Katika kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, wadau wa sekta ya habari nchini wameeleza wasiwasi mkubwa juu ya hali ya uhuru wa vyombo vya habari, wakionya kuwa mwenendo wa kudorora unaendelea kushuhudiwa na unaweza kuathiri mustakabali wa demokrasia na haki ya kupata taarifa.



Akizungumza jijini Arusha Aprili 29, 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Anna Henga, alisema kuwa tathmini ya hali ya haki za binadamu nchini inaonesha kuwa sekta ya habari ni miongoni mwa zilizoathirika zaidi, hasa katika kipindi cha uchaguzi kilichopita.



Alifafanua kuwa katika kipindi hicho, wanahabari kadhaa walikamatwa kinyume cha taratibu, wengine kushikiliwa bila kufikishwa mahakamani, huku baadhi wakiripotiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha na wengine kuuawa. Matukio hayo yameripotiwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo Musoma, Dar es Salaam na Arusha.



“Matukio haya yanaashiria kuwepo kwa mazingira magumu kwa uhuru wa vyombo vya habari na usalama wa wanahabari nchini,” alisema Dkt. Henga.


Aidha, alieleza kuwa kufungwa kwa huduma za intaneti, hasa wakati wa uchaguzi, kumeendelea kuwa kikwazo kikubwa kwa vyombo vya habari vya mtandaoni. Alibainisha kuwa hatua hiyo inadhoofisha upatikanaji wa taarifa kwa wananchi na kuathiri uwazi.



“Unapofunga intaneti, unazuia kabisa uwezo wa vyombo vya habari kutekeleza majukumu yake katika zama za kidijitali,” alisisitiza.


Katika hatua nyingine, Dkt. Henga aligusia changamoto ya kufungiwa kwa baadhi ya vyombo vya habari kwa nyakati tofauti, hali inayodhoofisha ukuaji wa tasnia hiyo. Aliongeza kuwa hata katika robo ya kwanza ya mwaka 2026, matukio ya kukamatwa kwa wanahabari na kufungiwa kwa vyombo vya habari yameendelea kuripotiwa.



Akizungumzia suala la ubunifu, alisema kuwa hauwezi kustawi katika mazingira yenye hofu na vikwazo. Alifafanua kuwa wanahabari wanapofanya kazi katika mazingira yasiyo na uhuru, hulazimika kujikita katika maudhui ya kawaida badala ya yale yenye kuchochea mabadiliko chanya katika jamii.


“Mwanahabari hawezi kuwa mbunifu ikiwa hana uhuru wa kufanya kazi yake kwa uhuru na usalama,” alieleza.


Kuhusu mfumo wa kisheria, Dkt. Henga alieleza kuwa licha ya Katiba ya Tanzania Ibara ya 18 kulinda uhuru wa kutoa na kusambaza taarifa, bado kuna mapungufu katika baadhi ya sheria za habari na maudhui ambazo zinatajwa kukandamiza uhuru huo.


Alisisitiza umuhimu wa kufuata misingi ya haki (due process), akibainisha kuwa wanahabari na vyombo vya habari vinapaswa kupewa fursa ya kusikilizwa kabla ya kuchukuliwa hatua zozote za kisheria au kiutawala.


Aidha, alizungumzia mahusiano kati ya serikali na vyombo vya habari, akieleza kuwa bado yana mvutano, huku vyombo vya habari vikionekana kama wakosoaji badala ya washirika muhimu katika kukuza uwazi na uwajibikaji.


Katika mjadala uliofanyika sambamba na maadhimisho hayo, wadau mbalimbali walijadili mustakabali wa tasnia ya habari nchini, wakisisitiza umuhimu wa kuimarisha uadilifu wa habari katika enzi ya kidijitali na kupambana na changamoto ya taarifa potofu.


Maadhimisho ya mwaka huu, ambayo ni ya 33 nchini Tanzania, yamewakutanisha wanahabari, wahariri, wanazuoni, wanaharakati wa haki za binadamu pamoja na wawakilishi wa serikali, yakilenga kujadili nafasi ya vyombo vya habari katika kukuza demokrasia, uwazi na maendeleo endelevu.


Kwa ujumla, wadau wametoa wito kwa serikali kuchukua hatua madhubuti za kuboresha mazingira ya kisheria na kiutendaji ili kulinda uhuru wa vyombo vya habari. Wamesisitiza kuwa bila hatua hizo, hali inaweza kuendelea kudorora na kuathiri haki ya wananchi kupata taarifa sahihi kwa wakati pamoja na maendeleo ya kidemokrasia nchini.




ARUSHA: Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, huku msisitizo mkubwa ukiwekwa katika kuimarisha uhuru wa habari kama nguzo muhimu ya kukuza haki za binadamu na maendeleo endelevu.


