Cosato David Chumi, and
Kambarage Masato Wasira took their oaths of allegiance to replace Ng’waru Maghembe Jumaine, James Millya, and Angela Kizigha, who were elected to the Tanzania National Parliament.
In a strategic move to strengthen long-term digital cooperation, Estonia recently hosted European and East African partners to advance initiatives around Digital Public Infrastructure (DPI).
"Estonian companies have built globally recognized expertise in digital governance, interoperability, cybersecurity, and trusted digital services. Through this partnership with the East African Business Council, we want to create practical opportunities for cooperation, where companies from both regions can share knowledge, develop new partnerships, and build scalable digital solutions together. We see strong potential for long-term collaboration supporting East Africa’s rapidly growing digital transformation ambitions."
"Through this partnership with ITL Estonia, EABC aims to facilitate knowledge exchange, technology transfer, investment linkages, and private sector collaboration that will accelerate digital transformation, innovation, and regional integration across East Africa. We are confident that this cooperation will create new opportunities for businesses, especially SMEs and young innovators, to participate competitively in the global digital economy."
Happy Lazaro,Arusha
Kwa mara ya kwanza tangu kuanzisha mwaka 2016, Makumbusho ya Kumbukumbu ya Chifu Ndaskoi imeadhimisha Siku ya Makumbusho Duniani ikiongozwa na Kaulimbiu isemayo; "Miti na utamaduni; kuunganisha zamani na kesho"
Wakati wa sherehe hiyo Wadau mbalimbali pamoja na jamii wamehimizwa kuchukua hatua za makusudi kuenzi, kuhifadhi na kuridhisha utamaduni wetu wa Kiafrika ili kuthibiti mmomonyoko wa maadili unaoikabili ya jamii.
Aidha, wazazi wameombwa kuwajibika ipasavyo katika malezi ya watoto na vijana na vijana kuacha kukumbatia utandawazi bila kuangalia madhara yake.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Kumbukumbu ya Chifu Ndaskoi iliyopo kata ya Moshono Jijini Arusha, Ol-aiguenani Meshack Ndaskoi kwenye hafla ya kuadhimisho ya siku ya makumbusho duniani, iliyofanyika kwa kupanda miti ya asili zaidi ya mia moja katika eneo la Bustani ya kuhifadhi miti ya asili na mazingira ambayo ni sehemu ya Makumbusho hiyo.
Aidha miti hiyo ya asili ilioteshwa kama njia ya kudumisha utamaduni kwa sababu zinatumika katika masuala ya kiroho, madawa. rasilimali na chakula, utamaduni. Kuhifadhi na kutunza miti ya asili kuzuia katika hataria ya kupotea kutokana na shughuli za kibinadamu na mabadiliko ya tabia nchi.
Ameendelea kusema kuwa, jitihada za makusudi zinahitajika za kuweka mikakati madhubuti ya kuhifadhi mila na desturi zetu za Kiafrika kwa kuandaa mzingira yatakayohakikisha kwamba tunaridhisha mila na desturi zetu nzuri kwa vizazi vijavyo. kuondokana changamoto za kuongezeka kwa mmomonyoko wa maadili unaochangia ukosefu wa nidhamu pamoja na vijana wengi kupotea kimaisha .
Ndaskoi amesema kuwa, kutokana na utandawazi hivi sasa jamii nyingi zimeanza kuacha misingi ya malezi ya kiafrika jambo linalosababisha jamii hususan vijana kukosa uadilifu, heshima, ujasiri, umoja na mshikamano ndani ya jamii.
Ndaskoi amesema kuwa, makumbusho hiyo inajikita zaidi katika kuonyesha historia ya Arusha tangu mwishoni mwa karne ya 16 na Utamaduni wa jamii ya Wamaasai ambapo inatoa fursa kwa wadau pamoja na watu mbalimbali kujifunza na kujionea mambo mbalimbali kuhusu tulikotoka, tuloko ambayo ni muhimu katika kuleta maendeleo endelevu tunakokwenda.
