Happy Lazaro,Arusha 

Shirika linajishughulisha na uhifadhi wa Tembo la WILD SURVIVORS  waja na teknolojia ya kisasa ya utatuzi wa migogoro kati ya Tembo na jamii zinazopakana na hifadhi.


Hayo yamesemwa jijini Arusha leo na Afisa miradi ya jamii wa shirika hilo,Masalu John Masaka wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la 15 la kisayansi la TAWIRI  linalofanyika jijini Arusha .




Amesema kuwa lengo  la kushiriki kongamano hili  ni kuwaambia watu kazi wanazofanya ili kufanikisha hizi kazi za utatuzi wa migogoro kati ya tembo na jamii zinazopakana na hifadhi 

Amefafanua kuwa, lengo la kuanzishwa kwa shirika hilo ni kuhakikisha kwamba jamii zinazopakana na hifadhi zinaishi kwa amani na Tembo kwa kutumia njia rafiki kama mizinga ya nyuki .



Aidha ametoa wito kwa jamii  pamoja na wahifadhi kufanya kazi pamoja kwa kukutumia njia rafiki ili tuweze kuishi pamoja na tembo kwani idadi ya watu inapoongezeka na idadi wanyama inapoongezeka ardhi haiongeki ,hivyo tunahitajika kufanya kazi kwa pamoja  wakiwemo jamii iliyoathiriwa wahifadhi pamoja na wanyamapori.




" Tunafanya kazi zaidi za kuhifadhi Tembo kwa namna ambayo tunatatua migogoro kati ya Tembo na wakulima wanaopakana na hifadhi ."amesema Masaka .


"Tumekuja hapa kwenye mkutano huu kwa ajili ya kuwaeleza watu shughuli ambazo tunazifanya kwa mfano tunatumia mizinga ya nyuki ambayo inatoa mazao kama asali ambayo inakuwa faida kwa vikundi  vya akinamama katika vijiji ambavyo tunafanya kazi."amesama Masaka .



"Tumekuja pia kwenye huu mkutano kwa lengo la kueleza watu namna ambavyo tunakusanya data  na tunatumia vifaa gani tunatumia kamera  pamoja na teknolojia ya simu ambayo tunakuwa na application inayoitwa survey one two three tunatumia kukusanya data ."amesema .



Amefafanua kuwa tangu shirika lianzishwe wamepiga hatua kwani wameshaweka uzio wa mizinga  ya nyuki zaidi  ya kilometa 20 katika maeneo mbalimbali kwani wana uzio wa nyuki kilometa saba upande wa Ngorongoro vijiji vya wilaya ya Karatu na kilometa sita kwa upande wa serengeti na kilometa sita katika vijiji vya Rukwa katavi vijiji ambavyo vinapatikana na hifadhi ya Taifa Katavi .


"Tumeona mabadiliko yapo matukio ya Tembo kuingia mashambani  na kula mazao ya wakulima yamepungua na tumeona katika vijiji ambavyo tumefanya navyo kazi mwanzoni  ikiwemo Ngorongoro wakina mama wameanza kupata kipato kutokana na mazao ya nyuki ."amesema .



"Tunawafundisha na tunawapa mafunzo  ya namna ya kuweka uzio wa mizinga ya nyuki namna ya kuvuna mazao ya nyuki na na namna ya kuchakata na kuwaunganisha  na soko ."amefafanua  Masaka .



"Kwa uchunguzi ambao tumefanya ni kuwa tembo anawaogopa nyuki hivyo anavyokaribia karibu na mzinga wa nyuki na anapousukuma ule waya ambayo umeunganisha mzinga mmoja hadi mwingine  na nyuki anapotikiswa wakiwa na asali wale nyuki walinzi wanatoka nje kuangalia kitu ambacho kinataka kuchukua mazao yake ba wale nyuki wanapotoka nje wanatoa ile sauti na tembo akisikia anaamua kuondoka."ameongeza Masaka .



 


Wananchi wa Kitongoji ya Ormekeke Kijiji cha Nasipaoriong tarafa ya Ngorongoro wameanza kunufaika na mradi wa maji baada ya Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kuchimba kisima chenye uwezo wa kuzalisha lita 13,00 kwa saa na kujenga tanki  lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 135,000 kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo.



Akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo Kamishna wa Uhifadhi Ngorongoro Abdul-Razaq Badru ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kรผmeleta  manufaa makubwa  kwa wananchi wa maeneo ya Ormekeke, Nasipaoriong na Olduvai yaliyopo hifadhi ya Ngorongoro ambao kipindi cha kiangazi walilazimika kuhamishia mifugo maeneo ya mengine kufuata maji


“Mradi huu tuliuanza kwa  kuwashirikisha wananchi ikiwa ni utekelezaji wa kuboresha mahusiano ya NCAA na jamii kwa kutatua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo ambalo moja wapo ni maji, umeshakamilisha na kitongoji cha Ormekeke wameanza kutumia maji, rai yangu kwa wananchi ni kulinda na kusimamia miundombinu ya mradi huu kupitia kamati za maji na mazingira ambazo wameshaziunda” alisema  Kamishna Badru.



Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ormekeke Bw.  Oreteti Olenjorio ameeleza kuwa eneo la kitongoji hicho ni kame na halina chanzo chochote cha maji hivyo uamuzi wa Serikali kupitia mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kuchimba maji ni msaada mkubwa kwa matumizi ya wananchi na mifugo na kuahidi kulinda miundombinu ya mradi huo  kupitia jumuiya za maji na kuzingatia sheria za hifadhi.



Kwa mujibu wa Msimamizi wa Mradi huo Mhandisi Godlove Sengele pamoja na mradi huo kunufaisha wananchi na mifugo yao pia utahudumia Makumbusho ya Olduvai, Leakey Camp, Mtui Camp, Nyumba za Maaskari pamoja na jamii ambayo imejengewa vituo vinne vya kuchotea maji na vituo vitatu vya kunyweshea mifugo.




Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi, asema tawasifu ya Balozi Daniel Ole Njoolay ni hazina ya kipekee itakayodumu kwa vizazi vijavyo—hasa ikizingatiwa kwamba safari yake ya elimu, utumishi na uongozi imejaa miujiza, majaribu makubwa na ushindi uliopatikana kwa juhudi na uhodari.





Ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa kitabu cha Balozi Njoolay kilichofanyika Novemba 29, 2025 katika ukumbi wa Corridor Spring Hotel jijini Arusha kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, akiwemo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushurukiano wa Afrika Mashariki, James Millya, mabalozi na viongozi wastaafu.



  Prof. Kabudi alisema maisha ya Balozi Njoolay—hasa safari yake ya elimu na uongozi—yamejaa miujiza, vikwazo, ujasiri na maamuzi magumu yaliyojenga msingi wa mafanikio yake.


Katika hotuba hiyo yenye msisitizo mkubwa wa thamani ya kumbukumbu na usomaji wa vitabu, Prof. Kabudi alimshukuru Mungu kwa kuwezesha tukio hilo muhimu, huku akipongeza uthubutu wa Balozi Njoolay kuandika kitabu kinachoeleza simulizi ya maisha yake kuanzia utotoni hadi safari yake katika utumishi wa umma na diplomasia.



Alisema kitabu hicho ni zawadi muhimu kwa taifa, akibainisha kuwa ni wachache mno wenye moyo wa kuandika na kurithisha maarifa yao. Alikumbusha pia mazingira magumu aliyoyapitia Balozi Njoolay wakati jamii ya Maasai ilipokuwa ikiona elimu si jambo la lazima, hadi pale serikali ilipolazimisha watoto kwenda shule.



Prof. Kabudi aliwataka vijana na Watanzania kwa ujumla kusoma kitabu hicho ili kuishi na kujifunza kupitia uzoefu huo wa kipekee. Alihusisha umuhimu huo na desturi yake binafsi ya kusoma hotuba za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, akisema kuwa tawasifu na hotuba hizo bado zinatoa mwanga mkubwa katika zama za leo.


Akinukuu hotuba ya Nyerere ya mwaka 1965 iliyowasisitiza vijana kujenga na kulinda taifa, Prof. Kabudi alieleza kuwa taifa linaweza kudidimia kama vijana hawajengi misingi thabiti ya uzalendo, maadili na dhamira ya kulihudumia.