Maadhimisho hayo yamefanyika leo, Aprili 29, 2026, katika Hoteli ya Mount Meru jijini Arusha, yakikutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari, maafisa wa serikali, na washirika wa maendeleo.

Nafasi ya Habari katika Amani



Akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Kelvin Kanje, ameeleza kuwa vyombo vya habari vina nafasi ya kipekee katika kuandaa jamii iliyoelimika na yenye utulivu.



"Vyombo vya habari ni daraja muhimu katika kujenga jamii yenye amani. Ni wajibu wetu kuhakikisha kuwa tunatumia kalamu na maikrofoni zetu kuelimisha umma na kulinda umoja wa kitaifa," alisema Kanje.




Katika kuhakikisha malengo ya maadhimisho hayo yanafikiwa, viongozi mbalimbali wamekuwa mstari wa mbele kushiriki mijadala hiyo. 



Miongoni mwao ni Naibu Katibu Mtendaji (Programu) wa Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Khamis Khalid Said, ambaye amekuwa akifuatilia kwa umakini mijadala inayozingatia mchango wa vyombo vya habari huru katika kuimarisha demokrasia, uwajibikaji, na maendeleo endelevu. Uwepo wa viongozi wa ngazi za juu wa UNESCO unatoa picha ya uzito wa jukwaa hili katika kudumisha amani na misingi ya habari nchini

Kaulimbiu ya Mwaka 2026

Maadhimisho ya mwaka huu yameongozwa na kaulimbiu isemayo: "Kujenga Mustakabali wa Amani: Kukuza Uhuru wa Vyombo vya Habari kwa Ajili ya Haki za Binadamu, Maendeleo, na Usalama." Kaulimbiu hii imelenga kuikumbusha jamii kuwa bila uhuru wa habari, ni vigumu kufikia uwazi, uwajibikaji, na usalama wa kweli.

Weledi na Changamoto Zinazoibuka

Wadau walioshiriki tukio hilo wamepata fursa ya kujadili kwa kina hali ya tasnia ya habari nchini. Miongoni mwa mambo yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na:


Kukuza Weledi: Waandishi wa habari wametakiwa kuzingatia maadili ya kazi ili kutoa taarifa zenye ukweli na uhakika.

Kukabiliana na Changamoto: Mazungumzo yalihusu jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya teknolojia na changamoto nyingine zinazoibuka katika ulimwengu wa kidijitali.

Ulinzi wa Uhuru: Wito umetolewa kwa mamlaka na wadau kulinda mazingira ya kazi ya waandishi wa habari ili waweze kutekeleza majukumu yao bila uoga.


Kuhusu Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari

Siku hii huadhimishwa duniani kote kila mwaka ili kutathmini hali ya uhuru wa vyombo vya habari, kukumbusha serikali kuhusu wajibu wake wa kuheshimu uhuru huo, na kuwaenzi wanahabari waliopoteza maisha wakitekeleza majukumu yao.

Kwa kufanyika kwa maadhimisho haya, Tanzania inadhihirisha utayari wake wa kuendelea kuimarisha mazingira ya kidemokrasia na kuhakikisha habari inakuwa chombo cha mabadiliko chanya.






Katika juhudi za kuboresha utoaji wa huduma na kuongeza ufanisi wa kiutendaji, uongozi wa Jiji la Arusha umekabidhi rasmi magari mawili mapya pamoja na mfumo wa matangazo (PA System) kwa watumishi wake.



Vifaa hivyo vimenunuliwa kwa kutumia mapato ya ndani ya jiji, hatua inayoakisi uwezo wa halmashauri kujitegemea kifedha na kuendelea kuwekeza katika kuboresha mazingira ya kazi. Uamuzi huo ni sehemu ya mikakati ya jiji ya kuhakikisha huduma zinazotolewa kwa wananchi zinakuwa bora, za haraka na zenye tija.



Akizungumza katika hafla ya makabidhiano, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, John  Kayombo, amesema kuwa upatikanaji wa magari hayo na mfumo wa matangazo utarahisisha utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kila siku. Amebainisha kuwa vifaa hivyo vitasaidia shughuli kama ukusanyaji wa mapato, ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, pamoja na utoaji wa taarifa kwa umma kwa wakati.



Aidha, amewahimiza watumishi waliokabidhiwa vifaa hivyo kuvitunza na kuvitumia ipasavyo ili viweze kudumu na kuleta manufaa kwa jiji na wananchi wake.

Kwa upande wao, baadhi ya watumishi wamepongeza hatua hiyo, wakieleza kuwa itaboresha utendaji wao na kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Hafla ya makabidhiano imefanyika katika viwanja vya Jiji la Arusha na kuhudhuriwa na watumishi pamoja na viongozi mbalimbali wa jiji hilo.

