Rais wa Urusi Vladimir Putin ameamuru jeshi la Urusi kuweka vikosi vyake vya nyuklia katika "tahadhari maalum" - kiwango cha juu cha tahadhari kwa Vikosi vya Kimkakati vya Kombora vya Urusi.
Akizungumza na maafisa wakuu wa kijeshi, akiwemo Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu, alisema mataifa ya Magharibi yamechukua "hatua zisizo za kirafiki" kwa Urusi na kuweka "vikwazo visivyo halali".
Rais wa Urusi Vladmir Putin ameamuru usimamizi wa jeshi kuweka kikosi maalum cha nyuklia katika hali "maalum" ya tahadhari.
Hii ni baada ya kile ambacho Moscow inakiita "taarifa za uchokozi" za nchi za muungano wa Nato.
Kiongozi huyo wa Urusi tayari alikuwa ametoa onyo fiche kwamba yuko tayari kutumia silaha za nyuklia anapoanza uvamizi wake nchini Ukraine.
Wiki iliyopita, alionya kwamba "yeyote anayejaribu kutuzuia" ataona matokeo "hujawahi kuona katika historia yako".
Maneno haya yalitafsiriwa kama kuashiria tishio la kutumia silaha za nyuklia ikiwa mataifa ya Magharibi yataweka nia ya kuzuia nia yake.
Mabadiliko haya yaliyotangazwa hadharani ni njia ya Moscow kutuma onyo. Kuweka kikosi hicho kwenye hali ya juu ya tahadhari kunarahisisha kurusha silaha kwa haraka zaidi.
Lakini haimaanishi kuwa kuna nia ya sasa ya kuzitumia silaha hizo za maangamizi.
Urusi ndio taifa lenye akiba kubwa zaidi ya silaha za nyuklia ulimwenguni lakini pia inajua kuwa Nato pia inaakiba inayotosha kuiangamiza Urusi ikiwa zingetumiwa.
Lakini lengo ni uwezekano wa kujaribu kuzuia uungwaji mkono wa Nato kwa Ukraine kwa kuzua hofu juu ya ni kwa kiasi gani yuko tayari kwenda na kuleta sintofahamu juu ya aina gani ya uungwaji mkono kwa Ukraine atauchukulia kuwa mwingi.
Chanzo BBC

0 Comments:
Post a Comment