PROFESA BAREGU AFARIKI DUNIA

Prof Mwesiga Baregu

  MJUMBE wa kamati Kuu ya Chama Cha Demekrasia na Maendeleo,(CHADEMA), Prof Mwesiga Baregu amefariki dunia kwenye hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akiendelea na matibabu. 


Taarifa kutoka kwa watu wa karibu na familia hiyo zimethibitisha kutokea kwa kifo hicho  ambapo taarifa rasmi itatolewa na familia.


Profesa, Baregu alilazwa hospitalini hapo Februari 16, mwaka huu baada ya kuugua ghafla akiwa nyumbani kwake.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa siku inayofuata na Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano Chadema, Tumaini Makene ilieleza kuwa hali ya  Prof Baregu iliendelea kuimarika taratibu tangu afikishwe hospitalini hapo ambapo alikuwa akipatiwa matibabu chini ya uangalizi maalum.


Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi ...


0 Comments:

Post a Comment