Samia; Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi Kama 'Maktaba Inayotembea'

 Samia; Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi Kama 'Maktaba Inayotembea' 

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hussein Ali Mwinyi wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Hayati Rais Mstaafu Dkt Ali Hassan Mwinyi muda mfupi kabla hajazikwa visiwani Zanzibar 
Samia Suluhu, ikiwa ya kumuaga Hayati Dkt. Ali Hassan Mwinyi, Rais staafu wa awamu ya 
Wake wa Hayati Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi,  Bibi Siti Mwinyi na Khadija Mwinyi / Picha : Ikulu Tanzania



Viongozi waliohudhuria mazishi ya Hayati ALi Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa awamu y apili Zanzibar /Picha: Ikulu Tanznaia 

Samia Suluhu Hassan amesifu kumbukumbu ya Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakati wa mazishi yake huko Zanzibar, akimtaja kuwa "maktaba inayotembea na inayosheheni vitabu vyenye mafunzo ya uadilifu na uzalendo." 

Alimkumbuka kama kigingi kilichosimama kukuza na kulea maendeleo ya nchi, na kuongeza kuwa licha ya changamoto alizokumbana nazo, aliweza kuliongoza taifa kwa uadilifu na mafanikio makubwa.


Rais Samia pia alimulika uongozi wa Marehemu Mwinyi katika kusukuma ajenda ya haki za binadamu na uongozi bora, pamoja na kuhimiza uhuru wa uandishi.


Amani Abeid Karume, Rais Mstaafu wa Zanzibar, aliwaomba Watanzania washikilie kauli ya hayati Dkt Mwinyi ya kusuluhisha nyoyo za wananchi, akisema maendeleo yanahitaji amani na utulivu. 


Hayati Rais Mstaafu Dkt Ali Hassan Mwinyi, ambaye alikuwa Mtanzania wa kwanza kuwa rais wa Zanzibar kisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anasifiwa kwa kuzipa nguvu taasisi za kiraia na kusimamia mageuzi ya kisasa, ikiwa ni pamoja na kurudisha mfumo wa vyama vingi nchini mwaka 1992 baada ya kufutwa mwaka 1965.



0 Comments:

Post a Comment