MAHAKAMA YATUPILIA MBALI PINGAMIZI LA MAWAKILI WA SABAYA

 

MAHAKAMA ya Hakimu Arusha, limetupilia mbali pingamizi lililowasilishwa na mawakili wa utetezi kwenye kesi ya aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake sita waliyokuwa wakipinga mahakama kupokea Counter book linalodaiwa kuorosha magari yalikuwa kwenye msafara wa Sabaya..

 

Uamuzi huo mdogo umetolewa leo Septemba 30, 2021 na Hakimu Mkazi, Patricia Kisinda anayesikiliza shauri hilo la uhujumu uchumi baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili na kuahirisha shauri hilo kwa muda kwa ajili ya kutoa uamuzi.

 

Amesema kuwa, mahakama imefikia uamuazi huo  kwa kuangalia ushahidi uliotolewa na shahidi wa tatu wa jamhuri, Adanbest Marandu,(61) ambaye ameieleza mahaka hiyo kuwa ana uelewa wa kutosha juu ya kielelezo alichotaka kukiwasilisha mahakamani hapo.

 

“Pingamizi kuwa kielelezo  hakijafuata matakwa ya kisheria na shahidi kihalali hana uhalali wa kutoa kielelezo hicho mahakamani, mahakama  imetupilia mbali na kukubali kielelezo hicho,” amesema Hakimu Kisinda wakati akitoa uamuzi huo mdogo.

 

 

Shahidi wa tatu upande wa Jamhuri, Adanbest Peter Marandu, (61) ambaye ni muangalizi wa geti (mlinzi) mfanyakazi kwa Fransis Mrosso akiongozwa na wakili wa Serikali Mwandamizi, Tarsila Gervas kutoa ushahidi wake

 

Sehemu ya mahojiano hayo yalikuwa kama ifuatavyo;

Wakili: Mzee Marandu unaishi wapi?

Shahidi: Shamsi

Wakili: Shamsi iko wapi?

Shahidi: Kata ya Elerai

Wakili:Una elimu gani?

Shahidi:Darasa la saba 1968-1975

Wakili:Unafanya kazi gani Arusha?

Shahidi:Nafanya kazi kwa Francis Mrosso,mwangalizi wa geti 

Wakili:Huyu Mrosso hilo geti unangaalia linahusu nini?

Shahidi:Magari ya kufanyiwa service na pump

Wakili:Hii kazi ya uangalizi kwa Mrosso umeifanya kwa muda gani?

Shahidi: Miaka sita

Wakili: Wewe kama.mwangalizi wa geti ni majukumu yapi unayo?

Shahidi: Kufugulia magari yanayoingia na kutoka, kuandika magari ‘time’ (muda) ya kuingia na kutoka na limeenda kwa nani

Wakili: Kitu kingine unachifanya?

Shahidi:Kutunza counter book yangu

Wakili:Hili ‘counter book’ linahusiana na nini?

Shahidi:Kurekodi magari yaliyoingia

 Wakili:Hili ‘Counter book’ unalitunzia wapi/

Shahidi:Nalitunzia pale pale ‘yard’.

Wakili:Hii yard iko wapi?

Shahidi:Iko Mbauda

Wakili:Hilo ‘counter book’ unaweza kulielzea likoje?

Shahidi:Ni jeusi, lina karatasi nyeupe juu na imeshikiliwa na solo tape,

 Wakili: Mwonekano wake?

Shahidi:Kwa ndani ukifungua nimeandika namba za simu za watu waliongia ndani nyuma ya hiyo counter book,nimechora mistari minne ya kutenganisha

Wakili:Umeeleza hili kaunta ndiyo unaweka rekidi za magari unaziwekaje?

Shahidi:Naandika tarehe na mwezi na code namba halafu gari linapoingia naandika namba zake na linaenda kwa nani na muda wa kuingia na kutoka

Wakili:Umesema unaingiza code namba ni utambulisho wa nini?

Shahidi:Code namba ya utambulisho kati ganvy na mwenzangu ay boss wangu

Wakili:Hii code inatokana na nini?

Shahidi:inatokana na tarehe

Wakili:umeeleza unaandika gari linaenda kwa nani kwa nini?

Shahidi:Nimeelekezwa na bosi ili ikitokea gari la mtu limetokea tatizo  ukicheki kwenye kitabu inaonyesha gari imeenda kwa fulani

Wakili:Mzee Marandu ukifika kazini asubuhi unafanya nini kuhusiana na counter book lako?

Shahidi:Nafanyia maaandalizi kulingana na tarehe

Wakili:Umeeleza gari inakoenda kwa namna inavyopaki mnapaki vitu?

Shahidi:Kila mtu na kitengo chake hivyo inatokana na namna….

Wakili: Mzee Marandu tarehe 22/1/2021 ukisikia unapata kumbukumbu zipi

Shahidi: 22 januari nakumbuka ilikuwa siku ya ijumaa,katika kumbukumbu  yangu nilifanya maandalizi pale getini nikachukua kaunta nikajaza tarehe,code namba 1730. Nikapokea magari hadi saa 8:35 mchana kuna gari ziliingia 3 zikifatana niliandika kwenye kitabu

 gari ya kwanza Nakumbuka ulikuwa ni T 144 CZU, la pili likaingia STL 5434 na la  tatu T 846 CTU.