"Makumbusho hii inatoa fursa pia kwa wanafunzi wa Shule za Maingj na Sekondari na vyuo na hata watalii kuweza kutembelea na kujifunza maswala mbalimbali ambayo yamesahaulika na yanatakiwa kuenziwa.
Alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuwezesha Makumbusho haya kuendelea kuwaidia jamii kuenzi mila na desturi zetu ili zisisahaulike katika jamii.
Naye Naibu Meya wa Jiji la ArushaJulius Ole Sekeyan akizungumza kwa niaba ya Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Maxmilian Iranghe amesema kuwa, jambo lililofanywa na Ol-aiguenani Meshack Ndaskoi la kuanzisha Makumbusho haya binafsi ni jambo zuri na linapaswa kuungwa mkono na wdau wote kwa kiwango kikubwa sana .
Amesema kuwa, Serikali ipo tayari kushirikiana kwa karibu sana na Makumbusho ya kumbukumbu ya Chifu Ndaskoi ambayo inalenga kuhifadhi na kukuza historia na desturi na mila za Wamaasai.
"Jitihada hizi zisizopigiwa upatu zilizofanywa na mwenzetu huyu ni kubwa na zinapaswa kuungwa mkono sana kwani zinasaidia sana kutukumbusha na kuenzi mila na desturi za jamii zetu kwa ajili ya manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo katika kudumisha utamaduni ."amesema .
Diwani wa kata ya Moshono, Ciriliel Mbise amewataka wananchi wa jiji la Arusha kujitokeza kwa wingi kutembelea makumbusho hiyo ili kuweza kujifunza historia ya Arusha na utamdaduni wa jamii ya Wamaasai na kuweza kuziendeleza .
Aidha Mbise ameitaka jamii kuenzi na kuthamini tamaduni zao ili kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kuvamiwa na utandawazi ambao umechangia kuporomoka kwa maadili katika jamii ..
Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio ya taasisi na mashirika ya umma nchini unategemea kwa kiwango kikubwa uimara wa mifumo ya utawala bora, uwajibikaji na uongozi wenye maono yanayolenga matokeo.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Chacha Marigiri, alipowasilisha mada kuhusu ‘Utawala bora katika mashirika ya Umma na Majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Hazina’ katika Mkutano wa Jukwaa la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma Zanzibar uliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip Airport.
Katika wasilisho lake Jumapili, Mei 24, 2026, Marigiri alisema kuwa kasi ya kufikia maendeleo endelevu haiwezi kupatikana kwa uwekezaji pekee, bali kupitia mifumo imara ya usimamizi inayohakikisha rasilimali za umma zinalindwa na kuzalisha kwa maendeleo ya Taifa.
Alisema thamani ya uwekezaji wa Serikali katika taasisi za umma na kampuni ambazo Serikali ina hisa chache kwa sasa imefikia Sh92.3 trilioni, hali inayodhihirisha umuhimu wa kuendelea kuimarisha mifumo ya utawala bora na usimamizi wa uwekezaji wa umma.
Kwa sasa Ofisi ya Msajili wa Hazina inasimamia uwekezaji wa umma wenye jumla ya taasisi 308, zikijumuisha taasisi za kibiashara, zisizo za kibiashara pamoja na uwekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Hali hiyo inaifanya OMH kuwa mhimili muhimu katika kulinda na kuongeza thamani ya mali za Serikali.
Bw. Marigiri alisema jukumu la OMH linaenda zaidi ya usimamizi wa kawaida mpaka kuhakikisha taasisi za umma zinaendeshwa kwa nidhamu ya kifedha, zinakuwa na ufanisi wa kiutendaji na zinaendana na vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.
