SABAYA AMWAGA MACHOZI AKIJITETEA, ADAI WAFANYABIASHARA WANA MKONO KWENYE KESI

 



ALIYEKUWA Mkuu wa wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya amemwaga machozi na kushindwa kujibu swali aliloulizwa na wakili wake juu ya madai ya kufanya mgao wa shilingi 90 milioni alizodaiwa kuchukua kwa mfanyabiashara Fransis Mrosso.

 

Aidha amedai kesi ya uhujumu uchumi  iliyopo mahakamani inatokana na maumivu ya wafanyabiashara wa Kilimanjaro kutokana na mtu wao kukosa ubunge.(hakumtaja jina)

 

Pia amemtaka  shahidi wa 13 upande wa Jamhuri, Ramadhani Rajab Juma, (39) aache kutengeneza magenge kwa madai kuwa anakutafuta watu waseme walimpa hela kwa kile alichoeleza kuwa hiyo si kazi ya serikali.

 

Sabaya ameyasema leo, Januari 19,2022 wakati akiongozwa na wakili wake, Moses Mahuna kutoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi, Patrisha Kisinda wa mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

  

Sabaya ambaye anajitete kama shahidi wa pili amedai kuwa Ramadhani ambaye ni afisa uchunguzi wa TAKUKURU analipwa na wafanyabiashara wa mkoani Kilimanjaro ambao hakuwataja.

 

“Maumivu ya wafanyabiashara wa Kilimanjaro kwa ajili ya mtu wao kushindwa wasiniwekee mimi kwa sababu ni chombo cha dola,” ameeleza Sabaya na kuongeza.

 

…Niliweka uhai wangu rehani nikifanya kazi za serikali mpaka nikatumiwa watu wa kuniua sasa Ramadhani kama chombo cha dola anatakiwa akae upande wa serikali sio kutengeneza magenge na kutafuta watu waseme tulimpa Sabaya pesa hiyo si kazi ya serikali”.

 

Kisha Wakili wake, Mahuna akamuuliza shahidi wa 13 alisema  shahidi huyo wa 13 alisema alipata taarifa fiche akasema uligawa fedha kwa vijana wako pale Tulia ... tena anadai mlikuwa chumbani.

 

Sabaya akakaa kwenye kiti kisha akawa anatokwa na machozi jambo lililomfanya wakili wake kusema “ Mheshimiwa naomba shahidi apumzike kwa sababu kuna mambo yanamfanya apate hisia. Mheshimiwa naomba nitoe swali hilo nitauliza lingine manake linampelekea shahidi kujisikia vibaya,”.

 

 

Maswali na majibu Sabaya akiongozwa na wakili wake, Moses Mahuna kutoa Ushahidi

 

Wakili:Lengai hapa mahakamani alikuja shahidi wa jamhuri namba 13,akasema wakati wa upelelezi wake alienda Kilimnajaro na alipofanya mahojiano na baadhi ya watu akiwemo shahidi wa kwanza aliambiwa wewe hukuwa na mahusiano mazuri na Mkuu wako wa mkoa wewe hulo unalizungumziaje?

 

Shahidi:Mheshimiwa  Hakimu huyo shahidi namba moja aliyemweleza shahidi namba 13 hayo,hakuna popote shahidi huyo wa kwanza  alipodai mimi nilikiwa DC Hai sikuwa na mahusiano mazuri na aliyekiwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro

Alichokiwa anafanya shahidi wa 13 aliacha upelelezi akaenda kuokota aina ya siasa zilizokiwa Kilimanajro akaleta hapa mahakamani.

 

Ni shahidi muongo aliyeacha upelelezi akajiingiaza kwenye siasa akaacha taaluma yake

 

 

Wakili:Pia hapa mahakamani alikuja shahidi 10 Francis Mrosso,alisema  anakufahamu kwa kukuona kwenye Tv au social media lakini alidai kwamba kabla ya siku ya 22/1/2021 aliwahi kukuona wewe kwenye mazishi katika wilaya ya Hai na yeye alienda mwenge mazishi hayo sababu rafiki yake anayeitwa Tosh alifiwa na mtoto.Wewe una utetezi gani juu ya madai hayo ya bwana mrosso.

 

Shahidi:Simfahamu mtu anayeitwa Tosh wala siwezi kwenda kwenye mazishi ya mtoto nisiyemfahamu.Taarifa hizo kama zilikuwa za kweli angeeleza katika maelezo ya polisi

Huo ushahidi alioutoa ni wa uongo.

 

 

Wakili:kwanini unasema hujahusika na mkataba huu wakati kuna sahihi yako kwenye mkataba huu?

 

Shahidi:Mheshimiwa Hakimu huu mkataba siutambui na mawakili wangu walieleeza hivyo na kwa kuwa nilishakanusha ilikuwa kazi ya mashtaka kuthibitisha huu mwandiko na hii sahihi ni ya kwangu.Hawakukiunganisha kwa sababu walijua italeta matokeo wasiyoyapenda.Hii sahihi siyo ya kwangu.

 

Wakili:Shahidi hapa mahakamani alikuja shahidi tatu, Adanbest Marandu,anasema yeye ni mlinzi wa getini na tarehe 22/1/2021 aliingiza rekodi za magari na moja T 144 CZU,STL 5434 na T 846 CTU alisema alikuona wewe ukiingia na magari hayo. Wewe kwa ushahidi  huo  una utetezi gani?

