SHIRIKA LA WILD SURVIVORS WAJA NA TEKNOLOJIA YA KISASA YA UTATUZI WA MIGOGORO KATI YA TEMBO NA JAMII

  

Happy Lazaro,Arusha 

Shirika linajishughulisha na uhifadhi wa Tembo la WILD SURVIVORS  waja na teknolojia ya kisasa ya utatuzi wa migogoro kati ya Tembo na jamii zinazopakana na hifadhi.


Hayo yamesemwa jijini Arusha leo na Afisa miradi ya jamii wa shirika hilo,Masalu John Masaka wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la 15 la kisayansi la TAWIRI  linalofanyika jijini Arusha .




Amesema kuwa lengo  la kushiriki kongamano hili  ni kuwaambia watu kazi wanazofanya ili kufanikisha hizi kazi za utatuzi wa migogoro kati ya tembo na jamii zinazopakana na hifadhi 

Amefafanua kuwa, lengo la kuanzishwa kwa shirika hilo ni kuhakikisha kwamba jamii zinazopakana na hifadhi zinaishi kwa amani na Tembo kwa kutumia njia rafiki kama mizinga ya nyuki .



Aidha ametoa wito kwa jamii  pamoja na wahifadhi kufanya kazi pamoja kwa kukutumia njia rafiki ili tuweze kuishi pamoja na tembo kwani idadi ya watu inapoongezeka na idadi wanyama inapoongezeka ardhi haiongeki ,hivyo tunahitajika kufanya kazi kwa pamoja  wakiwemo jamii iliyoathiriwa wahifadhi pamoja na wanyamapori.




" Tunafanya kazi zaidi za kuhifadhi Tembo kwa namna ambayo tunatatua migogoro kati ya Tembo na wakulima wanaopakana na hifadhi ."amesema Masaka .


"Tumekuja hapa kwenye mkutano huu kwa ajili ya kuwaeleza watu shughuli ambazo tunazifanya kwa mfano tunatumia mizinga ya nyuki ambayo inatoa mazao kama asali ambayo inakuwa faida kwa vikundi  vya akinamama katika vijiji ambavyo tunafanya kazi."amesama Masaka .



"Tumekuja pia kwenye huu mkutano kwa lengo la kueleza watu namna ambavyo tunakusanya data  na tunatumia vifaa gani tunatumia kamera  pamoja na teknolojia ya simu ambayo tunakuwa na application inayoitwa survey one two three tunatumia kukusanya data ."amesema .



Amefafanua kuwa tangu shirika lianzishwe wamepiga hatua kwani wameshaweka uzio wa mizinga  ya nyuki zaidi  ya kilometa 20 katika maeneo mbalimbali kwani wana uzio wa nyuki kilometa saba upande wa Ngorongoro vijiji vya wilaya ya Karatu na kilometa sita kwa upande wa serengeti na kilometa sita katika vijiji vya Rukwa katavi vijiji ambavyo vinapatikana na hifadhi ya Taifa Katavi .


"Tumeona mabadiliko yapo matukio ya Tembo kuingia mashambani  na kula mazao ya wakulima yamepungua na tumeona katika vijiji ambavyo tumefanya navyo kazi mwanzoni  ikiwemo Ngorongoro wakina mama wameanza kupata kipato kutokana na mazao ya nyuki ."amesema .



"Tunawafundisha na tunawapa mafunzo  ya namna ya kuweka uzio wa mizinga ya nyuki namna ya kuvuna mazao ya nyuki na na namna ya kuchakata na kuwaunganisha  na soko ."amefafanua  Masaka .



"Kwa uchunguzi ambao tumefanya ni kuwa tembo anawaogopa nyuki hivyo anavyokaribia karibu na mzinga wa nyuki na anapousukuma ule waya ambayo umeunganisha mzinga mmoja hadi mwingine  na nyuki anapotikiswa wakiwa na asali wale nyuki walinzi wanatoka nje kuangalia kitu ambacho kinataka kuchukua mazao yake ba wale nyuki wanapotoka nje wanatoa ile sauti na tembo akisikia anaamua kuondoka."ameongeza Masaka .



0 Comments:

Post a Comment