MAJALIWA AAGIZA TARURA WATEKELEZE AHADI ZILIZOTOLEWA NA JPM NA SAMIA






WAZIRI  Mkuu, Kasim Majaliwa ameuagiza uongozi wa Wakala wa barabara vijijini na mijini, (TARURA) kuhakikisha wanatekeleza ahadi zilizotolewa na Marais wa awamu mbili tofauti ya ujenzi wa barabara ya kilometa sita kuanzia Kikatiti mpaka Sakila wilayani Arumeru.

 

Ahadi hizo zilitolewa na Hayati Rais John Magufuli na Rais Samia Suluhu Hassan  kwa nyakati  tofauti wakati waliposimama kusalimia wananchi kwenye eneo la Kikatiti wakiwa njiani kuelekea jiji Arusha.

 


Waziri Mkuu Majaliwa leo Jumanne, JUni 20,2023 wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye jubilee ya miaka 40 tokea kuanzishwa kwa chuo cha Biblia Sakila kinachomilikiwa na  Kanisa la International Evangelism Church (IEC) ambacho kinatoa elimu bure ambapo zaidi ya wainjilisti, wachungaji na maaskofu 10,000 wamehitimu kwenye chuo hicho tokea kianzishwe.

 

Amesema  kuwa serikali inatambua mchango unaotolewa na  Askofu Mkuu  wa IEC, Dk  Elihudi Isangya kupitia  miradi ya maendeleo anayotekeleza kwenye mikoa ya  Arusha na Manyara katika sekta za elimu, afya, maji na maendeleo ya jamii.

 

Waziri mkuu waliwaagiza TARURA mkoa wa Arusha na wilaya ya Arumeru wakutane mara baada ya yeye kuondoka Arusha ili wajadiliane namna ya kutekeleza ujenzi wa barabara hiyo kutoka Kikatiti mpaka Sakila yenye kilometa sita.

 

Aidha alimuagiza meneja wa shirika la umeme nchini, (TANESCO) mkoani Arusha abaki kwenye chuo hicho pindi yeye na msafara wake unapoondoka ili aweze kupatia ufumbuzi wa suala la kukatika umeme mara kwa mara kwenye eneo hilo.

 


 

"Kabla sijaendelea na mazungumzo haya jana (Juni 19,2023) nilienda kumuaga kiongozi wangu mkuu, Rais, Samia Suluhu Hassan nikamwambia nakuja Sakila...  akasema niliwahi kusimama barabarani pale Kikatiti mikaahidi ujenzi wa barabara ya kuelekea Sakila hivyo amenituma kuleta salamu kwenu," alisema Majaliwa na kuongeza.

 ...Kwanza anawapongeza kwa kuifikia hii miaka 40 kwa mafanikio makubwa sana. Ameniagiza nipokee changamoto zote na nizifanyie kazi hivyo namezipokea na nyingine nitazifanyia kazi hapahapa," .

 

"Nimefurahi kusikia idadi kubwa ya wahitimu zaidi ya elfu 10 katika kipindi cha miaka 40 mbao kwa sasa wengine ni maaskofu, wachungaji na wainjilisti ama kwa hakika mmeweza kujitengenezea na kujiwekea akiba kwenye kazi ya Mungu,".

 

"Mmetusaidia sana serikali hasa katika kipindi hiki ambacho dunia imekumbwa na mmomonyoko wa maadili na chuo kimejikita kwenye kuhimiza imani kwa kuwa na somo la matendo ya huruma na amani. Wahitimu tumieni elimu hiyo kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla,".

 

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa amewapongeza kwa hatua yao ya kujiwekea malengo ya kuwnza ujenzi wa chuo kikuu kitakachotoa elimu kwa wananchi wote ikiwa ni mwendelezo wa mchango wa kanisa hilo kwa jamii.  

 

"Kwa miaka 20 mmekuwa mkitoa huduma ya kuchimba maji bure kwenye maeneo mbalimbali ....Sisi kwa upande wa serikali mnapoamua kuwekeza kwenye miradi ya maji tunawaona mkiunga mkono mpango wa serikali wenye kauli mbiu ya kumtua ndoo mama," alisema Waziri Mkuu.



 Kwa upande wake, Askofu Dkt. Issangya amemshukuru Rais Samia kwa kuimarisha maridhiano baina ya makundi ya jamii yakiwemo yale ya kisiasa na kuwatia moyo viongozi wa dini, hivyo kuwawezesha kutekeleaza majukumu yao kwa urahisi.



