NI MAMA ZETU NA DADA ZETU NI LEO. ..NI SIKU YAO TUWAHESHIMISHE;PROF NDAKIDEMI

 

Na Gift Mongi, Moshi

Ni maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani ambapo huadhimishwa May12 ya kila mwaka duniani kote .






Katika maadhimisho haya mbunge wa jimbo la Moshi Vijijini Prof Patrick Ndakidemi amesema mwanamke bado ana nguvu kwenye jamii na hivyo anastahili uwezeshwaji.


'Tunaungana na wanawake kwenye hii siku yao niseme mwanamke bado ana nguvu kwenye jamii wanapokwama sisi tutafanya 'anasema


Bi Theresia Komba ni mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (CCM)ambapo ameeleza umuhimu wa mwanamke katika familia na jamii kwa ujumla wake!


Mosi anasema ili jamii iweze kujikwamua katika nyanja zote lazima nyuma iwepo nguvu ya mwanamke ambaye ndiye muasisi wa mafanikio.


Pili mwanamke ni nyenzo katika mafanikio yoyote yale na katika hilo yapo mengi yanayoonekana kupitia mheshimiwa rais Dkt Samia Suluhu Hassan.


'Ndio kafanya mambo makubwa kwa kipindi kifupi tu huu ni ushahidi kuwa bado wanawake tunaweza!"anasema Bi Theresia


Anaenda mbali zaidi na kuongeza kubwa wanawake hawa kuaminika na kuonekana kama sio sehemu ya jamii kitu ambacho sio sahihi


'Mwanamke hakuaminika ilibidi ukitaka kufanikiwa umtegemee mwanaume ila sasa kuna utofauti  yaani tunajitambua'anasema Mwenyekiti huyo


Beatrice Mgaya ni mama wa mtoto mmoja anayeishi Pasua mjini Moshi ambapo anasema siku hii muhimu kwao alikua hakumbuki ila akawapa kongole wanawake wanaofanya vyema katika nyanja mbalimbali 


'Nisiseme uongo leo niliishi ila kwa wenzetu wanaofanya vyema hatuna budi kuwapongeza lakini kuwatia moyo vilevile 'anasema

0 Comments:

Post a Comment