IJUE SAFARI YA JPM KISIASA MANAKE MPAKA MAUTI YANAMKUTA

 ·1959- Azaliwa Chato kaskazini magharibi mwa Tanzania 

·1995- Achaguliwa kuwa mbunge kwa mara ya kwanza 

·2000- Ateuliwa kuwa Waziri

·2015- Achaguliwa kuwa rais kwa muhula wake wa kwanza 

·2020- Achaguliwa kwa kipindi cha pili kuwa rais 

·2020 Novemba tarehe 5 – Aapishwa kwa muhula wa Pili 

·2021 Machi Tarehe 7- Uvumi unaanza kuenea kuhusu aliko rais Magufuli baada ya kukosa kuonekana kwa muda wa wiki moja

·2021 Machi tarehe 11 – Vyama mbali mbali vya Upinzani nchini Tanzania vyataka kujua hali ya rais Magufuli na aliko

·2021 Machi Tarehe 12 -Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akana kwamba rais Magufuli anaugua asema yupo ‘ buheri wa afya na anaendelea kuchapa kazi’ 

·2021 Machi Tarehe 15 – Makamu wa Rais Samia Suluhu awapa Watanzania ‘salamu’ kutoka kwa Rais Magufuli huku hofu ikizidi kuhusu hali yake na aliko 

·2021 Machi, tarehe 6 - Alazwa katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete kwa tatizo la moyo la mfumo wa umeme 

·2021 Machi tarehe 7 - Aliruhusiwa kurejea kazini 

·2021 Machi tarehe 14 - Alikimbizwa Hospitali ya Mzena Dar es Salaam kuendelea na matibabu

·2021 Machi tarehe 17 saa kumi na mbili jioni - Magufuli afariki dunia 

·2021 Machi tarehe 17 Usiku – Makamu wa rais Samia Suluhu atangaza kupitia runinga kifo cha rais Magufuli .Siku 14 za maombolezo zatangazwa.Bendera kupeperushwa nusu mlingoti.

0 Comments:

Post a Comment