, na tunapenda kuwaahidi wateja wetu kuwa tumejipanga vyema zaidi kuendeleza na kuiboresha sekta hii ya burudani kwa viwango vya juu zaidi," alisema kwa kujiamini Catherine.


Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo amejivunia namna biashara hiyo ilivyoweza kuwa mkombozi kwa vijana kwa kutengeneza fursa za ajira kwa wale ambao hapo awali hawakuwa na kazi kabisa.


"Kama mnavyojionea wenyewe, hapa tuna mabinti warembo na wachapakazi ambao ni sehemu ya nembo yetu. Pia tuna vijana mahiri wa muziki (DJs) na wataalamu wa kuchoma nyama tamu na zenye ladha ya kipekee, ambao wote kwa pamoja ndio siri na nguzo ya mafanikio ya Princess," aliongeza.


Kufuatia hatua hiyo, Catherine ametoa wito na mwaliko rasmi kwa Watanzania wote na wakazi wa jiji la Arusha kujitokeza kwa wingi kesho kusherehekea kwa pamoja mafanikio hayo, ambapo kutakuwa na mfululizo wa burudani za kusisimua, vinywaji vya kila aina, na vyakula vya kutosha.