DK PIMA NA WENZAKE WAFUNGWA MIAKA 20, ZIJUE KESI NYINGINE ZINAZOWAKABILI

Dk John Pima na washitakiwa wenzake wakiongea na wakili wao, Moses Mahuna

ALIYEKUWA Mkurugenzi  wa jiji la Arusha dkt John Pima na wenzake wawili wamehukumiwa  kifungo cha miaka 20 jela  baada ya kukutwa na hatia ya makosa ya uhujumu uchumi yaliyokuwa yakiwakabili.


Wengine waliohukumiwa pamoja na Pima ni pamoja na aliyekuwa Mwekahazina wa jiji la Arusha Mariam Mshana na aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji, Innocent Maduhu.


Hukumu hiyo imetolewa leo Agosti 31,2023 na Hakimu Mkazi, Saraphina Nsana wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha aliyekuwa akisikiliza shauri hilo la uhujumu uchumi  namba 5 /2022.


Hakimu Nsana amesema kuwa baada ya kupitia ushahidi wa pande zote mbili imejiridhisha pasipo shaka na  ushahidi wa upande wa mashtaka na kuwatia hatiani.


"Kwa kuzingatia ushahidi huo na kwamba kama washtakiwa wanarekodi ya makosa ya jinai ,na utegemezi wa familia mahakama inawahukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka 20 kila mmoja na iwapo kama hamjaridhika na adhabu hiyo nafasi ya kukata rufaa ipo wazi".


Hata hivyo bado Dk. Pima na wenzake wanakabiliwa na kesi nyingine mbali na kesi hiyo ya Uhujumu Uchumi ,namba 5/ 2022. 


Awali,Katika kesi hiyo namba 5/2022 Dk Pima na wenzake walikuwa wanakabiliwa na mashitaka sita  ya uhujumu uchumi na  mawili ya utakatishaji fedha ambayo hayana dhamana.


Mashitaka mengine ni kutumia nyaraka kwa nia ya kumdanganya mwajiri ,ufujaji na ubadhirifu ambayo Dk Pima na wenzake walisomewa Juni 21, mwaka huu mbele ya hakimu Mkazi wa mahakama hiyo , Bittony Mwakisu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 5/2022.

Dk Pima na wenzake kwani Juni 17, 2022 walifikishwa mahakamani hapo wakikabiliwa na makosa nane ya ufujaji wa mali ya umma na kughushi nyaraka katika kesi mbili za uhujumu uchumi.


Ambapo kesi hiyo inawakabili washitakiwa watano wakiwemo   waliokuwa wachumi katika jiji hilo, Nuru Ginana na Alex Daniel.


Katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 5/2022, iliyosemwa Juni 21, 2022 huu washtakiwa hao wanakabiliwa na makosa sita ambapo kosa la kwanza linalowakabili ni ufujaji na ubadhirifu wa Sh103 milioni, kosa la pili na la tatu ni kutumia nyaraka kwa malengo ya kumdanganya mwajiri.



Kosa la tano linalomkabili Maduhu peke yake  ni utakatishaji fedha huku la sita likiwa ni la utakatishaji fedha linawakabili washitakiwa wote watatu.


Akiwasomea mashitaka hayo, Wakili wa Serikali, Charles Kagilwa alieleza mahakamani hapo kuwa shitaka la kwanza linawakabili washitakiwa wote watatu ambapo ni la ufujaji na ubadhirifu kinyume cha sheria ya uhujumi uchumi na sheria za kuzuia na kupambana na rushwa.


lidai mahakamani hapo kuwa  washitakiwa wote katika tarehe tofauti kati ya Machi 28, 2022 na April 14,2022 huu wakiwa wameajiriwa wa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI wakiwa kama mkurugenzi wa halmashauri jiji la Arusha, Mkuu wa Idara ya Fedha na  mkuu wa Idara ya Uchumi na Mipango waliweza kutumia milioni 103 ambazo zimekuja kwao kupitia nafasi zao.


Wakili wa serikali Kagilwa alieleza kuwa  shitaka la pili linawakabili washitakawa wote watatu ambapo wanadaiwa  walituma  nyaraka kwa nia ya kumdanganya mwajiri wao kinyume cha sheria za kuzuia na kupambana na rushwa na uhujumi uchumi.