Alitaja maeneo muhimu ya mamlaka na majukumu ya OMH kuwa ni pamoja na kusimamia utendaji wa taasisi za umma, kufuatilia faida na marejesho ya Serikali kupitia gawio, kushauri kuhusu uteuzi na tathmini ya bodi, kufanya tathmini ya utendaji pamoja na kushauri Serikali kuhusu maamuzi ya uwekezaji.
Katika hatua nyingine, aliwataka wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu kuendelea kuimarisha mifumo ya utawala kwenye taasisi zao kwa kuzingatia matumizi ya teknolojia, usimamizi wa vihatarishi, usimamizi wa maadili pamoja na maamuzi inayozingatia takwimu.
Alisema uzoefu wa mataifa yaliyofanikiwa kiuchumi kama Singapore, Norway, China na Malaysia unaonesha kuwa mafanikio ya uwekezaji wa umma yanategemea zaidi ubora wa usimamizi kuliko ukubwa wa uwekezaji wenyewe.
“Taifa lolote halifanikiwi kwa kumiliki taasisi za umma pekee; mafanikio yanatokana na namna taasisi hizo zinavyosimamiwa kwa weledi, uwajibikaji na malengo muda mrefu,” alisema.
Aidha, alibainisha kuwa OMH imeandaa Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu (2025/26–2049/50) unaolenga kuifanya ofisi hiyo kuwa kichocheo cha upanuzi wa uchumi kupitia uwekezaji wa Serikali na hasa katika sekta za kimkakati ikiwemo usafirishaji, nishati, fedha, kilimo, viwanda, utalii na madini.
Alisema mafanikio ya uwekezaji wa umma yataendelea kutegemea ushirikiano wa karibu kati ya bodi za taasisi, watendaji wakuu, Serikali na taasisi za usimamizi ili kujenga taasisi imara, zenye ushindani na zinazotoa matokeo yanayopimika kwa maendeleo ya Taifa.
Happy Lazaro,Arusha .
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude,amezindua rasmi chapa yake mpya ya gesi safi ya kupikia, LOTI GAS,huku akisisitiza umuhimu wa matumizi ya nishati safi kwa maendeleo ya afya, mazingira na uchumi wa wananchi.
Aidha Mkuu wa wilaya huyo ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wananchi hao kutumia nishati hiyo kwa wingi ili kutunza mazingira .
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkude ameipongeza kampuni ya LOTI GAS kwa uwekezaji wake ambao amesema unaenda sambamba na dira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa lengo la kupunguza matumizi ya kuni na mkaa ili kulinda mazingira pamoja na afya za wananchi.
Mkude amesema mwitikio wa matumizi ya nishati safi nchini umefikia asilimia 28.6, huku juhudi mbalimbali zikiendelea kuhakikisha taifa linafikia malengo yaliyojiwekea katika sekta hiyo muhimu.
"Uwekezaji wa kampuni ya LOTI GAS umefungua fursa za ajira kwa vijana na kuchangia kukuza uchumi wa Mkoa wa Arusha pamoja na taifa kwa ujumla."amesema Mkude .
Aidha ameihimiza menejimenti na watumishi wote wa LOTI GAS kuhakikisha wanazingatia viwango vya usalama, ubora wa bidhaa pamoja na kutoa huduma bora kwa wateja ili kujenga imani kwa wananchi.
"Nawasihi wananchi wa Arusha na Watanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa ya matumizi ya nishati safi, akibainisha kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wenye nia njema ili kuweka mazingira bora ya biashara na maendeleo nchini."amesema Mkude .
Akizungumza kwenye uzinduzi huo ,Mkurugenzi wa Loti Energies, Collins Kimaro amesema kuwa , dira ya kampuni hiyo ni kuona Tanzania ambayo kila nyumba—kuanzia Arusha hadi maeneo ya vijijini—inaweza kutumia nishati safi ya kupikia kwa usalama, kwa upatikanaji rahisi na kwa gharama rafiki.