 


When we think of a Tanzanian safari, we picture the majestic Serengeti or the Great Migration from a bird’s-eye view. But for Serengeti Balloon Safaris, the secret to a world-class experience isn't just the scenery—it’s the people.

With over 35 years of soaring above the clouds, this award-winning pioneer is now launching a different kind of mission: The Trailblazers Guide Apprenticeship Program 2026.

 Closing the Gap: From Theory to the Field

Tanzania’s tourism is booming, contributing roughly 17% to the country’s GDP. However, a major challenge persists: many graduates leave school with diplomas but lack the practical, "deployable" skills the industry demands.

Managing Director John Corse puts it simply: “Investing in people is just as critical as delivering exceptional guest experiences.”

What is the Trailblazers Program?

Launched in 2025, this isn't your average internship. It is a rigorous, fully-funded intensive course followed by structured mentorship. The program has already grown from 22 to 28 participants, including a focused effort to bring more women into this traditionally male-dominated field.

The Training Toolkit includes:


* Off-Road Mastery: Defensive and off-road driving.

* Safety First: Wilderness first aid and strict safety protocols.

* Technical Savvy: Vehicle maintenance and TANAPA regulations.

* The "Luxury" Touch: High-end customer service for global travelers.


 Real Impact, Real Careers

For participants like Shamsila Kiula, the change is immediate. “I feel fully competent to work anywhere,” he shares. “I have received far more than classroom training.”

The top 10 trainees from the group secure a two-year apprenticeship as transfer drivers, while others are supported in finding roles across the wider tourism sector.

The Big Picture

In a region where only 39% of graduates are considered "job-ready," Serengeti Balloon Safaris is stepping up where it matters most. By bridging the gap between education and employment, they aren't just training staff—they are safeguarding the long-term sustainability of Tanzania as a premium destination.

The lesson is clear: To stay competitive on the global stage, we must invest in human capital. The scenery brings them here, but the service brings them back.




๐Ÿšจ


Na Mwandishi Wetu

Dar Es Salaam



Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi (CCM)mkoa wa Kilimanjaro Thomas Ngawaiya amesema kuwa serikali imesikia kilio cha wananchi walio wengi walioathiriwa na matukio ya vurugu za kabla na baada ya uchaguzi octoba 2025.


Leo April 23.2026 rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amepokea ripoti ya tume iliyoundwa kuchunguza matukio ya vurugu zilizojitokeza kabla na baada ya uchaguzi mkuu mwaka Jana iliyowasilishwa na mwenyekiti wake jaji mkuu mstaafu Othman Chande.



Katika mapendelezo ya tume hiyo ni pamoja na serikali kugharamikia matibabu kwa wale walioathiriwa sambamba na kiwasaidia vifaa na kufanya tahimini ya hasara zilizojitokeza ili kuweza kutoa kifuta machozi kwa walioathiriwa.


Ngawaiya amesema kuwa jambo Hilo lililopendekezwa na tume na kupokelewa na mheshimiwa rais limeonyesha kuwa serikali inawajali wananchi wake na kuwa tukip Hilo halikuwa na taswira nzuri kwa taifa.


'Kiukweli hapa serikali imesikia kilio cha wananchi wengi ila katika hili ni jambo zuri maana wapo walioathiriwa na walikuwa hawahusiki kwa namba yoyote Ile na vurugu hizo'amesema


Amesema kuwa vurugu zile hazikuwa na jambo jema ndani yake na kuwa wapo wengine walitumia mwanya huo katika kutaenda vitendo vya kihalifu ikiwemo wizi wa mali za watu pamoja na uharibifu wa mali.


Kwa mujibu wa Ngawaiya ambaye pia amehawi kuhudumu kama mbunge wa Jimbo la Moshi vijijini(2000-2005)ni kuwa na yeye ni mhanga katika vurugu hizo kwani baadhi ya mali zake zilizoharibika na nyingine kupotea.


'Mimi mwenyewe ni muathirika katika matukio yale mali zangu vikiwemo viti viliharibiwa na vingine viliibiwa sasa kama kutafanyika tahimini yakuona juu ya hasara Ile ni jambo jema'anasema


Anaongeza kuwa hakuna haki inayotafutwa kwa njiร  ya vurugu kama zilivyofanyika na badala yake watu hukaa katika meza ya mazungimzo ili kupata majibu kwa kile wanachokidai au kukitafuta.


Anasema vurugu zile hasipaswi kujirudia tena na si jambo la kufumbia macho kwani haileti picha nzuri kwa taifa na hata nje ya taifa kwa ujumla wake.


