Hatua inazochukua Marekani kufuatia Kombora la Jana


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson amelaani vikali jaribio la hivi karibuni la kombora lililofanywa na Korea Kaskazini, akilielezea kuwa ni kombora linalovuka mabara-ICBM.

Alitoa taarifa jana Jumanne kufuatia tangazo la Korea Kaskazini kuwa imefanikiwa katikia jaribio lake la kwanza la ICBM.

Afisa wa serikali ya Marekani aliiambia NHK jana Jumanne kuwa kombora hilo huenda likawa ni ICBM lenye awamu mbili.

Jeshi la Marekani Kamandi ya Pasifiki ilisema mapema kuwa utafiti wake wa awali unaonyesha kuwa kombora lilirorushwa linaweza kuwa la masafa ya kati.

0 Comments:

Post a Comment