Wakili: Unaweza kukumbuka yalikuwa yanafananaje?

Shahidi:ile ya kwanza ilikua rangi nyeusi ya pili nyeupe la tatu la tatu rangi ya ugoro

Wakili:Na baada ya magari kuingia nini kiliendelea?

Shahidi:Niliona watu saba  walishuka wakaangaza macho kushoto kulia kushoto kulia wakaingia kwa Mrosso wakatoka nje mmoja akabaki ndani. Sikujua kilichoendelea mle ndani kwani getini hadi ofisini ni hatua 60

 

Wakili:Hao watu saba ukiambiwa umzungumzie mmoja mmoja unaweza kuwazungumziaje?

Shahidi:Sitaweza kuwazungumzia chochote.

Wakili: Umsema uliona watu saba fafanua uliona nini?

Shahidi:Walishuka wakaingia ndani mmoja akabaki wengine wakabaki ..Nilimuona akiwa ndani kwa mhasibu.Huyo bwana niliyemuona pale ni mtu mmoja anaongea na mhasibu,nilimuona Sabaya.

Wakili:Sabaya ni nani

Shahidi:Mkuu wa wilaya ya Hai

Wakili:ulifahamuje ni Sabaya na ni DC wa Hai?

Shahidi:Huwa namuona kwenye TV 

Wakili:Na kwa kuwa ulimuona na namna ulivyomfahamu kwa hiyo siku alikuwa yukoje?

Shahidi:Alikuwa amenyoa panki,amevaa kaunda suti ya mikono mirefu ya rangi kama bluu alikuwa amenyoa oo

Wakili:Sasa mzee Marandu hii siku uliandika kwenye counter book, nikikuonyesha hilo counter  boook utawezaje kuthibitisha hiki ndo kitabu ulichoandika magari uliyoyataja?

Shahidi:Lina rangi nyeusi,ina karatasi nyeupe juu imeshikiliwa na solo tape

Tar 22 code namba 1730

Kingine tarehe 23/1/2021 boss alinifuata akaniuliza kama nimeandika zote nikamtajia namba zake tofauti na magari mengine yote.

 

Wakili: Mzee Marandu baada ya kumtaja Sabaya kumuona nini kiliendeela akiwa ofisini

Shahidi: Sikujua chochote kilichoendelea ila walitoka tena kwa pamoja magari yote na Mrosso alitoka nje ya geti kwa miguu akiwa na mtu mmoja kati ya wale. Magari yalitoka saa 9:15

Wakili: Kuna daftari naomba nimpe shahidi aweze kueleza hii mahakama ni nini?.

Liangalie tueleze ni kitu gani?

Shahidi:hili ni counter  book la kuhifadhi kumbukumbu yangiu

Wakili: Angalia maingizo ya tarehe 22 angalia kama unaweza kutambua na ni kwa sababu zipi anayatambua?

Shahidi:Nimeyatambua mimi ndo niliyerekodi  magari yote yaliyoingia code namba 1730 na maingizo ya magari matatu ambayo nimeweka tiki haya hapa (huku akionyesha mahakama)

Wakili:Unaiambia nini mahakama kuhusiana na maingizo hayo?

Shahidi:ningeiomba mahakama ichukue kama kithibitisho.

 

Wakili wa utetezi, Moses Mahuna akasimama: Utetezi mshitakiwa wa kwanza  wa 1 na 2 tunapingamizi dogo la kisheria juu ya kupokelewa kwa kitabu hiki. Mheshimiwa  kabla ya kitabu kutolewa na tumekiona kimetolewa kwenye mikoba ya wakili msomi wa serikali, Tarsila ndiye aliyekuja na hiki kitabu kwenye mikoba yake. Wakili  msomi hatuelewi hatuelezi yeye binafsi alikipata wapi hiki kitabu ana anamuonyesha shahidi na kumtaka shahidi akitoe mahakamani.

Kitabu chenyewe kinaonekana kimetumika mwisho tarehe 27/5?2021 inaonyesha kilikuwa upande wa uchunguzi, wakili hatuelezi chain of custody kama sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai inavyoelekeza( akataja kifungu cha sheria).

 

Atueleze kimepatikanaje wakili amekitoa wapi ni dhahiri kwamba ushahidi huu kwa namna yoyote vile kwa kuwa hakuna na shahidi mwenyewe akatoa kwenye mifuko yake.

 

Ushahidi huu haukupatikana kwa kufuata sheria umekiuka (anataja kifungu cha sheria na kufafanua )

Tunaomba ushahidi huu usipokelewe ni batili umekiuka sheriia za nchi, sheria za makosa ya jinai.

 

Ni ombi letu mhakama ikatae kupokea ushahidi huu

 

Wakili wa utetezi, Freedoline Gwemelo: Tunapinga vikali kupokelewa kielelezo hiki tukisapoti yale yote aliyosema wakili wa mshitakiwa wa kwanza na wa pili tukiongezea yafuatayo;

1.Msisitizo wa sheria 

Lengo ya kifungu ni kuzuia ‘tamped’ ya kielelezo kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine tuwe na uhakika kielelzo hakijawahi kuwa na  hakijawa ‘tamped’.

Tunasisitiza kielelezo hiki kisipokelewe kwa sababu kinatia shaka kwa sisi mawakili, watuhumiwa na mahakama hii.

0 Comments:

Post a Comment