Mara baada ya kupokea ripoti hiyo ya tume rais Dkt Samia Suluhu Hassan amelihutubia taifa na kusema kuwa ataunda tume itakofanya tahimini ya athari walizopata wananchi na kuona jinsi ya kuweza kuwapa kifuta machozi.





Happy Lazaro.Arusha .

WAZAZI wametakiwa kuwalea watoto wao kimaadili ,huku wakiwapangia kazi za nyumbani pamoja na kuendeleza shughuli za ujasiriamali ambazo wamekuwa wakifundishwa shuleni hapo.



Hayo yamesemwa jijini Arusha na Mkuu wa shule ya sekondari St.Mary's Duluti iliyopo jijini Arusha ,Br.Protas Mangu akizungumza kwenye mahafali ya 13 ya kidato cha 6 ambapo jumla ya wanafunzi 25 wamehitimu masomo yao.




Aidha amewataka wazazi kuhakikisha wanawapa watoto wao kazi za kufanya ili waweze kujiajiri badala ya kuwaacha kukaa bila shughuli zozote kwani tayari shule ilishawajengea msingi mzuri wa kuweza kujiajiri .




"Wasikae wakitegemea taaluma waliyofundishwa tu bali waendelee kujiajiri huku wakifuga kuku ,ng'ombe,kufanya biashara na waache tabia ya kuwadekeza watoto na kuwaachia wadada wa kazi wafanye kila kitu jambo ambalo halitakiwi kabisa ."amesema .



Br.Mangu amesema kuwa, shule imeanzishwa mwaka 2007 na mahafali haya wamelenga wanafunzi wao waonyeshe bidii na ujuzi wao katika kuendeleza taaluma ambayo wanapata shuleni .


Aidha amewaasa wahitimu hao kusoma kwa bidii kwani mitihani inayokuja sasa hivi haihitaji kukariri bali kile wanachofundishwa darasani wanatakiwa wakiweke kwenye maisha ya kawaida.


Aidha amewataka wanafunzi hao kuwa makini katika kujibu maswali na kuyaorodhesha maswali wakipewa .


"Nawaasa nyie kidato cha sita muendelee kuwa na nidhamu nzuri kwani hapa sisi hatuwafundishi mambo ya taaluma tu bali tunawafundisha swala zima la maadili ,mambo ya kiroho pamoja na mambo ya michezo pia "amesema .


Aidha amefafanua kuwa wanafunzi hao wakitaka kufaulu vizuri lazima watangulize mbele swala zima la maadili .


Aidha amewataka wazazi kuhakikisha wanawalea vizuri kwani nidhamu waliyopata shuleni haitoshi kwani wao pia wana kazi kubwa ya kuwalea watoto pindi wanapokuwa nyumbani .


Ameongeza kuwa watoto hao bado ni wadogo na wanahitaji muongozo mkubwa kutoka kwa wazazi .


"Wazazi tunatangaza kuna nafasi pia ya kidato cha tano mwaka huu mwezi wa saba tunawakaribisha sana hapa shuleni watoto waweze kufundisha maswala ya taaluma na kila mmoja anajua namna ambavyo mwaka jana ufaulu ulikuwa mzuri sana wa kidato cha sita na kidato cha nne ."amesema 




Kwa upande wake mgenirasmi katika mahafali hayo ,Meneja wa tawi la NMB Usa River Hermelinda Lasihwaki amewataka wahitimu hao kuyaendeleza yale yote waliyofundishwa shuleni hapo ikiwemo swala zima la maadili kwani hilo ndilo ufunguo wa kila kitu.


"Nimeona namna ambavyo shule imewaandaa vizuri kwa kuwafundisha somo la ujasiriamali kwa vitendo ambalo mkilitumia vizuri litawasaidia sana kujiajiri 

badala ya kutegemea kuajiriwa ."amesema Lasihwaki.



 


Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam 


Kuendelea kuthamini na kununua bidhaa zinazozalishwa hapa nchini kunatajwa ni chachu katika kukuza uchumi wetu kwa mtu mmoja mmoja hadi taifa kwa ujumla wake.


Mathalani bidhaa hizi zinazozalishwa hapa nchini licha ya kuwa zinaenda kutoa fursa za soko la ajira lakini pia huchangia pato kwa wanaouza malighafi hizo moja kwa moja



Kiwanda cha kuzalisha bidhaa za ngozi cha Woisso Original Products (WOP)kilichopo Salasala jijini hapa ni miongoni kwa viwanda vinavyozalisha bidhaa za ngozi hapa nchini na kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa sekta hiyo ya ngozi.



