MUME AMUUA MKE ARUSHA KWA KUMPIGA RUNGU KICHWANI NA KUMKATA KWA MAPANGA

Mama wa Marehemu, Jamillah Ramadhan, (48), alisema kuwa amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mwanae huyo wa kwanza kati ya watoto watatu aliokuwa nao huku akidai kuwa mpaka sasa hajaelewa ni kwa nini Lomayan aliamua kumuua.

“Mara kwa mara walikuwa akigombana wanayazungumza wanayamaliza wanarudi kulea watoto wao sijui ni kitu gani kilimuongia huyu kijana mpaka kuamua kumuua mwanangu na sijui nani atawalea hao watoto manake naye kakimbia,” alisema Jamilah huku akilia.

Mmoja wa ndugu wa marehemu alisema kuwa baada ya kupata taarifa walienda kumuona marehemu Agnes kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mount Meru ambapo walipomuangalia maeneo ya uso walimuona ana alama kichwani na katobolewa na kitu chonye ncha kali juu ya mdomo na pana tundu.


Agnes Lucas, (28) enzi za uhai wake

MKAZI wa Ilboru, Lucas Lomayan, anadaiwa kumuua mkewe, Agnes Lucas, (28), maarufu kama Asha kwa kumpiga kichwani na kitu kizito na kumkata maeneo mbalimbali ya mwili na kitu chenye ncha kali kisha kutoweka nyumbani kwao.

Inadaiwa Lomayan ambaye hufanya kazi ya kuuza nyama ya ng’ombe kwenye bucha maeneo hayo aliwafungia watoto wao sebuleni huku akiwatisha kwa rungu ili wasipige kelele ambapo aliingia chumbani na kumpiga mkewe ambaye alikuwa akilia lakini majirani hawakuweza kutoa msaada kwa madai kuwa ilikuwa ni mazoea yao kupigana mara kwa mara.

Tukio hilo lililovuta hisia za wengi jijini hapa lilitokea usiku wa kuamkia jana maeneo ya Ilboru karibu na Kwa Mollel ambapo kwenye nyumba hiyo zinaishi familia tatu wakiwemo ndugu wawili wa Lomayan na mpangaji mmoja.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo bado hawajajua chanzo chake ila alidai kuwa kifo cha marehemu kimetokana na kupigwa na kitu kizito kichwani na wanaendelea na juhudi za kumtafuta Lomayan.  
WATOTO WA MAREHEMU WANENA
Watoto wa Marehemu, Jesca (10) na Jackson, (5) walisema kuwa baba yao alikuwa na tabia ya kumpiga mama yao mara kwa mara ambapo amekuwa akiwakataza wasipige kelele vinginevyo wakikaidi amekuwa akiwajeruhi.

Jackson alisema kuwa  kuna siku alipiga kelele baba yake alimpiga kwa kutumia rungu kwenye mkono wa kushoto huku Jesca akidai kuwa yeye kuna wakati aliwahi kupiga kelele baba yake akampiga na ubapa wa panga mgongoni hali iliyomsababisha akapatiwe matibabu hospitali.

“Jana mama alichelewa kuja alikuja kama saa nne usiku, alipokuja baba akafunga mlango akaanza kumpiga, sisi tulikuwa tunalia taratibu, (anawaza kidogo) baba alikuja kunywa maji kwenye friji akanigusa na rungu hapa kwenye shavu (la kushoto) Huyu Jakson hakusikia alikuwa ameshalala.

“ Mama alilia sana na mimi nikawa nalia kimyakimya mpaka nikapitiwa na usingizi, nilipoamka asubuhi tukakuta baba hayupo ila mama yupo kitandani, nikabandika chai nikaenda kumsalimia mama akawa haitiki ndiyo nikaenda kumuita mama Oscar,” alisema Jesca.
Alisema kuwa chumbani kwa wazazi wake kulikuwa kumetapakaa damu chini na kitandani alikokuwa amelala mama yao.
MAJIRANI WANENA
Mama Oscar ambaye ni jirani wa marehemu aliyeolewa na kaka wa Lomayan, alisema kuwa hakusikia wakati Lomayani akimpiga mkewe ila asubuhi watoto wa marehemu walimuita wakimwambia kuwa wanamuita mama yao haitiki.

“Nilienda nikamkuta amelala akielekea ukutani huku mwili wake ukiwa umevimba nilivyomuona nilidhani anahitaji kupelekwa hospitali hivyo nikatoka nje nikawaita ndugu zetu walipomuangalia wakabaini kuwa kashakufa,” alisema Mama Oscar ambaye alidai kuwa haelewi chochote zaidi kwani baada ya hapo alipoteza fahamu.

Majirani wengine waliongea kwa sharti la kutotajwa majina yao walisema kuwa Lomayan amekuwa na tabia ya kumpiga na kumjeruhi mkewe kwa kumkata na panga mara kwa mara ambapo walisema kuwa marehemu Agnes alikuwa ana alama mbili kubwa usoni alizoshonwa baada ya kukatwa na mumewe siku za nyuma .

“Jana sisi tulisikia kelele kama kuanzia saa tatu hivi usiku lakini hatukuamka kwa sababu ni kawaida yao, sisi tunakaa kwa huku nyuma ya nyumba yao na ziliendelea mpaka kwenye saa tisa usiku tukajua wameelewana wakaamua kulala” alisema jirani huyyo.

Alisema kuwa asubuhi waliposikia kuwa mama Jesca amefariki walifika kwenye nyumba hiyo na kukuta damu zikiwa zimetapakaa chumbani nyingi zikiwa chini na nyingine kitandani huku mwili wa marehemu ukiwa umefunikwa na balnketi lakini walipomfunua walikuta akiwa hana nguo hata moja huku ukiwa umevimba sana.

Jirani mwingone alisema kuwa alipomuangalia marehemu alikuwa amebonyea kichwa eneo la kisogoni na juu kidogo ya paji la uso ambapo alikuwa ametapaa damu kwenye maeneo mbalimbali ya mwili hivyo ilimuia vigumu kubaini ni maeneo gani hasa aliyojeruhiwa.
“Kila mtu anatunyooshea kidople majirani kwa nini hatukusaidia lakini ukweli unajulikana kabisa marehemu na mume wake kila wiki ni lazima wapigane na hata akijeruhiwa anaenda kwao anakaa kidogo wanarudi na wakati mwingine hata kwao haendi anachofanya anaenda hospitali anashinwa anarudi sasa tungeingiliaje kwa hali kama hiyo?,” alihoji jirani mwingine.


MAMA WA MAREHEMU ANENA

Mama wa Marehemu, Jamillah Ramadhan, (48), alisema kuwa amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mwanae huyo wa kwanza kati ya watoto watatu aliokuwa nao huku akidai kuwa mpaka sasa hajaelewa ni kwa nini Lomayan aliamua kumuua.

“Mara kwa mara walikuwa akigombana wanayazungumza wanayamaliza wanarudi kulea watoto wao sijui ni kitu gani kilimuongia huyu kijana mpaka kuamua kumuua mwanangu na sijui nani atawalea hao watoto manake naye kakimbia,” alisema Jamilah huku akilia.

Mmoja wa ndugu wa marehemu alisema kuwa baada ya kupata taarifa walienda kumuona marehemu Agnes kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mount Meru ambapo walipomuangalia maeneo ya uso walimuona ana alama kichwani na katobolewa na kitu chonye ncha kali juu ya mdomo na pana tundu.







Sent from my iPhone

0 Comments:

Post a Comment