ALIYEKUWA Mkuu wa wilaya
ya Hai, Lengai Ole Sabaya ameieleza mahakama hajui eneo la Kwa Mrombo kama lipo
jijini na wilayani Arusha.
Aidha, amesema kuwa
laini ya simu yenye namba 0758707171 ameisajili kwa jina lake lakini yeye si mmiliki
na inatumiwa na mke wake, Jesca Thomas kwenye shughuli zake.
Ameyasema hayo leo mbele
ya hakimu Mkazi, Patricia Kisinda wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha kwa
nyakati tofauti wakati akiulizwa maswali ya dodoso na mawakili wa serikali
Neema Mbwana, Ofmed Mtenga, Felix Kwetukia na mwendesha mashitaka wa Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, (TAKUKURU), Richard Jacopia.
Sabaya alidai kuwa
kuanzia siku ya kwanza amesomewa mashitaka mahakamni hakujua kama Kwa Mrombo
iko jijini Arusha licha ya kuwa amewahi Mwenyekiti wa UV CCM mkoani Arusha .
Sehemu ya mahojiano ya
wakili wa serikali mwandamizi, Kwetukia na Sabaya .
WAKILI:Wewe ni mzaliwa
wa Arusha na ulishawahi kuwa Mwenyekiti wa UVCCm mkoa wa Arusha
SABAYA:Ndio
WAKILI:Unafahamu kuwa
kwa Mrombo ipo jijini na wilaya ya Arusha
SABAYA:Sifahamu
Wakili Kwetuki akaomba
hati ya mashitaka kwa hakimu na kumtaka Sabaya aisome mashitaka yote matano
ambayo katika kusoma kwake alimuelekeza asome sehemu iliyoandikwa wilaya na
maeneo mbalimbali katika wilaya ya Arusha.
WAKILI:Kuanzia siku ya
kwanza ulielewa kuwa kwa Mrombo ni ndani ya wilaya na jiji la Arusha
SABAYA:Sikuelwa kwa kuwa
hati ipo disputed
WAKILI: walikuja baadhi
ya mashihidi hapa makahamani wakataja maeneo hapa Point zone, walieleza Mbauda
walieleza Sombetini walieleza Sakina. Waliulizwa swali lolote kukanusha
kuwa haya maeneo hayopo ndani ya jiji la Arusha
SABAYA: Ndiyo lipo
Baada ya Hakimu Dkt
Kisinda Kuingia Kwenye chumba cha mahakama na mawakiki wa pande zote mbili
kujitambulisha.
Hakimu akamueleza
Mshitakiwa Lengai Ole Sabaya kuwa Mahakama inamkumbusha kuwa bado yuko chini ya
Kiapo azingatie Kusema ukweli.
Akiwa mbele upande
wa kizimba cha kulia Sabaya akaanza kujibu maswali.
Sehemu ya maswali ya
dodoso ya mawakili wa serikali na majibu ya Sabaya.
Wakili Neema Mbwana
WAKILI:Ukiongozwa na wakili
Mahuna ulisema una ndoa ulioa lini na ulimuoa nani
SABAYA: nilifunga ndoa
tarehe 15.7.2018 na nilimuoa Jesca Thomas na ndoa yao ilifungiwa katika kanisa
la Central Sabbath Church. Wasiamizi wa ndoa Elibariki Nko na mama Ruth Urassa
WAKILI: Umeleta hati
yoyote kuthibitisha kuwa umeoa
SABAYA:Kwenye hati ya
mashitaka hakuna sehemu inayolalamikia ndoa yangu
WAKILI:Umeleta
uthibitisho hapa mahakamani
SABAYA:Ndio uthibitisho
ni Mimi hapa mume wake
WAKILI:Umeleta
uthibitisho wa maandishi wa cheti hapa mahakamani
SABAYA: Sijaleta lakini
Mimi ndie mume wake na ndo ushahidi wenyewe
WAKILI:kwajinsi
ulivojieleza ulieleza kuwa ulikuwa mteule wa Rais na Jinsi ulivyojieleza
ulisema uliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya
SABAYA:Ndio
WAKILI: Ulikula kiapo
cha ukuu wa wilaya
SABAYA:Ndio
WAKILI:Kama uliapa
unakubaliana na Mimi kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria
SABAYA:Upo sahihi
WAKILI:Unafahamu kuwa
dhima ya umilikiji wa laini ya simu ni swala la kisheria
SABAYA:Ndio nafahamu
WAKILI:0758707171
nakumbuka namba hiyo ilizungumziwa hapa mahakamani
SABAYA:Nakumbuka
WAKILI:Na namba hiyo
ilikuwa na Usajili wa Lengai ole Sabaya
SABAYA:Ni sahihi
nakumbuka
WAKILI: Mheshimiwa
naomba kielelezo cha tatu upande wa jamhuri akampatia shahidi ni taarifa
ziilizo wasilishwa mahakamani na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom
WAKILI: Hiyo picha iliyopo hapo ni yanani
Kwenye hiyo karatasi
SABAYA:Ni picha ya
inayofanana na Muonekano Wangu
WAKILI:Naomba usome
maelezo yaliyopo hapo chini
Sabaya: Namba hiyo ya
simu imesajili na kumilikishwa kuwa Lengai Ole Sabaya .