Alidai kuwa mnamo tarehe 27 machi mwaka huu katika jiji wilaya na mkoa wa Arusha washitakuwa hao  wakiwa wameajirikiwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kutumia nyaraka, dokezo walitoa taarifa zao uongo kuonyesha kwamba Maduhu aliomba masurufu kwa ajili ya kununua mchanga moramu shilingi milioni 103 kwa nia ya kutengeneza matofali wakati wakijua ni uongo.

Katika kosa la tatu ilidaiwa mahakamani hapo kuwa  washitakiwa wote walitumia nyaraka kumdanganya mwajiri wao ambapo mnamo tarehe 27 machi, huu katika jiji wilaya na mkoa wa arusha kwa nafasi ya mkurugenzi  wa jiji la Arusha, Mkuu wa kitengo cha fedha na Mkuu wa  kitengo cha mipango na uchumi waliweza kumdanganya mwajiri.


lidaiwa waliandaa maombi ya masurufu ya safari zikiwa na taarifa za udanganyifu wakijifanya bwana, Innocent Maduhu ambaye ni mchumi aliomba malipo ya kiwanda cha ujenzi wa kiwanda cha matofali kiasi  cha shilingi milioni 103.


Ilidaiwa katika shitaka la nne washitakiwa hao walitumia nyaraka kwa nia ya kumdanganya mwajiri wao ambapo mnamo Aprili 28, mwaka huu walijifanya kuonyesha Maduhu alirejesha fedha za ununuaji 'material' kwa ajili ya ununuaji wa vifaa vya kujenga kiwanda cha matofali wakati wakijua si kweli.

Shitaka la tano la utakatishaji fedha linalomkabili, Madihu peke yake ambapo anadaiwa  mnamo Aprili , mwaka huu alijipatia gari yenye namba za usajili T 844 DYY aina ya Subaru Forester kwa fedha ambazo ni zao la uhalifu la  kumdanganya mwajiri wake

Wakili Kagilwa alisoma shitaka la sita la utakatishaji fedha linalowakabili washitakiwa wote watatu   wanadaiwa kuwa katika terehe tofauti kati ya Machi 23, mwaka huu na Mei 25, mwaka huu walijipatia fedha taslim sh milioni 103 wakati wakijua fedha hizo zilitokana na zao la uhalifu la kumdanganya mwajiri wao.



Awali Juni 17,2022, Dk Pima na wenzake wanne walifikishwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Bittony Mwakisu, wakikabiliwa na makosa nane katika kesi mbili za uhujumu uchumi.




Dk Pima na wenzake watatu Innocent Maduhu (aliyekuwa mchumi wa Jiji), Nuru Ginana (mchumi), Alex Daniel (mchumi), 




Hata hivyo mshitakiwa mwingine ni Mshana ambaye alikuwa Mwekahazina wa Jiji hilo  hakuwepo mahakamani hapo, hivyo upande wa Jamhuri ukaomba  mahakama kutoa hati ya wito na kukamatwa kwa mshitakiwa huyo ambaye ni wa pili katika kesi zote.


Jamhuri iliwakilishwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Akisa Mhando na Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Hamidu Simbano huku Dk Pima na Maduhu wakiwakilishwa na Wakili Valintine Nyalu.


Katika kesi ya kwanza,  Dk Pima, Mariam, Maduhu na Ginana wanakabiliwa na mashitaka manne ambayo ni ufujaji na ubadhirifu huku makosa mengine yakiwa ni matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri.


Aidha washitakiwa hao wataendelea kukaa mahabusu baada ya kushindwa kukidhi masharti ya dhamana ambapo kila mmoja anapaswa kuwa na wadhamini wawili watakaoweka kiasi cha shilingi 32 milioni au kuwasilisha hati ya mali isiyohamishika yenye thamani hiyo ambapo hawakuweza kukamilisha masharti hayo.




Awali katika kesi ya kwanza ya uhujumu uchumi namba 3/2022 inawakabili Dk Pima,Mariam,Maduhu na Ginana wanakabiliwa na mashitaka manne ambayo ni ufujaji na ubadhirifu huku makosa mengine yakiwa ni matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri.


Kosa la kwanza ni ufujaji na ubadhirifu ambapo kwa pamoja wanadaiwa kati ya Aprili 14 hadi 16 mwaka huu,katika wilaya na Mkoa wa Arusha wakiwa waajiriwa wa serikali,walitenda  kosa la ufujaji na ubadhirifu wa fedha  Sh67 milioni.


