HIKI HAPA CHANZO KIFO CHA JPM

 

RAIS, John Pombe Magufuli ameaga Dunia.

Kifo cha Magufuli kimetangazwa rasmi usiku wa  Jumatano Machi 17, mwaka huu na makamu wake Samia Hassan Suluhu.

Amesema kwamba rais Magufuli aliaga dunia katika hospitali ya Mzena iliopo jijini Dar es Salam kutokana na matatizo ya moyo.

Akithibitisha kifo hicho Suluhu amesema kwamba rais Magufuli alianza kuugua mnamo tarehe 14 mwezi Machi na kulazwa katika hospitali hiyo ambapo alifariki.

0 Comments:

Post a Comment