HIZI HAPA SABABU ZA MAHAKAMA KUMPA DHAMANA MADELEKA


WAKILI wa kujitegemea, Peter Madeleka, ameibwaga serikali baada ya mahakama Kuu Kanda ya Arusha kukubaliana na maombi yake ya kupatiwa haki ya dhamana.

Aidha mahakama hiyo imempa marshati ya dhamana kuwa ni kuweka dhamana ya shilingi milioni moja na kudhaminiwa na mtu mmoja anayeaminika.

Uamuzi huo wa Jaji, Yohane Masara, aliyesikiliza rufaa hiyo namba 87/2023 umesomwa leo, Septemba 9, 2023 na Kaimu Msajili wa Mahakama hiyo, Boniface Semroki. 

Akisoma uamuzi huo, Semroki ambaye pia ni Hakimu Mkazi Mwandamizi, amesema kuwa baada ya mahakama kupitia hoja za pande zote mbili umejiridhidha pasipo na shaka kuwa kesi inayomkabili Madeleka ni yankujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ambayo kimsingi mashitaka hayo yana dhamana.


Kwenye shauri hilo upande wa Jamhuri umewakilishwa na Mawakili wa Serikali, Elidineni Njiro, Tusaje Samuel na Joyce Mafie huku mleta maombi, wakili, Madeleka amekiwakilishwa na mawakili, Boniface Mwabukusi, Revocatus Myela,  Simon Mbwambo na Jonas Masiaye 

Uamuzi huo wa jaji Masara umesema kuwa kwenye shauri la msingi DPP alifanyia marekebisho hati ya mashitaka akaondoa mashitaka ya kutakatisha fedha ambayo hayana na dhamana na kuacha mashitaka ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ambayo yana dhamana.

Baada ya kufanya makubaliano na ofisi ya DPP ya plea bargaining  alilipa shilingi milioni mbili ambapo mahakamani alikiri kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuhukumiwa kifungo cha miaka mitatu au faini ya shilingi laki mbili ambapo alilipa faini hiyo.

Semroki amesema  mahakama  kuwa kimsingi hati ya mashitaka iliyokuwa hai (exist) mahakamani ni ile ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kwani ndiyo iliyotumika kufanya uamuzi wa mwisho wa mahakama kwenye shauri hilo namna 40/2020.

Awali Madeleka ambaye amekaa mahabusu kwenye gereza la  Kisongo siku 57 kuanzia julai  17,2023 baada ya  Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Fadhil Mbelwa, kutoa  uamuzi huo mdogo kuhusiana na hatima ya dhamana ya Madeleka anayekabiliwa na makosa 10 ikiwemo utakatishaji fedha.

Hakimu Mbelwa alisema kutokana na uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Julai 17,2023,ambao uliondoa zoezi la makubaliano ya kukiri kosa 'plea bargain', hivyo akasema na hati ya mashitaka iliyofanyiwa marekebisho ambayo ilikuwa na makosa yenye dhamana imefutwa.

Alisema kilichoamuliwa na Jaji Aisha Bade wa Mahakama hiyo ni kuondoa zoezi la makubaliano hayo na kuwa kufutwa kwa mwenendo huo hati inayomshitaki ni ya awali ambayo ina makosa 10 ikiwemo la utakatishaji fedha ambalo halina na dhamana kisheria hivyo mshitakiwa ataendelea kukaa mahabusu.


Agosti 1,2023  ya Hakimu Mkazi Arusha,ilitoa uamuzi mdogo ambao ulitupilia mbali ombi la dhamana ya wakili huyo lililowailishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanne wanaoongozwa na Wakili, Mwabukusi

0 Comments:

Post a Comment