Happy Lazaro.Arusha .
WAZAZI wametakiwa kuwalea watoto wao kimaadili ,huku wakiwapangia kazi za nyumbani pamoja na kuendeleza shughuli za ujasiriamali ambazo wamekuwa wakifundishwa shuleni hapo.
Hayo yamesemwa jijini Arusha na Mkuu wa shule ya sekondari St.Mary's Duluti iliyopo jijini Arusha ,Br.Protas Mangu akizungumza kwenye mahafali ya 13 ya kidato cha 6 ambapo jumla ya wanafunzi 25 wamehitimu masomo yao.
Aidha amewataka wazazi kuhakikisha wanawapa watoto wao kazi za kufanya ili waweze kujiajiri badala ya kuwaacha kukaa bila shughuli zozote kwani tayari shule ilishawajengea msingi mzuri wa kuweza kujiajiri .
"Wasikae wakitegemea taaluma waliyofundishwa tu bali waendelee kujiajiri huku wakifuga kuku ,ng'ombe,kufanya biashara na waache tabia ya kuwadekeza watoto na kuwaachia wadada wa kazi wafanye kila kitu jambo ambalo halitakiwi kabisa ."amesema .
Br.Mangu amesema kuwa, shule imeanzishwa mwaka 2007 na mahafali haya wamelenga wanafunzi wao waonyeshe bidii na ujuzi wao katika kuendeleza taaluma ambayo wanapata shuleni .
Aidha amewaasa wahitimu hao kusoma kwa bidii kwani mitihani inayokuja sasa hivi haihitaji kukariri bali kile wanachofundishwa darasani wanatakiwa wakiweke kwenye maisha ya kawaida.
Aidha amewataka wanafunzi hao kuwa makini katika kujibu maswali na kuyaorodhesha maswali wakipewa .
"Nawaasa nyie kidato cha sita muendelee kuwa na nidhamu nzuri kwani hapa sisi hatuwafundishi mambo ya taaluma tu bali tunawafundisha swala zima la maadili ,mambo ya kiroho pamoja na mambo ya michezo pia "amesema .
Aidha amefafanua kuwa wanafunzi hao wakitaka kufaulu vizuri lazima watangulize mbele swala zima la maadili .
Aidha amewataka wazazi kuhakikisha wanawalea vizuri kwani nidhamu waliyopata shuleni haitoshi kwani wao pia wana kazi kubwa ya kuwalea watoto pindi wanapokuwa nyumbani .
Ameongeza kuwa watoto hao bado ni wadogo na wanahitaji muongozo mkubwa kutoka kwa wazazi .
"Wazazi tunatangaza kuna nafasi pia ya kidato cha tano mwaka huu mwezi wa saba tunawakaribisha sana hapa shuleni watoto waweze kufundisha maswala ya taaluma na kila mmoja anajua namna ambavyo mwaka jana ufaulu ulikuwa mzuri sana wa kidato cha sita na kidato cha nne ."amesema
Kwa upande wake mgenirasmi katika mahafali hayo ,Meneja wa tawi la NMB Usa River Hermelinda Lasihwaki amewataka wahitimu hao kuyaendeleza yale yote waliyofundishwa shuleni hapo ikiwemo swala zima la maadili kwani hilo ndilo ufunguo wa kila kitu.
"Nimeona namna ambavyo shule imewaandaa vizuri kwa kuwafundisha somo la ujasiriamali kwa vitendo ambalo mkilitumia vizuri litawasaidia sana kujiajiri
badala ya kutegemea kuajiriwa ."amesema Lasihwaki.


















































