Mahakama ya Kisutu imekubali kuwapa dhamana, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watano kwa sharti kila mmoja awe na wadhamini wawili huku kila mshtakiwa akitakiwa kusaini dhamana ya maandishi ya Sh milioni 20.
Pia wadhamini watasaini kiwango hicho cha fedha ambapo washtakiwa wakiwa nje kwa dhamana wanatakiwa kuripoti polisi mara moja kwa wiki kila siku ya alhamisi.
Uamuzi huo mdogo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri anayesikiliza shauri hilo linalovuta hisia za wengi.
Hata hivyo uamuzi huo umetolewa bila washitakiwa hao kuwepo mahakamani baada ya Ofisa wa Magereza Inspekta Shaban kuieleza mahakama "Mbowe na wenzake wameshindwa kufika Mahakamani hapo kusomewa uamuzi wao kuhusu dhamana kwa sababu gari walilopanda limearibika."

0 Comments:
Post a Comment