Deepak Gupta (25)
akiwa amelazwa katika hospitali ya seliani ndani ya chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) mara baada ya kukatwa mguu wake wa kushoto
kutokana na mguu huo kujeruhiwa vibaya kwa bomu.
akiwa amelazwa katika hospitali ya seliani ndani ya chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) mara baada ya kukatwa mguu wake wa kushoto
kutokana na mguu huo kujeruhiwa vibaya kwa bomu.
Mtoto
Manci Gupta akiwa amelala anasikilizia maumivu ya miguu aliyoumia
mara baada ya kulipukiwa na bomu yeye na familia yao wakati wameenda
kupata chakula cha usiku katika mgahawa huo
Munisha Gupta (42)na mme wake,Mahush
Gupta (42) akiwa wameegemeana wote wamezurika katika mlipuko wa bomu
hilo wakati wameenda kupata chakula cha usiku
Gupta (42) akiwa wameegemeana wote wamezurika katika mlipuko wa bomu
hilo wakati wameenda kupata chakula cha usiku
picha ikionyesha askari wa jeshi la wananchi kitengo cha mabom wakiwa
katika eneo la tukio ambalo bumu lilirushwa ndani ya mgahawa wa
ujulikanao kwa jina la Traditional Indian Cusine ulipo pembeni ya
hotel ya gmkana
katika eneo la tukio ambalo bumu lilirushwa ndani ya mgahawa wa
ujulikanao kwa jina la Traditional Indian Cusine ulipo pembeni ya
hotel ya gmkana
muonekano wa eneo la tukio
SEHEMU ambayo inasemekana bomu lilitua mara baada ya kutupwa
![]() |
| Mkurugenzi wa tiba wa hospitali ya Seliani Dr. Paulo akiongea na waandishi wa habari |
Watu nane wamejeruhiwa kwa kitu kinachodhaniwa kuwa bomu lilolotupwa kwenye mgahawa wa Dhawa uliopo mbele ya gymkhana club jijini Arusha.
Mkurugenzi wa tiba wa hospitali ya Seliani Dr. Paulo Kisanga alisema kuwa tukio hilo
lilitokea jana majira ya saa 4:30 usiku katika eneo kwani walianza kupokea
wagonjwa hao kuanzia majira
ya saa tano kasoro na saatano .
Alisema kuwa walipokea wagonjwa nane ambao waliumia sana
katika maeneo ya miguu ambapo alibainisha kuwa katika wagonjwa hao na ne kuna
mmoja ambaye aliletwa akiwa na hali mbaya sana kitu ambacho kiliwalazimu
kumfanyia upasuaji usiku huo huo.
“kati yawagonjwa hao nane mmoja aliletwa akiwa mahututi sana
kwani mguu wake ulikuwa umeadhiriwa sana na bomu hilo hivyo ikatulazimu kumkata mguu mmoja wa kushoto ,mgonjwa
huyo, Deepak Gupta (25) mwanaume na sasa
hivi anaendelea vyema kidogo na yupokatika chumba cha ICU ndani ya
hospitali hii yetu ya Seliani”alisema Kisanga
Alisema kuwa katika
majeruhi au nane aliowapokea wanawake wako watatu huku wanaume wakiwa watano na
kubainisha kuwa wote wameshafanyiwa upasuaji na wapo wodini kwa ajili ya
uangalizi wa madaktari
Aidha aliwataja majeruhi hao kwa majina kuwa ni pamoja
na Vinod Suvesh(37), Ritwik Khandelval
(13),Raj Rajin(30),Prateck Saver,manci Gupta(14) ,Manisha Gupta (36),Mahush
Gupta(42) pamoja na Deepak Gupta (25)
wote wakiwa na asili ya kiasia
Kisanga
alisema kuwa kwa mujibu wa wagonjwa hao walio waliofika hapo hospitali
walidai kuwa bomu hilo lilirushwa kwa kupitia dirishani.





0 Comments:
Post a Comment