Mkurugenzi wa kiwanda hicho Kenneth Woisso anasema kuwa bidhaa za ngozi zinazozalishwa hapa nchini kwa kiasi kikubwa zinachangia ukuaji wa pato la taifa uzalishaji wa ajira sanjari na kuzalisha wataalam wa utengenezaji wa bidhaa hizo


'Sekta hii ina faida na kama ilivyo hata vijana wanapata utaalamu hapa namna yakutengeneza bidhaa hizi hivyo kuwawezesha kujiajiri pia lakini katika masoko pia tunaendelea kujitangaza vyema'anasema



Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo ni kuwa ipo haja kwa sasa kwa watu kuwa na uelewa wakutosha kwa kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini kwani faida yake ni kubwa na huuzwa kwa bei inayoendana na hali halisi ya kipato cha mtanzania


Anasema wapo baadhi ya watu ambao hupenda kukimbilia bidhaa za ngozi kutoka nje ya nchi bila kujua athari zake kiuchumi na kuwa mataifa mengine hutumia mwanya huo kuzalisha bidhaa zenye mfanano wa ngozi hivyo kudidimiza soko la ndani.


Woisso anasema ikiwa jamii ya kitanzania itaendelea kuwa na mwamko wa kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini kama ilivyo kwa sasa ni kuwa kwa kipindi kifupi sekta hiyo itaenda kupiga hatua kubwa zaidi ya sasa


'Tunazalisha bidhaa mbali mbali zitokanazo na ngozi kama mikoba,mikanda,viti,viatu pochi na vingine vingi hii ni kuhakikisha katika uzalishaji wetu kila aina ya bidhaa unaoitaka ya ngozi utaipata hapa WOP'anasema


Michael Mshiu anasema sekta ya ngozi inaenda kufanya vizuri kama jitihada za maksudi zitafanywa ikiwa ni pamoja na kuthamini wazalishaji wa ndani badala ya kukimbilia zitokazo nje


'Hali hii ni lazima tuongeze jitihada za maksudi katika kuhakikisha sekta hii inaenda kukua ikiwa ni pamoja na kuendelea kuthamini bidhaa za wazalishaji wazawa'anasema



 


Na Mwandishi Wetu - Rombo


ILI kuweza kufanya shughuli za kimaendeleo zenye uhakika ni lazima kuhisisha makazi bora na salama yakudumu ili kuondokana na wasiwasi wakubomokewa na nyumba hususan katika kipindi kama hili cha mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali hapa nchini.



Kuwa na makazi salama ni  kuhakikisha wa kuwa nguvu na akili zitatumika katika kufanya mambo mengine ya kimaendeleo badala yakuishi kwa wasiwasi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.


Kwa maana hiyo katika kupata suluhisho hilo kwa mikoa ya kanda ya kaskazini yaani Arusha,Tanga,Manyara na Kilimanjaro kwa sasa wameweza kupata mkombozi wa kuwezesha upatikanaji wa makazi hayo kwa gharama nafuu.



Rock Block ni kampuni ya kizawa liyopo wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro inayojihusisha na uzalishaji na usambazaji wa malighafi mbali mbali za ujenzi ikiwemo matofali yatokanayo na mwamba.


Fabian Woisso ni mkurugenzi wa kampuni hiyo ambapo anasema kuwa kwa zaidi ya miaka kumi sasa wameweza kufikisha huduma hiyo kwa watu mbali mbali pia taasisi lengo likiwa ni kuboresha makazi.



'Tangu tumeanza uzalishaji miaka kumi iliyopita tumeshawafikia wateja mbali mbali na kimsingi wameridhishwa na huduma hii ambayo ni rafiki kwani inapunguza gharama katika ujenzi'anasema


Anasema kuwa malighafi hizo hutokana na miamba moja kwa moja na hivyo kazi yao kubwa ni kuikata au kuichonga kadri mteja anavyohitaji na uimara wake ni wa uhakika kwani hauathiriwi na magadi au fangasi.


Mkurugenzi huyo anasema kuwa wafanyabiashara wengi wanaouza malighafi za ujenzi ikiwemo matofali hutumia kiwango kidogo cha saruji lengo likiwa ni kuzalisha matofali mengi kwa gharama ndogo ili kujipatia faida nono.


Kutokana na hali hiyo hupelekea wanunuzi kupata hasara kwa kipindi kifupi ikiwemo matofali kuvunjika wakati wa kupakia au kuyashusha tofauti na hayo yatokanayo na miamba migumu.


Hilda Mathew ambaye ni dalali wa vifaa vya ujenzi ikiwemo matofali,mchanga na moramu anasema kuwa matofali yatokanayo na miamba yamekuwa na wateja wengi kutokana na unafuu wake wa bei ikilinganishwa na yale yakufyatua.


