SABAYA ADAI CCTV ZINAZOONYESHWA MAHAKAMAI NI MOVIE

 

ALIYEKUWA Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amedai kuwa hakuona CCTV video zilizoonyesha eneo la ukumbi (hall) ndani ya benki ya CRDB tawi la Kwa Mrombo zilizotolewa na kupokelewa kisha zikaonyeshwa mahakamani hapo kwa kile alichodai aliona 'movie'.

 

Ametoa majibu hayo leo mbele ya hakimu Mkazi, Patricia Kisinda wa mahakama ya wilaya ya Monduli anayesikiliza shauri hilo kwenye mahakama ya hakimu Mkazi Arusha wakati akiulizwa maswali ya dodoso na wakili wa serikali Mwandamizi, Felix Kwetukia.

 


Sabaya ambaye katika hatua za awali alidai hakuiona kabisa video hiyo lakini wakili wa Serikali alipozidi kumbana huku akimkumbusha kuwa video hizo zilionyeshwa kwa nyakati tofauti na shahidi wa nane wa Jamhuri, Johnson Kisaka na  shahidi wa 10 Fransis Mrosso ndipo akakiri kuona 'movie'.

 

Sehemu ya mahojiano hayo ni kama ifuatavyo

 

WAKILI:alikuja shahidi wa 10 Mrosso akadai kuwa bwana Macha (Jackson) alikuwa amevaa tisheti ya mistari

SABAYA: alieleza hivyo 

WAKILI: Kwenye CCTV video za benki ya CRDB bank hall uliziona

SABAYA:Sikuziona 

WAKILI: CCTV video  za CRDB kwa mrombo zikichezwa hapa mahakamani hukuona

SABAYA: Sikuona

WAKILI: Wakati zikichezwa ulikuwa umelala?

SABAYA: Nimesema sikuziona

WAKILI:Zilipoletwa kwa mara ya kwanza na shahidi wa nane wa Jamhuri Johnson Kisaka hapa uliziona

SABAYA: Sikuziona niliona movie.

WAKILI: Vilevile alikuja Mrosso zikachezwa kuanzia saa 10.04 mpaka 11.15 uliziona hukuziona 

SABAYA:sikuziona

 

 

 

Wakili wa serikali Mwandamizi, Felix Kwetukia akimhoji Sabaya maswali ya dodoso

Wakili:Suala la usajili wa simu liko kisheria na si kwa matakwa ya mtu binafsi

Shahidi: Ndiyo nakubali 

Wakili: Unakubaliana  na mimi sheria ya usajili inaweka vifungu hususani kifungu namba 12, moja sheria inakataza kuazimisha laini za simu.

Shahidi. Sikubaliani

Wakili : Kwa wewe uliyekuwa na dhamana ya kuilinda  na kutetea sheria unakubaliana kuwa hairuhusiwi kuazimisha laini ya simu

Shahidi: Unaweza kuiazimisha kwa mtu

Wakili: kwa sheria ipi

Shahidi: Sheria hiyo inatoa masharti

Wakili: Wewe ulikuwa na dhamana ya ukuu wa wilaya ukasajili line ya simu kwa kitambulisho cha NIDA halafu ukaiazimisha kwa mtu mwingine

Shahidi: Inaweza kwa mujibu wa sheria

Wakili: Sheria gani inayosema hivyo

Shahidi: Katika sheria ya mawasiliano

 Wakili: Nilikusikia ukisema kuwa bwana Ramadhani Juma alikuja gerezani  akawashawishi wenzako watoe maelezo ya kukukandamiza wewe anajua kwa namna gani atawatoa kwenye kesi mahakamani 

Shahidi: Ni kweli

Wakili: Ramadhani alikuja hapa alitoa ushahidi wakati akitoa ushahidi aliulizwa maswali ya dodoso mawakili wako walimuuliza juu ya hilo

Shahidi: Aliulizwa na mawakili wawili

 

