NgÅ©gÄ© wa Thiong’o, mmoja wa waandishi mashuhuri wa fasihi ya kisasa ya Afrika, ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 87. Kwa zaidi ya miongo sita, NgÅ©gÄ© alisimulia hadithi za mapambano ya ukombozi, udhalimu wa ukoloni, na matumaini ya Afrika huru. Alikuwa mwandishi, mwanafalsafa, na mtetezi shupavu wa lugha za Kiafrika, ambaye alikataa kufungwa na mipaka ya lugha, siasa, wala mateso ya kibinafsi.
Alizaliwa mwaka wa 1938 katika kijiji cha Kamiriithu karibu na Limuru, wakati Kenya bado ilikuwa chini ya utawala wa kikoloni wa Uingereza. Akiwa mtoto wa familia maskini ya wakulima, wazazi wake walifanya juhudi kubwa kumpeleka katika shule ya upili ya Alliance, ambapo aliibuka kuwa mwanafunzi mwenye ari na akili pevu.
Mnamo 1959, Ngũgĩ alielekea Uganda kusomea katika Chuo Kikuu cha Makerere, ambapo aliandika riwaya yake ya kwanza, Weep Not, Child. Chinua Achebe, mwandishi wa Things Fall Apart, aliona uwezo mkubwa ndani yake na kumsaidia kuchapisha kitabu hicho nchini Uingereza.
"Achebe ndiye aliyeniweka kwenye ramani ya fasihi. Aliona kitu ambacho hata mimi sikuwa nimekiona," aliwahi kusema Ngũgĩ.
Mwaka wa 1977, NgÅ©gÄ© alifanya uamuzi wa kubadili jina kutoka James Thiong’o NgÅ©gÄ© kuwa NgÅ©gÄ© wa Thiong’o – ishara ya kujikomboa kutoka kwa majina ya kikoloni. Mwaka huo pia alikamilisha Petals of Blood, riwaya ya mwisho kuandika kwa Kiingereza, iliyowakosoa vikali viongozi wa Kenya huru kwa kuwa mabwanyenye wa aina mpya.
Katika mwaka huo huo, alishiriki katika uandishi wa tamthilia Ngaahika Ndeenda (Nitaolewa Ninapotaka), ambayo ilipigwa marufuku na serikali. Hapo ndipo alikamatwa na kufungwa jela kwa mwaka mmoja bila mashitaka.
Ngũgĩ alilazimika kuingia uhamishoni, akiishi Uingereza na kisha Marekani, ambako alifundisha katika vyuo vikuu vya Yale, New York na California Irvine. Alikaa nje ya Kenya kwa miaka 22, hadi alipopokelewa kama shujaa mwaka wa 2004.
Ngũgĩ hakuwahi kujibu hadharani madai hayo.
Katika miaka yake ya mwisho, alikabiliwa na changamoto kubwa za kiafya: saratani ya kibofu, matatizo ya moyo na figo. Mwaka 2019, alipitia upasuaji wa moyo mara tatu. Alikuwa mpambanaji hadi mwisho – akishinda hata ugonjwa uliotabiriwa kumuua.
NgÅ©gÄ© wa Thiong’o sasa ametoweka, lakini kazi zake – A Grain of Wheat, The River Between, Devil on the Cross, Matigari – na ndoto yake ya Afrika inayojieleza kwa sauti yake yenyewe, zitaendelea kuishi milele.




0 Comments:
Post a Comment