Aidha imewahakikishia
kuwa nao bega kwa bega kuhakikisha kiwanda hicho kinakamilika kwa wakati huku
ikiwataka Seed.Co kuwapa taarifa endapo watapata changamoto au vikwazo vyovyote
vilivyo ndani ya uwezo wa serikali waweze kuwaondolea.
Pongezi hizo
zimetolewa Agosti 18,2023 na mkuu wa mkoa wa Arusha, John Mongela wakati
akizindua ujenzi huo kwa kuchimba msingi na kupanda mti kwenye eneo la ujenzi
lililopo kata ya Kisongo wilayani Arumeru mkoani Arusha kunapojengwa kiwanda
hicho.
Awali, Mkurugenzi Mkuu
wa Seed.Co, Morgan Nzwere alisema kuwa kwa kipindi kirefu wamekuwa Tanzania
wakiendesha shughuli zao kwenye maeneo ya kukodi lakini kwa
sasa mahitaji ya mbegu yamekuwa makubwa zaidi hivyo wameamua kuwekeza kwenye
ujenzi wa kiwanda hicho cha kuchakata mbegu na ghala la kuzihifadhia ili
kuongeza ufanisi mara mbili zaidi .
"Uwepo wa kiwanda hiki utaongeza ajira si tu za kiwandani bali pia kwa wakulima wetu ambapo mbali ya kuzalisha mazao kwa ajili ya kuuzia walaji lakini sasa watazalisha mazao kwa ajili ya mbegu watakazoziuzia kiwanda cha Seed.Co," alisema Dk Shuma na kuongeza.
0 Comments:
Post a Comment