Katika kuhimiza usomaji wa vitabu, Prof. Kabudi aliainisha manufaa kadhaa ikiwemo kupanua maarifa, kuchochea ubunifu, kuimarisha maadili na kuongeza uwezo wa kujenga hoja na kufanya maamuzi sahihi. Aliitaka jamii, hasa familia, kuwahamasisha watoto na vijana kusoma vitabu kama sehemu ya malezi na ujenzi wa fikra.


Kwa waandishi wa vitabu, aliwasihi kuendelea kuandika bila kukata tamaa licha ya changamoto ya wananchi wengi kutopenda kusoma. Aliwatia moyo kwamba kila kitabu ni chombo cha maarifa kitakachowanufaisha wengi katika siku za usoni.


Prof. Kabudi alimpongeza Balozi Njoolay kwa uzalendo na utumishi wake uliotukuka, akisema amekuwa mfano bora wa kuigwa na viongozi pamoja na vijana nchini. Pia alishauri kitabu hicho kisambazwe kwa njia za kidijitali ili kuwafikia wasomaji wengi zaidi ndani na nje ya Tanzania.


Baada ya hotuba hiyo, Waziri Kabudi alizindua rasmi kitabu cha Balozi Daniel Ole Njoolay, akiitimisha shughuli hiyo kwa wito wa kuenzi na kuishi hekima iliyomo katika kurasa zake.


 



Katika hafla ya uzinduzi wa kitabu chake Tawasifu ya Balozi Daniel Ole Njoolay, iliyohudhuria na viongozi mbalimbali wakiwemo Mgeni Rasmi, Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Habari; pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Millya, Balozi Daniel Ole Njoolay alitoa risala yenye kugusa hisia kuhusu maisha yake, safari ya elimu na utumishi wake kwa umma.



Balozi Ole Njoolay alieleza kuwa chanzo cha kitabu hicho:
“Uamuzi wa kuandika kitabu hiki nilichukua miaka mitatu iliyopita, baada ya msukumo wa marafiki wengi ambao kwa muda mrefu walinishauri kufanya hivyo. Baadhi yao wapo hapa leo. Kitabu hiki kinaeleza maisha yangu na utumishi wangu kwa umma, safari ambayo kwa sehemu kubwa imejaa miujiza.”

Safari ya Elimu Katika Mazingira Magumu



Balozi Njoolay alisimulia changamoto za kupata elimu katika jamii ya Kimasai kipindi hicho, ambako wazazi walikataa watoto kwenda shule wakiamini ni sawa na ‘kuwapoteza’.

“Wazee walipokubaliana angalau kila boma litoe mtoto mmoja, mzazi alichagua mtoto ambaye si ‘rasilimali kubwa sana’. Mimi nilichaguliwa kwa sababu nilikuwa sichungi mbuzi vizuri,” alisema kwa utani uliochekesha ukumbi.


Alieleza kuwa alipoanza shule, mzazi alilazimika kulipa ada mwaka mmoja baada ya kuanza masomo. Baada ya baba yake kufariki dunia, watu walimwambia mama yake aache kumsomesha kwa kuwa alikuwa mjane.
“Hata hivyo, mama yangu hakukata tamaa. Nilipofaulu kwenda sekondari, aliniuliza kama nataka kuendelea. Nilimwambia ndiyo, akaniambia basi tuuze ng’ombe iliyobaki. Huo ndio ulikuwa msingi wa safari yangu.”

Uongozi Bila “Godfather”



Akimweleza hadhira jinsi alivyoingia kwenye uongozi, Balozi Njoolay alisema matukio mengi katika maisha yake yalikuwa ya kipekee.
“Nilishinda ujumbe wa NEC (Vijana) nikiwa na miaka 29. Nilikuwa mgeni kabisa ndani ya chama, lakini nikaomba kura kwa mara ya kwanza na nikachaguliwa,” alisema.

Aliendelea kueleza kuwa uteuzi wake kuwa Mkuu wa Mkoa kwa miaka 16 ulikuwa “maajabu mengine”, na zaidi ni uteuzi wake kuwa Balozi licha ya kutokuwa mwanadiplomasia kwa taaluma.
“Walioniteua waliridhika na utendaji wangu, na wananchi waliridhika na utendaji wangu. Huo ndio ulikuwa msingi wa safari yangu ya uongozi.”

