MWINYI ALIENDAJE ZANZIBAR?:

  MWINYI ALIENDAJE ZANZIBAR?:





Baba yake,  alitaka awe mwanazuoni wa Kiislamu, akampeleka  Unguja akasome madrasa. Alimuacha kwa rafiki yake anaitwa Suwedi Bin Mgeni. Maisha hapo nyumbani kwa Mgeni hayakuwa rahisi kwa sababu mke wa Swedi Mgeni hakukubaliana na suala la Ali kuwa hapo kwake, hivyo akamgeuza kijakazi, akiosha vyombo, kuteka maji na kazi nyingine za kwa kiwango kisichomfaa mtoto. Lakini  kwa mapenzi makubwa ya Swedi Mgeni, Ali aenda shule , akawa mwalimu na baadae kuingi kwenye uongozi hata kuwa Rais.


UWAZIRI: Mwaka 1970, Ali aliteuliwa kuwa Waziri, 1972 akawa Waziri wa Afya, 1975 akawa Waziri wa Mambo ya Ndani. 1977 yalitokea mauwaji ya kutisha huko Shinyanga na Mwanza, jambo ambalo lilimfanya Ali aamue kujiuzulu (aliona yeye kama Waziri wa Mambo ya Ndani alipaswa kuwajibika). 1978 akawa Balozi huko Misri, 1981 akarudishwa kwenye Uwaziri (Maliasli na Utalii na Baadae Waziri wa Nchi - Ofisi ya Rais).


URAIS WA ZNZ: Januari 1982, #Mwinyi alialikwa kwenye kikao cha CCM huko Dodoma, hakuwa Mjumbe wa Kamati Kuu. Alikosa sehemu nzuri ya kulala kulingana na cheo cha Uwaziri na Ujumba wa NEC, akishia kulala kwenye vyumba vya Wanafunzi pale CBE.

.

Kwenye mkutano kikawaka (mjadala ulikuwa kuhusu Muungano/ Serikali tatu). Wajumbe toka Zanzibar wakagawanyika kwenye Makundi: Wakombozi/Walinzi wa Mapinduzi na Frontliners (Mwinyi hakuwa kwenye kundi lolote). Hao Frontliners ndio walishinikiza kujiuzulu kwa Rais wa Zanzibar wa wakati huo (Alhaj Aboud Jumbe aliyefariki 2016). Januari 29,1982 Jumbe akajiuzulu, swali kubwa likawa nani atakuwa Rais wa #Zanzibar?.


Mwinyi hakutegemea kuwa Rais, watu walipendekeza jina lake. Baada ya mjadala mkali wa majina (kukaimu Urais), Mwalimu Nyerere akatafuta mtu mmoja kumaliza mjadala. Nyerere alimuamini sana Shekhe Thabiti Kombo, wakati wa mkutano Kombo alikuwa amelazwa KCMC Moshi. Nyerere akamtumia ndege aje Dodoma, akamuomba ashauri nani akaimu Urais, Thabiti Kombo akasema “ Twende na #AliHassanMwinyi”. Mwinyi akakaimu Urais.


Machi 10 1984, NEC ikakaa kujadili majina kwa ajili ya uchaguzi maalum, majina yalikuwa mawili tu: Shekhe Idriss Abdulwakil na Mzee Mwinyi. Shekhe Abdulwakil akaomba jina lake liondolewe, Mwinyi akabaki na ndio akawa Rais Wa Zanzibar hadi mwaka 1985.


Jina la #MzeeRuksa lilianzia pale. Mwinyi alipandisha mishahara ya wafanyakazi wa Zanzibar, sekt binafsi ikaruhusiwa kuingiza chakula Zanzibar, kukawa na usafiri rahisi kwa umma (zile Chai Maharage zilianzia hapo), na ruksa nyingine kibao).


URAIS WA TANZANIA: 1985 Mwalimu Nyerere alimua kung’atuka madarakani. Kulikuwa na majina matatu: Mwinyi, Dkt Salim Ahmed Salim (chaguo namba 1 la Mwalimu Nyerere) na Mzee Rashid Kawawa. 


Kawawa alijiweka pembeni, Dkt Salim Ahmed Salim akakumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa wajumbe wa Zanzibar. Mwinyi akaja kushinda na kuwa Rais wa Awamu ya Pili wa JMT.


NYERERE ALIMPINGA?: Ni kweli kwamba Mzee Mwinyi hakuwa chaguo ka kwanza la Nyerere (hii kaeleza Mwinyi mwenyewe), lakini hakumkataa. Mwinyi anasema Nyerere angeamua kuzuia Mwinyi asiwe Rais angeweza, hasa kwa kutumia kofia yake kama Mwenyekiti wa CCM, na nguvu yake ya ushawishi. Kwa ufupi Nyerere alikuwa na chaguo lake, lakini alikubaliana na mawazo ya wengi. Alimnadi Mwinyi kwenye uchaguzi, alimpa ushirikiano katika uongozi wake (Kuna  nyakati walitofautiana kimtazamo, mfano kwenye mtazamo juu mauwaji ya Rwanda, na mwaka 1994 hotuba ya Mwalimu Nyerere kwenye siku ya Wafanyakazi huko Mbeya).


Kuelezea heshima yake kwa Nyerere, Mwinyi anasema; huwezi kufananizha Mlima Kilimanajaro na kichuguu, kama wangeshindanishwa, Mwinyi alijiona kuwa kichuguu mbele ya Mlima Kilimanjaro.


Mwinyi ni muungwana asiye na makuu, mfano halisi wa kuinuliwa toka mavumbini kwenda juu sana. 


Habari kwa msaada wa mitandao ya kijamii 

0 Comments:

Post a Comment