MZEE
, Iddy Nzella Maganga, (89) ameamua kuzivunja nyumba zake mbili
zenye thamani ya zaidi ya shilingi 200 milioni kwa madai kuwa baadhi ya watoto
wake wana nia ovu juu ya nyumba hizo kwani wamekuwa wakimtesa kwa lengo la
kumdhulumu mali hizo.
Amesema uamuzi huo ameuchukua akiwa na
akili timamu na amefanya ili kuwakomesha watoto wasiotaka kufanyakazi
wakisubiri mali za urithi .
Akiongea
na waandishi wa habari JUali 12, 2022 nje ya nyumba hizo zilizopo maeneo ya
Ngarenaro NHC jijini Arusha mzee huyo alisema kuwa watoto wake hao
wa kiume wamekuwa wakimtesa ikiwemo kumfungia kwenye chumba cha giza kwa
wiki moja bila kumpa chakula hali iliyomazimu kula kunyesi.
Maganga ambaye alifiwa na mke wake wa ndoa ,
amesema kuwa alifikia uamuzi wa kuzivunja nyumba hizo baada ya kubaini
baadhi ya watoto wake wakiongozwa na Abdalah Maganga wanania ovu
juu ya mali zake na huenda akafa siku sio nyingi .
"Hii nyumba ni mali yangu nilijenga na
mke wangu ambaye kwa sasa ni marehemu, huyu mtoto Abdalah alinifungia ndani
wiki moja nikiwa nakula kinyesi changu sijitambuli na nilikuja kuokolewa na
mtoto wangu wa kike, anaiwa Jasmin na mume wake baada ya kuvunja kitasa
na kunitoa na kunipeleka hospitali, " alisema Mzee Maganga na kuongeza.
…Jirani yangu anaitwa mama Masawe ambaye
nilikuwa nikienda kuchukua chakula kwake alimpigia simu mtoto wangu Jasmin na
kumwambia kuwà mbona mzee Abdalah haonekani siku ya nne akija kuchukua
chakula ,ndipo Jasmin na mumewe walipokuja na kukuta Abdalah amenifungia ndani,
".
AELEZA UKATILI ZAIDI ALIOFANYIWA
Mzee Maganga ambaye ana watoto sita,
kwa sasa anaishi kwa mtoto wake, Jasmin maeneo ya Kwa Morombo ambapo amefafanua
kuwa mtoto wake, Abdallah alikuwa na nia mbaya juu yake, kutaka afariki dunia
ili ajimilikishe nyumba hiyo kinyume cha sheria.
Alisema licha ya kuwa hiyo nyumba hizo ni
mali yake lakini Abdallah alikuwa hamruhusu kuingia ndani ya nyumba
hizo hata pale anapokuwa akitafuta msaada kwa kijana huyo, alikuwa akifunga
milango na geti la kuingilia ndani.
Hivyo Mzee Maganga aliwataka watoto wake,
Abdallah na Riziki kukaa mbali na mali zake, watafute mali zao kwani
baada ya kufanikiwa kubomoa nyumba hiyo anampango wa kuliuza eneo hilo muda
wowote kuanzia sasa.
"Baada ya kupata fahamu nilianza
taratibu za kuuza nyumba yangu lakini kila nikifika na mteja nafungiwa
nje na mwanangu Abdallah hataki niingie ndani hata
kujisaidia,"alisema Mzee Maganga kwa uchungu.
Naye mtoto wa mzee huyo, Jasmin
alisema kuwa alimwokoa baba yake akiwa kwenye hali mbaya baada ya kumkuta
hajitambui na amefungiwa kwenye chumba kidogo kwa wiki moja bila kupatiwa
chakula wala maji.
"Nilimkuta baba yangu akiwa kwenye hali
mbaya sana alikuwa haongei, chumba kilikuwa na giza kimefungwa na kinanuka
kinyesi na alikuwa akila kinyesi chake, nilimpeleka hospitali na baada ya
kupatiwa matibabu alipata nafuu na kurejea katika hali ya kawaida na sasa
naishi naye,"alisema Jasmin.
MTOTO WAKE ASEMA ANAMWACHIA MUNGU
Kwa upande wake, Abdallah
alikanusha madai yaliyotolewa na baba yake ya kumfungia kwenye chumba kwa
wiki nzima bila chakula huku akidai kuwa yeye anaishi kwenye nyumba hiyo kama
mwangalizi mara baada ya mama yake kufariki huku akidai mahusiano na baba yake
yalianza kudorora tokea alipoenda kuishi kwa mdogo wake, Jasmini.
Alisema kuwa alishtushwa sana kuona kundi la
watu zaidi ya 50 wakivamia nyumba hiyo siku ya jumamosi wiki iliyopita na
kufanya uharibifu.
Abdallah alisema kuwa alijitahidi kutafuta
msaada polisi lakini hakuupata kwa wakati kwani polisi walifika kwa kuchelewa
na kukuta tayari nyumba zote zimevunja na vitu kutolewa nje.
"Mimi sina ugomvi na baba yangu ila sina
mawasiliano naye kwa muda baada ya kuchukuliwa na kuishi na mdogo wangu Jasmin,
nitakachofanya kwa sasa ni kumwachia Mungu tu,"alisema Abdalah.
Mdogo wake Mzee Maganga, Hassan
Abdalah, alisema hana mawasiliano na kaka yake ingawa alishauri
kuwa kitendo kilichotokea kinapaswa kumalizika kisheria mahakamani.
Tukio hilo limekuwa gunzo kwenye maeneo mbalimbali
ya jiji la Arusha huku wengi wakionekana kuunga mkono hatua aliyochukua mzee
Maganga kwa kile wanachoeleza kuwa kwa sasa vijana wengi hawataki kufanya kazi
wamekaa wakivizia ni lini wazazi wao watakufa ili warithi mali.
Mkazi wa Terati, Thomas Laizer alisema kuwa
afadhali wazee sasa wakaamka pale wanapoona vijana wanawaombea wafe ili warithi
basi wauze mali zao na wazitumie taratibu mpaka hapo Mungu atakapowachukua.
Hata hivyo wananchi wengine walipinga kwa
kile walichodai kuwa mwanadamu anapoishi inapendeza anapoondoka basi aache kwa
familia kitu ambacho kitakuwa ukumbusho wa maisha yake hivyo mzee huyo angeweza
kuchukua hatua nyingine kuwaadhibu vijana wake lakini si kuvunja nyumba.
0 Comments:
Post a Comment