Shukrani kwa Mwandishi

Katika risala hiyo, Balozi Njoolay alimpongeza na kumshukuru mwandishi mkongwe wa habari, Bw. Hassan Hassan.
“Amebeba jukumu kubwa katika uandishi wa kitabu hiki. Amefanya kazi kwa uadilifu na umakini mkubwa,” alisema.

Wito kwa Vijana na Wasomaji

Balozi Njoolay alisema lengo lake kuu ni kuwainua na kuwapa dira vijana wa sasa, hasa wale wanaotamani kutumikia taifa.
“Baadhi ya watu walinisukuma kuyaandika haya ili viongozi vijana wapate kujifunza. Ni imani yangu kwamba mtafurahia kukisoma na huenda mkafaidika nacho. Mungu awabariki sana,” alihitimisha.

Uzinduzi huo uliendelea kwa furaha na tafakuri, huku hadhira ikionyesha kuthamini mchango wa Balozi Ole Njoolay—kiongozi ambaye safari yake ni somo la ujasiri, kujituma na uaminifu katika utumishi wa umma.


 


Arusha, Tanzania — Uzinduzi wa kitabu Tawasifu ya Balozi Daniel Ole Njoolay umefanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali, wabunge, wanadiplomasia, wasomi, viongozi wa dini, pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.



Katika hafla hiyo, Salim Salim, kwa niaba ya kamati ya maandalizi, aliwasilisha muhtasari wa yaliyomo ndani ya kitabu hicho na kusisitiza kuwa ni miongoni mwa kazi bora zaidi za kihistoria na kiwasifu kuwahi kuandikwa na mtumishi wa umma nchini Tanzania.



Akiwasilisha muhtasari huo, Salim alisema kwamba mara tu alipokianza kitabu hicho, hakutaka kukiweka chini kwa sababu simulizi za Balozi Njoolay zinamvuta msomaji kutoka ukurasa mmoja hadi mwingine.

“Balozi anafanana na wazee wetu wa zamani ambao walikuwa mabingwa wa kutoa hadithi. Daniel is a master storyteller,” alisema.

Sifa za viongozi wakuu wa Taifa



Katika muhta
sari wake, Salim alinukuu maneno ya viongozi wakuu wa nchi yaliyomo kwenye kitabu hicho, ikiwemo Dibaji iliyoandikwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Joseph Sinde Warioba, ambaye alimwelezea Balozi Njoolay kama kiongozi wa mfano wa kuigwa.

Katika maneno yake yaliyohifadhiwa mwishoni mwa kitabu, Mhe. Warioba anasema:

“Sifa zake ni mfano wa kuigwa. Amefanya kazi ndani ya umma kwa bidii, ubunifu, uadilifu na uaminifu… nimekisoma kitabu hiki kwa msisimko. Kina mengi ya kujifunza, hasa kwa vijana wanaoanza maisha ya utumishi na uongozi.”

Salim pia alinukuu maneno ya Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa (apumzike pema peponi), aliyewahi kumwambia Balozi:

“Mkuu, ninachokupendea huwa unasema ukweli hata kama ule ukweli unaniumiza.”

Zaidi ya tawasifu ya kawaida



Salim alifafanua kuwa kitabu hicho hakisimulii tu historia ya maisha ya Balozi Njoolay, bali kinafundisha maadili, unyenyekevu, uongozi na misingi ya utu wa mtu. Alisema maneno tawasifu au wasifu hayatoshi kueleza uzito wa yaliyomo ndani ya kitabu hicho.

“Kitabu hiki ni ushuhuda hai (a living testimony) wa jinsi Daniel alivyojibu kwa ukarimu wito wa kutumikia na kushirikiana na Muumba. Kina kusukuma kufikiri, kujiangalia, na kutathmini ubora na udhaifu wa maisha yako,” alisisitiza.

