Familia moja ya baba na mtoto imehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kusafirisha bangi kinyume cha sheria, kutoka wilayani Nzega mkoani Tabora kwenda mkoani Shinyanga. Tukio hilo limetajwa kuwa ni sehemu ya biashara haramu ya dawa za kulevya inayozidi kushamiri katika baadhi ya maeneo nchini.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Nzega, chini ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Saturini Mushi, iliwatia hatiani jana washBaba na Mtoto Wahukumiwa Kifungo cha Maisha kwa Kusafirisha Bangiitakiwa hao kwa kosa la uhujumu uchumi baada ya kupatikana na ushahidi wa kutosha wa kuhusika na usafirishaji wa bangi.
"Hii iwe fundisho kwa wote wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya. Sheria ipo wazi, na haitavumilia uhalifu huu," alisema Hakimu Mushi wakati akisoma hukumu.
Aliwataja waliohukumiwa kuwa ni Ally Thabit (45) na mtoto wake Jonas Ally Thabit (23), wote wakazi wa Nzega. Alisema kuwa ni muhimu hukumu hii iwe mwanzo wa kukomesha vitendo vya kilimo na usambazaji wa bangi kinyume na sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika ushahidi uliowasilishwa mahakamani, Mwendesha Mashtaka Meshaki Lyabonge kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya alieleza kuwa tukio hilo lilitokea mnamo Machi 13, 2024, katika Msitu wa Mabatini, Kijiji cha Kigandu, Kata ya Mogwa, ambapo watuhumiwa walikamatwa na magunia ya bangi wakiwa wanayapeleka mkoani Shinyanga kwa kutumia pikipiki.
"Naomba mahakama itoe adhabu kali iwe fundisho kwa wengine wanaojihusisha na biashara hii haramu," alisema Lyabonge, akiwasilisha kesi namba 7152 ya mwaka 2024.
Watuhumiwa hao waliiomba Mahakama iwapunguzie adhabu kwa madai kuwa ni kosa lao la kwanza na kuahidi kutorudia tena, lakini Hakimu Mushi alikataa ombi hilo na kutoa hukumu ya kifungo cha maisha jela.
"Sheria inatakiwa ifuatwe. Uhalifu huu hauwezi kuvumiliwa. Mnayo haki ya kukata rufaa kama hamkuridhika na hukumu hii," alihitimisha.

0 Comments:
Post a Comment