KDF: Jenerali Francis Ogolla Akitangazwa Kufariki Katika Ajali ya Ndege

 KDF: Jenerali Francis Ogolla Akitangazwa Kufariki Katika Ajali ya Ndege




Rais William Ruto ametangaza siku tatu za maombolezo kufuatia kifo cha Jenerali Francis Ogolla, afisa mkuu wa kijeshi wa Kenya, na maafisa wengine tisa katika ajali ya ndege. 

Bendera zitapeperushwa nusu mlingoti kuanzia Ijumaa, tarehe 19 Aprili, kama heshima kwa maafisa hao waliofariki wakiwa kazini.


Jenerali Ogolla alikuwa afisa shupavu aliyefariki akiwa kazini katika eneo la kaskazini mwa Kenya, ambalo limekuwa likikumbwa na visa vya wizi wa mifugo. 


Alikuwa katika shughuli ya kufungua shule zilizofungwa kufuatia mashambulizi ya majambazi na pia alikuwa akitembelea maafisa wa kijeshi waliotumwa katika eneo hilo kuleta utulivu.


Jenerali Francis Ogolla aliteuliwa na Rais Ruto Aprili mwaka jana baada ya kuwa Kamanda wa Jeshi la Anga na Naibu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi. Alikuwa mshauri mkuu wa kijeshi wa Rais na Baraza la Mawaziri.


Pamoja na Jenerali Ogolla, maafisa wengine waliofariki katika ajali hiyo ni:


Brigedia Swale Saidi

Kanali Duncan Keittany

Luteni Kanali David Sawe

Meja George Benson Magondu

Kapteni Sora Mohamed

Kapteni Hillary Litali

Sajenti Mwandamizi John Kinyua Mureithi

Sajenti Cliphonce Omondi

Sajenti Rose Nyawira

Ajali hiyo imeleta majonzi makubwa katika taifa hilo la Afrika Mashariki.




0 Comments:

Post a Comment