'Matofali ya miamba(Rock Block)soko lake ni nzuri kwani wateja wanayapenda sababu gharama zinakuwa chini kwani kuyashusha hakuna gharama tena na hayavunjiki hivyo utumiaji wa saruji unakuwa ni mdogo maana hakuna maungio mengi'anasema



 


Na Mwandishi Wetu, Moshi


Katika kuhakikisha kuwa shule  kongwe katika kata ya Mwika Kusini iliyopo wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro zinarudi katika ubora wake wananchi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wameanza kuzikร rabati shule hizo kwa nguvu zao wenyewe kama walivyofanya kwenye mradi wa barabara.


Wananchi hao waliweza kukarabari barabara zenye urefu wa  takribani kilomita 64 hususan katika kijiji cha  Kiruweni ambapo fedha zaidi ya milioni 600 zilitumika kwa kuchimba barabara hizo sambamba na uwekaji wa moramu na ujengaji wa  kingo za maji.


Baada ya kufanikiwa kwa kiwango kikubwa wananchi hao kwa sasa wamejikita katika kuongeza nguvu kwa kukarabati shule kongwe ili ziweze kuwa na mazingira rafiki katika utoaji wa elimu sambamba na kuwa na muonekano wa kisasa.


Tayari zoezi hilo limeanza katika shule ya msingi Karoro ambapo ujenzi wa choo cha walimu unaendelea ili kuondoa adha iliyokuwa ikiwakumba walimu wapatao 6 kujisaidia choo kimoja na wanafunzi



Pia ukarabati wa ofisi ya walimu uwekaji wa sakafu katika baadhi ya vyumba vya madarasa shule ya msingi Mawanda unaendelea na umefikia hatua nzuri ila bado haujakamilika


Hata hivyo bweni la wasichana katika shule ya sekondari Mangi Marialle unaendelea ambapo sasa pindi litakapokamilika huenda kiwango cha ufaulu kwa wasichana kikaongezeka.



John Tarimo ni diwani wa kata ya Mwika Kusini ambapo amesema wananchi hao kwa sasa wamejikita katika kuchangamkia maendeleo na kuwa bado miradi hiyo hajakamilika na michango bado inahitajika ili mambo mengine yafuate


'Hawa ni wananchi wenye maono waliona ni vyema kufanya kile wanachokiona kinafaa kwa muda huo na sio kusubiri serikali ifanye kila jambo kwani mengine yapo ndani ya uwezo wetu'anasema


Anasema kuwa wananchi hao wameamini kuwa maendeleo yataletwa na wao wenyewe na ndio maana wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wanafikia kile wanachokiamini badala ya kuishi kwa kusubiria kila kitu waletewe.


Kaanael Malle mkazi wa Mawanda anasema maono ya wadau hao wa maendeleo kutaenda kuifufua shule yao na iweze kuwa na mazingira rafiki ya utoaji wa elimu tofauti na ilivyokuwa hapo awali  mithili ya ghofu.





Na Mwandishi Wetu

Moshi


BARABARA zenye urefu wa kilomita 64 zilizojengwa kwa nguvu za wananchi na wadau, wa maendeleo katika kijiji cha Kiruweni kata ya Mwika Kusini wilaya ya Moshi zipo hatarini kuharibika baada ya malori yanayodaiwa kubeba vifaa vya ujenzi kuzitumia kama njia ya ukwepaji ushuru.


Baadhi ya malori ambayo yanadaiwa kubeba vifaa hivyo kama mchanga, mawe, kokoto, na matofali kutoka wilaya ya Rombo eneo la Holili huzitumia kama njia ya ukwepaji wa ushuru wa halmashauri na pia kukwepa kupitia katika mizani.


Mwenyekiti wa kitongoji cha Kiruweni kati Jackson Machang'u amesema kuwa ipo haja ya mamlaka husika kuangalia upya jambo hilo kwani linasababisha hasara mara mbili ikiwemo kuharibu barabara lakini pia kuikosesha halmashauri mapato.


Amesema kuchelewa kudhibiti malori hayo kunaenda kuleta athari kubwa zaidi ikiwemo kuharibu barabara hizo zilizojengwa kwa nguvu za wananchi kwani hubeba mzigo mkubwa tofauti na viwango vilivyowekwa kisheria.


"Ipo haja ya mamlaka zinazohusika sasa kuona hili tatizo kwa sababunkwa siku sio chini ya malori 60 hadi 70 yanapita hivyo inaweza kuona ni nanma gani tatizo lilivyo kubwa katika eneo letu hili'amesema



John Tarimo diwani wa kata ya Mwika Kusini amesema kuwa tayari ameshapata malalamiko hayo na kuwa tayari ameshayafikisha kwa mamlaka husika ili kuweza kuchukuliwa kwa hatua kabla athari hazijawa kubwa zaidi ya hivi

 sasa.