WAKILI: Si ni kweli kwamba
wewe kama mkuu wa wilaya ya Hai ulikuwa maarufu ulikuwa unafahamika na watu
wengi
SABAYA:Hapana Mimi
Sikuwa maarufu
WAKILI:Samahani naomba
kubadilisha swali
Wakili:Wewe ulipokuwa
Mkuu wa wilaya mteuliwa wa Rais si ni kweli wananchi wengi walikuwa
wanakufahamu
SABAYA:Sio kweli
WAKILI:Unaweza kututajia
namba ya ufungwa
SABAYA:Namba ya
ufungwa
WAKILI:Unaweza sababu
zilizopelekea wewe kuwa Mfungwa
SABAYA:Hiyo sababu bado
ipo mahakamani za juu inayobishaniwa mimi kuitwa mfungwa
WAKILI:Mheshimiwa naomba
kumpa wakili mwingine aendelee.
Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU,
Jacopiya
WAKILI:Ni kweli kwamba
uteuzi wako ulitenguliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
SABAYA:Sikutenguliwa
nilisimamishwa kazi
WAKILI:Ni kweli kwamba
ulisimamishwa kazi kwa ajili ya kupisha tuhuma zilizokuwa zinakukabili.
SABAYA:Sikuwa na tuhuma
WAKILI:Kwanini barua ya
kukusimamisha kazi iliandika usimesimamishwa kupisha uchunguzi ulikuwa
uchunguzi wa Afya.
SABAYA: Barua iliandikwa
kupisha uchunguzi haikuandika tuhuma zozote.
SABAYA:Siwezi kuongelea
maelekezo ya Mheshimiwa Rais hapa mahakamani
WAKILI:Unakubaliana na mimi
kwamba uchunguzi uliosemwa uchunguzwe ndo matokeo ya kesi iliyokufikisha hapa
mahakamani.
SABAYA:Sikubaliani maana
hakuna uchunguzi uliofanyika
WAKILI:Ni kweli Kwamba
mbele ya Mahakama hii unashitakiwa na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Sio
kikundi chochote wala mtu binafsi au kikundi cha kisiasa
SABAYA:Sikubaliani na
wewe
WAKILI:Unashitakiwa na
nani
SABAYA:Na waliotengeneza
kesi hii
WAKILI: Mheshimiwa
naomba hati ya Mashitaka na Kumapatia Sabaya Aisome.
WAKILI:Soma hapo juu
hiyo hati ya Mashitaka imendikwaje
SABAYA:Republic dhidi ya
Lengai ole Sabaya na wenzake
WAKILI:Kwahiyo hapo ni
Jumhuri dhidi ya Lengai ole Sabaya si
ndio
SABAYA: Ndo unaniambia
hapa kuwa Republic ndo Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania lakini Kwenye hati hii
imeandika neno Republic tu
WAKILI:Niwapi
wameandikwa Kwenye hati ya mashitaka hao waliotengeneza hiyo kesi
SABAYA:Sijaona kama
wameandikwa Kwenye hati ya Mashitaka
WAKILI:
SABAYA:Jamhuri haikutoa
ushahidi waliotoa ushahidi ni Watu
WAKILI:Kuna kosa lolote
mtu kuja kutoa ushahidi mahakamani
SABAYA:Kunakosa ushahidi
wa uongo
WAKILI: Simu namba 0758717170
ni kweli kwamba Imesajiliwa kuwa majina yako
SABAYA:Ndio imesajiliwa
kwa jina langu
WAKILI: Iliwasiliana
0745978686 siku ya tarehe 22.1.2021 iliwasiliana na Mshitakiwa namba mbili
SABAYA:Sijui kwakuwa
hiyo namba Sikuwa naitumia mimi
WAKILI:Mroso alisema
kuwa tarehe 22.1.2021 mshitakiwa wa pili na wa sita na wa saba walikuwepo kwa Mrombo
SABAYA:Sijui ushahidi wa
huyo mtu aliousema
WAKILI:Utakubaliana na
Mimi kuwa mnashitakiwa kwa ushahidi na sio muujiza
SABAYA:Sikubaliani na
wewe na hakuna ushahidi wowote wa maana ulioteletwa kudhibitisha hilo.