WAKILI: Kuna swali lolote bwana Ramadhani Juma aliulizwa juu ya utetezi wako kuwa alijua atafanyaje huko mbele mahakamani namna ya kuwatoa watuhumiwa wengine mahakamani hapa kwenye kesi

SABAYA: Aliulizwa

WAKILI:alikuja bwana Ramadhani Juma kuna swali lolote aliloulizwa juu ya mkataba wa gari baina yako wewe na Oilcom wa ununuzi wa gari kwamba alikabidhiwa na bi Jesca

SABAYA: Aliulizwa

WAKILI:Unatambua kwamba mahakama ni  chombo huru 

SABAYA:Natambua

WAKILI:Unatambua mahakama katika kutenda wajibu wake wa kutoa haki haiingiliwi na chombo chochote cha dola

SABAYA: Haipaswi kuingiliwa

 

WAKILI:Kwa hiyo unakubaliana na mimi kwamba Ramadhani Juma hana uwezo wala mamlaka kuingilia mahakama katika utendaji wake

SABAYA: Hana 

WAKILI:Alikuja shahidi namba 11 Bw Shabani katika ushahidi wake alisema aliwakuta wewe pamoja na mshitakiwa wa pili, wa tatu, wa tano  pamoja na mke wako ndiyo alivyosema hapa mahakamani 

SABAYA:Ndiyo alisema hivyo

WAKILI: Wakati akitoa ushahidi hapa mahakamani aliulizwa kuwa aliwakamata nyie wanaume wanne na mwanamke mmoja mkiwa sehemu moja 

SABAYA:Aliulizwa 

WAKILI: Kuna swali lolote aliloulizwa la kukanusha kuwa aliwakamata wewe mtuhumiwa namba mbili, tatu,  na tano silvester pamoja na mkeo  mkiwa mahali pamoja

SABAYA: Aliulizwa na akakanusha

WAKILI:Alikuja bwana Sabri shahidi namba 12 pamoja na ushahidi wake wote alituletea mkataba wa gari kuna swali lolote aliulizwa hapa juu ya sahihi na jina lako

SABAYA: ndiyo aliulizwa

WAKILI: nasema specifical jina na sahihi yako

……

 

WAKILI: Bwana Lengai narudi nyuma kidogo kuwa uliazimisha namba ya simu, huko nitarudi baadaye kidogo,  unafahamu mahakama inaweza kumkuta mtu hatiani hata kwa kosa ambalo haliko kwenye hati na mashitska

SABAYA: Nafahamu

WAKILI:Hadi sasa hivi hakuna uthibitisho uliotoa wa maandishi kutoka vodacom ulioleta hapa mahakamani kuwa laini ya simu uliyoisajili inatumiwa na mtu mwingine 

SABAYA: Sijawasiliana na vodacom

WAKILI: Na hata alipokuja shahidi bwana James Wawenje toka vodacom hakuulizwa swali lolote juu ya namba yako uliyosajili kwa kitambulisho chako cha nida inatumiwa na mtu mwingine 

SABAYA:Aliulizwa

WAKILI:Nasema hii namna 0758707171 alithibitisha inatumiwa na mtu mwingine hii namba iliyosajiliwa kwa kitambulisho chako na particulars zako inatumiwa na mtu mwingine 

SABAYA: Hajaulizwa manake yeye alileta ushahidi wake

 

WAKILI: Kaulizwa hajaulizwa

SABAYA: Hajaulizwa

WAKILI: Una kubaliana na mimi kwamba jambo moja kwenye kesi si lazima lithibitishwe na mashahidi 20

SABAYA: Uliiza swali vizuri

WAKILI: Uliulizwa kuwa mtu haufungwi kwa kuleta mashahidi wengi

SABAYA:

WAKILI: Shahidi mmoja anaweza kuthibitidha jambo linalobishaniwa 

SABAYA: Mh kama ni swali la Ngemela naomba nijibu kwa jibu nililojibu

 

