WATU wenye ulemavu wa kutosikia (Viziwi) wamesema wamechoka kupokea viporo vya habari ambapo wametaka serikali na vyombo vya habari kuweka wakalimani wa lugha za alama ili na wao wapate haki ya mawasiliano kama wanavyopata wananchi wengine.
Aidha wameitaka ofisi ya Waziri Mkuu kuonyesha mfano kwa kuanzisha bodi inayosimamia lugha ya alama kama ilivyo kwa bodi zingine.
Hayo yalisemwa leo Desemba mosi, 2022 na Mwenyekiti wa chama cha Viziwi nchini, ( CHAVITA), Selina Mlemba wakati akizungumzia maandalizi ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu duniani ambayo kitaifa yanafanyija jijini arusha.
Alisema kuwa vyombo vingi vya habari havina wakalimani wa lugha na hata wakiwa nao huwatumia kwenye vipindi vichache huku akidai walalimani hao huonyeshwa kwenye picha ndogo na rangi inayotumika haiwawezeshi wenye ulemvu kumuona.
"Karibu hotuba zote za viongozi wetu wa kitaifa hutolewa bila kuwapo mkalimani, mbaya zaidi mara chache tumekuwa tukipata viporo tena katika nyakati ambazo si sahihi," alisema Mlemba kwa masikitiko na kuongeza.
...Mfano mzuri mara nyingi hotuba za Rais hazihusishi wakalimani na hivyo kutupita kana kwamba Amiri Jeshi huyu mkuu wa Taifa si kiongozi wetu,".
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Kanisa la Viziwi Tanzania, Mchungaji, Joseph Hiza alisema wanajisikia vibaya wanapokosa hotuba za Rais pale anapohutumia Taifa au kuzindua miradi mbalimbali jambo alilosema kuwa walemavu wana haki ya kupata taarifa hiyo kama wananchi wengine.
alisema kuwa matatizo ya walemavu hasa viziwi na wasioona ni ya kimawasiliano hivyo wamekuwa wakisahaulika kwenye mipanho, sera na utoaji huduma mbalimbali ikiwemo habari na elimu.
"Kutokana na changamoto ya mawasiliano walemavu wamejikita kwenye hatari hata ya kupata maambukizi ya magonjwa ya kuambukiza niliwahi kukutana na vijana niliosoma nao kule Njombe kule kuna jamii kubwa ya watu wenye ulemavu wa kusikia," alisema Hiza na kuongeza.
0 Comments:
Post a Comment