Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza ongezeko la majimbo ya uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ambapo majimbo nane mapya yameongezwa, yakiwemo Jimbo la Ilongero na mengine kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara.
Majimbo mapya yaliyotangazwa ni pamoja na Jimbo la Manyoni Magharibi kugawanywa na kuzaa Jimbo la Itigi, Jimbo la Singida Mashariki kuwa Jimbo la Ikungi Mashariki, Jimbo la Singida Magharibi kuwa Jimbo la Ikungi Magharibi, Jimbo la Tabora Kaskazini kuwa Jimbo la Uyui, na Jimbo la Handeni Vijijini kuwa Jimbo la Handeni.
Uamuzi huu unalenga kuhakikisha uwakilishi wa wananchi unaboreshwa kutokana na ongezeko la watu na mahitaji ya uwakilishi wa karibu zaidi kutoka kwa wabunge na madiwani.


0 Comments:
Post a Comment