WAKILI: Jambo moja katika kesi linaweza kuthibitishwa na shahidi mmoja na si lazima kuleta mashahidi lukuki

SABAYA:Sijaelewa alipoulizwa mara ya pili akasema inategemea quality ya mashahidi

WAKILI: Jibu swali langu unaweza au hawezi 

SABAYA:

WAKILI: Alikuja shahidi namba 10 Mrosso na 13 Ramadhani Juma wakawatambua Mrosso aliwatambua watu aliokuwa nao kule benki miongoni mwao akiwemo Macha (Jackson) na alimshika bega hapa makahamani

SABAYA:Macha yupi

WAKILI:Mshitakiwa namba sita na wewe pia alikushika bega

SABAYA:Ndiyo

 

WAKILI:Akadai kuwa bwana Macha alikuwa amevaa tisheti ya mistari

SABAYA: Alieleza hivyo 

WAKILI: Kwenye CCTV za CRDB Kwa Mrombo eneo benki hall ulizona hapa mahakani

SABAYA:Sikuziona 

WAKILI:CCTV  za CRDB Kwa Mrombo zikichezwa hapa mahakani haukuona 

SABAYA:Sikuona

WAKILI: Wakati zikichezwa ulikuwa umelala 

SABAYA: Nimesema sikuziona

WAKILI:Zilipoletwa kwa mara ya kwanza na Johnson Kisaka hapa mahakamani  uliziona

SABAYA: Sikuziona niliona ‘movie’

 

WAKILI: vilevile alikuja Mrosso zikachezwa kuanzia saa 10.04 jioni mpaka 11.15 jioni ulizona hukuziona 

SABAYA:Sikuziona

WAKILI: Uliongea hapa juu ya kutoletwa cheti cha seizure hapa mahakama kunaondoa ukweli kwamba ile gari imekamatwa

SABAYA: Inaondoa

WAKILI:Inaondoa ukweli kuwa ile gari inashikiliwa PCCB mpaka likaletwa hapa mahakamani

SABAYA:Inaondoa ndiyo inaondoa

WAKILI:Katika hilohilo alikuja bwana Shaban akaeleza kuwa yeye ndiyo alikamata lile gari T 222 BDY 25/ 5/ 2021 na akaliendesha mpaka ofisi za PCCB upanga ulimsikia iz akisema hivyo hapa mahakamani

SABAYA: Hakusema hivyo

……

WAKILI:Katika ushahidi wako ulisema kuwa Mrosso  hakuwa katika position hivyo asingeweza kujaza magari yanayoingia na kutoka kwani hata magari yakitoka akiwa chini ya ulinzi 

SABAYA: Hayo si maelezo yangu ya ushahidi

WAKILI: Ulimsikia bwana Marandu akisema yeye ndiyo alikuwa akijaza kile kitabu

SABAYA:Sikumsikia kwa sababu  

WAKILI: Baasi haukumsikia, vilevile kuna maswali uliulizwa na wenzangu ni kweli ulisimamishwa ukuu wa wilaya ili kupisha uchunguzi

SABAYA: Ni sahihi

WAKILI: Polisi wana kitengo cha uchunguzi kiko chini ya DCI

SABAYA: Sahihi

WAKILI: Unakubaliana na mimi polisi wanachunguza makosa ya jinai

SABAYA:Nakubali

WAKILI: Na TAKUKURU ni chombo cha uchunguzi

SABAYA: Kinachohusu makosa ya rushwa 

WAKILI:Ni kweli kwamba hadi sasa hakuna shahidi yeyeto kutoka polisi aliyekuja kutoa ushahidi kwenye kesi hii 

SABAYA: Hakuna

WAKILI: Kwenye ya jinai namba 105/ 2021 ambayo imekwisha na na hii economic case na 272021 inayoendelea

SABAYA:sahihi

 

WAKILI: ni kweli kwamba kesi namba 105 2021 ilipelelezwa na polisi 

SABAYA: Hakuna mtu alinihoji

WAKILI: Ni kweli kwamba hakuna mtu hata mmoja wa TAKUKURU akihusika na hiyo kesi.