Amesema ukweli ni kuwa barabara hizo zinapoharibika tatizo litabaki palepale kama ilivyo kuwa mwanzoni na kuwa kama sehemu ya kijiji hawezi kukubali kuona jitihada za wananรงhi hao zinakwamisha kwa maslahi ya watu wachache


'Ikumbukwe tulitumia muda na fedha nyingi katika mradi huu wa barabara sasa maslahi ya wachache yasituharibie na kuturudisha kule tulipotoka mwanzoni'amesema





ARUSHA: Maandalizi ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yameshika kasi jijini Arusha, huku Serikali ikisisitiza kukamilika kwa wakati kwa miradi ya kimkakati ya barabara itakayohudumia mashindano hayo makubwa barani Afrika.



Akizungumza Aprili 17, 2026, wakati wa ziara ya ufuatiliaji wa miradi hiyo, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amebainisha kuwa ujenzi wa miundombinu ni kipaumbele cha kimkakati cha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kuhakikisha Tanzania inatoa taswira ya kipekee wakati wa michuano hiyo.

 Miradi ya Kilometa 13 Kukamilika Mapema



Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta, ameeleza kuwa mkandarasi China Civil Engineering Construction Company (CCECC) ameanza kazi rasmi tangu Aprili 10, 2026. Ingawa mradi wote wa barabara ya Mbauda – Losinyai unatarajiwa kukamilika mwaka 2029, kipaumbele kimewekwa kwenye kipande cha kilometa 13 ambacho lazima kikamilike kabla ya AFCON 2027 kuanza.

Mchanganuo wa Barabara Hizo:


* Mbauda – Bondeni City (km 9): Itajengwa kwa njia nne na kuwekwa taa.

* Tanganyika Packers – Makutano ya Arusha Bypass (km 4): Itakamilika mapema kurahisisha usafiri.

* Soko la Kilombero – Msikiti wa Ngarenaro – Kisongo (km 9.1): Itajengwa kwa njia nne kuelekea Kisongo.



Waziri Ulega aliongeza kuwa barabara hizi si tu kwa ajili ya mashindano, bali zitasaidia kutatua kero ya muda mrefu ya mafuriko jijini Arusha kutokana na ujenzi wa mitaro mikubwa ya kisasa.

 Bilioni 27 Zaidhinishwa, Mkandarasi Alipwa

Katika kuhakikisha kazi haiingiliwi na vikwazo vya kifedha, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameidhinisha jumla ya shilingi bilioni 27. Kati ya hizo, bilioni 17.6 tayari zimekwishalipwa kwa mkandarasi kama malipo ya awali, huku bilioni 10 zikitengwa kwa ajili ya kuwafidia wananchi waliopisha mradi huo.

 Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba Asisitiza Amani


Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania kuendelea kulinda na kudumisha amani, akieleza kuwa miradi mikubwa kama hiyo ya maendeleo haiwezi kutekelezeka bila utulivu.



"Tuwe makini na watu wanaohamasisha uvunjifu wa amani. Lazima tulinde amani ya nchi yetu ili tuweze kuendeleza shughuli hizi za maendeleo," alisisitiza Dkt. Mwigulu wakati akihutubia wananchi katika eneo la Kona ya Mbauda.



Kukamilika kwa barabara hizi kutabadili sura ya Jiji la Arusha, kupunguza msongamano, na kuweka mazingira rafiki kwa wageni na wenyeji wakati wa shamrashamra za AFCON 2027.



 

Mwandishi wetu,Njombe.



Chama cha wafanyakazi katika vyombo vya habari Tanzania(JOWUTA),kimetaka ushirikishwaji zaidi wa vyombo vya habari katika maadhimisho ya kitaifa ya Mei Mosi mkoani Njombe.


JOWUTA  inashiriki Mei Mosi yake ya kwanza mwaka huu kama mwanachama wa shirikisho la vyama.vya wafanyakazi nchini(TUCTA) na inatarajia kutoa zawadi kwa wafanyakazi bora katika vyombo vya habari.



Akizungumza katika kikao hicho,Mwenyekiti wa JOWUTA Taifa,Mussa Juma licha ya kupongeza Kamati ya Habari na Matangazo ya Mei Mosi kitaifa, alisema bado ushiriki wa vyombo vya habari ni sio mkubwa.


Juma alisema, Kamati hiyo inapaswa kuvishirikisha zaidi vyombo vingi.vya habaro ikiwepo mitandao ya kijamii,Magazeti,Luninga na Radio kuwapa habari na matangazo.