Alikilinganisha kitabu hicho na kazi kubwa za viongozi maarufu duniani kama Nelson Mandela (Long Walk to Freedom), Barack Obama (Dreams from My Father), na Mahatma Gandhi (All Men Are Brothers), akisisitiza kuwa kitabu cha Ole Njoolay nacho kina nafasi ya kutafsiriwa kwa Kiingereza siku zijazo.

Hazina kwa Taifa

Mwisho wa hotuba yake, Salim Salim alisema wazi kuwa Balozi Daniel Ole Njoolay ni hazina muhimu kwa Taifa la Tanzania, na kwamba bado kuna haja kubwa ya kuendelea kumtumia katika majukumu ya kitaifa.

Akihitimisha, alinukuu maneno ya Mchungaji Martin Luther King Jr.:

“Swali kuu la kujiuliza maishani ni hili: Unawafanyia nini watu wengine?”

“Mhe. Daniel anaelewa uzito wa swali hili, na amelifanyia kazi kwa kiwango cha juu sana. Lakini haya yote hayatoshi kusimuliwa—ni lazima usome kitabu mwenyewe,” aliongeza.

Uzinduzi huo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari Prof. Palamagamba Kabudi ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria akiwemo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, James Millya, Mbunge wa Arumeru Magharibi, Dr Lukunay,  viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, ( CCM) , viongozi wa umma wastaafu  na watu mashuhuri. 



Waziri wa Maliasili na utalii Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ameelekeza taasisi za uhifadhi kuimarisha matumizi ya teknolojia za kisasa katika uhifadhi na ulinzi wa rasilimali za wanyamapori ili kupunguza migogoro kati ya binadamu na wanyamapori.



Dkt. Kijaji ametoa maelekezo hayo leo tarehe 28 Novemba, 2025 wakati akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro wakati wa ziara ya kujitambulisha kwenye taasisi na kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo.



Katika kikao hicho . Waziri Kijaji ameelekeza kuwa kila taasisi ni lazima iwekeze kwenye teknolojia za kฤฑsasa ili kuimarisha ulinzi wa rasilimali za nchi ambazo ni kichocheo cha wageni mbalimbali kutembelea nchi yetu.



Kwa upande wake naibu waziri wa wizara hiyo Hamad Hassan Chande amewataka watumishi katika sekta ya uhifadhi na utalii kufanya kazi kwa kuzingatia weledi na ubunifu katika kuwahudumia wageni.



Akiwatambulisha viongozi hao kwa menejimenti ya Ngorongoro Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi amewataka watumishi wa mamlaka hiyo kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuharakisha mipango ya serikali inatekelezwa.



Mapema viongozi hao wa wizara walipata fursa ya kukagua ujenzi wa Makao makuu ya mamlaka hiyo, kukagua shughuli za utalii katika lango La Loduare na Makumbusho ya kihistoria ya Urithi ya Jiopaki ya Ngorongoro (Urithi Geo Museum)

 


Arusha — Donkeys in Tanzania are facing a serious threat of extinction due to illegal cross-border trade that involves secretly transporting the animals out of the country, the Animal Welfare Association of Tanzania (ASPA) has warned.



Diana Msemo, Animal Welfare Education Officer at ASPA, issued the alert during a media training held over the weekend in Arusha. She explained that the growing demand for donkey skins has fueled a dangerous black market, causing a sharp decline in donkey populations.

Msemo noted that donkeys are the second most important livestock species in Tanzania—after cattle—due to their significant contribution to the national economy and the daily lives of pastoralist communities.

“There is a high demand for donkeys, especially in neighboring countries like Kenya, where they are secretly slaughtered. Donkeys are smuggled out of Tanzania through unofficial routes and end up in the skin trade,” she said.

Donkeys, commonly used for farming, transportation, and domestic chores, play a crucial role in supporting pastoralist families. Msemo emphasized that donkeys are not only work animals but also essential to children in pastoralist households, enabling them to fulfill daily duties and attend school.



ASPA’s Community Development Officer, Albert Mbwambo, stressed the need for communities to recognize the importance of donkeys and protect them. “Despite the rapid loss of donkeys, we must continue educating the public on the dangers of this illegal trade and ensure these animals are preserved and valued,” Mbwambo said.

ASPA is working with partners such as BROOKE East Africa to advocate for animal welfare and raise public awareness of the consequences of the illegal donkey trade.


