SABAYA; SIKUJUA NIJITETEE SIKUWA WAPI

  

ALIYEKUWA Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amesema alishindwa kuwasilisha mahakamani taarifa ya kutokuwa eneo la tukio kwani hakujua ajitetee hakuwa eneo lipi kati ya yaliyotajwa mahakamano.

 

Ameyasema hayo leo Februari 7, 2022 mbele ya hakimu Mkazi Mwandamizi, Patricia Kisinda anayesikiliza shauri hilo la uhujumu uchumi namna 27/2021 kwenye mahakama ya hakimu mkazi Arusha wakati akiongozwa kutoa ushahidi  (re examination) na wakili wake, Moses Mahuna.

 

 Sabaya amesema kuwa wakati akihojiwa maswali ya dodoso na mawakili wa serikali alionyeshwa hati ya mashitaka kisha akaulizwa ni kwa nini hakutoa taarifa kuwa atajitetea kuwa hakuwa eneo la tukio na akajibu hakujua ajitetee hakuwa kwenye tukio eneo gani .

 

 

"Wakati anauliza swali alinionyesha hati na kwa mujibu wa hati nilishindwa kutoa taarifa kwa sababu sikujua najitetea sipo wapi na wakati ushahidi unaendelea uliletwa maeneo mengi ambayo hayapo kwenye hati ya mashitaka hadi maeneo ya Dar es Salaam yalitajwa tukashindwa kuelewa tunajitetea hatukuwa wapi," ameeleza Sabaya.

 

Katika hatua nyingine shauri hilo limeahirishwa mpaka Februari 16, mwaka huu kwani mawakili wa utetezi wana mashauri mengine kwenye mahakama ya rufani ikiwemo shauri lingine la  Sabaya linalotarajiwa kusikilizwa Februari 24,mwaka huu hivyo  wanaomba muda kwa ajili ya maandalizi.

 

 

Wakili Mahuna aliwasilisha ombi la kuahirishwa kwa shauti hilo mara baada ya Sabaya kumaliza kutoa ushahidi wake ambapo alisema wanaweza kuleta shahidi mwingine mmoja lakini kwa muda uliobaki wanaona hatamaliza kutoa ushahidi wake.

 

"Sababu ya kuleta ombi hili baadhi ya mawakili tuna kesi kwenye mahakaman ya rufaaa kesho tarehe  8,15 na licha ya kesi hizi tuna kesi nyingine ya rufaa inayomhusisha mshitakiwa wa kwanza (Sabaya) na  wa tano Silvester Nyengu ambao wapo katika kesi hii," alieleza Mahuna na kuongeza.

 

...Na mawakili ni hawa hawa na kulingana na 'nature' ya kesi inahitaji maandalizi ya kina na kutokana na kesi zingine na kesi hiyo ya jumatatu tulikuwa na ombi kwamba mahakama yako ionelee vema kuahiriaha shauri hili kwa leo hadi tarehe 16 Februari ili tuendelee na mashahidi wengine waliobaki,".

 

 

Kwa upande wa Jamhuri wakili wa serikali Mwandamizi, Janet Sekule alisema hawana pingamizi na ombi hilo la upande wa utetezi huku akionyedha mashaka yake kuwa hawajaleta hati za wito wa mahakama kuthinitisha kuwa kweli wana kesi kwenye mahakama ya rufani kama wanavyodai.

 

 

"Hatuna pingamizi na ombi la utetezi ingawaje hawajaleta hati za wito kuthibitisha kama wana kesi kama wanavyodai tuko tayari kuendelea kwa tarehe waliyoomba kwani sheria iko wazi kuwa panapokuwa na mashauri kwenye mahakama za juu mahakama za chini zinasubiri," alieleza Wakili Sekule

 

Hakimu Kisinda alisema kuwa amekubaliana na ombi la kuahirisha shauri hilo mpaka februari 16, mwaka huu.

 

 

 

 

Wakili wa utetezi Moses Mahuna akimuongoza  Sabaya kuboresha ushahidi wake (re examination) 

 

Wakili:Bwana Lengai wakati unahojiwa na mawakili wasomi wa jamhuri uliulizwa swali ukajibu hukuona CCTV  footage ikichezwa hapa mahakamani ulikuwa na maana gani?