Shitaka la pili ni matumizi ya nyaraka kwa malengo la kumdanganya mwajiri ambapo wanadaiwa kutumia nyaraka iliyokuwa na kichwa cha habari dokezo lenye maelezo kuwa Nuru amenunua na kusambaza moramu yenye thamani ya Sh65 milioni kwa ajili ya Soko la Samunge huku wakijua nyaraka hiyo siyo ya kweli na wakimdanganya mwajiri.


Shitaka la tatu ilidaiwa kuwa ni matumizi ya nyaraka kwa malengo ya kumdanganya mwajiri,ambapo wanadaiwa Aprili 14,2022 wakiwa na nia ovu walitumia nyaraka ya maombi ya masurufu(safari) ikionyesha Nuri amenunua na kusambaza moramu ya Sh65 milioni huku wakijua wanamdanganya mwajiri wao.


Alitaja shitaka la nne kuwa ni matumizi mabaya ya nyaraka kwa malengo ya kumdangaya mwajiri ambapo wanadaiwa Aprili 28,mwaka huu wakiwa na nia ovu ua kumdanganya mwajiri walitumia nyaraka ya marejesho ya masurufu ikionyesha Nuru amefanya marejesho ya Sh65 milioni ikiwa ni malipo maalum ya  kazi za nje ya kituo chake cha kazi.


Katika kesi ya pili ya uhujumu uchumi namba 4/2022 washitakiwa ni Dk Pima,Mariam,Maduhu na Daniel wanakabiliwa na makosa manne ikiwemo la ufujaji na ubadhirifu pamoja na matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri.


Akiwasomea mashtaka hayo,Wakili Akisa alidai kosa la kwanza ni ufujaji na ubadhirifu ambapo kati ya Aprili 14 hadi 16,mwaka huu wakiwa waajiriwa wa serikali kwa pamoja na kwa nia ovu walifanya ufujaji na ubadhirifu wa fedha za umma kwa matumizi yao binafsi Sh65 milioni iliyokuwa imetolewa kwa ajili ya matumizi ya umma.


Alitaja shitaka la pili katika kesi hiyo kuwa ni matumizi ya nyaraka kwa malengo ya kumdanganya mwajiri kinyume na sheria ambapo wanadaiwa Aprili 14,mwaka huu walimdanganya mwajiri kupitia nyaraka yenye dokezo lililokuwa linahusiana na shughuli za kila siku za mwajiri ambapo walidanganya Daniel amenunua na kusambaza moramu yenye thamani ya Sh65 milioni huku wakijua kwa kufanya hivyo ni kumdanganywa mwajiri.


Alidai shitaka la tatu kuwa ni matumizi ya nyaraka kwa malengo ya kumdanganya mwajiri ambapo,Aprili 14,mwaka juu wakiwa na nia ovu walitumia nyaraka ya maombi ya masurufu,ikiwa na maelezo ya uongo yakionyesha Daniel amesambaza moramu kwa ajili ya matengenezo ya barabara hivyo adai Shilingi 65 milioni huku wakijua wanamdanganya mwajiri wao.

Shitaka la nne ni matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri ambapo wanadaiwa kwa pamoja wakiwa na nia ovu kupitia nyaraka iliyokuwa na kichwa cha habari marejesho ya masurufu iliyoandikwa Aprili 26,2022 iliyohusiana na shughuli za mwajiri.




Alidai nyaraka hiyo ilikuwa na maelezo ya udanganyifu kuwa Alex anafanya marejesho ya Shilingi 65 milioni ikiwa ni matumizi ya kusambaza moramu katika taasisi mbalimbali za serikali kwa ajili ya kutengeneza barabara huku wakijua kwa kufanya hivyo wanamdanganya mwajiri.


Aidha washitakiwa hao walikana kutenda makosa hayo ambapo Mahakama ilitoa masharti ya dhamana kuwa kila mshitakiwa awe na wadhamini wawili kila mmoja adeposit Sh32.5 milioni au hati ya mali isiyohamishika yenye thamani kama hiyo.


Washitakiwa hao walitakiwa kutokusafiri nje ya mipaka ya  Tanzania na kuwasilisha hati zao sa kusafiria ambapo pia walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kuwa wataendelea kukaa mahabusu hadi watakapotimiza masharti hayo.


Mashauri haya yamekuja baada ya Mei 24,2022, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuwasimamisha kazi maafisa sita wa Jiji hilo kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za jiji na tuhuma za kughushi nyaraka.





 







0 Comments:

Post a Comment