 



MKUU wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Profesa Haruna Mapesa amesema katika siku za usoni wanatarajia kuanzisha Shahada za Uzamivu (PhD) katika chuo hicho.



Amesema hayo leo wakati akizungumza kwenye Kusanyiko la Wahitimu Waliosoma katika chuo hicho kwenye Ukumbi wa Utamaduni.



Katika kusanyiko hilo kulikuwa na mada moja, inayosema Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kinavyojipambanua katika  Kuchagiza Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Vijana.



Amesema kwa sasa wanatoa kozi kuanzia Stashahada, Astashada, Shahada ya kwanza na ya Umahiri, hivyo kwa siku za karibuni wataanza kutoa Shahada ya Uzamivu.


"Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kina walimu zaidi ya 100 wenye PhD, hivyo tuna nguvu na ujasiri wa kuanzia shahada hiyo hapa kwetu, wahitaji wajiandae," amesema.



Amesema ubora wa chuo hicho umezidi kuongezeka, ambapo kila mwaka wahitimu wanaongezeka.


Profesa Mapesa amesema mwaka 2020 wanafunzi 3,154 walihitimu, 2021 wahitimu 4,159, 2022 wahitimu 5,691, 2023 wahitimu 5,499 na 2024 wahitimu 

5,255


Mafanikio hayo ni juhudi za watumishi, serikali na wanafunzi, hivyo dhamira yao ni kuendelea kubakia katika hali hiyo.


Amesema wanaendelea kufanya maboresho kuhakikisha MNMA inaendelea kuwa bora zaidi.


"Mipango ya chuo ni kuboresha mifumo ya teknolojia, kununua kompyuta za kisasa, madarasa janja na vingine vingi ambao vinaenda kisasa," amesema.


Mkuu huyo wa chuo amewataka vijana kulinda amani ya nchi na wasidanganyike kwa lolote kwani watashindwa kutimiza ndoto yao.


Amesema chuo hiki kinamuenzi Mwalimu Julius Nyerere kwa vitendo, hivyo natamani kuona wanafunzi wanakengeuka na kwenda kinyume 


Aidha, Profesa Mapesa ametoa vyeti kwa wahitimu waliofanya vizuri zaidi katika kila kozi.


Mkuu wa chuo amesema wamepokea changamoto ikiwemo uratibu wa baraza la chuo ambapo ameahidi kuwepo mratibu.


Amesema mratibu atahakikisha uchaguzi unafanyika kwa haraka, kuweza kuendesha mambo kwa weledi na wakati.


"Haya ambayo nimesema yanaenda kutekelezwa kwa kasi ya 5G kwani dhamira yetu ni kuhakikisha chuo chetu kinafanya vizuri," amesema.


Profesa Mapesa amesema dhamira yake ni kuona kila kusanyiko linakuwa na mkutano mkuu ambao utaweza kujadilia mambo ya chuo kwa kina.


Amesema pia watahakikisha kunakuwepo na mifumo rasmi ambayo itafanyika kikatiba baraza hilo litakuwa limepiga hatua kubwa na kusaidia chuo.


Katibu wa Kusanyiko la Wahitimu, Jumanne Muruga alipokipongeza chuo kuongeza program hadi kufikia 50, huku idadi ya usajili wa wanafunzi ikiongeze siku hadi siku.


"Kwa sasa MNMA inasajili kwa mwaka zaidi ya wanafunzi 12,197, hii ni hatua kubwa sana ni ushahidi kuwa chuo kimekuwa," amesema.


Muruga alipongeza uamuzi wa chuo kushiriki kikamilifu kwenye michezo hali ambayo inatangaza chuo kitaifa na kimataifa.


Kupitia kusanyiko hilo Katibu huyo aliomba chuo kuweka ofisi ya mratibu wa baraza la wahitimu na kufanyika uchaguzi wa viongozi wapya kwani waliopo wamehudumu kwa muda mrefu.


Kwa upande wake Mtoa Mada katika Kusanyiko hilo, Dk Ahmed Sovu amesema MNMA inamejipaga kuwa kitovu cha teknolojia hapa nchini.