Aidha amefafanua kuwa , tofauti ya Loti Gas ni kwamba inakuletea amani kwani afya inalindwa kwa sababu hamna moshi,mitungi misafi na mipya na amani kutokana na usalama, imepimwa na ina vigezo vyote na ni bei rafiki.
Aidha ameongeza kuwa,gas hiyo inapatikana kwa urahisi, madukani au kwa delivery .ambapo mteja anapelekewa sehemu yoyote .
"Uzinduzi huu umefanyika chini ya kampeni ya “Tupo Jikoni na Loti – Gesi ya
Kuaminika Kwako”, ambapo uzinduzi huo umeambatana na shindano la kupika supu lililoonyesha matokeo mazuri na ladha ya kuvutia, kuthibitisha ubora wa Loti Gas katika matumizi ya kila siku."amesema Mkurugenzi Kimaro.
Uzinduzi huo ambao umefanyika katika ukumbi wa Aim Mall Arusha ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali ambao kwa pamoja wamepongeza kampuni ya Loti Energies kwa uwekezaji huu inayounga mkono malengo ya serikali ya kuendeleza nishati safi ya kupikia kwa Watanzania wote.
"Uzinduzi ulionyesha pia uwepo wa wakala wengi wa Loti Gas, jambo linalothibitisha
kuwa tayari Loti Gas imeanza kupatikana sokoni Arusha, ikiwa na mitungi ya kilo 6 na
kilo 15, na mpango wa kupanua zaidi kadri mahitaji yanavyoongezeka."amesema Kimaro.
Na Mwandishi wa OMH
Dar es Salaam. Tanzania imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China katika mageuzi ya mashirika ya umma, ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa serikali wa kuongeza ufanisi, faida na uwajibikaji katika uwekezaji wa umma.
Nia hiyo ilibainishwa Jumatatu, Mei 18, 2026, wakati Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian, pamoja na ujumbe wake, walipotembelea Ofisi ya Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na menejimenti ikiongozwa na Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, kuhusu uwekezaji, maendeleo ya miundombinu na uhamishaji wa teknolojia.
Akizungumza katika kikao hicho, Mchechu alisema Tanzania inalenga kujifunza kutoka China katika kusimamia na kuleta mageuzi ya mashirika ya umma kupitia mfumo wa Tume ya Usimamizi na Uendeshaji wa Mali za Serikali ya China (SASAC), akibainisha kuwa Ofisi ya Msajili wa Hazina ni taasisi ya kimkakati yenye dhamana ya kusimamia uwekezaji wa Serikali.
Alisema kutokana na jukumu hilo, Ofisi ya Msajili wa Hazina inaona umuhimu wa kuwa na ushirikiano wa karibu na taasisi za China, hususan katika maeneo ya uwekezaji, usimamizi wa mashirika ya umma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
“Tunapofanya mageuzi ya taasisi zetu, tunataka kujifunza kutoka kwa nchi ambazo zimefanikiwa kupitia njia hii. China ni mojawapo ya mifano bora duniani katika kufanya mageuzi kwenye mashirika ya umma,” alisema.
Mchechu alisema baadhi ya mashirika yanayosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina tayari yana ushirikiano mzuri na taasisi mbalimbali za China, hali ambayo imeongeza umuhimu wa kuimarisha zaidi ushirikiano kati ya pande hizo mbili.
Pande hizo mbili pia zilijadili umuhimu wa kubadilishana uzoefu katika usimamizi wa mashirika ya umma, utekelezaji wa mageuzi ya taasisi pamoja na maendeleo ya miundombinu na uhamishaji wa teknolojia.
Mchechu alisema Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa sasa inasimamia taasisi na kampuni 308 ambazo serikali ina uwekezaji, zikiwemo 252 ambazo Serikali ina hisa nyingi.
Alieleza kuwa uwekezaji huo umefanywa katika sekta mbalimbali muhimu ikiwemo usafiri wa anga, nishati, mafuta na gesi pamoja na madini.