SABAYA: Mheshimiwa hayo mambo yanabishaniwa mahakamani hivyo siwezi kuzungumza

WAKILI: Katika kesi inayoendelea hadi tunafunga ushahidi hakuna afisa kutoka polisi aliyefika isipokuwa watu watatu wa TAKUKURU

SABAYA: Ni sahihi

WAKILI:Ni kweli kwamba kwenye kesi namba 105/ 2021 uliopewa nafasi ya kujitetea ukiwa na mawakili wako

SABAYA: Hiyo kesi iko mahakamani siwezi kuzungumzia

WAKILI: Kwenye kesi hii inayoendelea umepewa haki ya kusikilizwa na kujitetea ukiwa na mawakili wako

SABAYA: Ndiyo nimepewa haki ya kusikilizwa 

 

WAKILI: Wakati bwana mrosso akitoa ushahidi wake hapa mahakamani ni kweli kwamba wewe ulielekeza kuwa toa milioni 90 vinginevyo tuondoke wewe

SABAYA: Siyo kweli

WAKILI:Ni kweli kwamba kwa mujibu wa CCTV footage ambazo wewe unasema huzijui mnamo au  tuliache kwanza . Hivi kweli mtu mmoja anaruhusiwa kuwa na mitandao ya makampuni yote 

SABAYA: Anaruhusiwa 

WAKILI: Na ukweli kwa mujibu wa CCTV footage ambazo unasema huzijui kuanzia saa 10 43 mpaka saa 10 45 mtu aliyetambuliwa na Mrosso kama Macha alikuwa anaongea na simu

SABAYA: Siitambui hiyo CCTV

WAKILI: Unajua au haujui

SABAYA: mh hakuna CCTV  iliyoletwa hapa mahakamani

 

WAKILI:Ulisema mshitakuwa wa sita (Silvester Nyegu) hakuwa wakala wako kukupokelea fedha 

SABAYA: Mh nilikuwa najibu swali la Ngemela (Wakili wa utetezi)

WAKILI:Shahidi wa 10 alikuja hapa akasema ulimkabidhi vijana wawili ili waende CRDB  tawi la kwa Mrombo ili wakalete hela

SABAYA: Hakusema unaongeza maneno

WAKILI: Ni kweli kwamba bwana Mrosso alitoa ufafanuzi wa kukosewa kwa akaunti yake hapa mahakamani

SABAYA: Hakutoa

WAKILI:Uliulizwa swali hapa jana ukajibu hapa hujui juu ya bwana Mrosso

……

WAKILI: nitamuuliza swali kutokana hati ya mashitaka Kuongoza matendo ya uhalifu, matendo ya rushwa, matumizi mabaya ya madaraka katika mashataka haya lipo hilo la kisiasa

SABAYA: Mashitaka ni ya kisiasa hilo ndiyo jibu langu

 

Mheshimiwa yangu ni hayo, mengine Janet ataendelea 

 

 

 

Wakili wa serikali mwandamizi, Janet Segule

 

 

 

 

WAKILI: Sabaya habari ya kwako pole sana nina maswali machache kama hatutazungushana katika kujibishana . Umesema ulikuwa dc hai

SABAYA:Kweli

WAKILI: Nitakuwa sahihi nikisema wakati ukipata uteuzi huo kuna watu wengine waliteuliwa kuwa maDC

SABAYA: Sahihi

WAKILI: Nitakuwa sahihi nikisema kuwa katika maDC mliochaguliwa kwa kipindi chako ni wewe pekee umefunguliwa mashitaka mawili  na moja unatumikia kifungo

SABAYA:Sifahamu

 

WAKILI: Vilevile umeeleza mahakama kuwa ulisimamishwa ili kupisha uchunguzi

SABAYA:Aliyenisimamisha ndiyo anaweza kujua hilo siwezi kumsemea mh Rais.