Dkt Sovu amesema dhamira ya chuo ni kuona vijana wanaohitimu wanaenda kuleta mabadiliko yao, jamii na nchi kwa ujumla.





Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), leo Novemba 27, 2025 alifanya ziara maalum katika  Makao Makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) jijini Arusha, ambapo alikagua shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hii muhimu. Katika ziara hiyo, Waziri Kijaji alisisitiza kuwa uhifadhi ni msingi wa uhai, uchumi, na fahari ya Taifa letu.



Waziri Kijaji pia aliweka wazi kuwa ni muhimu kwa wananchi kushirikishwa katika ulinzi wa rasilimali za taifa, kwa kuwa wao ndio walinzi wa awali katika kuhakikisha rasilimali zinatunzwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho. Aliendelea kusema:

“Tunahimizana sisi Tanzania kuwa namba moja katika utalii Afrika na duniani, tuna misingi yote ya kuwa namba moja ndani ya Afrika na dunia.”



Katika ziara hiyo, Waziri Kijaji aliielekeza Menejimenti ya TANAPA kuboresha maslahi ya watumishi ili kuongeza chachu ya utoaji wa huduma bora kwa wageni na ulinzi wa rasilimali. 



Alisema lengo la Serikali ni kufikia watalii milioni nane ifikapo mwaka 2030, na kwamba taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, kama TANAPA, zinajukumu kubwa kuhakikisha malengo haya yanafikiwa.



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamad Chande (Mb), alisisitiza kuwa uhifadhi ni heshima ya taifa, na kwamba maafisa na askari wa uhifadhi wana wajibu wa kulinda rasilimali za taifa kwa wivu mkubwa, masaa 24. 


Alisema kuwa ni muhimu kuendelea kuboresha miundombinu ya utalii ili kuhakikisha watalii wanapata huduma bora na kuhamasisha utalii wa ndani na nje ya nchi.



Kamishina wa Uhifadhi TANAPA, Mussa Nassoro Kuji, alieleza kuwa ujio wa Waziri ni chachu ya kuimarisha juhudi za uhifadhi na kwamba TANAPA itaendelea kutumia teknolojia na mbinu za kisasa kulinda bioanuai na kuboresha mifumo ya ulinzi wa wanyamapori.


Ziara hiyo ilijumuisha pia hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, ambapo viongozi walipata wasaa wa kujionea vivutio vilivyopo na shughuli za utalii zinazofanywa katika hifadhi hiyo.




 

 By Woinde Shizza , Arusha 

The digital transport service Bolt has drawn major attention in Arusha after being credited for expanding job opportunities for both young people and I'mwomen, becoming a strong part of the fast-growing digital economy in Tanzania



This was highlighted during a gathering of more than 100 public relations officers from different African institutions, held at the East African Community Conference Hall in Arusha, where discussions focused on how digital platforms are reshaping employment across the continent



Presenting on behalf of Bolt Tanzania, the company’s Public Relations manager said Bolt has significantly increased  financial opportunities  for Tanzanians, especially young people who rely on motorcycles and cars to earn daily income

According to the officer, the platform has also seen a notable rise in the number of women joining as drivers, a positive shift in a sector that was once dominated by men



He noted that this trend has helped reduce unemployment and created a reliable source of income through technology, adding that Bolt is continuing to improve its systems to ensure both drivers and customers receive safe and efficient services

Communication experts at the meeting said companies like Bolt represent a new direction in Africa’s job market—one that should be supported by governments, youth groups and financial institutions to boost income and strengthen local economies

Some Bolt drivers in Arusha said the platform has helped them earn more stable daily income compared to the past, when they had limited access to customers

They urged the government to continue creating a friendly environment for digital companies in order to open more opportunities for young people and women across the country

 




Arusha, Tanzania“Since its establishment, the African Institute of International Law has become an important pillar of legal scholarship on our continent. 




Through its seminars, training programs and research initiatives, it continues to advance critical conversations, including the promotion and protection of women’s rights,” said Dr. Ines Kajiru, as she delivered a statement on behalf of the Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation during the official opening of the regional seminar in Arusha.



