Kifo cha SP Chiko Kufuatia Ajali ya Gari: Maziko Kufanyika Kesho Kijitonyama



Ajali mbaya imetokea maeneo ya Gongolamboto mwisho, karibu na Kilima cha kuingia Pugu Sekondari, ambapo aliyekuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Chanika (OCD), SP Awadh Mohamed Chiko, amefariki dunia. Ajali hiyo ilihusisha basi aina ya Eicher ambalo lilitangulia na kugonga gari la SP Awadh, akiwa ndani ya Prado akielekea kazini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, ACP Yustino Mgonja, amethibitisha tukio hilo akitangaza kifo cha SP Awadh muda mfupi uliopita kupitia kurasa rasmi za mitandao ya kijamii za Jeshi la Polisi Tanzania.

"Kwa masikitiko makubwa, SP Awadh Mohamed Chiko amefariki dunia leo asubuhi kufuatia ajali iliyotokea eneo la Pugu Sekondari, baada ya basi aina ya Eicher kugongana na gari lake aina ya Prado," alisema msemaji wa familia.

Kwa mujibu wa mashuhuda, basi hilo lilikuwa likitokea upande mmoja na kumgonga SP Awadh, ambaye alipoteza maisha kwenye tukio hilo.

Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hospitali ya Kipolisi Barracks Kilwa Road kwa uchunguzi wa awali.

Maziko ya SP Awadh Mohamed Chiko yanatarajiwa kufanyika kesho, ambapo mwili wake utaswaliwa katika msikiti wa Akachube, uliopo Kijitonyama, kabla ya kusafirishwa kwa maziko. Familia inasema kuwa msiba huu umeleta huzuni kubwa katika jamii, huku wakimwomboleza kwa pamoja na kumuomba Mungu amuweke mahali pema peponi.

"Kwa sasa, msiba upo nyumbani kwa marehemu, Kijitonyama, Mtaa wa Bukoba, ambapo familia inajumuika kwa maombolezo na maandalizi ya maziko," aliongeza msemaji wa familia.

Polisi na maafisa wa usalama wameendelea kufanya uchunguzi juu ya ajali hii, huku familia ikisema itakuwa na mchakato wa kutoa taarifa kamili baada ya uchunguzi kukamilika.

Historia ya Familia: Baba wa SP Awadh Marehemu CP Mohamed Awadh Chiko

SP Awadh Mohamed Chiko alikuwa mtoto wa marehemu SACP Mohamed Awadh Chiko, ambaye pia aliwahi kushika wadhifa mkubwa katika Jeshi la Polisi la Tanzania. 

SACP Mohamed Awadh Chiko aliwahi kuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, nafasi aliyoihudumu kwa kipindi kirefu na kuacha alama kubwa katika utendaji wa Jeshi la Polisi. 


Baada ya kustaafu, alihamishiwa Makao Makuu ya Polisi kabla ya kufariki dunia Januari 22, 2017. 

Marehemu SACP Mohamed Awadh Chiko alijulikana kwa juhudi zake za kukuza usalama na kudumisha amani katika mkoa wa Kilimanjaro na maeneo mengine aliyopita.

0 Comments:

Post a Comment