Amesema uimara wa Serikali umewawezesha viongozi wa dini zote nchini kupendana, kufanya kazi kwa kushirikiana, kuaminiana na kuheshimiana.





 Awali, Askofu wa Arusha wa IEC, Dkt, Israil Maasa alisema kuwa tokea chuo hicho cha biblia Sakila  kianzishwe mwaka 1983 kimetoa mafunzo kwa watumishi zaidi ya elfu10 kutoka ndani na nje ya nchi ambapo kwa sasa wana malengo ya kujenga Chuo Kikuu.


Alisema kuwa  IEC imejenga  zahanati inayotoa huduma bure kwa jamii ya wananchi wanaoishi Sakila ambayo wanataka kuiboresha ili ifikie hadhi ya hospitali ,   chuo cha ufundi  Maji ya Chai, shule ya awali, shule ya msingi SLUYS na sekondari ya Hebron yenye kutoa elimu mpaka kidato cha sita. 

 

"Chuo hiki kimechimba maji kwenye maeneo mengi bila kudai chochote mfano kwenye uwanja wa Sheikh  Amri Abeid (Arusha), katika shule za msingi na sekondari Sinoni Unga Limitedi  jijini Arusha, kituo cha walekavu Usa River na kwenye hospitali ya wilaya ya Arumeru," alisema Dkt Maasa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Jukwaa la Maridhiano na Amani nchini. 

 

Amesema kuwa wamechimba maji kwenye eneo la  Ngaramtoni na Mringaringa na  na kufunga mtambo wa solar hivyo wananchi wanapata maji bila shida yoyote.

 

Dkt Maasa amesema kuwa Chuo kimekuwa mdau katika ujenzi wa zahanati wilayani Simanjiro na wamechimba visima vinne na kufunga mitambo ya umeme wa sola hivyo maji yanapatikana bila shida yoyote.ì

Hata hivyo  amesema kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni ubovu wa barabara kutoka barabara kuu ya Moshi Arusha mpaka chuoni hapo ambayo imejengwa kwa kiwango cha changarawe lakini haipitiki kirahisi.

 

“ Barabara ni changamoto na hili tunafurahi kwamba umepita  umeiona. Kutoka Kikatiti mpaka Sakila ambayo Rais wa awamu ya tano John Magufuli aliposimama katika eneo la Kikatiti akielekea Arusha aliahidi kuijenga na mama Samia (Rais Samia Suluhu Hassan) alisimama hapo alipokumbushwa alisema inawezekana,” alisema Dkt Maasa

 

Changamoto nyingine aliyomweeza Waziri Mkuu ni ya umeme kukatika mara kwa mara kwenye eneo hilo linalotumiwa na wanachuo na  wakufunzi wao pamoja shule za awali, msingi na sekondari pamoja zahanati ya afya.

 

Amesema kuwa IEC  wanatoa huduma ya kusaidia wazee kwa kuwapa chakula na huduma za afya huku wakiwa na kituo cha watoto yatima ambacho  huwapatia huduma zote muhimu ambapo watoto hao mbali ya chakula,mavazi,  malazi na  matibabua pia hupatiwa elimu kuanzia shule ya awali sekondari na chuo cha ufundi kwenye shule za kanisa hilo.

 

IEC pia inamiliki kituo Kituo cha radio cha New Life kinachotoa elimu kwa jamii sanjari na kueneza neno la Mungu na huduma ya maombi makanisa mengi yameanzishwa na waliohitimu katika chuo hicho.

 


Naye, kofu wa Kanisa la International Evangelism la nchini Congo, Askofu Byamungu Magala ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kudumisha amani na utulivu.



“Tanzania ni Taifa ambalo limejaa amani na utulivu na ni Taifa ambalo halina ubaguzi wa dini wala kabila, Taifa zuri linalopokea wageni bila ya shida yoyote. Nawapongeza viongozi wa Taifa hili,” amesiwitiza Askofu Magala ambaye pia ni mhitimu wa chuo hicho.


Amesema nchini kwao kuna matatizo hawana utulivu, hivyo hawawezezi kumuamudu Mwenyezi Mungu kwa amani kama ilivyo Tanzania.


“Kila ninapokuja hapa namuomba Mungu nasi atupe amani. Amani hii mliyonayo mnatakiwa kuilinda kwa sababu Taifa bila amani raia watakuwa na matatizo makubwa, sisi watu wanauawa kinyama

 


0 Comments:

Post a Comment