Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa pongezi kwa taasisi ambazo zimefanikiwa kutoa gawio, akithibitisha kuwa sera, miongozo, na mazingira yaliyowekwa na serikali yamewawezesha kufanya kazi. Amewataka taasisi zingine kufuata mfano huo.
Akizungumza leo Ikulu Dar es Salaam alipokuwa akipokea gawio la Shilingi bilioni 637 kutoka kwenye mashirika na taasisi 145, Rais Samia ameonyesha furaha yake kutokana na mafanikio hayo. Amesema ni ishara nzuri kwa taasisi za umma kuongeza kasi ili kufikia mafanikio kama hayo.
Rais Samia ameelezea kufurahishwa kwake na mchango wa taasisi zilizo chini ya serikali ambazo zimefanikiwa kutoa gawio, hata kama serikali ina hisa chache katika taasisi hizo.
Amesema mfano wa Benki ya NMB, Kampuni ya Twiga Mineral Corporation, Airtel Tanzania, Puma Energy, na TPC Moshi unaweza kuwa kichocheo kwa taasisi nyingine kufanya kazi kwa bidii zaidi.
Kuhusu mifumo ya kusomana, Rais Samia ameagiza hatua zichukuliwe haraka ili kuhakikisha mifumo hiyo inafanya kazi ifikapo Desemba mwaka huu. Amesisitiza umuhimu wa mashirika ya umma kubadilika na kuchangia katika pato la taifa, na amefurahishwa na hatua zilizopigwa hadi sasa kwenye mageuzi ya mashirika hayo.
Akitoa taarifa mbele ya Rais Samia, Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, ameelezea juhudi zinazofanywa na ofisi yake katika kusimamia mageuzi ya mashirika.
Ameeleza kuwa tija imeanza kuonekana, na kwamba zaidi ya taasisi 145 zimetoa gawio hadi sasa.
Lengo ni kupokea gawio la Shilingi bilioni 850, na kwa sasa wamepokea Shilingi bilioni 637 kutoka taasisi 149.
Mchechu ameongeza kuwa wako katika hatua za mwisho za kukamilisha mfumo wa kuripoti taarifa za utendaji wa watendaji wakuu wa taasisi.
Rais Samia amesema amepokea mafanikio makubwa kutoka taasisi ambazo serikali ina hisa chache, hivyo ni ujumbe kwa taasisi za serikali kuongeza kasi ili kufikia mafanikio. Amesema hayo leo Ikulu Dar es Salaam wakati akipokea gawio la Shilingi bilioni 637 kutoka kwenye mashirika na taasisi 145 kati ya 304 zinazochangia asilimia 15 ya mapato ghafi na zile ambazo serikali ina hisa na kusimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.
“Tumeona Benki ya NMB, Kampuni ya Twiga Mineral Corporation, Airtel Tanzania, Puma Energy na TPC Moshi wametoa gawio kubwa na sisi tuna hisa chache nadhani kila shirika lifanye kazi kwa juhudi ili kufikia kampuni hizi,” alisema. Mh. Rais Samia
Aidha, Rais Samia amesema kilichofanywa na Mashirika ya Umma kama Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania (TFS), Wakala wa Huduma za Meli Tanzania (TASAC) na BRELLA ni ushahidi tosha wa kuweka mifumo mizuri na kushirikisha wawekezaji.
“Wapo ambao walipiga kelele kwamba Ooh.. mama anauza bandari, lakini gawio la Shilingi bilioni 153.9 ya TPA ni matokeo ya wawekezaji ambao wapo pale imani yangu ni mwakani wataongeza,” amesema.
Kuhusu mifumo kusomana Rais Samia ameagiza mamlaka husika kuhakikisha ifikapo Desemba mwaka huu mifumo iweze kusomana na kwamba suala hilo limechukua muda mrefu. ambapo ameongeza kuwa hataki kusikia shirika ambalo mifumo yake haisomani na mingine.
Kiongozi huyo amesema alipoingia madarakani aliagiza mashirika ya umma na taasisi ambazo serikali ina hisa zibadilike na kuchangia katika pato la taifa, jambo ambalo limeanza kutekelezwa.
Awali akitoa taarifa yake mbele ya Rais Samia, Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu amesema ofisi yake inaendelea kusimamia mageuzi ya mashirika na tija imeanza kuonekana.
Mchechu amesema sheria inayosimamia ofisi ya Msajili wa Hazina inaelekeza mashirika kutumia si zaidi ya silimia 60 ya mapato yake iliyoyakusanya na kutoa gawio kwa serikali ambapo hadi sasa zaidi ya taasisi 145 zimetoa huku 159 zikitarajiwa kutoa kati ya 304.
Aidha, ameongeza kuwa taasisi zote zimeingia mkataba wa utendaji kazi kati ya bodi zao na ofisi ya Msajili wa Hazina na kwamba wapo katika hatua za mwisho za kukamilisha mfumo wa kuripoti taarifa za utendaji wa





0 Comments:
Post a Comment