MBUNGE NGORONGORO HAJULIKANI ALIPO


MBUNGE wa Ngorongoro, Emmanuel Oleshengay,(CCM) imeelezwa kuwa hajulikani ingawa  alikuwa akishikiliwa kwenye kituo cha polisi Karatu kuanzia juzi jioni ambapo jana mawakili wake waliporejea kwa ajili ya taratibu za dhamana waliambiwa hayupo.


Wakili wa mbunge huyo, Joseph OleShangay  alimweleza mwandisha wa habari hizi kuwa Agosti 21,2023  bunge huyo alihojiwa kwa kosa la kujeruhi watu wawili, Mwandishi wa habari, Habibu Mchange na mwananchi Lengai Ngoshie.

Amesema kuwa alihojiwa kuanzia saa 11 jioni mpaka saa nne usiku kwenye kituo cha polisi Karatu na polisi aliyejitambulisha kwa jina la Abdalah kutoka ofisi ya Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai, (RCO) Arusha.

" Walipomaliza kumhoji wakatuambia turudi leo (jana) kwa ajili ya mchakato wa dhamana lakini tumerudi leo tumeambiwa hayupo kituoni tumejaribu kuwauliza wote pale kituoni hakuna anayetueleza alipo na polisi waliofanya mahojiwano na mbunge jana wote hawapokei simu," amesema Wakili, Joseph na kuongeza

..Kuna watu walituambia kuwa mbunge Oleshangay alipelekwa Arusha na kuna mawakili wamefuatilia Arusha lakini mpaka tunapoongea hapa hatujui alipo,".

"Kosa la kujeruhi lina dhamana kisheria na sio uamuzi wa polisi kuamua wampe dhamana au la walipaswa wampe dhamana au kwa kuwa jana walishahojiana naye basi leo walipaswa kumfikisha mahakamani,".

Wakili Joseph alisema kuwa pia wamekuta watuhumiwa wengine 31 wanaoshikiliwa kwa tuhuma jizohizo za kuwashambulia watu jao wawili ambapo 21 wako kwenye kituo cha polisi Karatu na wengine 10 wanashikiliwa kwenye kituo cha polisi Manyara Kibaoni.

Amesema kuwa polisi Karatu ni kama wanawatunza watuhumiwa hao kwani wenye mamlaka nao ni polisi wa Ngorongoro na ofisi ya RCO, Arusha.



 

 

Awali kabla ya kukamatwa mbunge Shangay, aliwaeleza wandishi wa habari jijini Arusha kuwa alifika kwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai mkoani Arusha, (RCO) kwa ajili ya kujisalimisha lakini akambiwa anatakiwa aende Karatu.

MAWAKILI wanaomtetea mbunge wa Ngorongoro, Emmanuel OleShangay juzi wakijadiliana jambo kabla ya kwenda kuripoti polisi. kuanzia kushoto ni  Joseph Oleshangay, Yonas Masyaya, Nicolas Senteu na Ngeyani Orormunyei. Mbunge  Emmanuel oleshangay katikati




Mbunge huyo alikuwa ameambatana na mawakili wanaomtetea akiwemo, Joseph Oleshangay, Yonas Masyaya, Nicolas Senteu na Ngeyani Orormunyei.

 

“Leo nimefika kuripoti kwa RCO kama jana (Agosti 20,2023) nilivyofanya mawasiliano na Spika (wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tulia Akson) na Waziri wa Mambo ya Ndani (Hamad Masauni) nimeripoti muda wa saa sita mchana ameniambia suala langu ameliacha kwa Afisa Upelelezi wa wilaya ya Ngorongoro a,mbapo ofisi wameihamishi Karatu,” alisema OleShangay na kuongeza .

 

 

…Hivyo ninatakiwa kwenda Karatu kwa ajili ya mahojiano . Lakini suala wanaloenda kunihoji ni la kutengenezwa kwani hata mkiangalia ukiona kuna mabango yameandaliwa kule Kapenjiro hata jina la mbunge lipo lakini ukiangalia mimi tokea nimechaguliwa sijawahi kufika kule,”.

 

 

Mbunge huyo alisema kuwa kwenye mabango yao wameandika ‘mbunge anatunyima kuondoka’ jambo alilodai kuwa hilo jambo limejengwa huku akisisitiza kuwa hata hilo tukio la Enduleni hakuwepo ni tukio lililotengenezwa huku akieleza kuwa haelewi nia ya wanaofanya hayo na kwanini watu hao wameamua kunitaja mimi.

 

Waandishi hao walishambuliwa na wananchi wakiwa mnadani kwenye kijiji cha Enduleni Agosti 15,mwaka huu ambapo video imesambaa mitandaoni ikimuonyesha mmoja wao, Habib Mchange wa Jamvi la Habari akitumia kipaza sauti kuwahamasisha wananchi hao kuhama.

 

Waandishi wengine walijeruhiwa kwenye tukio hilo na vyombo wanavyofanyia kazi kwenye mabano ni Ferdinand Shayo, (ITV) na Denis Msaky,(Mwandishi wa Kujitegemea).

 

 

Akitolea ufafanuzi taarifa inayosambaa  kwenye mitandao ya kijamii kuwa amewakashifu polisi alisema kuwa si kweli kwani video hiyo imekatwa baadhi ya maneno kwani anachokumbuka akiwa kijiji cha Nainokanoka alipokea taarifa ya wananchi wa kijiji hicho pamoja na Nailelai kwamba askari wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro,(NCAA) wanawaonea wananchi.

 

“Nilichosema kwa Kauli yangu kama mbunge Jeshi la polisi linaendeshwa kwa mujibu wa sheria na wanasheria zao, PGO zao wanapoenda kumkamata mtu yeyote kwenye makazi yao wanazifuata,” alisema na kuongeza.

 

…Hao wengine wanaoenda kuwakamata kwenye makazi yao si jeshi la polisi ninaowafahamu mimi wale nilikuwa nawazungumzia ni ‘rangers’ (askari wa hifadhi) ambao wanaenda kwenye makazi ya watu usiku wanafyatua risasi wakina mama mimba zinatoka ndiyo maanda nikasema hawa ni vibaka kama vibaka wengine ambao wanapswa kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria za jamhuri ya Muungano wa Tanzani,”.

 

 

Alisema kmuwa akiongea na wananchi hao aliwaeleza kuwa jeshi la polisi likitaka kwenda kukamata mtu ni lazima wafuate taratibu ikiwemo kuambatana na viongozi wa eneo husika akiwemo balozi na mwenyekiti.

 

Akielezea namna mbunge Oleshangay alivyokamatwa , Diwani wa Kata ya Elelai ,James Moringe alisema alikuwa ameongozana na Mbunge aliyekuwa anatii maelekezo ya RCO ya kwenda kuripoti kituo cha Polisi Karatu.

 

Hata hivyo walipofika Karatu  eneo la Rhotia walisimamishwa na Polisi ambao walimchukuwa Mbunge huyo katika gari lao.

 


 

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, (RPC) Jastine Masejo hazikuzaa matunda kwani simu yake ilikuwa inaita muda wote bila kupokelewa.

 





0 Comments:

Post a Comment