Aidha, alisema serikali inaendelea na mageuzi ya kupunguza utegemezi wa ruzuku, kuongeza mchango wa gawio serikalini, kuimarisha uwajibikaji wa taasisi na kutoa uhuru zaidi wa kiutendaji kwa mashirika ya umma.
“Hata kama tunataka uchumi uongozwe na sekta binafsi, sekta ya umma isiyo na ufanisi itaendelea kuwa kikwazo kwa sekta binafsi kustawi,” alisisitiza.
Katika mazungumzo hayo, Bw. Mchechu pia aligusia ushirikiano unaoendelea kati ya Tanzania na China katika miradi ya kimkakati ikiwemo usafiri wa majini, madini na uendeshaji wa bandari.
Pia aliishukuru China kwa kuendelea kutoa fursa za mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, akieleza kuwa watumishi sita walinufaika na mafunzo mwaka jana huku wengine watatu wakitarajiwa kupata mafunzo mwaka huu.
“Mafunzo haya yamekuja wakati muafaka na yana mchango mkubwa katika kujenga uwezo wa watumishi wetu,” alisema.
Akizungumza katika kikao hicho, Balozi Mingjian alisema China iko tayari kushirikiana na Tanzania katika kubadilishana uzoefu wa mageuzi ya kiuchumi na mabadiliko ya taasisi.
Alisema sera ya Mageuzi na Ufunguaji Uchumi ya China iliyoanza mwaka 1978 ilisaidia kuibadilisha nchi hiyo kiuchumi licha ya changamoto kubwa katika miaka ya awali ya utekelezaji.
“Tuko tayari kabisa kushirikiana na ndugu zetu wa Tanzania katika uzoefu huu wa kitaasisi,” alisema.
Aliongeza kuwa China itaendelea kuunga mkono ajenda ya Tanzania ya viwanda kupitia biashara, miundombinu, teknolojia na mafunzo ya watumishi.
Pia alibainisha kuwa serikali ya China itaendelea kutoa nafasi za mafunzo kwa watumishi wa umma wa Tanzania katika maeneo ya mabadiliko ya kidijitali, utawala na usimamizi wa uchumi.
Balozi mingjian alisema Tanzania na China zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu wenye kuaminiana, akitaja ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini China mwaka 2022 kuwa sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya mataifa hayo mawili.
Kikao hicho pia kilijadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika uongezaji thamani wa madini, ambapo Tanzania inalenga kuanzisha viwanda vya ndani vya kusafisha na kuchakata madini ya kimkakati.
Vilevile, pande hizo mbili zilijadili mustakabali wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), ambayo mwaka huu inatimiza miaka 50 ya uendeshaji wa kibiashara.
The Tanzanian government has continued to invest heavily in tourism infrastructure development as part of broader efforts to strengthen the sector’s competitiveness and increase its contribution to the national economy.
Speaking in Parliament in Dodoma on May 15, 2026, the Minister for Natural Resources and Tourism, Ashatu Kijaji said the government has made major progress in improving access and services within key tourist destinations across the country.
While presenting the ministry’s revenue and expenditure estimates for the 2026/27 financial year, Dr Kijaji revealed that the government completed the construction of three airstrips in Nyerere National Park and Ruaha National Park. She added that construction of the Mikumi Airstrip is expected to be completed by October 2026.
The minister further explained that eight additional airstrips located in Mikumi, Ruaha, Nyerere and Serengeti National Park have been rehabilitated to improve transportation services for tourists visiting the parks.
According to Dr Kijaji, the government has also constructed and rehabilitated 3,757.92 kilometers of roads and 523.14 kilometers of walking trails in protected areas, making it easier for visitors to access tourist attractions.
Tourism infrastructure has also been strengthened through the construction of six visitor rest areas and nine entry gates in Nyerere, Mikumi and Ruaha national parks.
