SHAHIDI KESI YA SABAYA ANG'AKA ASIULIZWE KINACHOMLIZA, HAKUMBUKI JINA LA ALIYEMPA ENEO LA KUJENGA KIBANDA

 


SHAHIDI wa nne upande wa utetezi, John Odemba (49) kwenye kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili pamoja na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole amemjia juu wakili wa serikali akimtaka asimuulize kwa nini analia mahakamni hapo.

  

Hayo yamejiri leo wakati shahidi huyo akihojiwa maswali ya dodoso na wakili wa Serikali mwandamizi, Ofmed Mtenga mbele ya hakimu Mkazi Mwandamizi, Patricia Kisinda anayesikiliza shauri hilo namba 27/2021 kwenye mahakama ya hakimu Mkazi Arusha.

 

Odemba ambaye pia ni mshitakiwa wa nne kwenye shauri hilo alimwambia wakili huyo hivyo ambaye alitaka kujua sababu za yeye kumwaga machozi mahakamani inatokana na yeye kujutia makosa yake akamjibu usiniulize kuhusu kulia kwangu kwani wewe unaonaje.

 

Shahidi aliendelea kuieleza mahakama kuwa hajui anakuja lini jijini Arusha ila ni zaidi ya miaka nane huku akisistiza kuwa hakumbuki mwaka halisi ambapo wakati wakili Mtenga akiendelea kumbana juu ya swali hilo ghafla wakili wake, Moses Mahuna alisimama akamuombea ruhusa ya kwenye chooni.

 

Hakimu aliridhia huku akimuuliza wakili huyo mbona shahidi hajaomba kisha ghafla mshitakiwa wa kwanza, Sabaya naye akasimama akielekea mlangoni jambo lilimfanya hakimu kuhoji kwani uliomba ruhusa kwa ajili ya mshitakiwa yupi ambapo wakili,  Mahuna alisema ni Odemba ila nadhani na Sabaya naye alikuwa anahitaji.

 

 

Baada ya shahidi huyo kurejea,  aliendelea kujibu maswali ya Dodoso ya wakili, Mtenga ambapo alieleza kuwa yeye alikuwa mfanyabiashara wa nguo za mtumba akiwa na mtaji wa milioni tatu lakini hana leseni wala namna ya mlipa kodi, (TIN) isipokuwa ana kitambulisho cha mjariamali.

 

Odemba alieleza mahakamani hapo kuwa anafanya biashara hiyo kwenye kibanda alichojenga kwenye kiwanja cha mtu asiyemjua huku akimuuliza wakili Mtenga anataka amtaje jina huyo mtu kwani anamjua?.

 

Hata hivyo amesema hawezi kuleta kitambulidho hicho cha Mjasiriamali mahakamani hapo ambacho hakina jina lake ila namna tu kwani kipo kwa wakili wake, Fridolini Bwemelo ambaye hakuwepo mahakamani hapo leo.

 

Odemba alieleza kuwa alikutana na maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, (TAKUKURU) akiwa mahabusu kwenye gereza Kuu la Kisongo ingawa mara ya pili hawakuweza kuzungumza nao baada ya kushindwa  kuelewana hivyo bwana jela msaidizi akawafunguza.

 

Hata hivyo alisema hayuko tayari kumleta bwana jela msaidizi wala askari magereza waliosikia mazungumzo baina yao na maafisa hao wa TAKUKURU licha yankuwa anawafahamu na wapo kwenye gereza hilo kwani hawahusiki na kesi hivyo akaitaka mahakama kuamini maneno yake aliyoyatoa chini ya kiapo.

 

Sehemu ya mahojiano mahakamani hapo wakati wakili wa serikali mwandamizi, Ofmed Mtenga akimuuliza shahidi, Odemba maswali ya dodoso

 

Wakili: Bwana Odemba mbona unalia unajuta ?

Shahidi; Wewe unaona nini

Wakili; Nakuuliza kujua

Shahidi;  usiniulize kulia kwangu

Wakili; umesema unaishi wapi

Shahidi; Njiro Arusha 

Wakili; Umesema umeishi Arusha miaka nane

Shahidi; Zaidi ya miaka nane

Wakili: Ulikuja lini Arusha

Shahidi; Sikumbuki siku wala mwaka ila zaidi ya miaka nane

Wakili; Wewe umesoma 

Shahidi; Ndiyo

Wakili; Mpaka la ngapi

Shahidi; la saba

Wakili; Wapi kwingine umewahi kuishi 

Shahidi; Bukoba, Dar es Salaam na Arusha

Wakili; Na haujui Arusha ulikuja lini

Shahidi; zaidi ya miaka nane nyuma

Wakili; Mwaka gani

Shahidi; zaidi ya miaka nane nyuma

Wakili; unauzia mitumba kwenye nyumba ya nani.

Shahidi Nimejenga kibanda 

Wakili; Kwenye kiwanja cha nani

Shahidi; Pale ninapoishi, kwenye sehemu ninapoishi nimeomba sehemu nikajenga kibanda

Wakili; Nitajie jina la huyo mtu

Shahidi; nikutajie huyo mtu unamjua? simjui jina

Wakili; Na Njiro unakaa kwenye nyumba ya nani?

Shahidi; Niko kwangu

Wakili; Kwenye nyumba ya kwako plot namba ngapi

Shahidi; Sijapata namba ya kiwanja

Wakili; Hizo nguo zako unazouza huwa unachukua wapi?

Shahidi; Tengeru krokoni na Moshi

Wakili; Una leseni kwenye biashara zako hizo

Shahidi; Ninayo

Wakili; Unayo TIN

Shahidi; Nina kitambulisho cha mjasiriamali mdogo

Wakili; Kiko  wapi

Shahidi; Anacho wakili wangu Gwemelo

Wakili; Mtaji wako ni mkubwa kiasi gani

Shahidi; Milioni 3

Wakili; Unataka kuongea na wenzako naona unachezesha mdomo

Shahidi; Naongea nao nini


0 Comments:

Post a Comment