 

Shahidi:Kati ya hizi gari tatu  sifahamu gari lolote. Mkanganyiko kwenye maelezo ya mtu aliyeleta kielelezo hiki na alieleza mahakama kuwa haoni kwa miaka sita iliyopita. Hangeweza kuandaa kulelezo hiki na aliaema alisaidiwa kuandika magari haya na Mrosso .

 

 

Wakili:Kililetwa kilelezo cha pili ni hati ya kuomba kupatiwa taarifa, ndiyo kilipelekea kupatikamaa kielezo cha tatu cha utetezi wako ukoje kuhusiana na kielelezo cha pili.,

 

Shahidi:Hii barua inatoka Takukuru kwenda kwa Mkurugenzi  mkuu wa Vodacom pamoja na maekezo mengine barua imeomba mawasiliano ya simu na sms katika kipindi cha 20/1/2021 hadi 25/1/2021 zimeombwa namba tatu 0758 707171 Lengai ole Sabaya 0759 78686 Enock Mnkeni 0746 935569 Ramwel Macha.

Naombaa mahakama inipe kielelezo namba tatu,

Barua inayotoka vodacom kwenda PCCB  kwenye maelezo wanasema pamoja na barua hii 0746 935569 haijafanya mawasiliano katika kipindi hiki……

 

Shahidi 10 na 13 wakadai ndani ya ile gari alimtambua kijana mmoja mshitakiwa wa sita akisema alitumia simu yake kufanya mawasiliano na mshitakiwa  wa kwanza

 

Wakili:Sasa bwana Lengai hapa mahakamani alikuja shahidi wa 13  anasema katika upelelezi wake alibaini kwamba wewe Sabaya na watu aliowaita vijana wako mliunda genge na mlikutana Point Zone (hotel) kupanga kwenda Kwa Mrosso ili kutenda makosa ya kihalifu wewe una utetezi gani juu ya amdai haya

 

Shahidi: Hilo ni genge la Ramadhani analipwa wafanyabishara ….

Maumivu ya wafanyabiashara wa Kilimanjaro kwa ajili ya mtu wao kushindwa ubunge wasiniwekee mimi kwa sababu ni chombo cha dola ….Niliweka uhai wangu rehani nikifanya kazi za serikali mpaka nikatumiwa watu wa kuniua sasa Ramadhani kama chombo cha dola anatakiwa akae upande wa serikali sio kutengeneza magenge na kutafuta watu waseme tulimpa sabaya pesa hiyo si kazi ya serikali.

 

Wakili: Shahidi huyo wa 13 alisema alipata taarifa fiche akasema uligawa fedha kwa vijana wako pale Tulia hoteli ... tena anadai mlikuwa chumbani.

 

Shahidi: Kimya akakaa kwenye kiti akawa anatokwa na machozi.

 

Wakili:Mheshimiwa  naomba shahidi apumzike kwa sababu kuna mambo yanamfanya apate ‘feelings’ (hisia).

Mheshimiwa  naomba nitoe swali hilo nitauliza lingine manake linampelekea shahidi kujisikia vibaya....Huku Sabaya akilia wakili wake akachukua chupa ya maji kutoka kwenye meza ya mawakili wa Serikali akayakataa akasema amefunga.

 

 

AKAENDELEA KUHOJIWA 

Wakili:Hapa mahakamani unashtakiwa kwa kesi ya uhujumu uchumi namba  27/2021 wewe na watu wengine sita jumla mnakua saba unamfahamuje mtu anaitwa Enock Chagulani

 

Shahidi:Simfahamu mheshimiwa  hakimu hadi tarehe 4/6 tulipopandishwa naye mahakamani kwa mara ya kwanza.

 

Wakili:na je unamfahamuje mshitakiwa  Watson Mwahomange

 

Shahidi:Sijawahi kumsikia simfahamu nilisikia jina  hilo wakati linasomwa mahakama tarehe  4/6.

 

Wakili:Na je unafahamije mshitakiwa wa nne  John Aweyo?

 

Shahidi:Simfahamu naye nimfahamu siku hiyo tarehe 4/6.

 

Wakili:na je unamfahamuje mshitakiwa wa tano Silvester Nyegu

 

Shahidi:Nilikuwa namuona kama watumishi wengine anaofanya kazi chini ya ofisi  ya DED (MKurugenzi Halmshauri ya wilaya)  Hai,alikuwa miongoni mwa hao watumishi

 

Wakili:na kuana mtu anaitwa Jackson Macha je unamfahamuje

 

Shahidi:Mheshimiwa huyo tarehe 21.6.2021 aliletwa gerezani akiwa na mshitakiwa  wa saba  na walipifika gerezani niliambiwa wananitafuta wakaniuliza mimi ndiyo Sabaya wakasema wameunganishwa kwenye kesi yangu

waliponitafuta ndio niliwaona kwa mara ya kwanza

 

Wakili:unaposema gerezani unamaanisha nini.

 

 

Shahidi:Gereza Kuu Kisongo

 

Wakili:Sasa kuna mshtakiwa  wa mwisho Nathan Msuya huyu yeye naye unamfahamu vipi?

 

Shahidi:Huyo mshitakiwa wa saba alikuja na mshitakiwa wa sita  gerezani wakiulizia Sabaya ni nani na wakaniambia wameunganishwa kwenye kesi inayonikabili na hawakuwa wananifahamu.




0 Comments:

Post a Comment