BODI ya Nafaka na Mazao
Mchanganyiko Tanzania, (CPB) imefanikiwa kupanua wigo wa masoko la bidhaa zake
ambapo imeuza tani 120 ya unga wa ngano chapa Nguvu
kwenye nchi ya jirani ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
Shehena hiyo ya ngano
iliondoka nchini leo (Januari 7,2022) kwa njia ya barabara kuelekea kwenye Mji
wa Lubumbashi ulioko kwenye mkoa wa Katanga Juu.
Meneja wa CPB,
kanda ya Kaskazini, Hiza Kiluwasha akiongea na waandishi wa habari
jijini Arusha wakati magari yaliyobeba ngano hiyo yakiondoka kwenye kinu chao
cha kusagia nafaka alisema kuwa wamepata oda nyingine kutoa nchini Sudan
Kusini na Kenya.
Alisema kuwa unga wa
ngano chapa NGUVU umetokana na ngano iliyolimwa kwa mkataba kati ya CPB
na wakulima wa wilaya Siha, Karatu, Monduli na Hanang’ ambapo
waliwakopesha mbegu aina ya SC Select kisha wakawaunganisha na taasisi ya
fedha waliowakopesha fedha kwa ajili ya patiwa mikopo .
Soko hilo la unga wa
ngano chapa nguvu limekuja siku chache baada ya uamuzi wa wakuu wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki, (EAC) kuikubalia Jamhuri ya Kidemkrasia ya Kongo
kujiunga na jumuiya.
“Tuko hapa tunapakia
unga wa ngano tani 120 zinaenda Lubumbashi nchini DRC, lengo kuu hasa kwamba
tumefungua masoko ya nje ya nchi. Taasisi yetu iko chini ya Wizara ya Kilimo
ambayo imetupa jukumu la kufufua zao la ngano juhudi ambazo tumezianza msimu
uliopita wa kilimo mwaka 2021,” anaeleza Kiluwasha na kuongeza.
…Tulianza kwa kuingia
mikataba na wakulima wanaolima ngano kwenye mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na
Manyara kwa kuwapatia mbegu bora tuliyoiagiza nje ya nchi na kuwaunganisha na
taasisi za fedha ili waweze kununua mbolea na kupiga dawa kwa wakati ili wapate
mavuno mengi na mwisho sisi tukainunua ngano yao yote.
…Baada ya kuinunua ngano
hiyo ililetwa hapa kiwandani tukaisindika na tulipewa maagizo na serikali kuwa
unga wa ngano tutakaozalisha uuzwe hapa nchini na tutafute masoko nje ya nchi
sasa yamefunguka mbali ya hii tunayoipoeleka Lubumbashi kuna nyingine
itapelekwa Sudan ya Kusini, Kenya, Rwanda na Burundi.
….Yote hii ni katika
kuhakikisha mkulima wa ngano anapolima anakuwa na uhakika wa soko la bidhaa
hiyo na tayari tumeshaenda kwa wakulima kuingia makubaliano ya kuendesha kilimo
cha ngano cha mkataba kwa msimu wa kilimo wa mwaka huu 2022 ambayo unawahakikishia
wakulima soko la ngano yao kwani tutainunua yote.
….Mkataba huu unalenga
kuhakikisha mkulima wa ngano anapata mavuno bora yenye tija kwa kuhakikisha
anapata mkopo, mazao yake yanakuwa na kinga ya majanga kwa kuyakatia
bima, kuendesha kilimo kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo na wakati wa kuvuna
anakuwa na vifaa vya kuvunia hivyo ngano hiyo inakidhi vigezo vya ubora wa
ndani na wa kimataifa,”.
Hata hivyo, Kiluwasha
alisema kuwa mbali ya zao la ngano pia CPB inashughulika na mazao
mengine kama mahindi, maharage, mchele, kila kitu kinachohusu nafaka CPB
wananunua kuhakikisha wakulima wanakuwa na uhakika wa soko la mazao yao huku
akiwasisitiza wakulima kuhakikisha wanazingatia kanuni bora za kilimo.
“Sisi
tunawahakikishia wakulima tutanunua mazao yao na tutawalipa hapohapo,
hivyo wakulima walio Kanda ya Kaskazini kama una mahindi, ngano, maharage,
mchele wayalete sisi tutanunua kwa bei ya soko na tutawalipa kwa wakati, “
alisema Kiluwasha na kuongeza.