"Lakini pia ni muhimu maudhui ya matangazo yalenge kuonesha vitu vya kipekee vilivyopo mkoa wa Njombe"alisema


Juma aliahidi JOWUTA yenye wanachama wanahabari zaidi ya 400 nchi nzima  ipo tayari kushirikiana na kamati za Mei mosi kuongeza kazi za utangazaji na kuelezea umuhimu wa watanzania kushiriki maadhimisho hayo.



Naye Mwenyekiti wa Taifa wa RAAWU ,Jane Mihanji alikumbusha kamati ya hiyo kukumbuka umuhimu wa kugharamia magazeti ambayo yamekuwa yakitoa matoleo maalum ya Mei mosi kwa wakati.


"Matoleo haya ikiwepo jarida Uhuru wa kijani yamekuwa yakitoa makala maalum za utekelezwaji  wa miradi mbalimbali ya serikali na sekta binafsi na kugawanywa bure wa maelfu ya watu siku ya Mei Mosi "alisema


 Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Tumaini Nyamhokya alisema ,Njombe ina vitu vingi vya kuvitangaza kupitia maadhimisho ya Mei Mosi


"Mei mosi ni fursa kwa wakazi mkoa Njombe kuna mengi ya kutangaza mkoa huu ikiwepo kilimo kikubwa cha maparachichi,viasi mbatata,mbao na maporomoko ya maji na Utalii"alisema.



Wakati huo.huo,Kamati ya maandalizi ya Mei mosi kitaifa imetembelea maandalizi ya ujenzi wa uwanja Mei Mosi na kutaka kasi zaidi iongezwe ili ukamilike ifikapo.April.25 mwaka huu.





Arusha, Tanzania – April 13, 2026

The East African Legislative Assembly (EALA), sitting in its 4th Session of the 5th Assembly in Arusha, has taken a significant step toward strengthening regional efforts against human trafficking by considering the introduction of the East African Community Counter-Trafficking in Persons Bill, 2026.



The motion, moved by Fatuma Ndangiza, a Member of EALA representing Rwanda, and seconded by Gai Deng of South Sudan, seeks leave to table the Bill. The proposed law aims to establish a binding regional legal framework to prevent trafficking, protect victims, and enhance cross-border cooperation among East African Community (EAC) Partner States.

“The EAC must strengthen harmonized prevention and prosecution approaches while ensuring that victims receive comprehensive, rights-based support and meaningful access to justice,” said Ndangiza during the session.

A Stronger Regional Legal Framework

The proposed legislation responds to the evolving nature of trafficking, including the use of digital recruitment and organized criminal networks. It aligns with international instruments such as the Palermo Protocol, the Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination against Women, and the Maputo Protocol.

The Bill emphasizes:

  • Survivor-centered and human rights-based approaches

  • Gender-responsive and child-sensitive protection measures

  • Enhanced regional cooperation in investigations and prosecutions

  • Addressing root causes such as poverty, inequality, and conflict

It also mandates victim support services, including medical care, legal aid, education, and safe, voluntary repatriation.

Agroecology Bill Also Introduced

In a parallel development, EALA also considered the East African Community Agroecology Bill, 2026, introduced by Gideon Gatpan Thoar, a Member representing South Sudan, and seconded by Falhada Iman Dekow of Kenya.

The Bill aims to mainstream agroecological farming across the region by promoting sustainable agricultural practices that enhance biodiversity, soil health, and food security.

“This Bill provides a coherent framework for integrating ecological and social approaches into agriculture while safeguarding food sovereignty,” Thoar noted.

Key proposals include:

  • Establishment of National Agroecology Councils

  • Promotion of farmer-led innovation and traditional knowledge

  • Reduction of hazardous pesticide use

  • Strengthening climate resilience and sustainable food systems

The initiative has received support from Willow International, which focuses on restorative support services for trafficking survivors.

Oath-Taking Ceremony



During the same sitting, the Speaker of EALA, Joseph Ntakirutimana, presided over the swearing-in of James Kinyasi Milya as an ex-officio member.



Milya currently serves as Tanzania’s Deputy Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation, responsible for EAC Affairs. He previously served in EALA before being elected to Tanzania’s Parliament representing Simanjiro constituency under Chama Cha Mapinduzi (CCM).



Salary Crisis Sparks Concern

Meanwhile, the Assembly addressed concerns over delayed salaries for its members and staff. A motion moved by Kennedy Mukulia, representing South Sudan, led to the adoption of two resolutions urging immediate intervention.

“The Council of Ministers must urgently address the non-payment of salaries and ensure all deducted funds are returned,” Mukulia emphasized.

EALA members and staff have reportedly gone for months without pay, raising concerns about operational stability within the regional body.

The developments highlight EALA’s ongoing efforts to strengthen regional integration through legislative action, while also addressing internal challenges affecting its workforce.