KIMEI ATOA NENO NCHI KUKOPA

 

Na Gift Mongi, Moshi

Mbunge wa jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro Dkt Charles Kimei  amesema deni la taifa bado ni stahimilivu na kuwa si tishio kama ambavyo

inasemekana ambapo pia nchi nyingi duniani zimekuwa zikikopa ili

kujenga miundimbinu ambayo itawawezesha wananchi wake kufanya biashara sambamba na huduma mbali mbali.



Dkt Kimei alitoa kauli hiyo katika hafla ya kupokea vyumba 85 vya

madarasa vilivyojengwa kwa  shilioni bilioni 1.7 fedha ambazo ni kwa

maendeleo ya ustawi wa taifa katika mapambano ya ugonjwa  uviko 19

ambapo zoezi hilo kwa wilaya ya Moshi lilifanyika katika shule ya

sekondari Himo kwa kukabidhi vyumba vinne.


Kwa mujibu wa mbunge huyo ambaye pia ni mtaalamu wa uchumi na amewahi

pia kuhudumu katika sekta kadhaa za fedha nchini ikiwemo mkurugenzi

mtendaji wa benki ya CRDB ni kuwa bado taifa letu lina sifa za

kukopesheka  na ndio maana tumeendelea kuaminiwa na wahisani

mbalimbali ikiwemo mfuko wa fedha duniani na benki ya dunia.


“Sisi bado tupo katika hali nzuri ya kukopesheka na ndio maana rais

Samia Suluhu Hassan alivyoenda kukopa aliaminiwa mra moja tofauti

labda na mataifa mengine sisi bado tunayo rekodi nzuri katika mkopo na

suala la mkopo si aibu hatuanza sisi kukopa wala hatutakuwa wa

mwisho”alisema

0 Comments:

Post a Comment