SERIKALI imeipa kampuni ya kimataifa ya Surbana International Pty Ltd ya nchini Singapore kazi ya kuandaa mpango kamambe (master Plan) kwa ajili ya
majiji ya Arusha na Mwanza.
Kampuni hiyo inatakiwa
kukamilisha shughuli hiyo ndani ya miezi 13 tokea kusainiwa kwa mkataba.
Mkataba huo ulisainiwa juzi jijini
hapa na Katibu mkuu wa wizara wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo
ya makazi, Alphayo Kidata, na Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni hiyo, Kong
Wu Mun.
Aidha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa
Mulongo na Waziri wa Nchi wa Mambo ya Nje na Mambo ya Ndani wa Singapore
,Masagos Zulkiflg walikuwepo kushuhudia tukio hilo la utiaji saini huo .
Pia viongozi waandamizi kutoka
Wizarani na halmashauri za majiji ya Arusha na Mwanza waklikuwepo kushuhudia
tukio hilo.
Akizungumza mara baada ya kusaini
mkataba huo, Kidata alisema kuwa, tukio hilo ni mwendelezo wa mchakato uliokuwa
umeanza kufuatia mkataba wa makubaliano
ambao wizara ya ardhi ilisainiana na Singapore mwezi desemba 2013 kwa niaba ya serikali
ya Tanzania.
Alisema kuwa,lengo la kuanzisha
mradi huo kuwezesha miji iliyopangiliwa
vizuri na yenye maendeleo na kuondokana na msongamano wa magari pamoja na
nyumba zisizokuwa na mpangilio jijini Arusha .
“Kuwepo kwa mpango huu kutawezesha
kwa kiasi kikubwa sana kuishi katika mpangilio unaohitajika na kuchangia nchi
kupata maendeleo kwa kuwa na miundombinu ya kutosha katika maeneo yenye
mpangilio,” alisema Kidata .
Alisema kuwa wanatarajia kusaini
mkataba na kampuni ya China kwa ajili ya kuandaa mpango kamambe kwa ajili ya
mikoa ya Lindi na Mtwara ambayo inatazamiwa kukua kwa kasi kubwa kutokana na
kugunduliwa kwa nishati ya gesi.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi wa Mambo
ya Nje na Mambo ya Ndani wa Singapore , Zulkiflg alisema kuwa nchi yake
imejikita katika kusaidia mataifa yanayoendelea hasa kwa kuwasaidia kuandaa uwepo
wa mipango miji jambo alilodai kuwa itaharakisha maendeleo kwa kuhamasisha
uwekezaji toka mataifa mbalimbali.
Sent from my iPhone







0 Comments:
Post a Comment