WATANO MBARONI KWA UVUVI HARAMU


■Watano wakamatwa na vifaa vya kutengeneza vilipuzi vya baruti  vya uvuvi haramu wa baruti.


■Majahazi wawili yakamatwa na Mifuko ya sukari  550 kwa kukwepa ushuru.


■Mmoja akamatwa kwa utapeli na kujifanya Askari Polisi Kikosi cha Wanamaji.



Katika kipindi cha operesheni maalumu iliyotekelezwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Wanamaji Dar es Salaam kuanzia Januari 15, 2024, hadi sasa, jumla ya watuhumiwa watano wamekamatwa na kushikiliwa kutokana na tuhuma za kuhusika katika vitendo vya uvuvi haramu baharini pamoja na matumizi ya vilipuzi na mbolea ya Ammonium salfeti. Watuhumiwa hawa wanashikiliwa kwa makosa ya kuhatarisha usalama wa baharini na kukiuka sheria za uvuvi.


Miongoni mwa watuhumiwa hao, baadhi yao walikutwa na mbolea aina ya Ammonium salfeti yenye uzito wa kilogramu 200 na vilipuzi (detonators) aina mbalimbali, jumla yake ikiwa vipande 443. Operesheni hii inaonesha dhamira ya jeshi letu katika kukabiliana na vitisho vinavyotokana na uvuvi haramu kwa kutumia njia hatari kama milipuko.


Tutakapopata maelezo zaidi kuhusu mashtaka yao, tutahakikisha kuwafikisha mahakamani ili haki iweze kutendeka. Watuhumiwa hawa ni sehemu ya mtandao unaoshukiwa kuhusika na vitendo vya uvuvi haramu ambavyo vina athari kubwa si tu kwa mazingira bali pia kwa uchumi wa nchi yetu.

0 Comments:

Post a Comment