In addition, tourism centers have been established in the forests of Mount Meru Forest Reserve, Vikindu, Mwambesi, Pindiro, Mount Rungwe and Lake Duluti. One tourist camp has also been constructed in the Kilombero Nature Forest Reserve.
Dr Kijaji said the investments are already delivering positive results, including improved accessibility to tourist attractions, enhanced visitor experiences, and increased employment and business opportunities for communities living near conservation areas.
She noted that the improvements have also contributed to higher government revenue and continued growth of the tourism industry.
Highlighting the impact of the improvements in Tanzania’s Southern Circuit, the minister said the number of tourists increased from 197,402 to 205,520 between July 2025 and April 2026. During the same period, revenue rose from 24.6bn/- to 27.7bn/-.
The minister said the achievements demonstrate the government’s commitment to continue improving tourism infrastructure in order to strengthen Tanzania’s position in the global tourism market, stimulate economic growth and improve the livelihoods of citizens.
Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza shilingi bilioni 38 katika Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) Kampasi ya Kikuletwa ili kuondoa kabisa uhaba wa wataalamu wa nishati jadidifu nchini.
Mradi huu mkubwa wa ujenzi wa mtambo wa kufua umeme kwa nguvu ya maji (Hydropower) unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo Novemba 2026, huku ukilenga kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Kanda ya Kaskazini.
Mratibu wa Mradi wa EASTRIP kutoka ATC na Kaimu Meneja wa Kampasi ya Kikuletwa, Mhandisi Sithole Mwakatage, amebainisha kuwa uwekezaji huo unajenga Kituo cha Umahiri cha Nishati Jadidifu kitakachotumia mfumo wa kisasa wa ujifunzaji kwa vitendo.
Aliyasema hayo wakati wajumbe wa Kamati Tendaji ya Usimamizi na Uongozi wa Mradi wa Kuendeleza Ujuzi (EASTRIP) walipotembelea kituo hicho kilichopo Hai mkoani Kilimanjaro leo Mei 14, 2025.
"Tumejenga kituo cha kufua umeme wa maji chenye uwezo wa kuzalisha megawati 1.65, ambacho kina dhana ya 'Factory for Teaching' (Kiwanda cha Kufundishia). Wanafunzi wanajifunza kwa vitendo kuanzia siku ya kwanza wanapoingia chuoni," alisema Mhandisi Mwakatage.
Teknolojia ya Kipekee Kusafisha Gridi ya Taifa
Mhandisi Mwakatage alieleza kuwa mtambo huo una upekee mkubwa wa kiteknolojia ukilinganisha na mitambo mingine nchini, kwani una uwezo wa kujiwasha wenyewe bila kutegemea nguvu ya gridi ya taifa wakati wa dharura (Black Start capability).
"Ni mtambo wa kisasa unaotegemea betri, na mfumo wake wa msisimko (excitation system) unatumia umeme kutoka vyanzo vya betri na kuanza kufua umeme. Mtambo huu uko kimkakati kuisaidia gridi pale inapokuwa imefeli," alifafanua Mwakatage.
Mradi huu unaenda kutatua changamoto ya muda mrefu ya mdororo wa voltage katika Kanda ya Kaskazini, hatua itakayookoa fedha za nchi zilizokuwa zikitumika kununua umeme nje ya nchi.
"Hapo awali, serikali ilikuwa imelazimika kununua umeme kutoka nchini Kenya kwa ajili ya kuimarisha voltage (Voltage Stabilization), lakini sasa uwepo wa mtambo huu unaenda kupunguza au kuondoa kabisa tatizo hilo."
Malengo Makuu na Hatua za Utekelezaji
Naye Mhandisi wa ATC anayesimamia mradi huo eneo la Kikuletwa, Mhandisi Adam Mfangavo, alieleza kuwa mradi una malengo makuu mawili: kutumika kama kituo cha umahiri cha mafunzo, uzalishaji, na ukarabati wa mifumo ya hydropower, pamoja na kuzalisha umeme utakaoingizwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia shirika la TANESCO.