…Sisi hapa tunaeneo
kubwa la kuhifadhi mazao hivyo tukinunua mazao kama mahindi, tunayasindika na
eneo la kuhifadhi ni kubwa kwa kabisa kuhakikisha mazao ghafi yote
tunayoyanunua kutoka kwa wakulima tunayaongezea ubora na kuyauza kama bidhaa.
…Kwenye mkataba huo
tuliweka bei ya kununua ngano hiyo kutoka wakulima iwe shilingi 800 kwa kilo
ambayo ni bei ya juu ukilinganisha na bei shilingi 500 waliyokuwa wakipewa na
wanunuzi binafsi ambayo lengo letu ilikuwa ni kuinua uchumi wa wa mkulima wa ngano
na limefanikiwa iliyokuwa ikitolewa,".
Dereva anayepeleka
shehena hiyo ya ngano nchi ya Jamhuri ya kidemorasia ya Kongo, Ernest Mollel
alisema kuwa wanatazamia kutumia siku 10 kuwa wamefikisha mzigo huo Lubumbashi.
“Napitia njia ya Arusha
Dodoma Iringa Mbeya Tunduma nitachukua takribani wiki moja na nusu nitakuwa
nimefika Lubumbashi,” alisema Mollel.
Afisa kilimo kutoka CPB,
Marco Ndonde anasema katika msimu uliopita wa mwaka 2021 bodi hiyo
iliingia mkataba na wakulima wenye jumla ya ekari 2,937 kwenye wilaya za
Siha mkoani Kilimanjaro, wilayani Hanang' mkoani Manyara na Karatu na
Monduli.
Alisema kuwa walipata
jumla ya tani 1,136 ya ngano ikiwa na ubora mzuri kwani CPB walihakikisha
wanakuwa karibu na wakulima katika hatua zote kuanzia shambani kuanzia hatua ya
mwanzo ya kuandaa shamba, uchambuzi wa mbegu bora, upandaji, utunzaji, uvunaji
na namna ya kuihifadhi kabla ya kuifikisha sokoni.
Afisa Ubora wa CPB,
Kanda ya Kaskazini, Kombo Abdalah alisema kuwa unga wa ngano chapa nguvu una
ubora uliothibitishwa na Shirika la Viwango nchini, (TBS) pamoja na
wa
Alisema kuwa ngano kabla
haijapokelewa kiwandani hapo kitu cha kwanza wanaangalia hali ya ukaukaji,
protin, uzito ainisho na gluten na baada ya unga kupatikana hurejea kuangalia
vitu hivyo ili kuhakikisha walaji wanapata kitu kilicho bora.
“Tukishaipokea ngano
hapa Kiwandani tunaiweka kwenye kihenga, hapo tunaendelea na shughuli za
kuiandaa ngano kwa ajili ya kuisaga kwa kuangalia kiwango cha unyevu ili iweze
kukoboleka vizuri na tupate unga mzuri,” anasema Kombo na kuongeza.
…Ukisaga ngano ikiwa
kavu zaidi unapata unga mchache na kitaalam manake hiyo ni hasara na ukiweka
maji mengi unga utatoka na unyevu hivyo unga utawahi kuharibika na utatengeneza
ukungu hivyo unga utakuwa haufai kwa matumizi ya binadamu,”.
Afisa Usagishaji wa
Kiwanda cha CPB, Kimweri Gasper alisema kuwa kiwanda hicho kina uwezo wa
kuchakata tani 120 za ngano kwa saa 24.
“Mashine zetu ni za
kisasa, kuna mashine za kubaini na kuondoa uchafu, mawe, vyuma na tukisaidiana
na watu wetu wa ubora ngano yetu hupimwa kuhakikisha kuwa haina sumu kuvu ili
iwe salama kwa mtumiaji wa mwisho,” anasisitiza Kimweri.
Afisa Masoko na Mauzo wa
CPB, Kapistorano Tweve alisema kuwa kuwa tokea wameingiza unga huo sokoni
umepokelewa vizuri na wananchi wa mikoa mbalimbali jambo alilodai kuwa linampa
uhakika na kwenye nchi za jirani nako utapolewa vizuri.
sawa na kilo 1, 136,000 ambayo ni sawa na gunia 11,360 zenye ujazo wa kilo 100 kwa kila moja.
0 Comments:
Post a Comment