MBUNGE ZUENA AKABIDHI SIMU JANJA ZA KUSAJILIA WANACHAMA UWT KILIMANJARO
Na Gift Mongi, Moshi
MBUNGE wa viti maalum kupitia mkoa wa Kilimanjaro, Zuena Bushiri amegawa simu janja kwa Umoja wa wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) wilaya saba za mkoa kwa lengo la kuzitumia kufanya usajili wa wanachama.
Aidha Mbunge huyo pia amekabidhi kadi 1000 za UWT lengo likiwa ni kuhamasisha wanawake kujiunga na Umoja huo lengo likiwa ni kuimarisha Chama na Jumuiya zake.
Akikabidhi simu na kadi hizo katika ofisi ya UWT Mkoa, Zuena alisema kuwa serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa ambazo zilikuwa ni kipaombele kwa wananchi.
Alisema kuwa, kutokana na kazi hizo wananchi wanajukumu la kumlipa asante Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumpa kura za kishindo wagombea wanaotokana na CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja na kumpa yeye kura za kishindo uchaguzi Mkuu 2025.


0 Comments:
Post a Comment