Happy Lazaro,Arusha
MAWAKALA WA BIMA wametakiwa kuzingatia uadilifu, pamoja na kujenga mahusiano imara na wateja, pamoja na kuendelea kujifunza ili kuendana na mabadiliko ya soko.
Hayo yamesemwa leo jijini Arusha na
Meneja wa Bima kanda ya kaskazini (TIRA) Dokta Emmanuel Lupilya wakati akizungumza kwenye kikao maalumu kilichowakutanisha mawakala wa bima kutoka jijini Arusha .
Dokta Lupilya amesema lengo la kikao hicho ni kujadili na kuweza kuboresha maswala mbalimbali ya bima pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi wa haraka.
Dokta Lupilya amesema kuwa,Wakala wa bima wametambuliwa kwa mchango wao mkubwa katika kulinda maisha na mali za Watanzania .
Dokta Lupilya amesema kuwa,kusanyiko hilo limewaleta kutambua mchango mkubwa hasa kwa mawakala wanaofanya kwa ajili ya nchi yetu .
"Ni dhahiri kuwa wanaendesha biashara hizi kwa kuzingatia weledi kwa kuthamini utu wa wananchi pamoja na udhubutu wao katika kuhakikisha wanalinda ndoto za watanzania ."amesema .
Ameongeza kuwa, mafanikio yao wanayofanya yasihesabiwe tu katika mikataba wanayoandika bali ihesabiwe katika watu wangapi wamewahubiria habari za bima watu wangapi wamewasaidia katika maswala yao pamoja na familia walizosaidia katika kuingia kwenye mfumo mzima wa bima .
"Kwa kufanya hivyo watakuwa wamehesabiwe ile thamani yao kwa kuelimisha jamii na imani waliyoonyesha kwa jamii kuwa bima sasa sio kitu cha anasa bali ni kitu cha muhimu na kila mwananchi lazima awe nacho ."amesema Dokta Lupilya.
"Swala la kutoa huduma z bima sio swala dogo ni swala zito na ni swala ambalo linahitaji weledi zaidi na mawakala hawa wamekuwa mfano wa kuigwa kwani wamekuwa lango la kuwezesha uelewa wa maswala la bima kwa jamii."amesema .
"Kilio changu mimi ni kuhakikisha kuwa kukua kwa sekta ya bima kuna mchangao mkubwa sana wa mawakala kuwezesha sekta kukua na mawakal hao wanafanya kazi kubwa ."amesema Dokta Lupilya.
Amesema kuwa lengo ni kuhakikisha mawakala wanakuwa na wao kama mamlaka ni kuhakikisha wanawawekea mazingira rafiki ambayo yatawawezesha kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa .
Aidha amewataka pia mawakala kufanyiwa mafunzo mara kwa mara katika maswala ya fedha ili wajue namna ya kutunza kile wanachokipata .
Aidha ametoa kwa makampuni kuonyesha mfano kwa maana ya kupeleka mafunzo ya maswala ya mahesabu ili wajue namna ya kuweza kukua na kuweza kujifunza teknolojia mpya kwani kuna wakati wataanza kuuza bidhaa zao kupitia teknolojia kwan8 teknolojia inauza zaidi .
"Tuwafundishe hawa namna ya kutumia teknolojia kwenye biashra ya bima na kwa kufanya hivyo tutafanikiwa kwa kiwango kikubwa sana ."amesema Dokta Lupilya.
Nao Baadhi ya mawakala wakizungumza kwenye kikamo hicho , wamesema kuwa ,malalamiko makubwa wanayolalamikia.ni swala la mzigo mkubwa ambao mawakala wanayabeba jambo ambalo mawakala wengi wanashindwa kuendesha hiyo biashara kutokana na changamoto hizo kwani soko limekuwa na ushindani mkubwa na gharama za uendeshaji zimekuwa kubwa kwani mabenki yameingia ambapo ameomba mamlaka hiyo iangalie namna ya kuwabeba mawakala na mawakala ndo wenye biashara ya moja kwa moja .
"Tunachoomba mhakikishe mnawabeba hawa mawakala kwani mzigo ni mkubwa sana na hawawezi na mjitahidi kuwawezesha mawakala na muwape motisha pia ."amesema .


















































