Mawaziri Waongeza Nguvu Kampeni ya Mama Samia Legal Aid

 


Arusha – Mawaziri wameongeza nguvu katika kampeni ya Mama Samia Legal Aid, ambayo imewanufaisha mamia ya wakazi wa Arusha tangu ilipoanza jijini hapa Machi 1, 2024. 


Kampeni hii ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayofanyika Machi 8, 2025, ambapo Arusha itakuwa mwenyeji.



Akizungumzia mafanikio ya kampeni hiyo, Ndejembi amesema: "Tunashukuru kuona kwamba wananchi wengi wameweza kupata msaada wa kisheria. Hii ni fursa kwao kuelewa haki zao na namna ya kuzilinda."

Wakizungumzia ujio wa mawaziri kuelekea maadhimisho hayo, baadhi ya Mama Lishe wa Mkoa wa Arusha wameeleza kuwa wanathamini juhudi zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Christian Makonda, ambazo zimewapatia fursa mbalimbali za kiuchumi na uwezeshaji.

"Tumeona mambo mengi mazuri tunayofanyiwa na Rais Samia pamoja na Mkuu wa Mkoa wetu. Kwa kweli, tumefaidika sana na hatuna wasiwasi. Kura zetu ni za Rais Samia kwenye uchaguzi mkuu ujao," amesema mmoja wa Mama Lishe.


Maandalizi ya maadhimisho hayo yanaendelea, huku kampeni ya msaada wa kisheria ikiendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu haki zao.

0 Comments:

Post a Comment