WAKILI: Ulidai kwamba kwenye mkataba wa gari ulioletwa na shahidi wa 12 na ulipokelewa bila pingamizi

SABAYA: Wakati mkataba unaletwa haikuwekwa pingamizi

WAKILI:Haikuwekewa 

SABAYA: Nilisema mkataba ule sio wa kwangu sikufanya nao manunuzi

WAKILI:Vilevile ukasema kwamba kwa nini jina lako limetokea kwenye mkataba huo na sahihi si ya kwako

SABAYA: Nilisema kuwa 

WAKILI:Ni sahihi kuwa mahakama ndiyo inachambua kijua uhalali wa ushahidi uliotolewa mahakamani

SABAYA:Mahakama ndiyo inauchambua

 

WAKILI:nikurudishe kwa mshitakiwa namba tano ulisema kuwa ulikuwa unamuona kama sehemu ya watumishi wa wilaya ya hai

SABAYA: Kama sehemu ya watumishi

WAKILI: Shahidi namna 12 Sabri katika ushahidi wake mahakamani alisema kuwa wakati mkiuziana gari mshitakiwa namba tano alikuwa eneo la black wood 

SABAYA: Alisema hivyo

WAKILI: Shahidi huyo alisema kuwa alishakutana na wewe pamoja na mshitakiwa huyo katika mkutano mkuu Dodoma

SABAYA: Hakusema kwenye mkutano mkuu

WAKILI:Kwenye mkutano wa CCM

SABAYA:Hakusema kwenye mkutano wa ccm

 

WAKILI:Na madai yote hayo ya kusema ya kukutana na mshitakiwa namba tano pamoja naye Black Wood pamoja na Dodoma hakuulizwa maswali

SABAYA: Aliulizwa 

WAKILI:Mkataba ulioletwa na Sabri ambacho ni mkataba wa mauziano ambapo kuna namba (anazitaja namba za simu mbili)  .... ulisema siyo ya kwako

SABAYA:Ndiyo nilisema si ya kwangu kwani tayari wameleta kielelezo kina namba nyingine.

WAKILI: Walisema wakati ukikamatwa ulikamatwa ulikuwa na namba mbili tofauti 0714 038888 0754 585458

SABAYA: Ndiyo na nilizitaja

WAKILI: Sasa Lengai nitakuwa sahihi nikisema kwamba si ajabu mtu kuwa namba zaidi ya moja na sheria haikatazi

SABAYA: Kuwa specific ni sheria au …… mimi nina namba mbili

WAKILI: Nitakuwa sahihi kuwa sheria haikatazi

SABAYA: Haikatazi

WAKILI: Hivyo ungeweza kuwa na zaidi ya hizo mbili

SABAYA: Nisingeweza ndiyo sababu ninazo hizo mbili tu

WAKILI:Kwenye count (shitaka) ya tano inahusiana na utakatishaji wa fedha ulidai kwamba unashangaa gari linadaiwa kunuliwa tarehe 2/ 2/ 2021 wakati hati ya mashitaka inakutuhumu kutakatidha fedha wakati hati ya mashitaka inakutuhumu kutakatisha fedha 22/ 1/ 2021 ulisema hivyo

SABAYA: Nilisema hivyo

WAKILI:Ni sahihi kwamba 22/ 1/ 2021 unayodaiwa kutakatisha fedha unazodaiwa kama rushwa kutoka kwa Mrosso na kuitakatisha ni tarehe kabla ya tarehe 2/ 2/2021 uliyodaiwa kutakatisha fedha 

SABAYA: Sahihi

 

WAKILI: Katika ushahidi wako ulisema kuwa Mrosso alijaza kitabu cha wanaoingia na kutoka mbele ya afisa wa TAKUKURU