Shahidi:Sikuona footage hiyo ikichezwa mahakamani na ni kweli sikuona sababu alikuja shahidi  wa saba ambaye ni mtaalam wa CRDB akaieleza mahakama kile alichokitoa kwa shahidi namba nane siyo kile alichokikuta mahakamani maana yake kilikuwa kimebadilishwa, kimeongezwa alisema hivyo.Alikuja shahidi wa tisa meneja wa benki Mary Kimasa akasema tarehe 1.6.2021 aliangalia hiyo CCTV kule benki kwa Mrombo na hakumuona mtu yoyote aliyepo hapa mahakamani katika footage hiyo

 

Wakili:Uliulizwa swali ukajibu video iliyopo hapa sicho kilichotokea kwa Mrombo ulikuwa na maana gani kujibu hivyo?

Shahidi:Nilikuwa na maana kwamba ile video halisi niliyoona na shahidi wa saba na tisa siyo halisi iliyoletwa mahakamani hasa baada ya kuingizwa kwenye mfumo mwingine na kubadilishwa uhalisia wake. Na shahidi namba saba alikiri kuna vitu vimeongezwa siyo halisi.

 

Wakili:Wakati unadodoswa na wakili Kwetukia ulijibu unaonekana simu ipo TANAPA, White Rose, Haile Selassie ulipokuwa ukijibu ipo katika hayo maeneo ulikuwa ukimanaisha nini

Shahidi:Kielelezo cha tatu nilikuwa nasisitiza ni mawasiliano ya simu ilipo na siyo mtu kama ilivyoelezwa na mtaalamu shahidi wa sita wa jamhuri

 

 

Wakili:Ulilizwa swali kwa kutumia kielelezo cha tatu ukaonyeshwa  mida mingi anakwambia mawasiliano yalifanyika Mbauda ukasema ni kweli kulingana na kielelezo ulikua na maana gani kusema ni kweli?

Shahidi:mimi nilikuwa nasoma kielelezo P3 ambacho kwanza ni kielelezo kinachotaka maelezo ya kitaalamu,nilieleza mahakama hii simu hiyo 0758 707171 alikuwa anatumia mke wangu Jesca Thomas ambaye alikuja hapa kama shahidi

Maswali simu ilikuwa Mbauda alipaswa kuulizwa yeye aliyekuwa anatumia simu siku hiyo, hawakumuuliza chochote maana walikubalaiana naye. Kuniuliza mimi walikuwa wananionea maana shahidi alikuwepo hapa

 

 

Wakili:uliulizwa swali ukajibu kwa muda huo uliotajwa simu haikutoka Arusha ulikuwa ukimaanisha nini?

Shahidi:Mhe Hakimu nilijuwa najibu kwa mujibu wa kielelezo mimi sikuwa na simu hiyo kujua ilikuwa wapi na inafanya nini mimi nilipewa tu nisome na nilisema aliyetoka Arusha kuja Boma (ng’ombe) ni mke wangu siyo simu na mimi nilimfungulia mlango usiku mke wangu

 

Wakili:Uliulizwa swali ukajibu hujui kwani shahidi namba mbili wa utetezi alitumia dakika 25 kupita Mbauda akielekea Kisongo

Shahidi:Hizo dakika 25 zipo kwenye kielelezo ambacho ni ripoti ya kitaalamu ambayo ripoti hiyo kwa mujibu wa mtaalum alisema inaeza kusoma umbali wa kilomita tano.

Shahidi wa pili (wa utetezi Jesca) angeulizwa angeweza kueleza yeye na siyo mimi

 

Wakili:Hapa mahakamani ulionyeshwa kielelezo P3 ukasema kwenye hicho kielelezo kuna incoming sms toka kwa namba ya Enock Mneki kwenye namba ya mtu anaitwa Lengai Sabaya ulikuwa unamaanisha nini

 

Shahidi:Kwa mujibu wa kielelezo P3 mawasiliano yalikuwa yanafanyika Kati ya hizo namba mbili ambapo nilisoma kwenye kielelezo na maana yangu ni kwamba waliopaswa kukielezea ni wale waliokuwa wanatumia simu na siyo mimi

 

 

Wakili:Uliulizwa swali akauliza kuna kipindi namba zilizosajiliwa kwa majina ya  Enock na Lengai ole Sabaya inaonekaa inasoma mnara mmoja sasa Sombetini two simu hizo zilisoma mnara wa Sombetini two  na ulipoulizwa inaonekana kuna 8 transaction ikiwemo sms incoming calls ulijibu ndio, ulikuwa ukimaanisha nini?

