Majaliwa Ashiriki Swala ya Idd El-Adh’haa Dar es Salaam



Leo tarehe 17 Juni 2024, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameungana na waumini wengine katika kuswali Swala ya Idd El-Adh’haa katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI BAKWATA, Kinondoni, Dar es Salaam. 



Baada ya sala, Majaliwa alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya Baraza la Kitaifa lililofanyika katika msikiti huo. Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa, Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande, na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila.



Hafla hii ni sehemu ya maadhimisho ya Idd El-Adh’haa ambayo hufanyika kila mwaka kwa jamii ya Waislamu duniani kote.

0 Comments:

Post a Comment