Representing the Director of Legal Affairs, Dr. Gift Kweka, Dr. Kajiru emphasized that Tanzania fully supports the mission and work of the African Institute of International Law (AIIL), noting that the Institute has significantly contributed to strengthening legal capacity and promoting dialogue on issues that shape African governance and human rights.

She extended warm greetings to participants who traveled from across Africa and beyond, commending AIIL for convening a high-level forum bringing together judges, prosecutors, scholars, policymakers, civil society leaders, and experts committed to advancing justice for women and girls.

Dr. Kajiru underscored that Tanzania remains deeply committed to promoting women’s rights in line with its Constitution and international and regional obligations, including the Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women (CEDAW) and the Maputo Protocol.

“We recognize that the empowerment of women and access to justice are essential to building a just, equitable and prosperous society,” she said, noting that the Government continues to strengthen laws, institutions, and public policies to combat gender-based violence and expand opportunities for women in all sectors.

She encouraged the African Institute of International Law to continue using its expertise to support the African Union’s vision of a continent rooted in good governance, human rights, and the rule of law, adding that gatherings such as this one enrich Tanzania’s role as a regional center for legal thought and cooperation.

Addressing the delegates, Dr. Kajiru urged participants—judges, lawyers, prosecutors, academics, and human rights defenders—to engage actively, share experiences, and challenge one another to propose practical solutions that can transform access to justice for women across Africa.

“To those representing their governments, I urge you to be influential voices when you return home, ensuring that recommendations from this seminar inform national policies, institutional practices, and legislative reforms,” she stated.

She reaffirmed Tanzania’s readiness to consider the recommendations that will emerge from the seminar, expressing confidence that the outcomes will strengthen both national and continental frameworks for the protection of women’s rights.

The seminar, themed “Strengthening Legal Frameworks and Access to Justice for Women in Africa,” brings together key actors in justice systems across the continent for a week of dialogue, training, and collaboration.

Concluding her address, Dr. Kajiru wished participants fruitful deliberations and an enriching stay in Tanzania.

“May this seminar mark a strong step toward justice, equality, and dignity for women in Africa,” she said.



Arusha, Tanzania – Ambassador Irene Kasyanju has warned that despite growing female representation across courts, parliaments, and governance institutions in Africa, the gap between legal frameworks and actual practice continues to deny many women the justice they deserve.


Too often, laws exist in books but not in practice, leaving women without the remedies and respect they deserve,” she stressed as she officially opened the seminar on Strengthening Legal Frameworks and Access to Justice for Women in Africa in Arusha.



Amb. Kasyanju, who serves on the Administrative Committee of the African Institute of International Law (AIIL), told participants that Africa has made commendable progress—through instruments such as CEDAW, the Maputo Protocol and Agenda 2063—but systemic challenges still impede women's full enjoyment of rights.

Reflecting on her long career, she traced her engagement with Arusha-based legal institutions to her decade-long service as Director of Legal Affairs in the Ministry of Foreign Affairs from 2005 to 2015.



When these institutions were being established, I found myself coming frequently to Arusha to support their setup—finding offices, residences for senior officials, and coordinating their legal and diplomatic needs,” she recalled. “I am humbled that my contribution was well received.

She emphasized the crucial role of AIIL in shaping an equitable legal culture on the continent.
Institutions such as the African Institute of International Law are indispensable. By convening this seminar, the Institute demonstrates its commitment to ensuring women's rights become a reality—not rhetoric—and that access to justice is a right, not a privilege.

Amb. Kasyanju further acknowledged the support of development partners, including the Swiss Federal Department of Foreign Affairs, whose contributions continue to strengthen human rights education.

Expressing appreciation to judges, lawyers, prosecutors, scholars, and civil society leaders participating in the workshop, she urged them to use the forum to develop impactful recommendations.

Together, we can build legal systems that ensure no woman is left behind. Justice requires strong institutions, gender-sensitive officials, adequate resources, and the removal of cultural and social barriers that silence women’s voices.

She concluded by formally declaring the seminar open, saying:
I now have the honor to declare the seminar on strengthening legal frameworks and access to justice for women in Africa officially open. May this week of dialogue be fruitful, inspiring, and transformative.

The seminar is taking place in Arusha, home to the African Court on Human and Peoples' Rights and the African Institute of International Law.