Mahakama Yawaachia Huru Mke wa bilionea Msuya na mwenzake.

 Mahakama Yawaachia Huru Mke wa bilionea Msuya na mwenzake.

Ndugu wa marehemu alia kwa uchungu 






Leo, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa uamuzi wa kesi iliyokuwa inamkabili Miriam Steven Mrita, mjane wa aliyekuwa mfanyabiashara mashuhuri wa madini mkoani Arusha, bilionea Erasto Msuya, pamoja na mshitakiwa mwenzake, Revocatus Everist Muyella, maarufu kama Ray, ambao walikuwa wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kukusudia.


Katika hukumu iliyotolewa leo, Mahakama imefikia uamuzi wa kuwaachilia huru washitakiwa hao baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao. 



Miriam na Ray walidaiwa kuhusika katika mauaji ya kikatili ya Aneth Elisaria Msuya, wifi wa Miriam, ambayo yalidaiwa kutokea Mei 26, 2016, huko nyumbani kwa Aneth Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam.


Kesi hiyo, ambayo ilianza mwaka 2018, imekuwa ikiendelea kwa miaka kadhaa huku washitakiwa wakiwa mahabusu. Hata hivyo, leo wamepata afueni baada ya Mahakama kuwakuta hawana hatia.


Uamuzi huu wa Mahakama umekuja baada ya kipindi kirefu cha kusikilizwa kwa ushahidi na hoja kutoka pande zote mbili. Familia za washitakiwa na jamii kwa ujumla zimepokea habari hii kwa furaha na utulivu.


Hukumu hii imepokelewa kwaa hisia tofauti ambapo wakati ndugu wa wshitakiwa hao wakifurahi na kuimba nhimbo za kumsifu !ungu ndugu wa marehemu Aneth walionekana wakilia kwa jchunhi.



Antuja Msuya ambaye ni Dada wa Marehemu Bilionea Erasto Msuya ameangua kilio  Mahakamani hapo jioni ya leo na kupaza sauti “ushahidi wote unaonekana Mtu anaambiwa hana hatia, niueni... niueni, niueni, bora nife” 


“Hakuna haki iliyotendeka maana ushahidi wote unaonekana na ushahidi upo na jinsi ilivyofanyika mwanzo hadi mwisho ila wameamua maamuzi yao Mahakama haijatenda haki, kuanzia Arusha wanapaka nyumba rangi, upare wanapaki nyumba rangi wanasema anatoka kwa gharama yoyote leo ametoka, Mungu ataamua,”  Antuja ameyasema hayo wwkati akisaidiwa na ndugu yake pamoja na polisi kutoka nje ya chumba cha mahakama.

 

Hata hivyo wakati Miriam wakitoka Mahakamani hapo, Ndugu na Jamaa waliofurahishwa na kuachiwa huru kwa wawili hao walisikika wakitamka baadhi ya maneno ya kumshukuru Mungu mbele ya Antuja “Yesu ni bwana, amefanya” 

https://habaritanzaniagracemacha.blogspot.com/2024/02/hukumu-ya-kesi-ya-mke-wa-bilione-msuya.html



0 Comments:

Post a Comment