![]() |
| Grace Macha na Mayalla wakifuatilia kwa makini mkutano huu ili kuweza kuhabarisha ipasavyo |
![]() |
| Mwenyekiti wa kamati ya mahusiano na utatuzi wa migogoro, bunge la Afrika Mashariki, Abubakar Zein, (Kenya) akifuatilia mjadala. |
![]() |
| Washiruiki ambao ni wenyeviti wa kamati mbalimbali za bunge la EALA, wawakilishi wa serikali toka nchi wanachama na wataalam wa EAC na wale kutoka taasisi za kimataifa wakifuatilia mjadala. |
TAASISI za usalama za nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, (EAC),
zimetakiwa kufanya kazi kwa kushirikiana huku wakitumia mfumo wa kisasa
wa sayansi na teknolojia katika kupeleleza ili kudhibiti matukio ya
uhalifu ambayo kutokana na kuongezeka kwa mtangamano wa wananchi kwa
kurahisisha mwingiliano kwenye mpaka na wahalifu nao hupita kwa urahisi.
Aidha imeelezwa kuwa nchi nyingi za EAC zimepakana na nchi ya
Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo ambayo iko kwenye vita vya wenyewe kwa
wenyewe hali inayopelekea kuongezeka kwa matukio ya uhalifu ikiwemo
upitishwaji wa pembe za ndovu na usafirishaji wa madawa ya kulevya
kutoka nchi hiyo sanjari na wizi wa magari kutoka nchi wananchama ambayo
hupelekwa Kongo.
Hayo yalisemwa jana jijini hapa na Mtaalam wa masuala ya usalama wa
EAC, Dkt. Leonard Onyonyi, wakati alipokuwa akielezea hali ya usalama
kwenye ukanda wa jumuiya hiyo kwenye mkutano wa siku mbili ulioandaliwa
na kamati ya mahusiano na utatuzi wa migogoro ya bunge la Afrika
Mashariki na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.
Alisema kuwa katika kuhakikisha eneo la EAC linakuwa salama ni vema
nchi wanachama zikaelimisha wananchi wake kuelewa na kujua wajibu wa
kulinda usalama ni wa kila mmoja na si kuachiwa serikali pekee ambazo
nazo zimeshauriwa kutumia wataalam na vifaa vya kisasa katika
kukabiliana na matukio hayo.
Dkt. Onyonyi alisema kuwa mifumo ya kudhibiti matukio ya
utakasaji fedha haramu ni vema ikaboreshwa ili iweze kufanya kazi
ipasavyo ya kuzuia na kubaini matukio hayo huku akitolea mfano kuwa
tayari imejulikana kuwa soko kuu la meno ya tembo liko nchini China
lakini bado haijajulikana malipo yanafanyikaje jambo alilodai kuwa
huenda hufanyika kwa kupitia bidhaa zinazokuja kwenye ukanda huu kwa
makontena jambo ambalo huzitakasa fedha hizo.
Akiongelea tatizo la kuongezeka kwa matukio ya usafirishaji wa
madawa ya kulevya huku akitolea mfano kiwango kikubwa kilichofanikiwa
kukamatwa kwenye nchi za Tanzania na kenya, mtaalam huyo alisema kuwa
mbali na kuwa eneo la EAC kuwa njia ya kuyapitisha kwenda mabara mengine
lakini soko la ndani pia limekuwa likiongezeka ambapo waathirika wakuu
ni vijana wenye umri wa chini ya miaka 20.
Alisema kuwa kwenye ukanda huu wa EAC matukio ya usafirishaji wa
binadamu yamekuwa yakijitokeza hasa wale wanaotolewa vijijini kupelekwa
maeneo ya mijini kwa ajili ya kufanya kazi za ndani na wengine
kufanyishwa biashara ya ngono, (ukahaba).
Awali Mwenyekiti wa makati hiyo ya bunge, Abubakar Zein, (Kenya),
alisema kuwa waliamua kuandaa mkutano huo kutokana na umuhimu wa amani
katika suala zima la maendeleo kwa kile alichodai kuwa mambo hayo mawili
yanategemeana kwani huwezi kuwa na amani kama hakuna maendeleo na
hauwezi kuwa na maendeleo kama hauna amani.
Alisema kuwa mkutano huo umelenga kujua chanzo cha migogoro kwenye
ukanda huu ili kujenga misingi ya kitaasisi kuitatua na
kuhakikisha haitokei jambo alilodai kuwa watafanikiwa kwani kwenye
mkutano huo kuna wataalam wakiwemo watafiti wa masuala ya migogoro,
watunga sera ambao ni wabunge na wawalikishi wa serikali toka nchi zote
tano.
Zein alisema kuwa wanalenga kuhakikisha kunakuwa na sera ya usalama
ambayo baadaye itatungiwa sheria ili kuhakikisha wananchi wote wa EAC
wanashiriki kulinda amani ambapo alisema kuwa mkutano huuu ulitanguliwa
na ule wa waandishi wa habari uliofanyika nairibi Nchini Kenya ambapo
baada ya huu kutakuwa na mkutano mwingine utakaowakutanisha wabunge wa
nchi wanachama wa jumuiya hii.
Sent from my iPhone





0 Comments:
Post a Comment