WAZIRI AIPONGEZA TANFOAM KUZALISHA BIDHAA BORA, ATOA MAGIZO MAZITO KWA JIJI LA ARUSHA


  

WAZIRI wa viwanda na biashara, Dkt. Ashatu Kijaji amekipongeza  kiwanda cha mgodoro cha TANFOAM kwa kutengeneza  bidhaa bora na nzuri zinazokidhi viwango hivyo kupendwa ndani na nje ya nchi.

 

Aidha amekipongeza kwa kuweza kuuza   bidhaa zake kwenye nchi za Afrika Mashariki huku akiwataka kuendelea na juhudi hizohizo ili kuweza kuuza bidhaa zao kwenye nchi zote barani Afrika.

Dkt. Kijaji amesema hayo leo Agosti  1, 2023 wakati alipotembelea hicho  kilichopo Jijini Arusha kujionea shughuli za uzalishaji magodoro na kisikiliza changamoto zinazowakabili .

 

Amesema kuwa Serikali inahakikisha inaweka mazingira bora kwa wafanyabiashara na wawekezaji  pamoja na kutatua changamoto walizonazo ili waweze kufanya shughuli zao kwa ufanisi.

“Natamani kuona bidhaa hizi zinafika soko huru la biashara Afrika nchi zote 54 zilizobaki ukiacha Tanzania kwani bidhaa inayozalishwa inakidhi viwango vya kimataifa  na hata kutoka nje ya Bara la Afrika kwani uwekezaji ni mkubwa na teknolojia ni kubwa kutoka kiwanda Cha Tanform Arusha,” amesema Waziri Kijaji.

 

Dkt KIjaji amesema kuwa wizara yake inatekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji ambapo moja msingi yake ni kuondoa majukumu yanayofanana kati ya Taasisi ili kurahisisha ufanyaji biashara  na uwekezaji nchini

Akiongea na uongozi wa kiwanda hicho, Dkt. Kijaji amezitaka Shirika la viwango nchini, (TBS), Mamlaka ya Mapato nchini, (TRA) na Wakala  wa Vipimo Nchini, (WMA)   kuacha kufanya majukumu yanayofanana na kuzitaka kushirikiana katika kuwahudumia wafanyabiashara na wawekezaji  ili kukuza biashara na uchumi wa Taifa

Amesema wizara itaenda kukaa na taasis hizo ili kuelewa kazi zinazofanyika na mwisho wa siku wawe na sera inayohitajika sokoni ili kuendelea kurahisisha mazingira ya ufanyaji biashara wa wafanyabiashara.

 

Aidha, Waziri Kijaji alimuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Arusha pamoja na uongozi wa mkoa kubadili utaratibu wa kuyalazimisha magari yanayobeba bidhaa kutoka viwandani kwa ajili ya kuzipeleka kwenye maduka kupitia kwenye mizani.

 

“Changamoto ya magari yanayobeba bidhaa kutoka kiwandani kwa ajili ya  na kupelekea dukani kutakiwa kwenda kwenye mizani ndipo wayapeleke  dukani hiyo siyo sahihi hivyo namuagiza mkurugenzi wa jiji na mkuu wa mkoa na timu yake kubadili utaratibu… changamoto isionekane ni safari ndefu hata kama wanataka kukusanya mapato,” ameagiza Waziri Kijaji.

 

Waziri Kijaji amesema kuwa wao kama wizara wanasimamia sera wataenda kuchunguza kama ni chanzo cha mapato ama ni kweli wanataka kulinda barabara kwani huwezi kutoa gari nje ya mji na kuirudisha haipendezi.

 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa TANFOAM, Meshack Jimmy ameishukuru Serikali kwa jitahada mbalimbali inazozifanya katika kutatua changamoto za wafanyabiashara na wawekezaji ili kuwawekea mazingira bora ya ufanyaji biashara na uwekezaji.

0 Comments:

Post a Comment