Mhandisi Mfangavo alifafanua kuwa mradi unatekelezwa katika awamu mbili:
Awamu ya Kwanza: Ujenzi wa majengo mawili na ufungaji wa mitambo ulikamilika rasmi Machi 2026.
Awamu ya Pili: Imeanza mwezi huu wa Mei 2026 na itachukua miezi sita hadi kukamilika kwake Novemba 2026.
"Novemba mwaka huu, mradi utaanza kuzalisha umeme kiasi cha Megawati 1.65, unaoweza kutosha kulisha umeme magorofa 100. Mtambo ukitengeneza umeme utaanza kusambaza kwenye gridi ya taifa na pia kutumika kwa ajili ya ufundishaji," alisema Mhandisi Mfangavo.
Mradi huu tayari unanufaisha jamii inayozunguka kituo kwa kupata fursa za ajira, huku wanafunzi wa fani za Hydropower, Nishati Jua (Solar), Mitambo (Mechanical), na Umeme wakipata mafunzo ya vitendo (Industrial Practical Training).
Kupaa kwa Idadi ya Wanafunzi na Miundombinu Mpya
Kutokana na maboresho haya, Kampasi ya Kikuletwa inajipanga kupokea ongezeko kubwa la wanafunzi kutoka 70 wa awali hadi kufikia 600 mara mradi utakapoanza kazi. Chuo kimejenga kampasi mpya yenye madarasa, karakana (workshops), na mabweni ya kutosha.
Katika hatua ya kipekee, chuo kimejenga hosteli maalum kwa ajili ya wanafunzi watu wazima wenye watoto ili kuwawezesha kusoma bila vikwazo. Mbali na nishati ya maji, kuna mipango ya kupanua kituo hicho ili kuwa na mashamba ya nishati ya jua (Solar Farm), nishati ya upepo (Wind Power), na nishati ya biogas ili kukifanya kuwa kituo kamili cha umahiri katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Wanafunzi wanaosoma chuoni hapo wameonyesha kuridhishwa na uwekezaji huo mkubwa unaowapa fursa ya kujifunza kwa vitendo na mazingira bora ya chuo.
"Ninaridhishwa sana na mafunzo yanayotolewa hapa chuoni pamoja na mandhari nzuri sana ya chuo hiki," alisema Christina Mushi, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza anayesomea fani ya Mabomba (Plumbing).
Naye mwanafunzi mwenzake, Paulo Ngoyaine, aliongeza kuwa: "Chuo kiko vizuri sana na mafunzo yake yanatolewa kwa vitendo zaidi, jambo linalotujengea uwezo mkubwa."
Kukamilika kwa mradi huu kunatajwa kuwa mkombozi wa soko la ajira nchini, kwani utazalisha nguvu kazi maalum (workforce) itakayosaidia kuendesha miradi mingine mikubwa ya kimkakati kama ule wa Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP), ambalo linahitaji wafanyakazi wataalam zaidi ya 2,000 kwa wakati mmoja.
Mradi wa EASTRIP ni wa kikanda unaotekelezwa katika nchi za Afrika Mashariki ambapo kwa upande wa Tanzania, mradi huo unahusisha ujenzi na uimarishaji wa vituo vya umahiri katika vyuo vitatu vikuu: Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Dar es Salaam (DIT), na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Vituo hivyo vinatarajiwa kutoa mafunzo ya kitaalamu na ya vitendo katika sekta za nishati jadidifu, teknolojia ya habari na mawasiliano, uchakataji ngozi, pamoja na usafirishaji wa anga.
Hatua hii inalenga kuongeza ujuzi wa vijana na kuimarisha ushindani wa kikanda katika soko la ajira.
Designed by Arusha Publicity | Developed by Gadiola Emanuel