SABAYA: Nilisema alijaza walipofika maafisa wa TAKUKURU

WAKILI: Ulikuwepo 

SABAYA: Hayo ni maelezo ya shahidi wa tatu wa jamhuri

WAKILI: Ok kwa maelezo yake. Nitarudi kwa mke wako shahidi namba mbili wa utetezi Jesca ni sahihi alisema kwamba aliwasiliana na broker (dalali) huyo wa mazao majira ya saa nane mchana na baada ya hapo hawakuwasiliana tena

SABAYA: Alisema walifanya mawasiliano

WAKILI: Wewe ulimsikia akisema kwamba alifanya mawasiliano na dalali majira ya saa nane mchana 

SABAYA: Alikuwa anajibu swali alisema alifanya mawasiliano saa nane na akasema alifanya mawasiliano baadaye na ipo kwenye ushahidi

WAKILI: Sabaya ni sahihi kwamba shahidi wako wa pili Jesca akitumia simu yako namba ...

 

 

SABAYA: Alisema kuwa siku hiyo 22/ 1/ 2021 alisema alikuja Arusha na majira ya usiku alirejea Hai

SABAYA: Sahihi

 

WAKILI: Alisema kuwa wakati akielekea Kisongo alipita Mbauda

SABAYA: Ni sahihi alitaja na maeneo mengine alisema kuwa pia anafanya biashara Mbauda

WAKILI: Na aliporudi alipita Majengo, Tripple A Mianzini wakati akielekea Hai 

SABAYA: ni sahihi aliyataja 

WAKILI: mh naomba kielelezo namba 3 Jesca  alisema alikuwa anatumia simu 0758707171 kuwasiliana na watu

SABAYA: Hakusema alitumia hiyo tu na simu nyingine  aliyokuwa nayo kwa mambo binafsi

WAKILI: Ana mambo binafsi

SABAYA: Kabisa 

 

WAKILI: Alisema ni saa ngapi alipita Mbauda kuelekea Kisongo

SABAYA: Sikumbuki saa

WAKILI: Sabaya naomba nikupatie kielezo namba tatu katika maelezo shahidi wa pili wa utetezi ambapo alisema alifanya mawasiliano na dalali kuanzia saa nane mpaka saa nne na dakika 8 usiku wa siku hiyo ya tarehe 22/ 1/ 2021 kuna sehemu yoyote unasoma Majengo 

SABAYA: Mh sijui mnara unaosoma Majengo mimi siwezi kujua mnara unaosoma Majengo

HAKIMU Janet kuwa specific

WAKILI: Akarudia swali

SABAYA:Mh hakimu hiyo itanipa shida kujibu labda kama anahitaji maoni yangu

HAKIMU Amekuuliza kwenye kielelezo kuna sehemu inasoma Majengo

SABAYA:Hakuna sehemu inasoma Majengo kwa mujibu wa kielelezo hicho

WAKILI: Kuna sehemu yoyote inayosoma Kisongo 

SABAYA: Kwa mujibu wa kielelezo hicho hakuna 

WAKILI:Lengai embu ikumbushe mahakama siku hiyo mke wako alirejea Hai saa ngapi

SABAYA: Usiku

WAKILI: Saa ngapi

SABAYA: Sikumbuki nilikuwa nimelala

WAKILI: Kwa mujibu wa kielelezo hiki namba tatu siku hiyo ya tarehe 22/ 1/ 2022 simu hii iliendelea kusomeka ikiwa arusha mpaka tarehe 25 /1 /2021

SABAYA: Mheshimiwa  kwa mujibu wa kielelezo simu hii ilisomeka ikiwa Arusha

 

Mh ni hayo tu kwa shahidi naomba kurejesha kielelezo namba tatu.

 

Wakili wa utetezi, Moses Mahuna tuko tayari kuendelea na re examination kulingana na muda wa mahakama lakini kama muda hauruhusu tuko tayari kuendelea siku nyingine itakayopangwa na mahakama.

 

Hakimu Kisinda, basi tutaendelea jumatatu

 

 

0 Comments:

Post a Comment