Shahidi:Aliniuliza swali akisoma kielelezo nilikua namaanisha ndo kiliandikwa kwenye kielelezo hicho

 

Wakili:Kuna swali ulijibu shahidi mmoja hawezi kuthibisha kesi ulikuwa na maana gani?

Shahidi:Nilikuwa na maana ya kwamba ni kwa mujibu wa sheria ushahidi wa shahidi mmoja lazima uchukuliwe kwa tahadhari sana kwamba katika mazingira ya mkanganyiko wa ushahidi wake mwenyewe hapaswi kuaminiwa na kuthibitisha shtaka la jinai kama hili atahitaji shahidi mwingine wa kumuunga mkono

 

Wakili:Uliulizwa hapa habari ya DAS kwamba ulikuwa naye siku nzima kwanini hukumleta kama shahidi ukajibu RAS alishawakilishwa na shahidi namba moja wa jamhuri na ushahidi wake umethibitisha hukutoka ofisini tarehe 22.1.2021 na ulikua unamaanisha nini?

Shahidi:Nilikuwa namaansiha shahidi namba moja wa Jamhuri ameieleza mahakama kwamba hana taarifa yoyote toka kwa DAS kwamba mimi ela gari wala dereva havikutima hai 22.1.2021 na akasema nilikuwepo ofisini siku hiyo na ningetoka lazima angefahamu na yule shahidi ni mkuu wake DAS sikua na uhitaji wa kumleta DAS kwani alishaeleza shahidi huyo

 

 

Wakili:Uliulizwa swali pia ukajibu hukutoa taarifa mahakamani kabla ya utetezi kuwa hukuwepo wilaya ya Arusha ulikuwa una maana gani kumaanisha kutoka taarifa mahakamani

 

Shahidi:Wakati anauliza swali alionyesha hati na kwa mujibu wa hati nilishindwa kutoa taarifa kwa sababu sikujua najitetea sipo wapi na wakati ushahidi unaendelea uliletwa maeneo mengi ambayo hayapo kwenye hati ya mashitaka hadi maeneo ya Dar es Salaam yalitajwa atukashindwa kuelewa tunajitetwa hatukuwa wapi

 

Wakili:uliulizwa kuhusu kupekuliwa usiku na mali kuchukuliwa bila nyaraka je ukaulizea kufanywa hivyo kunafanya wewe kuwa hujatenda makosa ukajibu ndio ulimanaisha nini

Shahidi:Kama sheria inataka mtu asipekuliwe usiku bila kibali cha hakimu mtu yoyote anayefanya hivyo hana tofauti na jambazi na maana yake ni kwamba yeye ndiye anakuwa mtu aliyethibitika kuvunja sheria mimi nabaki kuwa mtuhumiwa na nilimaanisha huwezi kuvunja sheria kwa madai ya kutafuta haki

 

Wakili:Uliulizwa hapa swali kwamba umeleta nyaraka yoyote kuonyesha TAKUKURU  baada ya mke wako kupeleka mkataba na kadi ya gari,ukajibu hao hawafuati sheria katika uchukuaji wa mali ulikuwa unamaanisha nini?

Shahidi:Nilimaanisha kwamba TAKUKURU wamechukua mali zangu na wanachukua mali za watu bila kufuata utaratibu wa kisheria kama walivyochukua gari yangu na vitu vingine…

 

Uthibitisho kwamba wanafanya hayo uko hapa mahakamani kwa kuwa wameleta gari ambayo walipaswa kuichukua kwa mujibu wa sheria akiwa ana hati ya ukamataji na risiti lakini hati hizo na risiti hawajaja nazo hapa mahakamani wasingeweza kumpa Jesca risiti kwani huo ni utaratibu wao wa kuvunja sheria kama walivyofanya kwenye gari


0 Comments:

Post a Comment