MAJALIWA ; VIONGOZI WA DINI TUSHIRIKIANE MAPAMBANO BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA

 


28 Septemba 2023, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasisitiza viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali katika mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya. Ametoa wito huu akimwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Baraza la Maulid lililofanyika kitaifa jijini Dodoma.



Ameeleza kuwa matumizi ya dawa za kulevya yana athari kubwa kwa taifa, hasa kwa vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa. Athari hizi ni pamoja na madhara ya kiuchumi, kiafya, na kimazingira, na pia zinaweza kuathiri uwezo wa mtu kufikiri.



Waziri Mkuu pia ametoa mwito kwa viongozi wa dini kuendelea kukemea mmomonyoko wa maadili katika jamii na kuhamasisha waumini kushiriki katika shughuli za kuongeza kipato. Amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani nchini, kwani amani ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa.


Kuhusu masuala ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka, Waziri Mkuu ameuhakikishia umma kuwa Serikali itachukua hatua kali dhidi ya wale watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo haramu.


Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Alhaj Nuhu Jabir Mruma, aliyekuwa miongoni mwa wasemaji, aliipongeza Serikali kwa juhudi zake za kuwaletea wananchi maendeleo katika sekta mbalimbali. Pia, aliiomba Serikali kuongeza wigo wa kutoa elimu ya uraia kwa kushirikiana na viongozi wa dini, ikiwa ni pamoja na kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024

0 Comments:

Post a Comment