WAKILI:Ukishakuwa
mtuhumiwa unaweza kuchagua mahabusu
SABAYA:Kwa kufuata
sheria sikulalamikia mahabusu nililalamikia jinsi sheria zilivyovunjwa
WAKILI:Ukiwa mtuhumiwa
una haki ya kuchagua mahabusu maana ulisema hapa kuwa ukiwekwa Kwenye mahabusu
ya Takukuru
SABAYA:Nilalamikia
kuwekwa mahabusu siku nane bila kuhojiwa wala Kusikilizwa.
WAKILI:Ukieleza
mahakamani kuwa ulipokamtwa ulipelekwa kwenye mahabusu ya TAKUKURU na siyo polisi.
SABAYA:Ndio
WAKILI:Swali langu sasa
mtuhumiwa anaweza akachagua mahabusu upelekwe polisi na sio TAKUKURU
SABAYA: TAKUKURU hawana
Mahabusu kwa Mujibu wa Sheria.
WAKILI:
SABAYA:Ndio Kwa Mujibu
wa Sheria
WAKILI:Sheria Gani
SABAYA:Kwa mujibu wa
sheria nilitakiwa kupekekwa polisi na sio mahabusu za TAKUKURU.
WAKILI:Kwa Sheria ipi na
kifungu kipi
SABAYA:Mh hakimu Hilo
ndo jibu langu
WAKILI:Kunasheria yoyote
ile inayokataza uchunguzi kumkamata mhalifu mahali popote
SABAYA:Nililalamikia
kukaguliwa usiku bila kibali cha kisheria na sheria hairuhusu kukaguliwa usiku
bila kufuata taratibu za kisheria.
WAKILI:Nikweli kwamba
pamoja na kulalamilia namna ulivyokamatwa
WAKILI:Hauwezi kutoa
uahalali kwa kufanya uharamu inawekezana mnanitendea uonevu ndiyo maana mnapita
‘short cut’ kwa kuvunja sheria
Wakili:Nikweli kwamba
katika watuhumiwa wote ni wewe pekee ulikuwa mtumishi wa umma
SABAYA: Sifahamu hao
wengine kama walikuwa watumishi wa umma maana siwafahamu.
WAKILI: Mheshimiwa
naomba kupatiwa hati ya mashitaka
WAKILI:Kwamujibu wa hati
ya mashitaka ni wewe tu ndiyo uliyeandikwa kuwa ni mtumishi wa serikali
SABAYA:Kwa Mujibu wa
hati ya mashitaka ni kweli imeandika hapa nini Mimi peke yangu nilikuwa
mtumishi wa serikali.
WAKILI:Kwa Mujibu wa
hiyo hati ya mashitaka ni wewe tu uliyekuwa na madaraka
SABAYA:Ni kweli nilikuwa
na utumishi wa Umma na sio madaraka kwa mujibu wa hati hiyo.
WAKILI:Ni kweli kwamba
kwa huo utumishi wa umma ulikuwa ni Mkuu wa wilaya
SABAYA:Nilikuwa Mkuu wa
wilaya ya Hai
Wakili:Sikweli kwamba
ulikuwa na Mamlaka na Madaraka
SABAYA:Ndio Nilikuwa na
Madaraka
WAKILI:Na Mamlaka
SABAYA:Mamlaka ni Jibu
Lako
WAKILI:Nikweli kwamba
Kwenye hati ya mashitaka haijaeleza kuwa watuhumiwa wengine hawana Madaraka na
Mamlaka
SABAYA : Mheshimiwa
hakimu wakili aeleze kama anajibu kutoka na hati ya mashitaka au anataka majibu
yangu kama Lengai Ole Sabaya
Wakili akafafanua kuwa
anauliza kutokana na Hati kutokana na Shahidi kuitambua hati hiyo
Sabaya akajibu kuwa yeye
hafahamu
WAKILI:Kwa kuwa wewe
ulikuwa pekee ndo mwenye Madaraka ni sahihi kuwa uliyatumia Madaraka yako
vibaya
SABAYA:Utakuwa hapo
sahihi
0 Comments:
Post a Comment