DEREVA TOYO AFUNGWA MIAKA 30 KWA KUBAKA MTOTO


DEREVA toyo, Maico Silvesta, (28) amehukumiwa kwenda jela miaka 30 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la  kumbaka mtoto wa wa kike wa miaka 10 ambaye ni mwanafunzi wa darasa la nne shule ya msingi Olomitu.


Mkazi huyo wa Maloloyi, Moshono,  Arusha amekutwa na hatia ya kumbaka mtoto huyo ambaye alimpatia pipi kisha akamwingiza kwenye chumba cha bibi yake na kumbaka huku akitishia kumuua endapo ataendelea kupiga kelele. 


Uamuzi huo umetolewa leo, Septemba 26,2023 na Hakimu, Itikija Nguvava wa Mahakama ya wilaya Arumeru aliyekuwa akisikiliza shauri hio la jinai namba 37/2023.

Akisoma uamuzo huo Hakimu Nguvava amesema kuwa amefikia uamuzi huo  baada ya kusikiliza hoja za pande zote ambapo upande wa jamhuri walileta mashahidi wanne huku mshitakiwa Maico akijitetea mwenyewe.

Awali, mahakama hiyo ilielezwa kuwa mnamo mwezi January mwaka huu mhanga akiwa anaishi na bibi yake , mjomba yake alikuja na rafki yake  (mshtakiwa Maico) nyumbani.

" Alimpa pipi (mhanga/mtoto) na kuondoka na baada ya kuondoka kesho yake (Maico) alirudi peke yake ambapo alimpeleka mhanga chumbani kwa bibi yake na akamvua nguo za ndani na kumbaka, mhanga alipiga kelele ila mshtakiwa alimziba mdomo na akamtishia akisema atamuua,".


Siku inayofuata ndipo ilipogundulika kufanyika kwa tukio hilo kwani mtoto huyo alikuwa hatembei vizuri ambapo alipohojiwa alisema kuwa amebakwa na mshitakiwa Maico.

Maico alikamatwa Februari 20,2023 ambapo alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Juni 15,2023.

0 Comments:

Post a Comment