MONGELA AHIMIZA MIGOGORO IMALIZWE KWA USULUHISHI


WADAU wa sheria wametakiwa kuisaidia jamii kuelewa umuhimu wa kumaliza migogoro kwa njia ya usuluhishi endapo si lazima kwenda mahakamani kwani  inapunguza uwezekano wa kutumia muda mwingi na rasilimali .


Hayo yameelezwa leo Januari 22, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela wakati akizindua wiki ya sheria mkoani hapa kwenye viwanja vya TBA ambapo kauli mbiu ni “Umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi endelevu wajibu wa mahakama na wadau,”.


Amesema kuwa wananchi watapata muda zaidi wa kujishughulisha kwenye shughuli za maendeleo badala ya kuwa kwenye migogoro na kesi mahakamani.

 

Mongela amesema kuwa utatuzi wa kesi kwa njia ya usuluhishi kwa kiasi kikubwa umesaidia wananchi kupata haki zao na kuokoa muda mwingi.

 

"Tunategemea mtaisadia jamii kuelewa zaidi faida ya usuluhishi wa migogoro na jinsi gani mnaweza  kusaidia kuondoa kutumia muda mwingi na rasilimali nyingi. Wakati mwingine mgogoro kuisha kwa sheria huacha makovu natumaini dhana hii inaweza kutusaidia sana," amesema Mongela na kuongeza 

...Sisi tutategemea sana wiki hii itumike  itoke kutoa elimu ya kutosha...Hapa Arusha mhimili wa mahakama umekuwa na mchango mkubwa sana. Unapoona utulivu wa mkoa wetu, tunapoona maendeleo makubwa kwenye mkoa wetu mhimili wa mahakama una mchango mkubwa sana,".


"Niwapongeze wadau wote wa sheria, Haki inazidi kutendeka zaidi na hata wananchi wanazidi kuona hivyo.Niombe mahakama kwa hatua tuliyofikia tuendelee na msimamo huo kusaidia wananchi,".

“Mahakama ndiyo chombo pekee kilichopewa nguvu ya kutoa haki kwa mujibu wa sheria.Sisi kama serikali tunaahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwenu pale panapohitajika,”



Mondela amesema kuwa sekta ya sheria inaweza kuchangia kudumisha amani na umoja nchini huku akihimiza kauli mbiu ya maadhimisho hayo kutekelezwa na wadau wote wa sheria.


“TLS (Chama Cha Wanasheria Tanganyika)  wasaidie na nyie na wadau kutoa elimu muone  jinsi mtakavyosaidia wiki hii mara nyingi watu wakitoka kwenye wiki hii mashauri mengi huisha kutokana na elimu hiyo,” alisisitiza Mongela.

Awali, Naibu Msajili Mahakama kuu Kanda ya Arusha, Judith Kamala amesema kuwa maadhisho hayo ya wiki ya sheria yataaambatana na shughuli mbalimbali zitakazofanyika ikiwemo kutoa elimu katika viwanja vya TBA, kutoa elimu kwa shule sita tofauti zilizopo  Arusha, gereza la mkoa la Kisongo na mahabusu ya watoto Arusha.

 

Aidha kutakuwa na hafla ya kutembelea watoto wahitaji na kuwapatia msaada, bonanza litakalowashirikisha wadau mbalimbali wa mahakama kutoka mikoa ya Manyara na Kilimanjaro.

 

Kilele cha maadhimisho hayo ya wiki ya sheria inatarajiwa kuwa Februari mosi, 2023 ambapo yanatarajiwa kufanyija kwenye a viwanja vya mahakama kuu.

 


Kwa upande wake, mwakilishi wa wakili wa serikali mfawidhi  mkoani hapa, wakili Zamaradi Yohannes amesema kuwa kama wadau wa haki watazingatia usuluhishi wa migogoro kwa njia ya utatuzi.


 







0 Comments:

Post a Comment