YANAYOENDELEA KESI YA MBOWE MAHAKAMA YA KISUTU








JESHI la polisi limeweka ulinzi mkali kwenye Mahakama ya Kisutu wakati 

 Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe  na viongozi wakuu wengine watano wa chama hicho wakitarajiwa kurejeshwa mahakamani hapo leo 

Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard, Mashauri leo anatarajiwa kutoa uamuzi endapo viongozi hao wapatiwe dhamana wawe uraiani au waendelee kushikiliwa mahabusu kwenye gereza la Segerea mpaka kesi hiyo itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.


Hatua ya viongozi hao kushikiliwa  kwenye gereza la Segerea tokea juzi inatokana na upande wa jamhuri kuwasilisha hoja mahakamani hapo wakitaka wanyimwe dhamana kwaaslahi ya umma hoja iliyopita  vikali na mawakili  viongozi hao ndipo hakimu akaahirisha shauri hilo mpaka leo kwa ajili ya kusoma uamuzi.

0 Comments:

Post a Comment