DIWANI KESSY: Tunakusanya zaidi ya 1.3 Billion , 10% Ya Kina Mama na Vijana. GRACE MACHA: Tumeshatoa Zaidi ya 76 Millioni kwa ajili ya mikopo kwa Kina mama na Vikundi vya Vijana...

Diwani wa Kaloleni Mh. Emanuel Kessy                           Bi. Grace Macha Mkurugenzi AVE
Diwani wa Kata ya Kaloleni Mh. Emanuel Kessy alikuwa mgeni rasmi katika Semina ya Mafunzo ya Uongozi na uadilifu wa Kifedha. Semina iliyoendeshwa na Kampuni ya Arusha Vicoba Empowerment Ltd kwa Kushirikiana na Meru Community Bank- MeCOB.

Full Video Hii Hapa Unaweza Kubofya Kitufe Cha Play hapo chini, Usikose kutazama VOA TV Breaking News Hapa
Awali akifungua Semina hiyo Mkurugenzi wa Arusha Vicoba Empowerment Bi. Grace Macha alisisitiza kuwa Mafunzo hayo yanalengo kuhakikisha wanopewa Fedha hizo wanazirudisha kwa wakati lakini pia kuzitumia kwa malengo tarajiwa.

Pamoja na Mambo mengine Mwenyekiti wa Arusha Vicoba Empowerment Bw. Hassan Moses aliwakumbusha washiriki ambao ni wananchi kutoka kwenye vikundi mbalimbali vya VICOBA wajue majukumu hasa ya uongozi kwenye Kikundi ili kurahisisha ushughulikiaji wa masuala yanayohusu kikundi.
Mwenyekiti wa Arusha Vicoba Empowerment Ltd Bw. Hassan Moses
Mgeni Rasmi Mh. Emanuel Kessy Diwani wa Kata ya Kaloleni Jijini Arusha alisema Halimashauri hiyo imejipanga ipasavyo kwa ajili ya Mikopo kwa ajili ya kina mama na vijana huku akisisitiza kuwa Halmashauri hiyo inakusanya zaidi ya BIlioni 1.3 kwa mwezi huku ikitenga asilimia kumi 10% kwa ajili ya mikopo kwa kina mama na vijana.

Nao Wananchi /Washiriki wa Semina hiyo walionesha kufurahishwa na mafunzo hayo pamoja huku wakiipongeza Arusha Vicoba Empowerment Ltd kwa kuwapa elimu hiyo pamoja na kuwakabidhi mikopo wanayopewa na Halmashauri kama ilivyopangwa na kwa wakati.




Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bi. Grace Macha Amesema kampuni hiyo tayari imetoa mikopo ya zaidi ya shilingi millioni 76 kutoka Halmashauri ya jiji la mikopo kwa kina mama na vikundi vya vijana.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo Kata ya Levolosi Bi. Joyce Kimbute ambaye pia alihudhuria Semina hiyo aliiambia Habaritanzaniagracemacha.com na VOA TV kuwa hatua ya Kampuni ya Arusha Vicoba Empowerment Ltd kutoa mafunzo hayo ni Hatua ya Kupongezwa huku akisisitiza vijana na kina mama kujiunga na vikundi mbalibali vya vicoba ili kujikwamua kiuchumi na kuachana na umasikini.
Afisa Maendeleo Kata Ya Levolosi Bi. Joyce Kimbute
Aidha katika Hatua nyingine Maafisa kutoka Meru Community Bank / Benki ya Wananchi Meru walielekeza Wanavicoba kujiwekea desturi ya kuwa na akaunti ya pamoja kwenye taasisi za kibenki kutokana na kuwa zitakuwa salama zaidi kuliko wangzitunza kwa njia nyinginezo.

Bw. Honest Mungure na Faith Ephata walieleza umuhimu wa kuhifadhi fedha benki toafuti na kutumia njia za wawekahazina. huku wakieleza utofauti wa kuwa na akaunti katika bnki ya Meru Community Bank na Benki zingine.
                Bw. Honest Mungure                                                                     Bw. Faith Ephata

0 Comments:

Post a Comment